Tundu Lissu kuitwa kwenye Kamati ya maadili ya madiwani Singida

watanzania tunasahau mapema au hatutaki kufikiri. Mzazi au Baba nyumbani kuchangisha watoto si dalili za kushindwa kuwa Baba ambaye ni responsible jamani? Pia, watanzania hulipa kodi mbalimbali, zinatumikaje? Kazi ya kodi ni kuleta maendeleo, za kwetu huenda wapi? Madawati, madawa, madarasa na vinginevyo ni jukumu la serikali na si watu kuchangishwa. Lissu yuko sahihi. Hawa watu wanatuchezea akili sana. Kodi ni nyingi twalipa then wanaishia kuzichakachua. Jaribu kufikiria halmashauri inapopewa kwa mfano milioni mia saba mwezi wa sita na ndo mwezi wa mwisho kumaliza mwaka wa fedha, inazitumiaje? Ni kwamba zinarudi hazina na kutafutiwa pa kuzitolea ili ziliwe. Tanzania mfumo wa uongozi umechoka sana. Wapo wachache sana but hawana nguvu ya kubadili chochote.
 
Yaani watu wengine nafikiri 'medula oblangata' zao zimeundwa na haja kubwa,
Haitoki hewani tu kua watu wasichangie, swala ni kwamba wanachangia nini? kwa niaba na faida ya nani?
Unalipia ushuru wa soko, je huduma muhimu kama choo, bafu, maji na usafi kwa ujumla hapo sokoni unaboreshwa?
Hapo hujajiuliza bado kama hakuna bajeti yoyote kutoka serikalin inayohusu uboreshaji wa hilo soko?
Ujinga wako kukubali kuchangia mafisadi bila kuhoji usikufanye u-generalize kwamba lazima na wa-singida nao wachangie
 
Kimsingi lisu yuko sahihi,amezuia wananchi wasichange mpaka maelezo ya kina yatakapotolewa kuwa hizo fedha zinatumikaje?pia fedha ya serikali za mitaa zinatumika vipi?tatizo liko wapi?
 
Hoja hii ni ovyo kivipi wakati nchi nzima michango inachangwa, kwa nini Singida Mashariki pekee ndio michango isiwepo?
unamaanisha watanzania wengi kutojua haki zao kunafanya hata wale wachache wanaoanza kujua wachange. Singida shikilieni msimamo wenu
 
Lissu ana hoja na inatakiwa kujibiwa kwa hoja, watu walichanga fedha nyingi na mbunge mmoja wa singida akatuhumiwa kutumia michango ya wananchi kufanyia arusi (Lazaro Nyalandu). Napita tu wakuu, mana hata mtoa hoja anampinga Lissu sijui anatumia tumbo au kichwa kufikiri
 
Tatizo kuu ni kwamba Wananchi walio wengi, kulingana na utafiti wangu hawakubaliani na vitendo vya Lissu vya kukodi vijana wa kihuni ili kuwapiga wakusanya michango! Madarasa mbalimbali ya Shule za Msingi na Sekondari ujenzi wake mpaka sasa umesimama kwa sababu ya vitisho ya Lissu na vijana wake!

Una ushauhidi na madai yako ? Better kufungua kesi basi maana hiyo ni crime kupiga watu vinginevyo huu ni upupu hata mimi nyumbani kwetu nilisema sitaki kuona mtu anakuja kuomba mchango wa maendeleo ya kijijini na I meant it sasa wajaribu waone nitakavyo wafanya .Tuache majungu .
 
