Tundu Lissu, tunduni - na Jerry C. Muro

Tundu Lissu, tunduni - na Jerry C. Muro

Baada ya kuisoma hiyo post ya Jerry Muro nilichogundua cha kwanza ni kuwa huyo jamaa lengo lake kwenye hilo bandiko lake ni kufanya personal attack kwa Tundu Lissu badala ya kujadili tukio la kuvamiwa hiyo kampuni ya mawakili wa IMMMA na kulipuliwa.

Hebu tuanze na hilo, Tundu Lissu alisoma taarifa hiyo akieleza wazi kuwa yale yalikuwa maamuzi ya BARAZA LA,UONGOZI LA TLS yaliyofanyika katika kikao chao kilichofanyika jana yake na yeye ameyasoma hayo maazimio ya kikao hicho akiwa ndiye Rais wa hiyo TLS.

Kwa mazingira hayo hapo tunaliona kosa LA kwanza la Jerry Muro la bandiko lake almost lote kumuattack Tundu Lissu as individual badala ya kulaumu BARAZA LA UONGOZI LA TLS!

Kosa LA pili ni kuwa yeye Jerry Muro amejikita zaidi katika kuhukumu kuwa maamuzi yaliyofanywa na Tundu Lissu na TLS "yake" ni maamuzi ya hovyo!

Kwanini nasema kuwa huo mtazamo wa Jerry kuwa haupo sahihi.

Iliyolipuliwa na bomu ni ofisi ya mawakili wa kampuni ya IMMMA na kutokana na tukio hilo LA kigaidi ni kuwa hao mawakili hawataweza kutekeleza shughuli zao kwa kipindi fulani kutokana na vitendea kazi vyao vingi kuwa "destroyed" na mabomu hayo yaliyolipuka.

Kwa maana hiyo naamini kwa kuzingatia kitu kinachoitwa SOLIDARITY, maamuzi ya TLS yako sahihi kwa kuwa yameonyesha MSHIKAMANO kwa tukio hilo la kinyama walilofanyiwa mawakili wenzao.

Tuje kwa upande wa waliotekeleza tukio hilo kuwa wamevalia sare za Polisi. Katika tamko lao TLS haijawahukumu moja kwa moja Jeshi la Polisi kuwa ndiyo waliotekekeza tukio hilo Bali imeomba uchunguzi wa haraka na wa kina ufanyike na vyombo vya usalama ili kuwabaini wale wote waliotekekeza tukio hilo LA kinyama ili waweze kuchukiliwa hatua za kisheria.

Kwa hiyo kwa msimamo huo sioni ni kwa vipi hatua hiyo ya TLS ichukuliwe kuwa imekaa kisiasa kwa mlengo wa Chama Fulani.

Pia nieleze sababu nyingine iliyofanya TLS waamue kuendesha huo mgomo wa siku 2 wa kutohudhuria proceedings zozote zitakazofanyika mahakamani siku hizo ingawa hata na wao wanajua kuwa itakuwa pia na madhara makubwa kwa wateja wao, lakini wakati mwingine kutokana na situation inayokukabili unalazimika kuchukua hatua ambayo ingawa kwa upande mwingine utakuwa na madhara lakini unalazimika kuchukua hatua hiyio ili kutoa shinikizo ili kufanyike hatua za haraka za tukio lililotokea.

Nimalizie pia kwa kueleza ni kwanini wananchi wamepunguza Imani kwa kiasi kikubwa kwa Jeshi LA Polisi kushughulikia matukio ya "design" hii ambayo yana dalili kuwa ni maelekezo toka juu....

Hebu tujiulize ni kwanini wale askari waliovamia kituo cha luninga cha Clouds wakiwa na silaha za moto wakiambatana na mtu mwenye wadhifa mkubwa jijini Dar na kutoa vitisho kwa watangazaji wa kituo hicho kuwa watu hao hawakuwahi kupandishwa kizimbani mahakamani kujibu tuhuma za kosa hilo la jinai?

Tujiulize pia swali la pili ni kwanini yule mtu aliyemtolea bastola Nape Nnauye mchana kweupe pale Protea Hotel na picha zikimtambulisha wazi kuwa yule ni nani, lakini hadi leo Jeshi letu la Polisi halikuwahi kumkamata MTU yule na kumfikisha mahakamani na kujibu tuhuma zake hizo za makosa ya jinai?

Nimalizie na suala la utekwaji wa msanii Roma Mkatoliki na kufanyiwa ukatili wa kutisha, ni kwanini Jeshi letu la Polisi hadi leo limeshindwa kuwakamata watu hao na kuwaburuza mahakamani kujibu tuhuma yao hiyo ya makosa ya jinai?

