Tunavyoagiza toka ng'ambo

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,478
39,996
Public Discourse II

Na. M. M. Mwanakijiji

Nilikuwa nazungumza na Mkulu mmoja wa idara siku chache zilizopita alisema kitu fulani ambacho wakati huo hakikunisumbua kichwa hadi sekunde chache zilizopita. Alikuwa anaulizia vitu fulani fulani kwa ajili ya matumizi ya ofisi yake mpya ambavyo angeweza kuagiza kutoka hapa au Uchina (mwenyewe alipenda vya hapa US).

Kutokana na mazungumzo hayo nikaulizia (katika kutosheleza udadisi wangu tu) kuwa kwani samani zake za ofisi amenunua wapi? Alicheka kidogo na kuniambia kuwa ziliagizwa toka Uarabuni (sijui kijiji gani); Katika kutaka kujua zaidi nikamuuliza na mazulia mmeyapata kutoka Magereza (lile Gereza la Maweni Tanga walikuwa wanatengeneza mazulia mazuri tu na kulikuwa/kipo kiwanda cha mazuria) akacheka tena kunishangaa na kusema Mazuria mazuri siku hizi yanatoka Omani huko na Qatar ingawa yeye alikokuwa mwanzoni (kabla ya wadhifa mpya) waliagiza ya kwao toka China huko huko.

Tukaendelea na mazungumzo mengine hadi hivi punde:

Hivi Maofisi ya serikali yanaagiza vitu gani nje ambavyo vingeweza kabisa kupatikana nchini katika ubora mzuri na kwa bei nafuu na hivyo kuchangia katika kutoa ajira, huduma na kukua kwa uchumi? Je kuna kitu chochote cha ofisini ambacho hakiwezi kupatikana Tanzania hadi twende nje? Hofu yangu ni kuwa tusipoangalia tutakuta tunaagiza hata watumishi kutoka nje na viongozi kutoka nje huku wenyewe tukiona fahari kwamba tunatumia vitu vya "ng'ambo"!

On the other hand, labda uzee umeanza kuniingia kwa kasi!!
 
Vitu kibao vinaagizwa nje hata kama vingeweza kupatikana hapa hapa. Kama makabati wapo watu wanachonga quality; kama furniture za mbao poa wapo watu wanaweza na sio kutuletea mambao yaliyotengenezwa na chenga/randa za mbao kama furniture nyingi za China; vitanda pia; hata majiko quality yapo Arusha(Tanalec); carpet hizo umetaja sasa sijui kama bado hicho kiwanda kinazalisha au watu wamsehakunywa zamaaaaaannniiii!!!

Kama ingewezekana itoke circular kwamba ofisi za serikali zi-procure locally as much as possible. Protection ya local industry should be first and foremost - during the industrial revolution governments nyingi duniani, principally US and England were highly protectionist of their local industrial products: we should also do the same.

Sadly, it seems everything is stacked up against us, all this made possible and facilitated by some of the biggest obstacles to development - World Bank, IMF, US government etc etc.
 
Kaka kweli hata mimi hapo umenigusa sana. hivi how can we protect our local industry ili ziweze kugrow na kutoa ajira za kutosha na maisha yaboreke.
hivi hizi sera na sheria zetu ndo tatizo au ni utekelezaji. kwa mfano procurement ya serikali kwenye wood products is very sisgnificant na yote inakwenda kwa wageni kama furniture centre, supreme alea na wengineo.
vipi taasisi zetu kama TBS, TRA katika hili?? Halafu chamber of commerce yetu(TCCIA) nayo sauti yao vipi au wameridhika kujuana na wakubwa kwenye party zao na wao kama viongozi kuneemeka kwa network kwenye system??

NAOMBA KUWASILISHA KWA MJADALA ZAIDI.
 
Mjadala huu wa kuagiza vitu kutoka ng'ambo (hata kama vinapatikana hapa nyumbani) ni mpana na kwa upande wangu mimi ni suala la ulimbukeni, wakati watanzania wengi walipopata ruhusa ya kumiliki seti za luninga na kuangalia mambo mengi ya nje (fikira tamthilia zinazotengenezwa amerika ya kusini na nyingine ) idadi yetu nzuri tu ilifikiria kuwa hakuna kitu kizuri kama kilichotengenezwa toka nje. Ilianzia majumbai kwa watu wenye 'uwezo' wa kati na sasa imekuwa ni 'fasheni' katika ofisi mbalimbali na hasa za umma.

