Tundu Lissu: CHADEMA haijapokea ruzuku hata senti 5, Baraza Kuu kukaa Machi au Aprili

Mkuu hutamuona Mbowe wala Mnyika anaongelea hii ishu ya akina Mdee. Tatizo mmefungwa na mahaba ya chama hamko tayari kuangalia upande mwingine wa shilingi. Nasisitiza Mchaga hajawahi kuniangusha kwenye shilingi. Kuna mambo mkijakiyajua huko mbeleni mtajiona wajinga sana. CCM na CDM ni walewale tu.
Yaani unamtetea mgogo Ndugai kwa kumponda Mbowe na Mnyika....kwa hiyo Mbowe aende akawatoe kwa nguvu pale bungeni? Haahaa mgogo kashasema wale ni wabunge hata Kama wamefukuzwa na chama Chao...
 
Hiyo taarifa ya Lisu imekosewa?! Kaandika hawawezi kuitisha kikao kuwajadili hao waasi.

Kikao kikifanyika April itakuwa bado ndani ya muda kikatiba (katiba ya chadema) kujadili rufaa ya hao waasi?
... hatutaitisha kikao kujadili waasi tu... hiyo sentensi umeielewaje, it means there other business to be discussed too.
 
Mzalendo aliyekimbia nchi yake?

..Siyo ajabu kwa mwanasiasa au mwanaharakati kukimbia utawala dhalimu wa kikatili nchini kwake.

..Wanasiasa wafuatao walipata kuishi ukimbizini kama hivi alivyofanya Tundu Lissu.

1.Yoweri Museveni [ uganda], 2.Salva Kiir [ South Sudan], 3. Arthur Mutharika [ Malawi ], 4. Felix Tshisekedi [ Drc] ,5. Jacob Zuma [ Afrika Kusini]
6. Sam Nujoma [ Namibia], 7. Emmerson Mnangagwa[zimbabwe], 8. Yasser Arafat [ Palestina], 9. Ayatollah Khomeini [ Iran], 10. Augustino Neto[ Angola], 11. Joaquim Chissano[ Msumbiji].
 
... hatutaitisha kikao kujadili waasi tu... hiyo sentensi umeielewaje, it means there other business to be discussed too.
Wabunge walifukuzwa Novemba 27 mwaka jana. Walikata rufaa ndani ya mwezi mmoja kama katiba inavyotaka.

Ninachoelewa ni kwamba kikao kikiitishwa April kitakuwa nje ya muda unaokubalika kikatiba (siku 90) kujadili rufaa yao.

Labda uongozi umeamua kukubali kinyemela yaishe, au wewe unaelewaje?!
 
Wabunge walifukuzwa Novemba 27 mwaka jana. Walikata rufaa ndani ya mwezi mmoja kama katiba inavyotaka.

Ninachoelewa ni kwamba kikao kikiitishwa April kitakuwa nje ya muda unaokubalika kikatiba (siku 90) kujadili rufaa yao.

Labda uongozi umeamua kukubali kinyemela yaishe, au wewe unaelewaje?!
Kwanini chama kipoteze muda na gharama kubwa kujadili ajenda moja ya ‘waasi’ ambao tayari aliyewateua kasema atawalinda kwa gharama yeyote?

Haraka ya nini be patient (you) they will get what they deserve.
 
Hongera bi.mdogo inaonekana una taarifa nyingi kwel znazomuhusu mumeo
Uko very shallow kwenye deep information za kinachoendelea nchini. Tundu Lissu alikuwaga mtetezi wa wanyonge kipindi cha Mkapa tu. Mwishoni mwa Jk ni mmojawapo wa waliowekewa pesa za Lowassa kwenye account. 2017 aliungana na EMMMA advocates kuwatetea ACACIA unadhani ilikuwa ni FREE?!?.. Alipambania wazungu mpaka kuwapatia nyaraka zilizosababisha Bombadier Q400 isije ishikiliwe CANADA July 2017 unafikiri ilikuwa ni bure tu!?.. Sababu umejawa na mahaba na unaongozwa na ushabiki huwezi kuelewa haya niliyokwambia. Kama umebahatika kuwa na ndugu yako yeyote kwenye system unayemuamini kamuulize kuhusu haya atakwambia, kama huna sina namna ya kukuhakikishia zaidi ya kukuacha uendelee kushabikia mambo usiyoyajua. Ila nilichowahi kuwaapia ni kuwa Lissu hawezi kuwa Raisi wa nchi hii sio 2020,2025 bali ni NEVER. Ni kutokana na record yake ya usaliti juu ya taifa hili. Faili lake lipo na ushahidi usiotia shaka upo.
 
We nguchiro ucjifanye unajua ya nchi hii kumbe ni chakubanga tu
Hakuna kitu chochote unachoelewa, nakuhakikishia uko very shallow kwenye information za ndani za nchi hii. Endelea kucheza na ngoma za vijiweni na ushabiki wa vyama. Pengine huko baadae utabahatika kuujua ukweli. Hujui lolote kuhusu Mbowe, Lissu, Mnyika na wengine wengi. Kwa kifupi unashabikia mambo usiyoyaelewa. Ila ukiamua kuutafuta ukweli utaupata Ila sio lazima. Watu Kama wewe uwepo wao ni muhimu pia.
 
