Tundu Lissu ni smart lawyer na very good mwanaharakati but he is a lousy politician....huwezi mtukana Nyerere na isi ku cost
Wakuu, hotuba ya Kamanda Lissu Bungeni jana nina uthubutu wa kusema, tena kwa ujasiri kwamba tangu Tanganyika huru iwepo hatujawahi kushuhudia hotuba kali kama ile. Ni hotuba ya kisomi iliyojaa kila aina ya vielelezo na ushahidi, zaidi ya vielelezo 70 (footnotes), sio mchezo.
Ili kukata mzizi wa fitna nawaomba advocates wa Serikali 2 waje na ushahidi na vielelezo visivyo na shaka kukanusha paper ya Kamanda Lissu na sio kupayukapayuka bila mpango wala hoja za maana. I can see kwanini jamaa wanang'ang'ania Serikali 2 kwa udi na uvumba lakini bahati mbaya kwao kadiri wanavyozidi uking'ang'anizi wao ndivyo wanavyozidi kuharibu na kuachwa uchi wa nyama.
Poleni watetezi wa Serikali 2 ambao mnadhani mna akili na uzalendo kuliko Jaji Joseph Warioba, the former Attorney General of the Republic, Prime Minister and VP; kuliko Dr. Salim A. Salim, the former Minister for Defence, Primer Minister, and OAU Chief; kuliko Judge Brig. Gen. Augustine Ramadhan, the former high ranking member of the People's Armed Forces, NEC Chair, and the Chief Justice of the Supreme Court of the People of Tanzania; kuliko magwiji wengine lukuki waliokuwa wamejazana kwenye Tume ya Warioba. Jengeni hoja mueleweke kama Kamanda Lissu alivyofanya na sio kupayuka kama wendawazimu.
Nilistuka sana kusikia eti Nape Nnauye, W. J. Malecela, na Madabida eti wanazunguka huko na huko "kumjibu" Warioba na timu yake iliyojaa vichwa! Are we serious? Kafulila aliuliza Bungeni, hivi Warioba ni binadamu wa kutukanwa nchi hii? Hata kama alifanya makosa anapaswa kukosolewa kwa staha sio kwa matusi ya dhahiri au ya kificho. Kama kweli ni waungwana, CCM wanapaswa kumwomba msamaha Mzee Warioba na watanzania kwa ujumla.
Nakala: Pasco, Chris Lukosi, et. al.
Mimi nipotoshe ili inisaidie nini?.
Mh. Tundu Lissu alianisha mambo manne katika muktadha wa makundi ndani ya CCM na kila jambo lilikuwa na kundi lake. Jambo la nne lilikuwa linamhusu Mwl. Nyerere na siasa za Zanzibar kama nilivyobainisha hapo juu.
Jaribu kuangalia video yake ili upate ukweli na kubainisha vizuri ninachokisema.
Mimi huwa nadhani wanasheria ni watu wazuri sana katika uwanja wa siasa hasa ukiangalia kwa kutumia darubini katika siasa za nchi za magharibi utakuta kuwa, viongozi wengi wa nchi hizo ni wanasheria na wamefanikiwa/wanafanikiwa katika siasa zao.
Kama hoja yako ni kweli, kwa nini inakuwa tofauti kwa Mh. Tundu Lissu?.
Siko hapa kukutaka ukubaliane na kile ninachikiandika. Unaweza ukakubali kutokubaliana lakini hauwezi kuundoa ukweli wa kile Mh. Tundu Lissu alikisema na amekisema kwa ufasaha kabisa.Ndiyo unapotosha tena unajaribu kumingo akili za watu wamuone lisu mtukutu,
-hukusikiliza wala kuisoma hotuba ya Lisu peke yako,
Jitafakali kwa kutumia hekima sisi sio wapuuzi wakukubaliana na propaganda zako kupindisha maneno nakuchomekea neno Nyerere pasipostahili ilikukidhi malengo yako.
Tundu Lissu, kwenye ili la kumponda Nyerere, pro-Chadema wapo kimya masikini.
Mtaipataje Tanganyika bila kupinga hadharani fikra za Nyerere aliyeiuwa? Inatakiwa kwa dhati kabisa mseme wazi kuwa Nyerere alifanya makosa kuiuwa Tanganyika, hapo mtaeleweka, bila hivyo? itatumika fimbo ya Nyerere na fikra za Nyerere na nyinyi hamuwezi kuukubali ukweli kuwa alikosea. Sijui unafaham?
Leo mnatafuta pakutokea, kila ataekuja na lake mtalitafutia sababu, mara oohh Shivji hivi, mara Oooh Warioba vile, mara Oooh Kikwete vile.
Amkeni na mseme tu Nyerere alifanya makosa makubwa sana kuiuwa Tanganyika, mbona hapo mnapata kigugumizi?
Na bila kukataa fikra za Nyerere kuhusu huu Muungano mtatafuta sana scapegoat.
Sasa mnailaumu Zanzibar ndiyo inawanyima Tanganyika yenu? mimi naona Wazanzibari wanawasaidia sana kwenye hii cause yenu ya kuitafuta Tanganyika lakini nyinyi ndio msiojijuwa muanzie wapi. Upo hapo ulipo? Anzeni kwa kuzipinga fikra za Nyerere kuhusu huu muungano, hiyo ndio shortcut pekee ya kupazia malalamiko yenu. Ukipenda usipende hilo halikwepeki.
Mwl. Nyerere hajatukanwa bali ukweli umesemwa labda useme kuwa, ukweli uliosemwa haujazoeleka Tanzania kusemwa!.Lissu omba radhi. Kumtukana Nyerere ni kuwatukana watanzania
Mkuu, nani amesema hapa kuwa Mwl. Nyerere hakuwa mwanadamu?.
Tukubalianemtu kuwa, Mh. Tundu Lissu amepasua jipu ambalo wengi waliogopa na wanaendelea kuogopa kulipasua. Kwa lugha inayoeleweka na wengi, amemchana chana Mwl. Nyerere na pamoja na kitabu chake cha Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania.
Tundu Lissu ni smart lawyer na very good mwanaharakati but he is a lousy politician....huwezi mtukana Nyerere na isi ku cost
Mkuu, hizo ndiyo hoja zenyewe kuhusu Muungano kwa sababu huwezi kusema kuhusu Muungano bila kumuhusisha Mwl. Nyerere.JULIUS NYERERE-Humanist,Politician ,and Thinker.-POLE SANA TUNDU LISU,HUNA HADHI YA KUMKEJELI BABA WA TAIFA,JIKITE KATIKA KUJENGA HOJA ZAKO TU,UTAELEWEKA.
Namuheshimu Lissu kwa michango yake bungeni lakini katika hili amenikera mno.alikuwa wapi kuyasema hayo enzi ya uhai wa Nyerere. Kama aliogopa kuchapwa viboko na akae kimya milele.adui wa nyerere mzee mtei atakuwa alimtuma tundu lisu amtukane nyerere
You have done!.No comment
Ndiyo unapotosha tena unajaribu kumingo akili za watu wamuone lisu mtukutu,
-hukusikiliza wala kuisoma hotuba ya Lisu peke yako,
Jitafakali kwa kutumia hekima sisi sio wapuuzi wakukubaliana na propaganda zako kupindisha maneno nakuchomekea neno Nyerere pasipostahili ilikukidhi malengo yako.
nyerere ndio role model wa dr.slaa, mbowe , yericko nyerere,bensaanane halafu tundu lisu anamtukana.. lisu hana adabu kwa viongozi wake wa chama