Nimekuwa nikichangia mara nyingi sana kuwa utashi wa kisiasa hushawishi sana maendeleo ya ndani, na hakuna haja ya kuweka siasa kwenye vitu vya msingi. Viwanda vingi ulivyotaja vimeuawa na walioviua kwa kujitajirisha wapo na wengine sasa ni wanasiasa wakubwa na wenye sauti.

Kwa hili ndoto za mchonga samani wa kati wa kitanzania kuendela ni ndogo sana kwa sababu anaziota asubuhi na hivyo kuchoka. TCCIA ipo kama haipo imekuwa ni taasisi ya kwenye hafla tu, na kwa hakika bado haiwakilishi wote hata kama itakuwa na vijitengo vingi sana sana ofisi zao nyingi wanishia kufanya kazi za kutoa huduma ya 'stationery tu

Ukichukua utajiri mkubwa wa misitu yenye mbao nzuri na adimu, ukachanganya na wataalamu tulionao wa ufundi wa samani utaweza kudhani kuwa maendeleo hayaepukiki. Lakini katika hali halisi, vitu ni tofauti. ofisi nyingi sasa zinaagiza hata stuli kutoka nje, tena zote hizi ni wooden!

Kikubwa hapa ninacholilia ni kwa sisi kutambua kuwa sector ya uchongaji na utengenezaji wa samani ni kubwa na muhimu, zaidi inaweza kutoa nafasi kubwa sana ya ajira kwa watanzania wengi. Najiuliza hivi tuliopo Tanzania huwa tunakumbuka kuhoji kuhusu suala la ajira tunazoambia na wanasiasa au ndo mambo ya kuzugana kuwa serikali imetengeneza ajira laki sita mpaka sasa!

Tunapoagiza (hii ni kwa watawala na watanzania wenye kudhani kuwa mafundi wetu hawawezi kutoa kitu cha uhakika na kizuri)



HUWEZI KUKITHAMINI MPAKA UKIPOTEZE
 
Wakuu heshima mbele..... MMM umeanzisha kitu ambacho kwa kweli kinahusiana na mambo mengi amabyo yameongelewa humu ndani ya baraza. Nakumbuka kuna thread nyingi ambapo haya maswala yalizungumziwa japo sio kwa kina. Kwa uharaka mimi nimegundua (my understanding) kwamba kuna:
1. Kasumba ya watu kuamini vya nje ni bora
2. 10% inayolipwa kwa watendaji wakiagiza vitu husika
3. Kifo cha makampuni yetu ya ndani (either naturally which I doubt au planned - General tyre, Mgololo etc)
4. Privatisation ya viwanda vyetu - hapa kidogo mimi naonelea kwamba kuna mushkeli sababu kuna baadhi ya so-called wawekezaji wamepewa viwanda/makampuni yetu na kuyaua kabisa kwa kutokujali quality no more!!

Kwa uharaka nadhani inabidi kama nchi turudi kwenye drawing board na kuamua namna ya kurekebisha jambo hili.... Mfano rahisi ni madawa ambapo wananchi/waTz wangapi wenye uwezo japo kidogo wanameza/wananunua madawa yaliyotengenezwa nje badala ya yale yaliyotengenezwa nchini? Mimi ni mmoja wao, tunapendelea dawa za nje tena Ulaya na sio India!

Tunaenda wapi?? MMM naona unahofia kuletwa/kuagizwa kwa watumishi na viongozi kutoka nje, well tayari tumeshafika huko.... tumesha na tunaendelea kuagiza kutokea mahousigeli (Malawi) mpaka management ya makampuni yetu (unakumbuka TANESCO na NET GROUP) and the list goes on and on!!!

Naomba kuwakilisha....
 
Lakini tunaweza kweli kulinda wale watengeneza furniture wa pale Keko Gerezani au wauza samani wa Manzese n.k? Je serikali ikiagiza kuwa vitu fulani lazima vinunuliwe ndani ya nchi itakuwa ni kuingilia "uchumi wa soko"? Hivi karibuni katika pita pita yangu niligundua kuwa wakati Rais amekuja kwenye Mkutano wa Umoja wa Mataifa alikuja na chakula cha futari kutoka ng'ambo (nadhani Uarabuni)!

Katika kuuliza uliza kwangu nikagundua pia kuwa pale Ikulu siku hizi kuagiza hata baadhi ya vyakula ni vile vya kutoka nje ya nchi. NIkakumbushwa jinsi ya Maduka fulani ya kigeni ambayo yameingiza nchini hadi nyanya na vitunguu kutoka ng'ambo na kuviacha vile vinavyodhalishwa maeneo ya Uyole Mbeya na wengine wameleta matunda damuk toka Afrika ya Kusini wakiyasahau yale ya Lushoto.

