Tundu 'Frankenstein' Lissu

Tundu 'Frankenstein' Lissu

Unakumbuka chopa 5 kata 3?

Unaweza kuniambia nini kilitokea mpaka usemi huo ukatokea?

Hivi kwanini tunajidanganya hata nafsi zetu?

Lisu hapati zaidi ya 20% ya kura.

Achilia mbali wabunge ambao mkifikisha 15 mshukuru Mungu

Kwani wakati huo wa chips tatu kata tatu tume ilikuwa huru? Kwanza unakumbuka ratio ya kura za wakati ule? Na unajua kipi kilitokea uchaguzi wa 2015? Inaonekana hujui siasa ndio maana unaangalia aliyetangazwa mshindi tu, bila kupima ushindi ulikuwa wa marafiki kiasi gani.

Ngoja nikupe mfano mrahisi wa mpira. Kabla ya Liverpool kuchukua ubingwa msimu huu, msimu uliopita walishindwa na Manchester City kwa point moja. Ila walianza msimu huu kwa nguvu ile ile hadi kuwa bingwa, huku wakiwaacha Mancity kwa zaidi ya point15+. Lazima ujue kusoma alama za nyakati, hiyo mifano yako ya zamani haina nafasi kwa sasa maana mazingira sio static na kuna mambo mengi sana yamebadilika. Kama wapinzani wamefanyiwa hujuma zote ndani ya hii miaka mitano na bado kwa sasa wana hamasa, utakuwa mwendawazimu kujisifia huku mifumo yote ya uchaguzi ikikubeba bila sababu za msingi.

Kutokana na hujuma dhidi ya cdm ndani ya hii miaka mitano, na kile alichofanya Magufuli, na propaganda zote chafu dhidi ya Lisu achia mbali shambulio lake, ilitakiwa apate watu wa idadi ya mikutano ya Hashimu Rungwe, sio hicho kinachoendelea. Kama uchaguzi utafanyika kwa utashi wa Magufuli, Lisu hata hizo 20% hafikishi, na wabunge au madiwani hata kufikia watano itakuwa maajabu. Ila sio kwa uchaguzi kwa maana ya kura halali.
 
Bila shaka muda huu upo kwa shemeji yako ukiwa umejificha uvunguni kwa aibu....amakweli kinywa cha mpumbavu hakina stara kwenye kunena maneno.
Kwanza kabisa huyo jamaa siyo wa kurudi leo wala kesho na hata akirudi kila kitu kwisha habari yake, kuna kiwango cha risaisi ambazo mwili wa Binadamu unaweza kuhimili, kupigwa risasi zote hizo siyo mchezo, huyo kwanza hata akifanya press conf. mtu akibamiza mlango tu kwa bahati mbaya atazimia atafikiri ni hitman wamemjia tena,

Kama ulishawahi kupigwa risasi au hata kukoswa tu unaweza kuelewa ninachomaanisha, hivyo ukiniuliza mimi huyo Tundu Lisu ndiyo basi tena its over, kwani sidhani hata kama ataweza kutembea tena, achilia bali hata tu kuinuka, atabakia jina tu kwa wafuasi wake kama vile Marando &Co., kwa kifupi they fvcked the guy up forever man, whoever shut him!
 
Mkuu oktoba siyo mbali!

Najua ni ngumu sana kwa mfuasi wa chadema kukubali kwamba tutashindwa! Hicho kichaka cha tume huru kipo miaka yote ndio mnajifichaga hapo!

Basi tufanye Lisu ni zaidi ya tume huru na atashinda urais huu wa oktoba kisha kuwa rais wa jamhuri ya muungano wa tz, akiwa na robo tatu ya wabunge wa bunge la jamhuri.

Usiku mwema mkuu.
CCM imechokwa nchi nzima tunajua mtaiaba hadharani ila siku zenu zinahesabika
 
Mkuu tindo, kwanza nikupongeze kwa kuwa mfuasi kindakindaki wa CHADEMA na hasa Lissu. Hongera za dhati.

