Tundu 'Frankenstein' Lissu

Tundu 'Frankenstein' Lissu

Nyomi?

Anafikia hata robo ya lile la Slaa 2010 na Lowasa 2015

Anafika vizuri sana, labda useme kwamba wakati ule ulikuwa na idadi kamili, na sasa una idadi kamili. Kinyume na hapo ni wivu kama wivu mwingine. Na isitoshe wakati wa Slaa na Lowassa hakukuwa na ndege, flyover, bwawa la umeme, reli, na wala hakukuwa na Katazo la kufanya siasa kwa wapinzani kama sasa.
 
Kwanza kabisa huyo jamaa siyo wa kurudi leo wala kesho na hata akirudi kila kitu kwisha habari yake, kuna kiwango cha risaisi ambazo mwili wa Binadamu unaweza kuhimili, kupigwa risasi zote hizo siyo mchezo, huyo kwanza hata akifanya press conf. mtu akibamiza mlango tu kwa bahati mbaya atazimia atafikiri ni hitman wamemjia tena,

Kama ulishawahi kupigwa risasi au hata kukoswa tu unaweza kuelewa ninachomaanisha, hivyo ukiniuliza mimi huyo Tundu Lisu ndiyo basi tena its over, kwani sidhani hata kama ataweza kutembea tena, achilia bali hata tu kuinuka, atabakia jina tu kwa wafuasi wake kama vile Marando &Co., kwa kifupi they fvcked the guy up forever man, whoever shut him!
Aaaaah nyie watesi wa lissu mnateseka sana.
 
Wacha kiherehere! Unadandia usiyoyafahamu! Mbona huyu ndiye amekuwa akisema eti Tundu Lissu anajitafutia umaarufu? Na wewe una akili fupi pia?
Wapi nimesema Tundu Lissu anajitafutia umaarufu?
 
Hatimaye, three years later utabiri wako unatimia. Lissu amepona na kurudi Tanzania, na mbaya zaidi amekuwa zaidi ya tishio kwa Magufuli na Serikali.

Watanzania wanampenda zaidi na anaenda kuwa Raisi wa Tanzania kwenye uchaguzi wa October 2020
Lisu kuwa Rais wa Tanzania sio rahisi na haitakuja kutokea
 
Sioni utamkamataje na kumfunga mtu ambaye kanusurika kuuwawa namna ile. Akili yangu inaniambia hata dhamiri yako, kama ni safi, basi itakusuta tu.

Hakika hii serikali ya awamu ya tano ilibugi stepu katika namna ya kumkabili Lissu na sasa amekuwa lidubwana ambaye anaweza asidhibitike tena.

Ni muda tu ndo utaotueleza.....
Wewe ni Mafiga Matatu no. 2 hapa Jamiiforums. Mafiga Matatu no.1 aliandika mambo 2012 yanayotabiri aina ya serikali itakayofuata baada ya Kikwete kuwa itakuwa katili na pia alitabiri 4 possible candidates akiwemo Magufuli. In short akipita mulemule.

Sasa wewe naye haya maandishi uliyaandika 2017 kuhusu Lisu na ugumu wa serikali ya John kumdhibiti atakaporejea. Na ndiyo tunayaona.

Big up man. Ulipita mulemule.
 
Kula kwanza yake matapishi yako ya mwanzo. Kimsingi kwenye ushindani kuna mshindi na mshindwa, hakuna mwenye tatizo na hilo, ila hakuna uwezekano wowote wa ccm kushinda zaidi ya 55% kihalali. Zile zama za ccm kushinda zaidi ya 60% zimeshapita na hazitakaa zirudi, na iwapo wapinzani watasimama kidete kutaka mshindi halali atangazwe, kwa vyovyote kutatokea machafuko, na kutokana na machafuko hayo kutatokea mabadiliko makubwa kwenye chaguzi za nchi hii. Na ikitokea mabadiliko tu ya mfumo wa uchaguzi, huo ndio utakuwa mwisho wa ccm, hicho chama cha kizazi kilichopita.
Naombea mambo yawe hivyo hivyo kama ulivyoandika, hatuwezi kutaliwa na lichama limoja miaka nenda rudi hadi watu wanajisahau.
 
