Tundu Lissu: Hotuba ya Rais Magufuli kuhusu Makontena ya Mchanga, inatia shaka ya rule of state

Kwa jinsi hiyo mikataba ilivyoandaliwa na inavoikaba Serikali zoezi la kuijadili upya ni kizungumkuti. Labda wanasheria wangeshauri kitaalam nchi itajiondoa vipi kwenye shimo hilo la mikataba mibovu bila kukiuka haki za wahusika kama zilivyoainishwa ndani ya mikataba hiyo.




Andiko limeainisha na limetoa mfano wa Rais wa Bolivia Evo Morales namna alivyofanikiwa kuzuia ujangiri wa kiuchumi nchini mwake,Magufuli alipaswa kufanya aliyoyafanya Evo kabla hajakimbilia "kuteka"mali za watu wanazozimiliki kihalali kabisa.Kwa mujibu wa mikataba yetu iliyosainiwa na Masultani Mangungo wa kizazi kipya chini ya awamu ya 3-4,mchanga huo ni mali ya mwekezaji,kuzuia mali ya mtu ni utekaji na hilo litapelekea Mwenye Mali kudai fidia.


.............................................................


Evo Morales wa Bolivia alikuwa na mikataba kama ya kwetu alipochaguliwa in December ya 2006. Cha kwanza alichofanya ni kuiondoa Bolivia kwenye MIGA Convention na kwenye bilateral investment treaties (BITs) zilizokuwa zinalazimisha international arbitration kwenye migogoro ya uwezekaji. Baada ya hapo ndio akabadilisha sheria na mikataba ya uwekezaji iliyoipa Bolivia sehemu kubwa ya umilikaji wa gesi na mafuta ya nchi yake. Of course, Morales is a Bolivarian na rafiki wa Castro, marehemu Hugo Chavez na wakushoto wengine. Magufuli is none of the above. He's a proto-fascist who believes in nothing but violent state power.
 
Mchanga kama kutetesi una dhahabu na wala si makinikia kama makubaliano yalivyo! Unataka uruhusiwe mchanga usafirishwe ushahidi utapata wapi?? Hebu tumieni akili kidogo basi..
Kama tulikosea kwenye mikataba nchi itaingia hasara kubwa mno.. tusubiri tu
 
Kikubwa anachosema Tundu Lissu ni kwamba Pombe kaikuta mikataba waliyoingia Mkapa na Kikwete. Haimaanishi kwamba anakubaliana nayo, la hasha.

Kikubwa ni namna ya kujinasua kwenye mikataba hiyo dhalimu. Evo Morales alitumia akili kujitoa kwanza. Hakuanza kutoa amri za kipuuzi ambazo zingeiletea Bolivia hasara mbele ya safari. Pombe analo la kujifunza hapa
 
Mambo yanayohitaji Sheria yaendeshwe kutumia Sheria. Mikataba ni Sheria. Ni vyema tukafuata maana kila mkataba una kipengele cha hamna ya Ana kuu una au kusuluhisha iwapo kutakuwa na mgogoro wa kimaslahi kwa pande yeyote ile. Tunachokifanya sasa kwa upande wa madini hakipo katika kipengele chochote. Zaidi sana ubabe huu utauingiza taifa katika majanga ya malipo makubwa sana ya fidia. Tunajiandaa kujikaangaa kwa mafuta yetu wenyewe. Sijui ni laana gani hii tuliyoipata nchi hii!!!
Hivi watz tumerogwa na nani?? Tunaibiwa bado tunawatetea wanaotuibia kwa kisingizio cha mkataba?? Mkataba unasema wasafirishe dhahabu au makinikia?? Raisi alichofanya ni sahihi kabisa kunatetesi/taarifa za kiintelinjesia kuwa mchanga huo sio makinikia kama mkataba unavyosema sasa Raisi anataka uchunguzi wa kitaalamu ufanyike kujiridhisha kama ni kweli au la sasa kosa lake ni nini??
 
unafiki na kujitafutia mtaji kwa wananchi kama unaipenda nchi yetu si ungemuandikia waraka kwake ukamshauri wewe ni kumponda hauna lengo la kuikuza nchi kiuchumi. wewe huo mfano wa bolivia ungemwambia. ila kila kukicha ni kumkosoa na sio kushauri, mpe way forward
Ungekuwa na akili angalau kidoooogo sana, usingeandika haya.

Kama Tundu Lissu anatafuta umaarufu kwa watu, hilo halimzuii mhusika kubeba la maana katika yote yaliyosemwa. Au hukuwepo nchini wakati anasema yeye hapangiwi cha kufanya?
 
Kuna sehemu nilimskia Prezidaa akidai kuwa kwenye huo mchanga kuna dhahabu na amewataka wataalamu wa jiolojia kuchunguza huo mchanga ndio maana kazuia. Mbona hili hawalizungumzii au mi nilisikia vibaya?. Je kuchanganya dhahabu na huo mchanga ni part ya mkataba?
 
Tatizo ni kwamba mkulu anadili na matawi badala ya mizizi, kuna mambo mengine anafanya kufurahisha tu watu lakini watu haohao baadae wanaanza kumkosoa na hii yote ni kwasababu hasikilizi ushauri kwa kuogopa sifa zitaenda kwa mshauri
 
unafiki na kujitafutia mtaji kwa wananchi kama unaipenda nchi yetu si ungemuandikia waraka kwake ukamshauri wewe ni kumponda hauna lengo la kuikuza nchi kiuchumi. wewe huo mfano wa bolivia ungemwambia. ila kila kukicha ni kumkosoa na sio kushauri, mpe way forward
Alioutuo Tundu Lissu ni ushauri tosha.Wewe ulitaka aende Ikulu akamshauri?.
 