Ni dhahiri kwa experience ya hayo matukio niliyoyataja yaliyotokea kwenye jiji la Dar yanakuwa yanatia mashaka kuwa hata tukio hili la uvamizi wa kampuni ya mawakili wa IMMMA nalo linaelekea kuwa la "style" ile ile ya hayo matukio ya awali yaliyotokea kwenye jiji hilo.
 
Wajerumani waliwauwa Mayahudi, lakini sasa wamekuwa wamoja kati ya watetezi wao wakubwa.

Makaburu walikuwa maadui wakubwa wa CCM lakini sasa hivi wamegeuka kuwa partners wao wakubwa kibiashara.

Kuna kitu kinaitwa change of priorities! Kila jambo lina umuhimu wake kwa wakati wake.
 
Suala la Rushwa alisafishwa Kisheria hivyo hakuhusika nalo bali lilikuwa ni la ' Kichuki ' zaidi dhidi yake kutoka katika ' Mamlaka ' fulani nchini ambayo ilichukiwa Kitendo cha Muro kuwaonyesha wakichukuwa ' rushwa '. Kuhusu Yanga ambako alikuwa ni Msemaji wake wala hajafukuzwa kama ambavyo Wewe na wenzako wengine mnasema bali mkataba wake ulifikia mwisho na wakati huo huo Jerry Muro alikuwa ameshapata ' shavu ' jingine tena la maana huko SUMATRA ambako yupo hadi sasa ' akitiririka ' na ' kuserereka ' vyake tena kwa raha zake huku akila ' bata ' ambazo pengine angeendelea kuwa Yanga hadi leo angezisikia tu ' ndotoni '.

Mwisho ushauri wangu tu mzuri Kwako ili kuonyesha kwamba kweli Wewe ni Great Thinker wa JF basi siku zingine uwe unajikita katika ' mada ' husika iliyopo na siyo ' Kushadadia ' vitu vingine ambavyo vingepaswa ' vishadadiwe ' sana na akina Dada, Mama na Bibi zetu ila bahati mbaya sana ' vinashadadiwa ' na Dume zima. Unatutia mno wasiwasi Sisi ' Wadindaji ' wenzako Mkuu kama kweli Wewe ni mwenzetu.
Asante kwa kumjibu vizuri.
 
Kwa kumbukumbu zangu na kama sikosei,Jerry Muro hata uvamizi wa Bashite clouds aliutetea hadharani.

Si hivyo tu,hata Manji alipokamatwa kwa mara ya kwanza kuhusiana na tuhuma za kutumia dawa za kulevya alionekana kuunga mkono kukamatwa kwake pale alipohojiwa channel 10 katika kipindi cha Mada Moto.

Huyo ndio Jerry.

U-DC unatafutwa kupitia migongo ya watu.
Una maana huyu jamaa haungi mkono wauza dawa za kulevya na watumiaji wa madawa ya kulevya?
Huyu atakuwa msaliti wa chama chetu huyu.
 
Jery Muro yupi huyu? Kama ni yule wa ITV enzi zile basi atafute kazi nyingine maana kila ambalo huanzisha huishaga vibaya. Namkumbuka ukiona anashughulikia jambo flani sana ujue kuna pilau. Vijana wa nyuma kidogo tunamjua .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Walishakutoa meno mkuu ulishabaki kama mbwa abwekaye tu.Mkuu mwalimu alisema mke wa kaisali hapaswi hata kituhumiwa tu nakumbuka ulishagongwa pingu kwa tuhuma za rushwa na uliponapona tu na ninahisi uponaji ule ndo ulipelekea wewe kugeuka kasuku wa watawala nadhani ndo walikuombelezea kikombe kikuepuke.
Turudi kwenye mada,Wewe in mmoja wa watu ambao waliwahi kuwatuhumu polisi tena kwa ushahidi kuwa siyo wqaminifu(baadhi yao)Kwa nini katika hili hautaki kuamini kuwa polisi wanaweza kuhusika?.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa hiyo wakati Mvungi anauawa viongoz wa TLS walikua ni hawa?
 
Jery Muro yupi huyu? Kama ni yule wa ITV enzi zile basi atafute kazi nyingine maana kila ambalo huanzisha huishaga vibaya. Namkumbuka ukiona anashughulikia jambo flani sana ujue kuna pilau. Vijana wa nyuma kidogo tunamjua .

Sent using Jamii Forums mobile app
Ndiye aliye rusha hilo bomu achunguzwe. Ana tabia za kuwa na vifaa vya polisi kama pingu nk. Walio rusha bomu walikuwa ktk sare za polisi.
 
Huyu jery anaonekana ni mwandishi aliyechagua mlengo wake wa kisiasa.

Ndio maana hata kipindi alichorithi kutoka kwa buhohela.pale ITV kimepoteza mvuto .
 
Mgomo (strikes) una faida sana hasa kwa nchi zenye demokrasia.

You are striking( protesting) so as to gain a concession.

