Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 15,502
- 19,341
Viumbe wote hawataki matatizo. Hata wanyama wakali kama simba, hawataki matatizo katika maisha yao, ndiyo maana huchukua tahadhari sana wakati wakiwinda ili wasijejikuta katika matatizo ya namna yoyote.
Kuna njia nyingi za kujiepusha na matatizo, zote zinaangukia katika makundi matatu kama ifuatavyo.
(a) Njia zinazoepusha mazingira yanayokaribisha matatizo; kwa hiyo matatizo hayatokei kabisa
(b) Njia zinazokabiliana na matatizo hayo ana kwa ana na kuhakikisha yanatoweka.
(c) Njia zinazotuondoa kwenye mazingira yenye matatizo na kutupeleka kule ambako hakuna matatizo tukiyaacha matatizo ya awali apo hapo yalipo.
Njia zote zina faida na hasara zake kama ifuatavyo:
(1) Njia zinazoepusha mazingira ya matatizo zinatumia raslimali nyingi kwani zinatabiri uwezekano wa matatizo kutokea hata kama utabiri huo siyo kweli. kwa mfano inabidi mtu ajenge nyumba kwa kutumia nondo ghali ili kujiimarisha na matatizo yaletwayo na kimbunga hata kama hakutatokea kimbunga chochote kwa miaka mingisa sana. Faida zake kubwa ni kuwa njia hizo hutukinga kabisa na madhara ya matatizo hayo iwapo yakiibuka.
(2) Njia za kukabiliana na matatizo ana kwa ana huwa pia zinatumia raslimali, na muda mwingi sana katika kukabiliana na matatizo hayo. Vile vile hakuna uhakika kama kweli kwa kutumia njia hii tunaweza kuyashinda matatizo yetu. Faida kubwa za njia hizi ni kuwa tukishakabiliana na tatizo na kulishinda, basi hata kama tatizo hilo litajirudia tena siku za mbeleni, halitakuwa na madhara kabisa kwa vile tutakuwa tunajua namna ya kulikabili.
(3) Njia rahisi sana ya kutusalimisha na matatizo ni kuyakimbia yanapotokea. Kila yanapotokea basi sisi tunaondoka katika mazingira ya matatizo hayo na kwenda sehemu nyingine. Pamoja na kuwa njia hii haitumii raslimali nyingi, tatizo lake kubwa ni kuwa kuna matatizo mengine ambayo ni vigumu kuyakimbia. Na hata kama kuna sehemu nyingi za kukimbilia, kuna wakati tunakuwa hatuna pa kukimbilia tena.
Je Tanzania tunatumia njia gani kukabiliana na matatizo yetu kama taifa?
Nilipofuatilia ule mjadala kati ya Mkapa na wanazuoni wa Kigoda cha Nyerere pale mlimani kuhusu sera yake ya ubinafsishaji, na hoja zilizotolewa na Mkapa, ikanijia wazi kichwani kuwa Mkapa alikuwa anatumia hiyo njia ya tatu kukabiliana na matatizo ya mashirika ya umma. Badala ya kukabiliana na matatizo yale ana kwa ana na kujenga mazingira ya kuzuia matatizo hayo yasijirudie, yeye alikuwa anayakaimbia matatizo hayo kwa kuwasukumia watu wengine waliojulikana kama wawezekezaji.
Leo hii Tanzania tuna matatizo ya urari wa mapato; badala ya serikali kukabiliana na tatizo hilo ana kwa ana kwa kuweka sera imara inayoihakikishia serikali mapao yake, sisi tunakimbilia pembeni na kuwaacha wafadhaili ndio wakabiliane na tatizo hilo.
Je kwa nchi hii iliyojaa matatizo, tutaendelea kuyakimbia hadi lini? Inabidi tujifunze tena namna ya kukabiliana na matatizo hayo ana kwa ana na kuyashinda.
Kuna njia nyingi za kujiepusha na matatizo, zote zinaangukia katika makundi matatu kama ifuatavyo.
(a) Njia zinazoepusha mazingira yanayokaribisha matatizo; kwa hiyo matatizo hayatokei kabisa
(b) Njia zinazokabiliana na matatizo hayo ana kwa ana na kuhakikisha yanatoweka.
(c) Njia zinazotuondoa kwenye mazingira yenye matatizo na kutupeleka kule ambako hakuna matatizo tukiyaacha matatizo ya awali apo hapo yalipo.
Njia zote zina faida na hasara zake kama ifuatavyo:
(1) Njia zinazoepusha mazingira ya matatizo zinatumia raslimali nyingi kwani zinatabiri uwezekano wa matatizo kutokea hata kama utabiri huo siyo kweli. kwa mfano inabidi mtu ajenge nyumba kwa kutumia nondo ghali ili kujiimarisha na matatizo yaletwayo na kimbunga hata kama hakutatokea kimbunga chochote kwa miaka mingisa sana. Faida zake kubwa ni kuwa njia hizo hutukinga kabisa na madhara ya matatizo hayo iwapo yakiibuka.
(2) Njia za kukabiliana na matatizo ana kwa ana huwa pia zinatumia raslimali, na muda mwingi sana katika kukabiliana na matatizo hayo. Vile vile hakuna uhakika kama kweli kwa kutumia njia hii tunaweza kuyashinda matatizo yetu. Faida kubwa za njia hizi ni kuwa tukishakabiliana na tatizo na kulishinda, basi hata kama tatizo hilo litajirudia tena siku za mbeleni, halitakuwa na madhara kabisa kwa vile tutakuwa tunajua namna ya kulikabili.
(3) Njia rahisi sana ya kutusalimisha na matatizo ni kuyakimbia yanapotokea. Kila yanapotokea basi sisi tunaondoka katika mazingira ya matatizo hayo na kwenda sehemu nyingine. Pamoja na kuwa njia hii haitumii raslimali nyingi, tatizo lake kubwa ni kuwa kuna matatizo mengine ambayo ni vigumu kuyakimbia. Na hata kama kuna sehemu nyingi za kukimbilia, kuna wakati tunakuwa hatuna pa kukimbilia tena.
Je Tanzania tunatumia njia gani kukabiliana na matatizo yetu kama taifa?
Nilipofuatilia ule mjadala kati ya Mkapa na wanazuoni wa Kigoda cha Nyerere pale mlimani kuhusu sera yake ya ubinafsishaji, na hoja zilizotolewa na Mkapa, ikanijia wazi kichwani kuwa Mkapa alikuwa anatumia hiyo njia ya tatu kukabiliana na matatizo ya mashirika ya umma. Badala ya kukabiliana na matatizo yale ana kwa ana na kujenga mazingira ya kuzuia matatizo hayo yasijirudie, yeye alikuwa anayakaimbia matatizo hayo kwa kuwasukumia watu wengine waliojulikana kama wawezekezaji.
Leo hii Tanzania tuna matatizo ya urari wa mapato; badala ya serikali kukabiliana na tatizo hilo ana kwa ana kwa kuweka sera imara inayoihakikishia serikali mapao yake, sisi tunakimbilia pembeni na kuwaacha wafadhaili ndio wakabiliane na tatizo hilo.
Je kwa nchi hii iliyojaa matatizo, tutaendelea kuyakimbia hadi lini? Inabidi tujifunze tena namna ya kukabiliana na matatizo hayo ana kwa ana na kuyashinda.