Ni vitu gani ambavyo Tanzania tunaweza kuvizalisha, kuvitengeneza na ambavyo kwa hakika hatuhitaji kuagiza kutoka nje ya nchi?
 
Nafikili kwanza ni kuangalia gharama za vitu vya ndani na vile vya nje ya nchi, ubora n.k
Katika gharama hasa fenicha, utanona kuwa fenicha nyingi za nyumbani zina gharama ya juu kulinganisha na fenicha kutoka Uarabuni.

Ubunifu wa mafundi seremala kwa upande mwingine unawaweka mbali katika ushindani wa kimataifa. Fenicha nyingi ambazo zipo kwenye soko zilizotengenezwa hapo nyumbani, ni ubunifu wa zaidi ya miaka kumi.

Ubora ni kigezo kingine, mafundi seremala wengi wanatumia mbao ambazo zipo chini ya viwango na hasa ambazo hazijakauka vizuri, hivyo kupunguza ubora wa fenicha na urefu wa maisha ya fenicha.
 
Last edited:
Nafikili kwanza ni kuangalia gharama za vitu vya ndani na vile vya nje ya nchi, ubora n.k
Katika gharama hasa fenicha, utanona kuwa fenicha nyingi za nyumbani zina gharama ya juu kulinganisha na fenicha kutoka Uarabuni.

Ubunifu wa mafundi seremala kwa upande mwingine unawaweka mbali katika ushindani wa kimataifa. Fenicha nyingi ambazo zipo kwenye soko zilizotengenezwa hapo nyumbani, ni ubunifu wa zaidi ya miaka kumi.

Ubora ni kigezo kingine, mafundi seremala wengi wanatumia mbao ambazo zipo chini ya viwango na hasa ambazo hazijakauka vizuri, hivyo kupunguza ubora wa fenicha na urefu wa maisha ya fenicha.

kwa hiyo kutokana na hayo yote suluhisho ni kuagiza kutoka nje?
 
Nikisema Ndivyo Tulivyo naambiwa eti nina "low self esteem".....

Kama mtu unashangaa ya kuagiza vitu kutoka ng'ambo vipi kumpeleka mkeo ng'ambo akajifungulie huko ili mtoto awe na uraia wa huko....
 
kwa hiyo kutokana na hayo yote suluhisho ni kuagiza kutoka nje?
Yapo mengi ya kufanya,

Kwanza ni Serikali kutambua bidhaa za ndani na kuzilinda, hii ni pamoja na kuangalia kodi mbalimbali za bidhaa za ndani na zile zinazotoka nje. Kuwepo na kampeni kubwa za kitaifa za kunadi bidhaa za ndani.

Wazalishaji wa ndani ni vema kujua nini mteja wao wanahitaji... wawe wabunifu zaidi, na waende na wakati. Hii itasaidia sana iwapo patafanyika kampeni ya kunadi bidhaa zao, kwani wateja wataweza kuridhika na bidhaa zao.

Kwa makusudi kabisa ni vema wakaongeza ubora wa bidhaa zao. Kwa mfano ni rahisi sana kuona aina mbalimbali za majani ya chai katika maduka ya kawaida toka Kenya kuliko kuona majani ya chai toka Tz.

Wawe na lengo katika kuzalisha na wanawalenga watu wa aina gani katika bidhaa zao. Kama ni fenicha za ofisi basi wajue nini ofisi inataka ili ipendeze na aina gani za fenicha zinafaa kwa ofisi.

Miaka ya huko nyuma ilikuwa ni rahisi kukuta fenicha ya nyumbani ikitumika ofisini. Na hata fenicha za nje ya nchi zilipoanza kuingia katika ofisi mbalimbali, mafundi seremala bado walishindwa kubadilika, hali kadhalika kwa fenicha za majumbani ama kwenye klabu na baa..

Wakulima wadogo wadogo wengi(hasa wa mijini) sasa wamekuwa wajanja katika hili. Wameweza kuhifadhi vizuri bidhaa zao katika kiwango cha hali ya juu na hivyo kuwavuta wageni wengi waishio nchini kununua bidhaa zao mitaani badala ya kwenda sokoni. Hii inaweza kutumika vilevile kuwavuta wazalendo kununua mazao ya wakulima wa ndani iwapo yatakuwa yameifadhiwa vema na katika ubunifu unaoendana na hali halisi ya nchi pasipo kuathiri bei ya bidhaa na mazingira ya nchi kwa ujumla.
 
