Tundu 'Frankenstein' Lissu

Tundu 'Frankenstein' Lissu

Yake yakianza kubwagwa ataufyata tu.. nafikiri kwake kuna ile kuachiwa na kuangaliwa huku hajui wajuayo.. na hawezi kupata cheo anachotaka hadi wenzake wakubali(ndio maana wanatendeana majanga yanayoendelea kusisukumia kama vile ni serikali). naona ataendelea kupiga mdomo tuuuuu na kuishia alipo.. akitokea kupewa cheo makombora yatarushwa pwaaaaaa..
acha uwongo wewe huoni aibu?
 
Lissu akirudi bongo atakuwa kapoa. Msitegemee yule lissu mpambanaji mliyemzoea...

Kwanza, kiakili hataweza kuwa sawa...

Pili, woga umeshamwingia. Mara nyingi alikuwa anasuguana na "wasiojulikana", ila kwa sasa hataweza tena kutumia lugha hii " niko radhi kufa, kutetea wananchi " ...

Tatu, wengi tulitegemea taharuki baada ya kupokea taarifa kuhusu kupigwa risasi. Lakini mambo yalikuwa kinyume. Raia waoga wanaendelea na kazi kama kawaida. Labda watu wa mitandao na magazeti " keyboard warriors"....

Kwa wale wanaofikiri kuwa atarudi kwenye hali yake ya awali waendelee na ndoto hiyo...
 
Yataka moyo sana ili kuweza kutamka maneno kama haya ww umevurugwa
Kwanza kabisa huyo jamaa siyo wa kurudi leo wala kesho na hata akirudi kila kitu kwisha habari yake, kuna kiwango cha risaisi ambazo mwili wa Binadamu unaweza kuhimili, kupigwa risasi zote hizo siyo mchezo, huyo kwanza hata akifanya press conf. mtu akibamiza mlango tu kwa bahati mbaya atazimia atafikiri ni hitman wamemjia tena, kama ulishawahi kupigwa risasi au hata kukoswa tu unaweza kuelewa ninachomaanisha, hivyo ukiniuliza mimi huyo Tundu Lisu ndiyo basi tena its over, kwani sidhani hata kama ataweza kutembea tena, achilia bali hata tu kuinuka, atabakia jina tu kwa wafuasi wake kama vile Marando &Co., kwa kifupi they fvcked the guy up forever whoever that shut him!
 
Nikisoma hizi comment humu ndani nashangaaaa sanaaaaaa.........hivi kwa nini watu wachumia tumbo wana DOUBLE FACE............!!!!!?????
 
Zile kamata kamata zisizo na kichwa wala miguu dhidi ya Tundu Lissu na zile kesi uchwara zote zilizofunguliwa dhidi yake naamini ndizo zilizompandisha chati huyo bwana katika huu utawala wa awamu ya tano.
...
Uzushi na propaganda kwenye siasa ni jambo la kawaida sana na la kutegemewa kuwepo. Mwanasiasa asiyezusha, asiyetia chumvi, na asiyepiga propaganda atakuwa kakosea fani.
...
Hakika hii serikali ya awamu ya tano ilibugi stepu katika namna ya kumkabili Lissu na sasa amekuwa lidubwana ambaye anaweza asidhibitike tena.

Ni muda tu ndo utaotueleza.....
Nawe Nyani Ngabu, umebugi kwa kujichanganya. Unasema siasa ni propaganda. Kwa hilo nami nakubaliana na wewe, lakini kilichofuatia, na ufafanuzi wako, kinakinzana na unachotaka tuelewe (rejea maandishi mazito katika bandiko lako).

Maudhui na jinsi ya kuendesha propaganda ndiko hutofautiana kati ya mtu na mtu, au kikundi kwa kikundi. Utofauti huo unatokana na lengo la hiyo propaganda.

Nikirejea mada yako, Mh Lissu na Serikali, kisiasa wote wamekuwa wakiendesha propaganda. Kwa kuwa serikali ina madaraka, imekuwa ikitumia, silaha yake hiyo, kuhakikisha propaganda yake inafanikiwa.

Labda tu tujadili ni aina gani ya propaganda hizo na usahihi wa jinsi zinavyoendeshwa. Je, matokeo yake ni hasi au chanya kwa wahusika?
 
..hili shambulizi la TL lilivyopangwa halikuwa na option ya kufeli.

..kwa hivyo waliopanga kumuua TL did not account on the possibility of him surviving.

..kwa kifupi shambulio hili litamfanya TL aaminike zaidi ktk kila analolisema.

..watu watajiuliza swali dogo tu: kama TL ni muongo kwanini walitaka kumuua?