Kuna sehemu nilimskia Prezidaa akidai kuwa kwenye huo mchanga kuna dhahabu na amewataka wataalamu wa jiolojia kuchunguza huo mchanga ndio maana kazuia. Mbona hili hawalizungumzii au mi nilisikia vibaya?. Je kuchanganya dhahabu na huo mchanga ni part ya mkataba?
si amtumie prof muhogo ameweka wasomi serikalini ili wafanye kazi ya kina
 
unafiki na kujitafutia mtaji kwa wananchi kama unaipenda nchi yetu si ungemuandikia waraka kwake ukamshauri wewe ni kumponda hauna lengo la kuikuza nchi kiuchumi. wewe huo mfano wa bolivia ungemwambia. ila kila kukicha ni kumkosoa na sio kushauri, mpe way forward
Tangu lini yule jamaa akashaurika.......? hamsikilizi mtu,.....! keshasema mwenyewe kuwa hapangiwi cha kufanya yeye ndo kila kitu..............sasa hapo sembuse ushauri wenyewe utoke kwa mtu wa upinzani ndio hataki ata kusikia...kama wao kwa wao tu wamemshindwa .....ndugu yetu Lissu atasikilizwa kweli .....You have to know nature ya mtu anayetaka apewe ushauri........
 
unafiki na kujitafutia mtaji kwa wananchi kama unaipenda nchi yetu si ungemuandikia waraka kwake ukamshauri wewe ni kumponda hauna lengo la kuikuza nchi kiuchumi. wewe huo mfano wa bolivia ungemwambia. ila kila kukicha ni kumkosoa na sio kushauri, mpe way forward
Tangu lini yule jamaa akashaurika.......? hamsikilizi mtu,.....! keshasema mwenyewe kuwa hapangiwi cha kufanya yeye ndo kila kitu..............sasa hapo sembuse ushauri wenyewe utoke kwa mtu wa upinzani ndio hataki ata kusikia...kama wao kwa wao tu wamemshindwa .....ndugu yetu Lissu atasikilizwa kweli .....You have to know nature ya mtu anayetaka apewe ushauri........
 
si amtumie prof muhogo ameweka wasomi serikalini ili wafanye kazi ya kina
Wasomi wetu nao wamekua waoga mno kila kitu ni ndio mkuu. Kama wangekua wanambishia na kumwelewesha hata yeye angepunguza makali. Sasa wanaposema ndio yeye anajiona yupo sawa
 
Hiyo point gani weka hapa na sio kuongelea kiujumla tu utadhani nyumbu anakimbizwa na chui



Kuna mtu anajiita kiongozi kwa kuchaguliwa na watu wa aina yako!Sishangai hata ayatendayo kwa sababu matendo yake yanaakisi akili za waliomchagua.Msome Lissu hapa kabla hujakurupuka na kuwadharirisha uliowachagua hadi wajihisi wamechaguliwa na wehu.

……......................................................................


Evo Morales wa Bolivia alikuwa na mikataba kama ya kwetu alipochaguliwa in December ya 2006. Cha kwanza alichofanya ni kuiondoa Bolivia kwenye MIGA Convention na kwenye bilateral investment treaties (BITs) zilizokuwa zinalazimisha international arbitration kwenye migogoro ya uwezekaji. Baada ya hapo ndio akabadilisha sheria na mikataba ya uwekezaji iliyoipa Bolivia sehemu kubwa ya umilikaji wa gesi na mafuta ya nchi yake. Of course, Morales is a Bolivarian na rafiki wa Castro, marehemu Hugo Chavez na wakushoto wengine. Magufuli is none of the above. He's a proto-fascist who believes in nothing but violent state power.
 
Ushauri mzuri kama Mh Rais atauzingatia kwa sasa. Wazungu waliowengi ni wezi sana na wanatumia ulafi na upumbavu wa viongozi wetu kututia umaskini. Rais tumia busara na hekima kututoa hapa vinginevyo tutaingia matatani. Yaani kwenye madini hapa ndipo napowachukia sana Marais waliopita kwani mikataba waliokuwa wanasaini kama kina Mangungu wa Msovero ndiyo inatutesa sasa. Mungu tuhurumie madini yetu wanayafaidi wageni kazi kweli kweli.
 
Lisu anapoteza mwelekeo japo mkulu kapotea zaidi
Andika utuambie tulipokosea,tulipokosea na tutakavyorekebisha, sio kukanusha na kuponda tu
Kwa jinsi hiyo mikataba ilivyoandaliwa na inavoikaba Serikali zoezi la kuijadili upya ni kizungumkuti. Labda wanasheria wangeshauri kitaalam nchi itajiondoa vipi kwenye shimo hilo la mikataba mibovu bila kukiuka haki za wahusika kama zilivyoainishwa ndani ya mikataba hiyo.
 
Tundu hayo unayoyatetea kwa maslahi ya nani,utadai mikataba ndio inayolinda yote hayo ,je mbona tuna mikataba mingi mibovu iliyotiwa saini kwa njia za rushwa kwa hiyo tuache tu kwa kuwa akina Kafumu waliruhusu,kwa mpango huu nashukuru Mungu ,Chadema mtaiona tu ikulu ,zamani mlijipambanua kama watetea haki na maslahi ya nchi ,siku hizi Chadema inateteta kila aina ya uozo,ufisadi.Chadema mshakuwa chama cha hovyo kabisa.
Unaelewa kinacho jadiliwa hapa?
 
Back
Top Bottom