I think hapa tuna-confuse issues kidogo, tunaongelea bidhaa ambazo ziko available hapa hapa nchini au tunaongela bidhaa zilizo tengenezwa Tanzania. As for me I can say that Bidhaa za nje which are available here in the country from my experience have been of a far better quality, more affordable then local substitutes and more easily accessible. Sasa procurement niende kusumbuka kwenye jua hadi kule gerezani just to prove I am protecting local industries, if local indusries real cared about growing they would first improve there service offering by looking at the quality of there goods, pricing strategies, and ease of access to these goods and services. As an example one can go to Furniture Centre and in a matter of hours have a office set up for 3 to 4 people with less the 2-3m, na guarantee juu and delivery arrangements, Gerezani maranyingi you have to make orders for goods that will take you 3 weeks to a month (na excuse chungu mbovu for further delay) and you still never end up with exactly what you want and the price will go up even after recieving a pro forma, there is no gurantee. My take is local manufactures need to get serious about there service offerings if they are to win the hearts of the local market, no one likes the fact that we buy goods produced elsewhere let alone order them from outside the country. But in all true honesty we are left with no choice. So local industry FIX UP and acheni biashara zaku babaisha and you will have all the customers you need!!!!
 
Yapo mengi ya kufanya,

Kwanza ni Serikali kutambua bidhaa za ndani na kuzilinda, hii ni pamoja na kuangalia kodi mbalimbali za bidhaa za ndani na zile zinazotoka nje. Kuwepo na kampeni kubwa za kitaifa za kunadi bidhaa za ndani.

Very good!

Wazalishaji wa ndani ni vema kujua nini mteja wao wanahitaji... wawe wabunifu zaidi, na waende na wakati. Hii itasaidia sana iwapo patafanyika kampeni ya kunadi bidhaa zao, kwani wateja wataweza kuridhika na bidhaa zao.

Very good!


Kwa makusudi kabisa ni vema wakaongeza ubora wa bidhaa zao. Kwa mfano ni rahisi sana kuona aina mbalimbali za majani ya chai katika maduka ya kawaida toka Kenya kuliko kuona majani ya chai toka Tz.

Tunaweza vipi kuwa na Quality Assurance katika bidhaa zetu mbalimbali kiasi cha kuweza kuweka katika ushindani? Wanaotengeneza samani kwa mfano ni kwa kiwango gani wanahitaji kufikia ili kuweza kusema bidhaa zao ni bora?


Wawe na lengo katika kuzalisha na wanawalenga watu wa aina gani katika bidhaa zao. Kama ni fenicha za ofisi basi wajue nini ofisi inataka ili ipendeze na aina gani za fenicha zinafaa kwa ofisi.

Wale tuliosoma kwenye shule za ufundi, je unakumbuka kufundishwa ufanyaji biashara bora, utawala pamoja na ufundi uliokuwa unasomea?


Miaka ya huko nyuma ilikuwa ni rahisi kukuta fenicha ya nyumbani ikitumika ofisini. Na hata fenicha za nje ya nchi zilipoanza kuingia katika ofisi mbalimbali, mafundi seremala bado walishindwa kubadilika, hali kadhalika kwa fenicha za majumbani ama kwenye klabu na baa..

Wakulima wadogo wadogo wengi(hasa wa mijini) sasa wamekuwa wajanja katika hili. Wameweza kuhifadhi vizuri bidhaa zao katika kiwango cha hali ya juu na hivyo kuwavuta wageni wengi waishio nchini kununua bidhaa zao mitaani badala ya kwenda sokoni. Hii inaweza kutumika vilevile kuwavuta wazalendo kununua mazao ya wakulima wa ndani iwapo yatakuwa yameifadhiwa vema na katika ubunifu unaoendana na hali halisi ya nchi pasipo kuathiri bei ya bidhaa na mazingira ya nchi kwa ujumla.

Vizuri sana Kibunango!
 
hivi SIDO bado ipo au ndio nayo tumesha uza,tatizo la serikali yetu,haijui nini cha kufanya,imewaacha watanzania wajitafutie kama kuku wa kienyeji ambaye anatoka asubuhi na kuchokora chokora chini na kisha jioni utafuta pa kulala.
tuna wataalamu wengi lakini hawajui ni nini cha kufanya zaidi ya kusoma vigazeti vya udaku na kupiga soga.
ilitakiwa hawa wataalamu wasimamie sekta zote za uzalishaji ili zifikie kiwango stahiki ,kuanzia kwenye kilimo,ujenzi, useremala,na vitu vyote vinavyozalishwa kwa ajili ya biashara ili kuwa na viwango,sio kungojea vigari vya zaidi ya miaka kumi.
 