..Hata kabla ya shambulizi hili, wiki chache kabla ya hapo, u could see kwamba TL alianza kuizidi serikali na CCM katika hoja na mambo aliyokuwa akiyasemea. Labda hali hiyo ya kuelekea kushindwa kujibu kila hoja ya TL ndiyo iliyolazimisha au kuharakisha shambulizi hili.

..Sasa ujengaji hoja wa TL, ujasiri wake, na huruma atakayokuwa akiipata toka kwa wananchi, ni challenge ambayo nadhani CCM hawajawahi kukutana nayo.

NB:

..Huko kwenu Marekani nadhani TL ungeweza kumfananisha na rapper mwenye kipaji kikubwa lakini akakosa street cred. Sasa baada ya kupigwa marisasi ghafla amepata street cred na kuanzia hapo most likely he will be unstoppable.
 
Nawe Nyani Ngabu, umebugi kwa kujichanganya. Unasema siasa ni propaganda. Kwa hilo nami nakubaliana na wewe, lakini kilichofuatia, na ufafanuzi wako, kinakinzana na unachotaka tuelewe (rejea maandishi mazito katika bandiko lako).

Maudhui na jinsi ya kuendesha propaganda ndiko hutofautiana kati ya mtu na mtu, au kikundi kwa kikundi. Utofauti huo unatokana na lengo la hiyo propaganda.

Nikirejea mada yako, Mh Lissu na Serikali, kisiasa wote wamekuwa wakiendesha propaganda. Kwa kuwa serikali ina madaraka, imekuwa ikitumia, silaha yake hiyo, kuhakikisha propaganda yake inafanikiwa.

Labda tu tujadili ni aina gani ya propaganda hizo na usahihi wa jinsi zinavyoendeshwa. Je, matokeo yake ni hasi au chanya kwa wahusika?
Hahaaa

Hueleweki.

Unasema nimejichanganya halafu unasema unakubaliana na mimi.

Wewe ndo umechanganyikiwa.
 
Lissu akirudi bongo atakuwa kapoa. Msitegemee yule lissu mpambanaji mliyemzoea...

Kwanza, kiakili hataweza kuwa sawa...

Pili, woga umeshamwingia. Mara nyingi alikuwa anasuguana na "wasiojulikana", ila kwa sasa hataweza tena kutumia lugha hii " niko radhi kufa, kutetea wananchi " ...

Tatu, wengi tulitegemea taharuki baada ya kupokea taarifa kuhusu kupigwa risasi. Lakini mambo yalikuwa kinyume. Raia waoga wanaendelea na kazi kama kawaida. Labda watu wa mitandao na magazeti " keyboard warriors"....

Kwa wale wanaofikiri kuwa atarudi kwenye hali yake ya awali waendelee na ndoto hiyo...

Namba 3 inaingia akilini,,RAIA waoga mno
 
Kwanza kabisa huyo jamaa siyo wa kurudi leo wala kesho na hata akirudi kila kitu kwisha habari yake, kuna kiwango cha risaisi ambazo mwili wa Binadamu unaweza kuhimili, kupigwa risasi zote hizo siyo mchezo, huyo kwanza hata akifanya press conf. mtu akibamiza mlango tu kwa bahati mbaya atazimia atafikiri ni hitman wamemjia tena, kama ulishawahi kupigwa risasi au hata kukoswa tu unaweza kuelewa ninachomaanisha, hivyo ukiniuliza mimi huyo Tundu Lisu ndiyo basi tena its over, kwani sidhani hata kama ataweza kutembea tena, achilia bali hata tu kuinuka, atabakia jina tu kwa wafuasi wake kama vile Marando &Co., kwa kifupi they fvcked the guy up forever man, whoever shut him!
Ni uzushi na uzandiki, ndicho mlichotaka hakikuwa na hakitakuwa kama usemavyo.
 
Kwanza kabisa huyo jamaa siyo wa kurudi leo wala kesho na hata akirudi kila kitu kwisha habari yake, kuna kiwango cha risaisi ambazo mwili wa Binadamu unaweza kuhimili, kupigwa risasi zote hizo siyo mchezo, huyo kwanza hata akifanya press conf. mtu akibamiza mlango tu kwa bahati mbaya atazimia atafikiri ni hitman wamemjia tena, kama ulishawahi kupigwa risasi au hata kukoswa tu unaweza kuelewa ninachomaanisha, hivyo ukiniuliza mimi huyo Tundu Lisu ndiyo basi tena its over, kwani sidhani hata kama ataweza kutembea tena, achilia bali hata tu kuinuka, atabakia jina tu kwa wafuasi wake kama vile Marando &Co., kwa kifupi they fvcked the guy up forever man, whoever shut him!
Obviously huna mifano ya walioumizwa na kurudia harakati zao kama kawaida
John McCain and Fifty Cents are case study
 
Zile kamata kamata zisizo na kichwa wala miguu dhidi ya Tundu Lissu na zile kesi uchwara zote zilizofunguliwa dhidi yake naamini ndizo zilizompandisha chati huyo bwana katika huu utawala wa awamu ya tano.