Mkuu ushindi ni mahesabu, na mahesabu yenyewe yanaanzia kwenye kujiandikisha katika daftari la mpiga kura,!

Nyie mlishayapuuza tangu zoezi linaanza, sasa hivi ndio mnajifariji kwa mafuriko ambayo hata Slaa alikuwa nayo.


Kiufupi sioni hasa ni wapi chadema mmejiwekea mikakati ili mshinde urais wa tz.

Yani muwe na zaidi ya 50% ya wabunge bara na Zanzibar
Kisha na muwe na zaidi 50 % kura za urais bara na Zanzibar

Sioni!

Haya mahesabu nimekupa vizuri kwenye uzi ule.
 
Nyomi?

Anafikia hata robo ya lile la Slaa 2010 na Lowasa 2015
Acha presha na papara mkuu na uwe mwepesi wa kuelewa. Umemsoma niliyemquote? Umeelewa kwa mujibu wa maelezo yake Tundu Lissu angekuwa wapi?

Nimesema hivyo ili kumrudisha ajisome na ajidharau sana kwa kujaribu kuingilia majukumu ya Mungu lakini Mungu amemuinua aliyemtabiria kuwa 'its over' sasa si tu its not over, wala si kushindwa kuinuka tena, bali anatembea bila hata magongo na anakusanya nyomi kila anapokwenda.

Sijaja kushindanisha nyomi la fulani na la fulani na la fulani lipi kubwa.
 
Kula kwanza yake matapishi yako ya mwanzo. Kimsingi kwenye ushindani kuna mshindi na mshindwa, hakuna mwenye tatizo na hilo, ila hakuna uwezekano wowote wa ccm kushinda zaidi ya 55% kihalali. Zile zama za ccm kushinda zaidi ya 60% zimeshapita na hazitakaa zirudi, na iwapo wapinzani watasimama kidete kutaka mshindi halali atangazwe, kwa vyovyote kutatokea machafuko, na kutokana na machafuko hayo kutatokea mabadiliko makubwa kwenye chaguzi za nchi hii. Na ikitokea mabadiliko tu ya mfumo wa uchaguzi, huo ndio utakuwa mwisho wa ccm, hicho chama cha kizazi kilichopita.
Mkuu tindo, kwanza nikupongeze kwa kuwa mfuasi kindakindaki wa CHADEMA na hasa Lissu. Hongera za dhati.

Je, unamshauri ajiandaeje, kampeni zikianza, kuhusu mambo kadhaa ikiwemo:
√ Sera na Mikakati mbadala ya maendeleo badala ya kung'ang'ania shutuma dhidi ya Serikali na viongozi wake, hasa Rais Magufuli na viongozi wa dini;
√ Kujibu tuhuma za ufisadi ndani ya chama chake dhidi ya M/Kiti wake, kama zilivyotolewa na zitaanikwa upya, wakati wa kampeni, na wanasiasa waliokihama chama;
√ Ushindani dhidi ya wagombea Urais wa vyama vingine vya upinzani ambao wanatofautiana kwa mbali na jinsi anavyojinasibu kwa wapiga kura, kuelekea kampeni za Uchaguzi Mkuu;
√ Ukimya wa Jeshi la Polisi kuhusu shambulio lilolenga kuondoa uhai wake; na
√ Kesi zake ambazo wadhamini walijiondoa, hivyo kisheria dhamana imefutwa. Isitoshe mara mwisho hakuhudhuria mahakamani kwa kisingizio za kiafya, lakini ameonekana akishiriki shughuli za kisiasa tofauti na hayo madai.

FUMBO MFUMBIE MJINGA ...
 
Back
Top Bottom