Je, unamshauri ajiandaeje, kampeni zikianza, kuhusu mambo kadhaa ikiwemo:
√ Sera na Mikakati mbadala ya maendeleo badala ya kung'ang'ania shutuma dhidi ya Serikali na viongozi wake, hasa Rais Magufuli na viongozi wa dini;
√ Kujibu tuhuma za ufisadi ndani ya chama chake dhidi ya M/Kiti wake, kama zilivyotolewa na zitaanikwa upya, wakati wa kampeni, na wanasiasa waliokihama chama;
√ Ushindani dhidi ya wagombea Urais wa vyama vingine vya upinzani ambao wanatofautiana kwa mbali na jinsi anavyojinasibu kwa wapiga kura, kuelekea kampeni za Uchaguzi Mkuu;
√ Ukimya wa Jeshi la Polisi kuhusu shambulio lilolenga kuondoa uhai wake; na
√ Kesi zake ambazo wadhamini walijiondoa, hivyo kisheria dhamana imefutwa. Isitoshe mara mwisho hakuhudhuria mahakamani kwa kisingizio za kiafya, lakini ameonekana akishiriki shughuli za kisiasa tofauti na hayo madai.

FUMBO MFUMBIE MJINGA ...

Kwanza kwa sasa kampeni bado, ila anasaka wadhamini, na Katazo haramu la kuzuia mikutano halali, aliye juu ya sheria kashaliondoa. Ngoja nijibu kwa mtiririko wako.
  1. Sera na mikakati ipo toka 2010, kinachofanyika sasa hivi ni kuiboresha tu. Tanzania ya 2010 na ya sasa mabadiliko ni madogo sana. Hivyo sera na ilani ya sasa itakuwa ni better version ya ilani na sera za 2010+2015. Na kwa taarifa yako wapiga kura wengi hawajali sera wala ilani, bali huchagua kwa hamasa na presentation ya mgombea. Labda kwakuwa rais anaamuliwa na kamati za ccm, hapo ndio Lisu hapiti.
  2. Hapo kwenye tuhuma mbona parahisi sana, itabidi na mgombea wa ccm ajibu tuhuma za 1.5t against 8b za cdm. Ndio maana tunataka mdahalo wa wagombea urais.
  3. Huo ushindani dhidi ya wagombea wengine wala haumtishi, na kimsingi hapo mshindani wake ni Magufuli ambaye hawezi siasa za hoja, zaidi ya mabavu na vitisho.
  4. Huo ukimya wa jeshi la polisi dhidi yake ana kipi cha kujibu? Kwani yeye ndio afisa upelelezi? Hapa inaonyesha hujui unasema nini.
  5. Hana hofu na kesi yoyote ya kubambikiwa na mtawala, hayo ni mambo ya kawaida sana kwenye nchi zenye vimelea vya kidictator. Kwa taarifa yako inapokuja kwenye suala la wapinzani, mahakama zetu zimejionyesha zinapokea maagizo vya Magufuli. Na Magufuli hana historia ya kushindana kwa box la kura, hivyo mahakama ndio salama yake ya sasa, lakini hakuna mahakama.
 
Mkuu oktoba siyo mbali!

Najua ni ngumu sana kwa mfuasi wa chadema kukubali kwamba tutashindwa! Hicho kichaka cha tume huru kipo miaka yote ndio mnajifichaga hapo!

Basi tufanye Lisu ni zaidi ya tume huru na atashinda urais huu wa oktoba kisha kuwa rais wa jamhuri ya muungano wa tz, akiwa na robo tatu ya wabunge wa bunge la jamhuri.

Usiku mwema mkuu.