Mara nyingi kama si zote hizo kamata kamata zilitokea baada ya yeye kutoa maneno makali dhidi ya serikali na rais.

Kuna nyakati alikuwa yupo sahihi na nyakati zingine alikuwa mzushi tu. Kwa mfano, aliposema nchi inaendeshwa kwa misingi ya kikabila na kikanda, huo ulikuwa ni uzushi tu. Zilikuwa ni propaganda tu.

Uzushi na propaganda kwenye siasa ni jambo la kawaida sana na la kutegemewa kuwepo. Mwanasiasa asiyezusha, asiyetia chumvi, na asiyepiga propaganda atakuwa kakosea fani.

Sasa mimi naamini hii serikali inafanya makosa sana katika kuwakamata na kuwafungulia mashitaka watu wanaoipinga na kuikosoa. Hizo kesi wanazofunguliwa ni vichekesho mtupu.

Katika kukosea kwao huko, naamini serikali imeunda lidubwana [monster] ambalo kuanzia sasa kwenda mbele itakuwa vigumu kulidhibiti. Lidubwana hili nalifananisha na lile lidubwana la kwenye filamu ya Frankestein.

Lidubwana hilo ndo Tundu Lissu. Hebu fikiria haya:

Jamaa keshaonyesha kuwa haogopi kuikosoa serikali wala kumsema vibaya rais [mambo ambayo ni ya kawaida sana kwenye demokrasia na ambayo yanahimizwa kufanyika].

Uthubutu na ujasiri wake huo ndo umepelekea yeye kukamatwa kamatwa na kufunguliwa vi kesi uchwara.

Uthubutu na ujasiri huo huo ndo si ajabu umepelekea yeye kushambuliwa kwa risasi kwa lengo la kutaka kumuua. Sijui kwa uhakika ni nani anayehusika na hilo shambulio.

Sasa pata picha atapopona na kurejea tena nchini na kuendelea na hatakati zake pale alipoishia!

Serikali itamfanya nini huyu mtu? Wataendelea kumsumbua na hizo kamata kamata zao na kumfungulia hivyo vi kesi uchwara mtu ambaye tayari ana huruma za umma kwa ujumla wake kutokana na yale yaliyomtokea?

Sioni utamkamataje na kumfunga mtu ambaye kanusurika kuuwawa namna ile. Akili yangu inaniambia hata dhamiri yako, kama ni safi, basi itakusuta tu.

Hakika hii serikali ya awamu ya tano ilibugi stepu katika namna ya kumkabili Lissu na sasa amekuwa lidubwana ambaye anaweza asidhibitike tena.

Ni muda tu ndo utaotueleza.....

Ni kama vile unasema wakammalizie ili asipone na kurejea kuendelea na harakati zake pale alipoishia. Kwamba unajiuliza serikali itamfanya nini tena mtu ambaye keshanusurika kifo, hinting ni serikali ilimkosakosa? Strange. Na unasema Lissu alishambuliwa kwa kuwa strategy ya vi kesi uchwara ilishindwa kumdhibiti? Na kwanini una-assume kwamba ni halali kwa serikali "kumkabili" na "kumdhibiti" Lissu? You sound like a Chief Strategist katika Ikulu ya Magufuli.
 
Katika kukosea kwao huko, naamini serikali imeunda lidubwana [monster] ambalo kuanzia sasa kwenda mbele itakuwa vigumu kulidhibiti. Lidubwana hili nalifananisha na lile lidubwana la kwenye filamu ya Frankestein.

Lidubwana hilo ndo Tundu Lissu. Hebu fikiria haya:

hata mimi niko ccm lakini namuunga mkono
Kwa hiyo unaunga mkono kwamba Mh. Tundu Antiphas Lissu ndiye lidubwasha (the evil moster) kwenye filamu ya Frankenstein ambaye kwa uovu wake baada ya kufinyangwa kazi yake ilikuwa ni kuuwa tu. Mleta mada ni wazi kachanganyikiwa lakini kwa wewe kuunga mkono jitihada za mleta mada kumfananisha Mh.Tundu Lissu na huyo ibilisi aliyeua watu kumeniacha hoi.
  • Ni lini Mh. Tundu Lissu amekuwa na kiu ya damu?
  • Ni lini Mh. Tundu Lissu ameishi kwa kujificha gizani?
  • Ni lini Mh. Tundu Lissu amekuwa moja katika wasioonekana?
Chuki za [B]Nyani Ngabu[/B] kwa Mh. Tundu Lissu zinaeleweka kwani zinachochewa na Genealogy ambayo haijamuacha salama, imemganda kama shati lililoloa. Ni chuki hizo hizo kutoka kwa watu wale wale zilizopelekea risasi zaidi ya 30 kushindiliwa mwilini mwa Mh.Tundu Lissu kwa lengo la kumuua. Lakini Mwenyezi Mungu katengua hukumu iliyotolewa na hao mashetani na kwa sasa hali yake inaimarika.