Vitu kibao vinaagizwa nje hata kama vingeweza kupatikana hapa hapa. Kama makabati wapo watu wanachonga quality; kama furniture za mbao poa wapo watu wanaweza na sio kutuletea mambao yaliyotengenezwa na chenga/randa za mbao kama furniture nyingi za China; vitanda pia; hata majiko quality yapo Arusha(Tanalec); carpet hizo umetaja sasa sijui kama bado hicho kiwanda kinazalisha au watu wamsehakunywa zamaaaaaannniiii!!!

Kama ingewezekana itoke circular kwamba ofisi za serikali zi-procure locally as much as possible. Protection ya local industry should be first and foremost - during the industrial revolution governments nyingi duniani, principally US and England were highly protectionist of their local industrial products: we should also do the same.

Sadly, it seems everything is stacked up against us, all this made possible and facilitated by some of the biggest obstacles to development - World Bank, IMF, US government etc etc.


Mkulu... sidhani kama uko sahihi...hawa jamaa ndio wanamlazimisha hata spika wa bunge la Tz kuagiza vazi lake toka nje???
 
I think hapa tuna-confuse issues kidogo, tunaongelea bidhaa ambazo ziko available hapa hapa nchini au tunaongela bidhaa zilizo tengenezwa Tanzania. As for me I can say that Bidhaa za nje which are available here in the country from my experience have been of a far better quality, more affordable then local substitutes and more easily accessible. Sasa procurement niende kusumbuka kwenye jua hadi kule gerezani just to prove I am protecting local industries, if local indusries real cared about growing they would first improve there service offering by looking at the quality of there goods, pricing strategies, and ease of access to these goods and services. As an example one can go to Furniture Centre and in a matter of hours have a office set up for 3 to 4 people with less the 2-3m, na guarantee juu and delivery arrangements, Gerezani maranyingi you have to make orders for goods that will take you 3 weeks to a month (na excuse chungu mbovu for further delay) and you still never end up with exactly what you want and the price will go up even after recieving a pro forma, there is no gurantee. My take is local manufactures need to get serious about there service offerings if they are to win the hearts of the local market, no one likes the fact that we buy goods produced elsewhere let alone order them from outside the country. But in all true honesty we are left with no choice. So local industry FIX UP and acheni biashara zaku babaisha and you will have all the customers you need!!!!

CEJ, when you buy a furniture from a supermarket or an outlet of a foreign manufacturer do you consider that somewhere along the way kuna hatua mbalimbali zimepitia hadi kufikia ile product unayoiona hapo? Unachozungumzia wewe ninavyoelewa ni vitu vya muhimu sana lakini vitu hivyo vimepitia hatua mbalimbali kufikia uzuri, urahisi wa bei na upatikanaji unaouona hapo.

Baadhi ya makampuni ya kimarekani yanayoagiza vitu kutoka nje au vitengenezwe kwa jina lao toka nje yanaweka matakwa yake wazi na mapema kuwa vitu vitengenezwe kwa kiwango gani, katika mazingira gani na hali gani na vifikie kiwango gani.

Sasa kuna ubaya gani kwa taasisi ya serikali kusema matakwa yake kwa wafanyabiashara wa vitu kama samani na kuona kiwango hicho kinafikiwa ndio wanunue bidhaa hizo?
 
Hoja ya kwanza ya Mwanakijiji ina mantiki kubwa sana, kwa kweli inazunguka katika mada ya kati ya Adam Smith katika "The Wealth of Nations". Kwamba sisi tuuze nje kile tu tunachoweza kutengeneza kwa ufanisi mkubwa, na tununue kutoka nje kile tu ambacho hatuwezi kutengeneza kwa ufanisi mkubwa.

Ukiangalia unaweza kuona kuagiza vitu kama samani kutoka nje hakuendani na maoni haya ya Adam Smith, na kunaweza kuwa ufujaji wa mali. Hili ni swala la msingi kabisa na bila shaka linatokea sana.Kwa sababu hii, maoni haya ya Mwanakijiji ni ya makini sana na hayapaswi kupuuzwa hata kidogo.