Unapoamua kugoma you must have something to claim.

Inawezekana unataka kitu fulani kichunguzwe au kama kimechunguzwa haujaridhika na matokeo yake.

Inawezekana unataka fulani aondolewe mahali fulani ndipo wewe ufike mahali hapo.

Inawezekana unachopata hakitoshi kwa hiyo unataka uongezewe.

Kuhusu mgomo wa TLS chini ya Tundu Lissu sijafaham wanataka nini maana nilisikia uchunguzi unaendelea.
 
kwel kla m2 n mlaji ad jery muro nae kafkia uku kwel tz amna mpenda haki kla m2 yupo kimaslah
 
Tundu Lissu, TUNDUNI
Na Jerry C. Muro

Nianze kwa Kutoa pole kwa jumuiya nzima ya wanasheria nchini, pole yangu sio ya tukio la IMMA advocates, Bali pole yangu ni ya kuchagua Rais wa TLS Chama Chenu 'MAHIRI' cha wanasheria Tanganyika - TLS Ndugu Tundu Lissu ambae AMEDHIHIRISHA kuwa ameanza Rasmi Safari ya Kuizika TLS, kupitia taarifa yake kwa vyombo vya Habari kuhusiana na Tukio la IMMA advocates.
Nianze kwa kuweka msingi wa HOJA yangu kuwa sifurahishwi na kilichotokea kwenye IMMA advocates, ila pia SIFURAHISHWI zaidi na "AKILI NDOGO" za Rais wenu katika hatua za AWALI za kushughulikia suala hili.

Mimi ni Profesional communicator kama mwandishi wa Habari, na Nyinyi wanasheria ni Profesional kwenye Sheria, ukisoma na Kusikiliza kwa umakini TAARIFA ya Mhe Rais wa TLS utagundua makosa makubwa sana ya KIUFUNDI ambayo yanaifanya taarifa nzima kuwa kama taarifa ya Mfalme "****" na kwa sisi MAFUNDI wa taarifa tunasema taarifa ikikosewa katika UANDAAJI na UWASILISHWAJI inakuwa imekosa MASHIKO, na hivyo taarifa nzima kuwa BATILI.

KWANINI BATILI
1. Taarifa iliyowasilishwa na Rais wa TLS tayari kwa kiasi kikubwaa ilishatolewa na Chama cha wananchi CUF [HASHTAG]#teammaalim[/HASHTAG], ukisoma taarifa ya cuf ambayo ilitoka siku moja kabla ya hii ya Rais utaona nachosema, ila hii ya Rais imewaka mbwembwe ya Vifungu Vifungu vingi vya SHERIA tu, ila taarifa zote zimeonyesha kuwa IMMA advocate ni WABIA katika kazi mana cuf inatetewa na IMMA advocate na Rais Lissu anatetewa na IMMA advocate hivyo wote WANAOMBELEZA DHORUBA YA MMBIA WAO., japo TLS ni Chama na Lissu ni Rais, na ni mteja wa IMMA katika hoja hii ya kwanza nimalizie kwa kusema tu Hoi taarifa ni BATILI kwa kuwa Imekuwa taarifa ya KISIASA na Imetolewa na wanasiasa wa vyama viwili tofauti, japo Mmoja ni Rais wa TLS, hapa utaona sasa Hatari ya kuwa na Rais wa TLS ambae ni mwanasiasa.

2. Taarifa ni BATILI kwa kuwa imeanza kwanza kwa KUHUKUMU kuwa Ofisi za IMMA advocate zimepigwa BOMU na POLISI, japo hizi ni taarifa za AWALI lakini kwa maoni yangu TAARIFA haikupaswa kujielekeza kwenye kazi za mamlaka nyingine, mana kama mmeshajua waliolipua ni POLISI basi hamkuitaji kutoa taarifa Bali kufuata SHERIA kuwashtaki POLISI.
Katika hoja hii MWENDELEZO wake inasema wanavitaka vyombo husika wakiwemo "WATUHUMIWA" Polisi kufanya uchunguzi, mbele zaidi tena wanataka kukutana na "MTUHUMIWA" boss wao IGP, hivi hii ni SAWA WANASHERIA, mnataka kukutana kufanya nini tena na IGP au mkurugenzi wa usalama wa taifa ambae majuzi juzi hapa wakati wa Sakata la Bombadier Rais "WENU "alishema kuwa mkurugenzi wa usalama wa taifa" ANAMFUATILIA FUATILIA "sasa iweje Leo aombe mwenyewe kukutana na" MTESI " wake, NDIO MANA NASEMA HAPA KUNA TATIZO YA HIKI CHAMA KUONGOZWA NA MWANASIASA, labda niwakumbushe tu hawa wanasiasa enzi ya Lowassa Walisema" mwizi" alipokwenda kwao wakamuita mfalme wa AMANI hawa ndio wana SIASA.

