Kwa hiyo unaunga mkono kwamba Mh. Tundu Antiphas Lissu ndiye lidubwasha (the evil moster) kwenye filamu ya Frankenstein ambaye kwa uovu wake baada ya kufinyangwa kazi yake ilikuwa ni kuuwa tu. Mleta mada ni wazi kachanganyikiwa lakini kwa wewe kuunga mkono jitihada za mleta mada kumfananisha Mh.Tundu Lissu na huyo ibilisi aliyeua watu kumeniacha hoi.
Chuki za Nyani Ngabu kwa Mh. Tundu Lissu zinaeleweka kwani zinachochewa na Genealogy ambayo haijamuacha salama, imemganda kama shati lililoloa. Ni chuki hizo hizo kutoka kwa watu wale wale zilizopelekea risasi zaidi ya 30 kushindiliwa mwilini mwa Mh.Tundu Lissu kwa lengo la kumuua. Lakin Mwenyezi Mungu katengua hukumu iliyotolewa na hao mashetani na kwa sasa hali yake inaimarika.
- Ni lini Mh. Tundu Lissu amekuwa na kiu ya damu?
- Ni lini Mh. Tundu Lissu ameishi kwa kujificha gizani?
- Ni lini Mh. Tundu Lissu amekuwa moja katika wasioonekana?
Hii hali imeleta sintofahamu kubwa kwa watu kama Nyani Ngabu...toka tukio limetokea hatulii na idadi ya mada alizoanzisha humu JF ni ushahidi wa utetezi wake dhaifu. Kama panya anauma na kupuliza kuondoa wingu lililotanga kugubika hisia za uhusika wa jamaa zake. Kiwewe kizito kimewakumba waliopanga, kuratibu na kutekeleza jaribio la kigaidi la kumuua Mh. Tundu Lissu...tuzidi kumuombea Mh. Lissu.
..nakuunga mkono 100%.
..binafsi sikupenda alivyotumia jina "Frankeinstein" ktk sentensi moja na jina la Tundu Lissu.
..lakini wakati mwingine inabidi uvumilie tu ktk kuchanganyika na hawa vijana wa Lumumba.
usiwambie hivyo bana). Akirudi tunampokea uwanja wa ndege anarukaruka kama ndama,Bashite macho chini.