Kwa nini watu hawataki kukubali pia hoja za Lissu. Jamani lini na wapi serikali imewahi kutoa taarifa za michango hiyo ya mbuzi, kuku, ngombe, shilingi elfu kumi cjui na vitu gani vingine nje ya utaratibu? Hoja za Lissu zijibiwe kwa hoja. Ni kweli wananchi wamezoeshwa kuonewa sasa ndo waendelee kuonewa tu? Kwa mfano amekuwa akisema kuna fedha zimetengwa kwa ajili ya madawati, kujenga madarasa na masuala mengine ya maendeleo na zipo katika taarifa za PM akisoma bungeni. Yaani iwapo fedha hizo zingetumika wananchi ama wasingechangiswa ama wangechangishwa kiasi kigogo wanachomudu wala wasingekimbizana na mgambo na kufanyiwa kila aina ya unyama huko vijijini.Lakini fedha hizo hazionekani, kwa sababu hiyo miradi haikufanyika. Sasa mawili, ama serikali inadananya kuwa imepeleka fedha wakati haijapeleka (tena anasema PM bungeni) au fedha zimepelekwa halafu zimeliwa! Mbona hakuna majibu ya hoja hizi. Lakini pia kwa nini fedha hizo za michango zisiwekwe katika utaratibu wa kukaguliwa na CAG, Serikali inaogopa nini kujibu hoja hizi. Hata ninyi watetezi wa hoja za madiwani hao na serikali ya kinyonyaji ya Singida. Hiyo michango iko kwa mujibu wa sheria ipi, maana Lissu amekuwa akitumia sheria kuipinga.
nakuunga mkono 100%. Wananchi tumezidi kuonewa jamani. Michango kibao mabadiliko ktk maendeleo hakuna
 
Tatizo kuu ni kwamba Wananchi walio wengi, kulingana na utafiti wangu hawakubaliani na vitendo vya Lissu vya kukodi vijana wa kihuni ili kuwapiga wakusanya michango! Madarasa mbalimbali ya Shule za Msingi na Sekondari ujenzi wake mpaka sasa umesimama kwa sababu ya vitisho ya Lissu na vijana wake!
Umepotoshwa nawe ukapotoka.
 
Una ushauhidi na madai yako ? Better kufungua kesi basi maana hiyo ni crime kupiga watu vinginevyo huu ni upupu hata mimi nyumbani kwetu nilisema sitaki kuona mtu anakuja kuomba mchango wa maendeleo ya kijijini na I meant it sasa wajaribu waone nitakavyo wafanya .Tuache majungu .
Sina "locus standi" ya kufungua kesi na vile vile kama kesi haijafunguliwa haimaanishi kwamba kitendo hakijatokea kabisa!
 
Lissu ana hoja na inatakiwa kujibiwa kwa hoja, watu walichanga fedha nyingi na mbunge mmoja wa singida akatuhumiwa kutumia michango ya wananchi kufanyia arusi (Lazaro Nyalandu). Napita tu wakuu, mana hata mtoa hoja anampinga Lissu sijui anatumia tumbo au kichwa kufikiri
Sidhani kama Lissu ni Mungu hata asikosolewe! Wewe mwenyewe umetoa allegations ambazo huna support yoyote dhidi ya Arusi ya Nyalandu, sasa mimi na wewe nani anatumia tumbo au kichwa kufikiri?
 
Kwa utafiti wako uliofanya ukweli ni upi?
Ukweli ni...wananchi wengi achilia mbali wa singida wamechoshwa na michango wasiyoona tija yake. Hata wananchi wa majimbo mengine wanatamani wangepata mbunge kama lissu anayeweza kuwaonyesha njia ya kupata haki zao. Halafu hao unaowaita wahuni sijui unathibitishaje?
 
Kama hakuna takwimu zinazo onyesha wananchi wamechanga kiasi gani na zimetumika vipi, namuunga mkono Tundu Lissu kwa 100% mpaka kila kitu kiwe wazi kwa wachangiaji!
Mkuu tupo pamoja hakuna cha mambo ya siri siri hapa tuambiene kila kitu,,,Go Go Lisu wala wasikutishe" Tupo pamoja.
 
Unaanzisha mada kujadili mtu hili hasitete wananchni wake? kweli wewe kilaza kabisa, unaongea kama mtoto wa bata unasema mwenyewe Lissu alisema wasichangie hadi taarifa ya michango itolewe sasa kwanini usitumie huu muda wako kuelimisha hao wajinga wenzio kutoa taarifa hiyo, wao wanashindwa nini kutoa taarifa ya fedha? waambie tumekwambia wewe na wao wote ni wajinga kama hawataki kutoa taarifa ya fedha.
 