Lakini pia Adam Smith ni mtetezi mkuu wa biashara huria, mfumo ambao tumeukumbatia. Anachosema Mwanakijiji ingawa kinaweza kutufaa, lakini pia kinaweza kuturudisha katika enzi za mfumo wa uchumi unaopangwa na serikali.Mfumo wa soko huru, na zaidi ya hapo nchi huru, unaruhusu watu kuamua wanachotaka, hata kama wanachofanya hakiwapi faida, ilimradi hawavunji sheria.Hata katika mfumo mchanganyiko, tukileta "protectionism" sana tutakosa "moral authority" ya kuwasema wakubwa wasiwape ruzuku wakulima wao wa mahindi, na kusababisha mahindi yetu yadode wakati tunanunua mahindi yao kwa bei ya chini kuliko ile ya mahindi kutoka Rukwa.

Tunaweza kusema kuwa hatujakomaa kiuchumi kiasi cha kuukumbatia mfumo huria kiasi hiki.Ikiwa Mwalimu Nyerere anakumbukwa sana na wanaharakati wapinga ubeberu kwa jinsi alivyompamia Ronald Reagan na swahiba wake Margaret Thatcher kwa kupendelea kuwapa ruzuku wakulima katika nchi tajiri kama Marekani kwa nini sisi kina baba Kabwela tusiweze kuweka mipaka katika kodi na sheria za kibiashara zetu itakayofanya kuagiza kutoka nje vitu visivyo ulazima ? Kwa sababu katika fikra mpya za kiuchumi, Adam Smith ametupwa na Paul Krugman.

Paul Krugman, mchumi kutoka Chuo Kikuu maarufu cha Princeton kilichotoa wachumi wetu maarufu kama kina Professor Malima, ameshinda nishani ya Nobel ya Uchumi mwaka huu kwa kuonyesha kuwa Adam Smith alikuwa anafikiri kwamba watu (nchi) wataagiza tu vitu wasivyoweza kutengeneza kwa "comparative advantage" na watauza nje tu vitu ambavyo wanaweza kutengeneza kwa "comparative advantage". Krugman katika tafiti zake amegundua hiki hakitokei, na kwamba mara nyingi watu hutaka vitu vyenye ubora, thamani na pengine hata mitindo tu tofauti, hivyo kusababisha watu wengine waache samani za Magereza na kutafuta za Uarabuni.

Kama lilivyoandika gazeti la Forbes la October 13 2008 katika makala ya kuielezea nishani ya Nobel ya Krugman.Nadharia ya Heckscher-Ohlin pia, ambayo inasema kwamba nchi yenye mtaji mkubwa ita export mtaji wake na nchi yenye wafanyakazi wengi ita export wafanyakazi wake, haielezei kwa nini nchi zinazofanana sana kiuchumi, kama sehemu za Ulaya na Marekani, zinafanya biashara sana kuliko nchi zisizofanana.

Ninafahamu dhana nzima ya kujifunga mkanda kwa uzalendo mkubwa ili tujikwamue kiuchumi, lakini utafanya nini kama mtu hataki kukubali uzalendo huu, na hataki kuwa sehemu ya kujifunga mkanda huku? Katika nchi huru, huna la kufanya.Mtu kama huyu anaweza hata kusamehewa kwa kuagiza vya nje ikiwa anaweza kukueleza alivyopata bidhaa hafifu kutoka hapa nyumbani.

Nakumbuka nilipokuwa shule ya msingi, nilikuwa napenda sana kuagiza vitu kila mara baba yangu alipokuwa akisafiri.Darasa la sita nikataka sana begi la mgongoni kutoka Paris, lakini baba aliniambia kama alivyopenda kuniambia mara nyingi -labda kwa kuwa na uMwanakijiji- kuwa mabegi yanapatikana tu hata Samora Avenue, lakini sikukubali.Mwishowe watoto wote tukapata mabegi ya mgongoni kutoka ulaya, roho zetu zikafurahi. Sasa nimekua naona baba alikuwa na maana gani, na mimi ninapatwa na yale yale wakati wapwa wanapoagiza vitu vya Marekani ambavyo vipi Tanzania.MAra nyingi kama si suala la ubora, linakuwa ni swala la ulimbwende.Tuchukue hili swala kama wito kwa viwanda vyetu vijue sio tu kutengeneza bidhaa zenye ubora zaidi (ubora ambao unajumuisha na mambo aliyoyataja CottonEyeJoe hapo juu kuhusu muda unaochukuliwa na ubora wa huduma nzima inayohusiana na upataji wa bidhaa) bali pia vijue kuvitangaza vizuri kiasi hata hawa walimbwende wapende kununua vitu vya Tanzania kwa hiyari yao, bila ya kushurutishwa kwa kodi na sheria.