Angeongea Mbowe au Mnyika waweza kuamini CHADEMA haijapokea ruzuku, Ila mtu yupo ulaya tena kwenye LOCKDOWN aje kujua ya account za chama bongo!?.. au wanacheza na akili za NYUMBU wa ufipa wakamtumia Lissu kuwatuliza. Mchaga kwenye shilingi hajawahi kuniangusha.

Toka jana nakuambia weka ushahidi wa cdm kupokea ruzuku maana ww upo hapo Tanzania na sio Belgium.
 
Mkuu umesoma Historia? Unajua kwanini Nelson Mandela alipendwa sana Afrika Kusini? Unajua kwanini Jacob Zuma alipendwa sana kuliko "Mtangulizi" wake Thabo Mbeki? Ukiwa na hayo majibu, tutaongea!!!!!

Hizi tunaita ni hekaya.
 
Angeongea Mbowe au Mnyika waweza kuamini CHADEMA haijapokea ruzuku, Ila mtu yupo ulaya tena kwenye LOCKDOWN aje kujua ya account za chama bongo!?.. au wanacheza na akili za NYUMBU wa ufipa wakamtumia Lissu kuwatuliza. Mchaga kwenye shilingi hajawahi kuniangusha.
Nyumbu ni wazazi wako.
 
"Hatujapokea ruzuku yoyote. Katibu Mkuu wa @ChademaTz aliandikiwa barua na Msajili wa Vyama vya siasa aende kwenye mkutano wa kujadili masuala ya ruzuku. Katibu mkuu alikataa, kama wanasema tumepokea ruzuku, waoneshe ni sehemu gani tumepokea na kusaini" Ndg. @TunduALissu,

"Ni kweli wabunge 19 tuliowafukuza wamekata rufaa. Kwenye kikao cha kamati kuu wiki iliyopita tumefanya maamuzi kuwa, kikao cha Baraza Kuu kitaitishwa kati ya mwezi Machi na Aprili, hatuwezi kuiitisha kikao cha Baraza Kuu eti tu kwa ajili ya kuwasikiliza hao waasi" @TunduALissu.
Kama mwenyekiti Mbowe alitoa tamko la maamuzi ya kamati juu ya watu hao kuwa wanakufukuzwa mara moja kwa nini Kamati Kuu haikutani haraka kutimiza takwa hilo. Kama maagizo ya kamati yalikuwa kujazwa maramoja kwa nafasi zao za uongozi katika chama, kwa nini mpaka leo hazijajazwa. Mnatoa mwanya huu wa muda wa nini? Au mmegundua ruzuku ni kidogo mnasubiri mpaka April zitakuwa zimeongezeka kidogo mchukuwe za mkupuo wa miezi yote ya nyuma maana kisheria bado ni zenu😃😃😃
 
CCM kimekuwa chama cha majambazi wanajikwapulia ruzuku yote %100 na kujinunulia mavieitee
 
Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara Ndg Tundu Lissu amesema, chama hakijapokea ruzuku yeyote toka serikalini, na kama kuna mtu ana ushahidi kuwa tumepokea basi auonyeshe, kaongeza kusema, fedha za ruzuku kwa vyama vya siasa ni chanzo kimoja tu cha mapato ya chama, kuna vyama havina ruzuku lakini vinaendesha shughuli zao. Chadema kina wanachama 6,700,000 hao wanachama ndio watakaoendesha shughuli za chama.

"Hatujapokea ruzuku yoyote. Katibu Mkuu wa @ChademaTz aliandikiwa barua na Msajili wa Vyama vya siasa aende kwenye mkutano wa kujadili masuala ya ruzuku. Katibu mkuu alikataa, kama wanasema tumepokea ruzuku, waoneshe ni sehemu gani tumepokea na kusaini" Ndg. @TunduALissu.

Kuhusu wanachama 19 waasi waliofukuzwa Lissu kasema, kazi ya Kamati Kuu ni kusimamia katiba na misingi ya chama na wala sio kusimamia kanuni za Bunge, kama wanakwenda bungeni sio kosa letu ni kosa la aliyewapokea.

"Kamati Kuu ya @ChademaTz imeketi na kuamua kuwa wabunge 19 ambao wameasi na kukiuka maamuzi ya chama tuliwafukuza uanachama, kwa mujibu wa katiba ya nchi yetu tangu 1965 tulipoingia rasmi katika mfumo wa chama kimoja mpaka leo, Mbunge akipoteza uanachama wa chama cha siasa anapoteza na ubunge, kama wanakwenda bungeni sio kosa letu ni kosa la wanaowapokea na kuwapa fedha za umma wakati si wabunge”.

"Ni kweli wabunge 19 tuliowafukuza wamekata rufaa. Kwenye kikao cha kamati kuu wiki iliyopita tumefanya maamuzi kuwa, kikao cha Baraza Kuu kitaitishwa kati ya mwezi Machi na Aprili, hatuwezi kuiitisha kikao cha Baraza Kuu eti tu kwa ajili ya kuwasikiliza hao waasi" @TunduALissu.
Atoe bank statement za Chama

 
Back
Top Bottom