Hiyo October ipo kila mwaka, nothing special, ila sio kwa kura. Sio lazima Lisu ashinde, ila kama ushindani ni halali na sio wa utashi wa Magufuli, hata akishinda sio ushindi wa kutambia. Kinachofanya ccm iwe na viti vingi vya ubunge sio kukubalika sana, bali ni mfumo mbovu wa uchaguzi, ambao hata mtoto mdogo anajua fika muundo wake sio sahihi kwa ushindani.
 
Kwanza kabisa huyo jamaa siyo wa kurudi leo wala kesho na hata akirudi kila kitu kwisha habari yake, kuna kiwango cha risaisi ambazo mwili wa Binadamu unaweza kuhimili, kupigwa risasi zote hizo siyo mchezo, huyo kwanza hata akifanya press conf. mtu akibamiza mlango tu kwa bahati mbaya atazimia atafikiri ni hitman wamemjia tena,

Kama ulishawahi kupigwa risasi au hata kukoswa tu unaweza kuelewa ninachomaanisha, hivyo ukiniuliza mimi huyo Tundu Lisu ndiyo basi tena its over, kwani sidhani hata kama ataweza kutembea tena, achilia bali hata tu kuinuka, atabakia jina tu kwa wafuasi wake kama vile Marando &Co., kwa kifupi they fvcked the guy up forever man, whoever shut him!
Dah Mungu mkubwa kuna waliokoment hivi ona sasa yuko wap na anafanya nn tumshukuru Mungu kwa kila jambo yeye ndo ajuae kesho yetu sio mwanadamu
 
Nyomi?

Anafikia hata robo ya lile la Slaa 2010 na Lowasa 2015
Jamaa mbona umekazania sana hii? Nani aliesema Dk Slaa na Lowassa walianguka kwenye Sanduku la kura?

Alafu kumbuka upinzani hauna mikutano miaka 5 afu wabunge kibao walikimbia achilia mbali viongozi kubanwa na dola.

Muda huo CCM wanazindua miradi na kujisifu wanajenga nchi hivyo walikua kila eneo unawakuta. Sasa ulitegemea 2020 kweli wangepata nyomi? Lissu mliemuita msaliti mlitegemea afikishe nyomi ndani ya wiki 3 toka atue nchini?

Tulizoea nyomi enzi za Slaa sababu siasa ilikua wazi ila kwa sasa ni suprise mzee hakuna aliyetegemea hta CCM walikua wanasubiri apate watu kumi waanze kejeli mitandaoni.

Ila haikuwa hivyo, upepo umebadilika kabisa
 
hivyo ukiniuliza mimi huyo Tundu Lisu ndiyo basi tena its over, kwani sidhani hata kama ataweza kutembea tena, achilia bali hata tu kuinuka, atabakia jina tu kwa wafuasi wake kama vile Marando &Co., kwa kifupi they fvcked the guy up forever man, whoever shut him!

Dua la kuku,, mkuu jifunze kuweka akiba ya maneno na kujipa muda.

Mungu sio Jacobo
 
Tafadhali muondowe mama yetu Samia kwenye hilo kundi, huyu mama ni mama kweli, hata Nairobi alikwenda hospitali kumjulia hali shujaa Lisu.

Mama Samia siyo dhalimu.

..nilimuona kwenye bunge maalum la katiba hayuko hivyo unavyomuelezea.

..pia alikwenda hospitali kumuangalia TL, wakamrekodi, na kutuma video za kumlisha maneno TL wakati yupo kitandani.
 
Hiyo October ipo kila mwaka, nothing special, ila sio kwa kura. Sio lazima Lisu ashinde, ila kama ushindani ni halali na sio wa utashi wa Magufuli, hata akishinda sio ushindi wa kutambia. Kinachofanya ccm iwe na viti vingi vya ubunge sio kukubalika sana, bali ni mfumo mbovu wa uchaguzi, ambao hata mtoto mdogo anajua fika muundo wake sio sahihi kwa ushindani.
Ungeweka wazi vigezo vya ushindani halali tujadiliane.
 
Back
Top Bottom