Mfano ni mzuri kabisa.
Tatizo lako unatumia hisia zaidi kuliko akili katika kumjadili huyo "mpendwa" wako Lissu.
Al-Watan keshasema ni heri mumuite Tundu Yesu kabisa.
Mfano wa jinsi Lissu atakavyokuwa mgumu kudhibitiwa na serikali kutokana na makosa ya hiyo serikali una ubaya gani hasa?
Mimi sijazungumzia ubaya wa Lissu. Sijasema matendo ya Lissu ni sawa na matendo ya Frankenstein. Kwanza Frankestein monster ni kiumbe wa kufikirika tu.
Kama ningemfananisha na Hitler hapo sawa.
Lakini katika muktadha wa hoja, kwamba CCM na serikali yake ndo wanahusika moja kwa moja katika kumpandisha chati Lissu na sasa hawatoweza tena kumdhibiti kama vile ambavyo yule mad scientist alivyotengeneza lile li monster aliloshindwa kulidhibiti...sioni kabisa kosa hapo.
Nipo sahihi kabisa.