Leo nilienda safari ya kumtembelea rafiki yangu ambaye yeye na mke wake wote hawana smart phone. Nilipofika nikamkuta mke wake na wageni akanieleza aliyoona jana wakati anaenda Kibaha. Anasema alipofika Gogoni akaona kuna magari ya polisi. Kwenye daladala wakaanza kujadili hilo.
Kwa sababu mimi nafutilia mitandaoni nikamwacha amalize stiry nzima nione picha ya kwenye mabasi inasemaje.
Huyo dada anasema watu walianza kulaani polisi na CCM. Anasema iweje polis wanashindwa kulinda mali zetu kwingine wanakuja kuzuia msafara wa Tundu Lissu.
Kisha nikamuuliza je kuna yeyote aniyeonekana kuitetea CCM kwenye gari hilo, akasema angetokea wangeweza hata kumpiga. Yaani hapakuwa ni mahala pa kuitetea CCM.
Kisha nikamuuliza nione kama watu walijua sababu ya msululu wa polisi akasema watu walijua Tundu Lissu anaenda kufanya kampeni hivyo polisi wamemzuia.
Baada ya hayo mimi nikaeleza ukweli wa kilichomzuia. Nikamweleza kwamba Tundu Lissu hakuwa anaenda kwenye kampeni bali alikuwa anaenda kwa wanachama wake Kibaha.
Nikamweleza tena huo msafara wa polisi uliondoka saa 12:20 jioni hivyo Tundu Lissu akaendelea na ratiba iliyocheleweshwa.
Baadaye mume wake akaja nikampa hiyo story na yeye akaongezea story nyingine ya basi alilokuwamo walikuwa wanaongelea leo kitendo cha Tundu Lissu kupanda mwendokasi. Basi zima liliongea hilo mwanzo hadi mwisho.
Anasema mama mmoja akaongea kwamba huu utakuwa uchaguzi wa kwanza nchini ambapo watu wanaenda kwenye uchaguzi huku kila mmoja akiwa na njaa.
Baadaye nikamwonyesha kwenye simu yangu jinsi Tundu Lissu alivyoshangiliwa Kariakoo na kwmaba huenda angeenda soko la Ndizi pale Mabibo na kwends Stendi ya Ubungo, kumkatia ndugu yake tiketi ya usafiri.
Nikamwonyesha na jinsi Tundu Lissu alivyoonana na balozi wa Marekani leo.
Sasa nataka kusema nini.
Kazi yangu ilikuwa kusikiliza na nilichotathmini ni hiki. Katika mabasi yote mawili aliponada yule dada na jingine alilopada mume wake kote wanaongelea Tundu Lissu. Ukiongelea CCM unaweza kutukanwa safari nzima. Hiyo ndiyo hali halisi.
Kingine ni kwamba kitendo cha Tume kumfungia Tundu Lissu kampeni walidhani itatafsiriwa kwamba ni mkorofi kumbe mahesabu yamekataa. Kumbe sympathy kwa Tundu Lissu ndiyo imeongezeka wakati huu maana kila mtu haachi kumuongelea.
Mimi ningetamani hata wamfungie kipindi chote hadi uchaguzi utakapoisha.
Ninachowashauri CHADEMA sijui kama watanielewa ni kwamba Tundu Lissu ikiwezekana hata kampeni asifanye kabisa hizi wiki tatu zilizobaki.
Hizi wiki tatu hakuna atakaloongeza au kupunguza maana kila kona ameshasikika.
Tundu Lissu alipopigwa risasi dunia nzima ikamjua. Picha yake ikionekana kwenye karatasi ya kupiga kura haihitaji umjue na hahitaji kampeni.
Tundu Lissu afanye alichofanya jana Kibaha ambacho binafsi kimenifurahisha. Jana katoa lecture nzuri ya namna ya kuzuia kuiba kura na kulinda kura.
Kaelimisha kwamba safari hii wanatakiwa wawe na matokeo yote ya vituo vyote nchi nzima. Mawakala waapishwe nchi nzima.
Haya mambo ni magumu kwa mwananchi wa kawaida lakini yanaeleweka kwa mawakala. Kampeni sasa iwe wakala afanye nini ajihadhari na nini.
Labda ni kwamba watu waende siku moja kabla kuhakikisha majina yao yako chumba gani maana wengine hufika siku ileile. Tumeshasikia kwamba kuna jeshi litapora kura kuanzia saa 08:00 au saa 10 jioni wakatu wana CCM watakuwa wameshapiga kura.