3. Taarifa ni BATILI, kwa sababu taarifa inataka WANASHERIA kugoma jumanne na jumatano, huu ni MGOMO ambao katika taarifa yao wanaomba ufanywe UCHUNGUZI, lakini pia kwenye taarifa yao wanaomba kuonana na kaimu Jaji Mkuu ambae mmekuja kusema tena hapo Chini ASUSIWE hamtaki kwenda kwenye mahakama anazoziongoza, JAMANI mnajua mnachofanya? Hii ni sawa na KUJITEKENYA MWENYEWE KISHA UKACHEKA MWENYEWE. nadhani Wasomi wana Sheria tukubaliane katika jambo moja MGOMO au KUONANA na "WATESI "wenu huwezi kushika mambo mawili kwa wakati Mmoja lazima MOJA litaponyoka.

4. Hii taarifa ni BATILI, kwa sababu imemtangaza MGOMO pasipo kusema ADUI ni Nani, hivi Hebu tuambieni mnagoma mkilenga KUMUUMIZA Nani? Kuwaumiza wateja wenu walioko MAGEREZANI au? Hivi nyinyi hii kazi ya UANASHERIA ni ya kujitolea katika kazi zenu zote? Hivi hakuna pesa mmechukua za wateja wenu ambazo mnapaswa kuzifanyia kazi, au TUSEME na nyinyi "WEZI" mnachukua hela za wateja wenu kisha mnagoma?
Hebu mtuambie Nani ADUI YENU basi.

MASWALI MAGUMU ZAIDI TLS.

1. Hivi Mbona walipouwawa *WANASHERIA* na *MAWAKILI* nguli nchini, tena waliowasomesha na kuwafundisha *HAMKUGOMA KUSHINIKIZA HAKI ITENDEKE KAMA HIVI LEO,* au mmesahau Vifo vya *"UTATA"* vya Mawakili Marehemu Kapinga, Marehemu Mvungi, Marehemu Mwaikusa? Kwa kuwa mnasahau ngoja tuwakumbushe tu *HAKUNA NAMNA*, Leo hao wazee wamekuwa *"LIABILITY"* kwenu halafu cuf, Lissu, acaccia zimekuwa *"ASSET"*kwenu?

2. Hivi tangu lini mmeanza kushirikiana press releases na vyama vya siasa mfano cuf?

3. Hivi TLS kimekuwa Chama cha Siasa, au kwakuwa Rais wenu ni mwanasiasa?

4. Mnawezaje kuitenganisha TLS na siasa?

5. Katika Sheria kuna neno linaitwa *"INNUENDO"*hivi mnajua maana ya hilo neno katika Sakata hili la IMMA advocate?

6. Hivi mnajua IMMA advocate ni kampuni "inayotajwa" KUCHOTA mabilioni ya fedha za EPA kupitia kampuni ya DEEP GREEN kiasi cha *BIlioni 8* zilichotwa, mnajua hilo? kama hamjui nendeni Brella kisha mkasome anuani za Kampuni ya *DEEP GREEN,* kisha mtangaze *MGOMO.*

7. Hivi mnajua huyu Rais wenu Lissu akiwa Bungeni mwaka 2012 Aliitaja kampuni ya IMMA advocate kuwa ilizitetea kampuni za TanGold na Deep green microfinances *KUCHOTA* pesa za EPA, halafu Leo HAWAHAWA imma advocate ndio wanaomtetea Lissu katika kesi zake?

Hivi mnajua maana ya vita ya *KIUCHUMI,* adui yako anaweza kutumia *MKEO, WATOTO* na hata Ndugu zako ili mradi *APATE USHINDI.*

Mwisho, Nawapenda sana *WANASHERIA,* mana najua mchango wao katika taifa la Tanzania, nawathamini sana Wanasheria wamaotanguliza *UZALENDO* kwa taifa Lao pamoja na changamoto tunazopitia kama taifa Changa, Nawapenda Wanasheria wanaosem *KWELI* kwa maslahi ya taifa Lao na Sio *MATUMBO* yao.

Sasa Sikilizeni, *AKILI ZA KUAMBIWA CHANGANYA NA ZAKO.LEO TUNDU, TUNDUNI.*

Wasalamu
*Jerry C. Muro*
*28/08 /2017*
Yanga ulitimuliwa sababu ya mambo kama haya,sasa wewe sio mwanasheria na pia uhusiki na TLS nini povu linakutoka,sikiliza Jerry zamani ulikuaga smart sana lkn toka uanze kufanya vitu kwa Sifa na kilazimisha umaarufu sasa umekuwa poyoyo sana,wanaetakiwa kuhoji na kuwa na wasiwasi na Chama chao ni Mawakili wenyewe wewe kimekupata nini
 
Back
Top Bottom