Mkuu tupo pamoja hakuna cha mambo ya siri siri hapa tuambiene kila kitu,,,Go Go Lisu wala wasikutishe" Tupo pamoja.
Magamba kama wana kubalika si waende tu kuwaelimisha wananchi umuhimu wa kuchangia nao watatoa...

Isije ikawa Lissu ndio kisingizio wakati umaskini umeletwa na magamba wenyewe...
 
Unaanzisha mada kujadili mtu hili hasitete wananchni wake? kweli wewe kilaza kabisa, unaongea kama mtoto wa bata unasema mwenyewe Lissu alisema wasichangie hadi taarifa ya michango itolewe sasa kwanini usitumie huu muda wako kuelimisha hao wajinga wenzio kutoa taarifa hiyo, wao wanashindwa nini kutoa taarifa ya fedha? waambie tumekwambia wewe na wao wote ni wajinga kama hawataki kutoa taarifa ya fedha.
Tatizo la Lissu ni kujiingiza kichwa kichwa, na ndio mtego wenyewe wa magamba, kwa kuwaambia wananchi kuwa wasichangie michango kwa kuwa yeye anajua fedha zilipo, kwa hiyo wananchi wanasubiri hizo "fedha za Lissu" ili waendelee na ujenzi wa madarasa!
 
Halafu hao unaowaita wahuni sijui unathibitishaje?
Nilisimuliwa na wananchi mbali mbali wa Jimbo husika wakilaani vitendo anavyowafanyia Tundu Lissu! Wamedai pia kwamba huyu Lissu hana lolote analofanya Jimboni kwake zaidi ya kutamba eti "amemshtaki hata Spika wa Bunge!" Ni majigambo (sound) tu hana lolote la maendeleo!
 
wananchi hao hawalipi kodi, yaani kuitwa na madiwani wa ccm wasiojua sheria kama lisu ndio unaona kuna jambo singida, kumbuka singida kwa lisu halmashauri inaongozwa na ccm haya yanategemewa huoni kama ni magamba tu haya. Yaani maendeleo yaletwe kwa michango huoni kama haelewani na ccm na si wananchi? Unapocukua take try to be more critical ndio maana hoja hii inaonekana hovyo
Well spoken man.... Good job.
 
Ni kwa sababu ya kuzuia michango ya maendeleo hadi taarifa za michango hiyo zitolewe! Baadhi ya Madiwani wamemwagiza Tundu Lissu atoe michango hiyo toka mfukoni mwake kama hataki watu wachangie, lakini Diwani mmoja amedai kwamba anajua kwamba Lissu ni mwanasheria lakini matendo yake hayafanani na taaluma yake! Hata hivyo Tundu Lissu ameshikilia msimamo wake wa kuzuia wananchi kuchangisha michango! Kwa hiyo imeamuliwa afikishwe kwenye Kamati ya Maadili ya Madiwani ili kumjadili! Source: Habari, Star Tv. My take: Kamanda Lissu kubali tu yaishe, Jimboni kwako hali si shwari kuhusu wewe! Ni ushauri usiohitaji malipo yoyote!

Watanzania bwana...wamezoea michango kila mahali. Na sasa wapo tayari kudaiwa michango bila taarifa?! Kweli hii nchi imejaa vilaza...
 
Nilisimuliwa na wananchi mbali mbali wa Jimbo husika wakilaani vitendo anavyowafanyia Tundu Lissu! Wamedai pia kwamba huyu Lissu hana lolote analofanya Jimboni kwake zaidi ya kutamba eti "amemshtaki hata Spika wa Bunge!" Ni majigambo (sound) tu hana lolote la maendeleo!
ulichofanya ni sawa na kuwauliza mashabiki wa Yanga kuwa Berko na Kaseja nani mkali, obvious jibu litakuwa Berko ni mkali. Probably na wewe wananchi uliowahoji ni wa chama tofauti na cha Lissu.Halafu kuhusu Lissu kutofanya kitu jimboni kwake. Weka propaganda pembeni na ujiulize swali hili. Hao wabunge waliokaa majimboni kwao miaka 20 wamefanya nini? Sasa ndio umgeukie Lissu na mwaka wake mmoja
 
Back
Top Bottom