Kama kuna kitu inabidi tukitilie mkazo, ni uwezo wetu wa kuweza kuuza nje bidhaa zetu kwa kiasi kikubwa kuliko tunavyoagiza kutoka nje.Na hili liangaliwe kutoka upande wa kutaka kuongeza bidhaa zinazouzwa nje kuliko upande wa kutaka kupunguza bidhaa zinazoagizwa kutoka nje, kwa sababu watu wanaagiza kutoka nje kwa sababu tofauti, na katika nchi huru inayofuatilisha mfumo wa soko huria, huwezi kumkataza mtu mwenye fedha zake asiagize kutoka nje.
 
Pundit, uhalisia wa ulimwengu wa leo hii kiuchumi unatulazimisha kabisa kukubali kuwa hatuwezi kuwa na "soko huru" lisiloangaliwa au kusimamiwa ipasavyo. Na ni wazi kabisa kuwa uchumi duniani unapangwa na unasimamiwa na hilo si tatizo hata kidogo na kwa hakika si kuturudisha nyuma.

La maana ambalo nafikiri ni muhimu ni kuhakikisha ni mambo gani serikali inaweza na inapaswa kufanya na mambo ambayo sekta binafsi inaweza kufanya. Sasa ni kwa kiasi gani serikali inapanga sera za kiuchumi na kwa kiasi gani inaacha huru ndio tofauti kubwa sana naamini kati ya Ubepari wa Kimarekani na ule wa Canada.

Zinapokuja nchi zetu hizi za daraja la tatu naamini tumefanya makosa makubwa sana kuacha sekta binafsi ijifanyie mambo yake yenyewe na hivyo kusababisha stagnation ya aina fulani katika maendeleo ya viwanda n.k Naamini serikali yetu inapaswa kuwa na mkono mkubwa katika mazingira fulani (hasa kwenye regulation, supervision na law enforcement) ya viwanda.

Kama serikali ingekuwa na uangalizi wa kutosha na kutoa adhabu kwa biashara zisizofikia kiwango ingelazimisha wafanyabiashara kuhakikisha kuwa wanatengeneza bidhaa zinazofaa. Maana nikikaa kufikiria hapa nakumbuka mojawapo ya restaurant nilizoingia kula chakula mara ya mwisho nilipokuwa kijijini ukweli ni kuwa haijabadilika, upishi ni ule ule, kuitisha oda vile vile n.k Sasa tutaweza kweli?
 
Pundit, uhalisia wa ulimwengu wa leo hii kiuchumi unatulazimisha kabisa kukubali kuwa hatuwezi kuwa na "soko huru" lisiloangaliwa au kusimamiwa ipasavyo. Na ni wazi kabisa kuwa uchumi duniani unapangwa na unasimamiwa na hilo si tatizo hata kidogo na kwa hakika si kuturudisha nyuma.

La maana ambalo nafikiri ni muhimu ni kuhakikisha ni mambo gani serikali inaweza na inapaswa kufanya na mambo ambayo sekta binafsi inaweza kufanya. Sasa ni kwa kiasi gani serikali inapanga sera za kiuchumi na kwa kiasi gani inaacha huru ndio tofauti kubwa sana naamini kati ya Ubepari wa Kimarekani na ule wa Canada.

Zinapokuja nchi zetu hizi za daraja la tatu naamini tumefanya makosa makubwa sana kuacha sekta binafsi ijifanyie mambo yake yenyewe na hivyo kusababisha stagnation ya aina fulani katika maendeleo ya viwanda n.k Naamini serikali yetu inapaswa kuwa na mkono mkubwa katika mazingira fulani (hasa kwenye regulation, supervision na law enforcement) ya viwanda.

Kama serikali ingekuwa na uangalizi wa kutosha na kutoa adhabu kwa biashara zisizofikia kiwango ingelazimisha wafanyabiashara kuhakikisha kuwa wanatengeneza bidhaa zinazofaa. Maana nikikaa kufikiria hapa nakumbuka mojawapo ya restaurant nilizoingia kula chakula mara ya mwisho nilipokuwa kijijini ukweli ni kuwa haijabadilika, upishi ni ule ule, kuitisha oda vile vile n.k Sasa tutaweza kweli?

Ningefurahi zaidi kama ubora wa bidhaa zetu, ikiwa ni pamoja na utangazwaji wake, vitapanda maradufu na kusababisha wanaoagiza bidhaa kutoka nje waache wenyewe kwa hiyari yao kuliko kwa sababu za kiserikali.

