Uchaguzi 2020 Tundu Lissu awataka wanachama kutoshangilia kwa hofu ya mapingamizi, afikiria kuweka pingamizi

Libya

JF-Expert Member
Nov 11, 2016
783
1,918


===========​


Tundu Lissu amewataka wanachama wasishangilie sana kwani wanatarajia mapingamizi hivyo wasubiri kesho mpaka saa kumi kuona hali itavyokuwa.

Tundu Lissu: Sio wao peke yako wanaojua kuandika mapingamizi na sisi tunajua hivyo usiku huu nitaangalia kitu gani tunacho ambacho tunaweza tukafanya ambacho sheria za uchaguzi zinaturuhusu, na sisi tunaweza tukaweka mapingamizi.

Kama kuna mtu anafikiria sisi tutakuwa wajibu mashtaka tu, wafikirie mara mbili. Mwisho nawaombeni, kesho ni siku muhimu kuliko leo. Kwa sisi tusiokuwa na serikali, mapolisi, tusiokuwa na watu wa kutulinda, tunahitaji nguvu ya umma, tunahitaji wingi wenu.

Nawaombeni sana mhamasishane mji huu na miji ya jirani na yeyote anayeweza kuwa Dodoma awe Dodoma ili kesho tuwe wengi zaidi tuone mpaka kufikia saa kumi jioni itakuwaje.
 
1598380724781.jpeg
 
Urais, Fomu kuhakikiwa na Kutangazwa Kuteuliwa , kisha kusubiria kama kuna pingamizi

Baada ya fomu kuhakikiwa na kutangazwa kuteuliwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi kuwa kila kitu kipo sawa kuna zoezi muhimu la kubandika majina ili umma kuwafahamu.

Muda wa pingamizi ni kuanzi saa 10:00 jioni ya tarehe 25 Agosti 2020 hadi saa 10:00 jioni siku inayofuata yaani tarehe 26 Agosti 2020.

Zoezi hilo muhimu ni hatua inayofuata ni kusikia kama wagombea wamewekewa pingamizi na wale wadau wanaotambulika na Tume ya Uchaguzi, kisha wagombea wateuliwa kupata nafasi ya kujibu.

Wenye haki ya kuweka pingamizi ngazi ya Urais na Makamu ni hawa wadau watatu yaani Mkurugenzi wa Uchaguzi, Msajili wa Vyama Vya Siasa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Pingamizi ngazi ya Urais linatakiwa kuletwa kwa maandishi katika fomu namba 9A na pingamizi hilo liwakilishwe ndani ya muda muafaka unaoanzia muda uliotajwa hapo juu na sababu za pingamizi litajwe.

Hivyo waliotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi ngazi ya Urais kama wateule baada ya kuhakiki fomu na nyaraka wote wanaweza kuwekewa pingamizi muda wowote kuanzia muda wa saa 10:00 jioni ya leo tarehe 25 Agosti 2020 na mwisho wa kuwakilisha pingamizi ni kesho saa 10:00 jioni tarehe 26 Agosti 2020.
 
Ni viziri ila akiwekewa yeye asianze kulialia kama mtoto wa mama wa kambo.
Lissu hakatai mapingamizi, ndio maana alirudi nchini licha yakua anajua mangapi yanayomsubiri.

Anachohitaji nihayo mapingamizi yafuate Sheria pasipo kumuonea wala kumpendelea.

Unazungumziaje, wabunge wenu kupitishwa bila kupingwa et zaidi wagombea wa vyama 15 wote hao wamekosea kujaza fomu, kwamba CCM ndio wamepatia? Huuu uhuni unauzungumziaje?
 
Back
Top Bottom