Sasa wakazanie elimu na kujiandaa kuzuia wizi wa kura. Wawe na software za kujumlisha matokeo ya kila kituo. Kila mu atengeneze Microsoft Excel Sheet ya jimbo walau moja ili kufikia saa 4 usiku mshindi wa kila kitu ameshajulikana.
Kwa sababu mimi nafutilia mitandaoni nikamwacha amalize stiry nzima nione picha ya kwenye mabasi inasemaje.
Huyo dada anasema watu walianza kulaani polisi na CCM. Anasema iweje polis wanashindwa kulinda mali zetu kwingine wanakuja kuzuia msafara wa Tundu Lissu.
Kisha nikamuuliza je kuna yeyote aniyeonekana kuitetea CCM kwenye gari hilo, akasema angetokea wangeweza hata kumpiga. Yaani hapakuwa ni mahala pa kuitetea CCM.
Kisha nikamuuliza nione kama watu walijua sababu ya msululu wa polisi akasema watu walijua Tundu Lissu anaenda kufanya kampeni hivyo polisi wamemzuia.
Baada ya hayo mimi nikaeleza ukweli wa kilichomzuia. Nikamweleza kwamba Tundu Lissu hakuwa anaenda kwenye kampeni bali alikuwa anaenda kwa wanachama wake Kibaha.
Nikamweleza tena huo msafara wa polisi uliondoka saa 12:20 jioni hivyo Tundu Lissu akaendelea na ratiba iliyocheleweshwa.
Baadaye mume wake akaja nikampa hiyo story na yeye akaongezea story nyingine ya basi alilokuwamo walikuwa wanaongelea leo kitendo cha Tundu Lissu kupanda mwendokasi. Basi zima liliongea hilo mwanzo hadi mwisho.
Anasema mama mmoja akaongea kwamba huu utakuwa uchaguzi wa kwanza nchini ambapo watu wanaenda kwenye uchaguzi huku kila mmoja akiwa na njaa.
Baadaye nikamwonyesha kwenye simu yangu jinsi Tundu Lissu alivyoshangiliwa Kariakoo na kwmaba huenda angeenda soko la Ndizi pale Mabibo na kwends Stendi ya Ubungo, kumkatia ndugu yake tiketi ya usafiri.
Nikamwonyesha na jinsi Tundu Lissu alivyoonana na balozi wa Marekani leo.
Sasa nataka kusema nini.
Kazi yangu ilikuwa kusikiliza na nilichotathmini ni hiki. Katika mabasi yote mawili aliponada yule dada na jingine alilopada mume wake kote wanaongelea Tundu Lissu. Ukiongelea CCM unaweza kutukanwa safari nzima. Hiyo ndiyo hali halisi.
Kingine ni kwamba kitendo cha Tume kumfungia Tundu Lissu kampeni walidhani itatafsiriwa kwamba ni mkorofi kumbe mahesabu yamekataa. Kumbe sympathy kwa Tundu Lissu ndiyo imeongezeka wakati huu maana kila mtu haachi kumuongelea.
Mimi ningetamani hata wamfungie kipindi chote hadi uchaguzi utakapoisha.
Ninachowashauri CHADEMA sijui kama watanielewa ni kwamba Tundu Lissu ikiwezekana hata kampeni asifanye kabisa hizi wiki tatu zilizobaki.
Hizi wiki tatu hakuna atakaloongeza au kupunguza maana kila kona ameshasikika.
Tundu Lissu alipopigwa risasi dunia nzima ikamjua. Picha yake ikionekana kwenye karatasi ya kupiga kura haihitaji umjue na hahitaji kampeni.
Tundu Lissu afanye alichofanya jana Kibaha ambacho binafsi kimenifurahisha. Jana katoa lecture nzuri ya namna ya kuzuia kuiba kura na kulinda kura.
Kaelimisha kwamba safari hii wanatakiwa wawe na matokeo yote ya vituo vyote nchi nzima. Mawakala waapishwe nchi nzima.
Haya mambo ni magumu kwa mwananchi wa kawaida lakini yanaeleweka kwa mawakala. Kampeni sasa iwe wakala afanye nini ajihadhari na nini.
Labda ni kwamba watu waende siku moja kabla kuhakikisha majina yao yako chumba gani maana wengine hufika siku ileile. Tumeshasikia kwamba kuna jeshi litapora kura kuanzia saa 08:00 au saa 10 jioni wakatu wana CCM watakuwa wameshapiga kura.
Sasa wakazanie elimu na kujiandaa kuzuia wizi wa kura. Wawe na software za kujumlisha matokeo ya kila kituo. Kila mu atengeneze Microsoft Excel Sheet ya jimbo walau moja ili kufikia saa 4 usiku mshindi wa kila kitu ameshajulikana.