Hii hali imeleta sintofahamu kubwa kwa watu kama [B]Nyani Ngabu[/B]...toka tukio limetokea hatulii na idadi ya mada alizoanzisha humu JF ni ushahidi wa utetezi wake dhaifu. Kama panya anauma na kupuliza kuondoa wingu lililotanga kugubika hisia za uhusika wa jamaa zake. Kiwewe kizito kimewakumba waliopanga, kuratibu na kutekeleza jaribio la kigaidi la kumuua Mh. Tundu Lissu...tuzidi kumuombea Mh. Lissu.
 
Hahaaa

Hueleweki.

Unasema nimejichanganya halafu unasema unakubaliana na mimi.

Wewe ndo umechanganyikiwa.
Nakubaliana nawe kuwa siasa ni propaganda, ila sikubaliani na hitimisho lako linalolenga kwamba ni Mh Lissu tu ndiye amekuwa akiendesha propaganda.

Kwa hitimisho lako Lissu ataibuka shujaa (dubwana umeandika), kwa mfano wa Frankestein! maana yake, kwako, ni kwamba kamata kamata na kufunguliwa kwake Lissu mashtaka na Serikali siyo propaganda, au!

Kwangu hata viongozi Serikalini wanaendesha propoganda za kudhoofisha upinzani, na ikibidi ufilie mbali. Lakini, bahati mbaya viongozi wa upinzani hawalioni hilo, na kama wanaliona wanalipuuzia. Kama hawipuuzii, mikakati yao ya kuzima huo mto uliowashwa na serikali, kufisha upinzani, waikarabati.

Kwa mfano, mkakati wa kunung'unika na kulalama kwenye vyombo vya habari making noises, ili dunia isikie, haujaleta matokeo wanayoyakusudia.
 
Kwanza kabisa huyo jamaa siyo wa kurudi leo wala kesho na hata akirudi kila kitu kwisha habari yake, kuna kiwango cha risaisi ambazo mwili wa Binadamu unaweza kuhimili, kupigwa risasi zote hizo siyo mchezo, huyo kwanza hata akifanya press conf. mtu akibamiza mlango tu kwa bahati mbaya atazimia atafikiri ni hitman wamemjia tena, kama ulishawahi kupigwa risasi au hata kukoswa tu unaweza kuelewa ninachomaanisha, hivyo ukiniuliza mimi huyo Tundu Lisu ndiyo basi tena its over, kwani sidhani hata kama ataweza kutembea tena, achilia bali hata tu kuinuka, atabakia jina tu kwa wafuasi wake kama vile Marando &Co., kwa kifupi they fvcked the guy up forever man, whoever shut him!

..Maelezo ya Alute Mughwai na Mh.Mbowe yanatoa picha tofauti na hii iliyoiweka hapa.

..huko aliko inaelekea yuko imara kiakili na kisaikolojia.

..wako ambao huwa na waoga baada ya kupata mikasa kama ya TL. na wapo ambao hupata ujasiri zaidi.

..kuna dalili kwamba TL atakuwa jasiri zaidi baada ya shambulizi hili.
 
Kwanza kabisa huyo jamaa siyo wa kurudi leo wala kesho na hata akirudi kila kitu kwisha habari yake, kuna kiwango cha risaisi ambazo mwili wa Binadamu unaweza kuhimili, kupigwa risasi zote hizo siyo mchezo, huyo kwanza hata akifanya press conf. mtu akibamiza mlango tu kwa bahati mbaya atazimia atafikiri ni hitman wamemjia tena, kama ulishawahi kupigwa risasi au hata kukoswa tu unaweza kuelewa ninachomaanisha, hivyo ukiniuliza mimi huyo Tundu Lisu ndiyo basi tena its over, kwani sidhani hata kama ataweza kutembea tena, achilia bali hata tu kuinuka, atabakia jina tu kwa wafuasi wake kama vile Marando &Co., kwa kifupi they fvcked the guy up forever man, whoever shut him!
Ulijua umemmaliza kweli wewe bwege na atakapo kuja utaona mziki wake labda ukatege bomu tena shame on you huoni ata aibu unaandika upuizi ningekutukana nikuvue boxer unabahati kuna ban
 
Back
Top Bottom