Tukiweza kutengeneza bidhaa nzuri mpaka waarabu waje kununua sifikiri kama watu wengi wataenda uarabuni kununua bidhaa zao zinazofanana, utakuwa na wachache lakini halitakuwa swala kubwa.

Maji tushayavulia nguo, hatuna budi kuyaoga.Ni ubora wa bidhaa tu pamoja na wananchi kuelimika kuhusu kupenda chao, hamna haja ya shuruti.Ukianza shuruti ndiyo mwanzo wa kusema "Mwanakijiji ana import ideas kutoka blogs za Marekani, tuna waandishi wetu hapa hapa kwa hiyo hatumtaki"

I bet you would not want that.
 
Hoja ya kwanza ya Mwanakijiji ina mantiki kubwa sana, kwa kweli inazunguka katika mada ya kati ya Adam Smith katika "The Wealth of Nations". Kwamba sisi tuuze nje kile tu tunachoweza kutengeneza kwa ufanisi mkubwa, na tununue kutoka nje kile tu ambacho hatuwezi kutengeneza kwa ufanisi mkubwa.

Ukiangalia unaweza kuona kuagiza vitu kama samani kutoka nje hakuendani na maoni haya ya Adam Smith, na kunaweza kuwa ufujaji wa mali. Hili ni swala la msingi kabisa na bila shaka linatokea sana.Kwa sababu hii, maoni haya ya Mwanakijiji ni ya makini sana na hayapaswi kupuuzwa hata kidogo.

Lakini pia Adam Smith ni mtetezi mkuu wa biashara huria, mfumo ambao tumeukumbatia. Anachosema Mwanakijiji ingawa kinaweza kutufaa, lakini pia kinaweza kuturudisha katika enzi za mfumo wa uchumi unaopangwa na serikali.Mfumo wa soko huru, na zaidi ya hapo nchi huru, unaruhusu watu kuamua wanachotaka, hata kama wanachofanya hakiwapi faida, ilimradi hawavunji sheria.Hata katika mfumo mchanganyiko, tukileta "protectionism" sana tutakosa "moral authority" ya kuwasema wakubwa wasiwape ruzuku wakulima wao wa mahindi, na kusababisha mahindi yetu yadode wakati tunanunua mahindi yao kwa bei ya chini kuliko ile ya mahindi kutoka Rukwa.

Tunaweza kusema kuwa hatujakomaa kiuchumi kiasi cha kuukumbatia mfumo huria kiasi hiki.Ikiwa Mwalimu Nyerere anakumbukwa sana na wanaharakati wapinga ubeberu kwa jinsi alivyompamia Ronald Reagan na swahiba wake Margaret Thatcher kwa kupendelea kuwapa ruzuku wakulima katika nchi tajiri kama Marekani kwa nini sisi kina baba Kabwela tusiweze kuweka mipaka katika kodi na sheria za kibiashara zetu itakayofanya kuagiza kutoka nje vitu visivyo ulazima ? Kwa sababu katika fikra mpya za kiuchumi, Adam Smith ametupwa na Paul Krugman.

Paul Krugman, mchumi kutoka Chuo Kikuu maarufu cha Princeton kilichotoa wachumi wetu maarufu kama kina Professor Malima, ameshinda nishani ya Nobel ya Uchumi mwaka huu kwa kuonyesha kuwa Adam Smith alikuwa anafikiri kwamba watu (nchi) wataagiza tu vitu wasivyoweza kutengeneza kwa "comparative advantage" na watauza nje tu vitu ambavyo wanaweza kutengeneza kwa "comparative advantage". Krugman katika tafiti zake amegundua hiki hakitokei, na kwamba mara nyingi watu hutaka vitu vyenye ubora, thamani na pengine hata mitindo tu tofauti, hivyo kusababisha watu wengine waache samani za Magereza na kutafuta za Uarabuni.

Kama lilivyoandika gazeti la Forbes la October 13 2008 katika makala ya kuielezea nishani ya Nobel ya Krugman.Nadharia ya Heckscher-Ohlin pia, ambayo inasema kwamba nchi yenye mtaji mkubwa ita export mtaji wake na nchi yenye wafanyakazi wengi ita export wafanyakazi wake, haielezei kwa nini nchi zinazofanana sana kiuchumi, kama sehemu za Ulaya na Marekani, zinafanya biashara sana kuliko nchi zisizofanana.

Ninafahamu dhana nzima ya kujifunga mkanda kwa uzalendo mkubwa ili tujikwamue kiuchumi, lakini utafanya nini kama mtu hataki kukubali uzalendo huu, na hataki kuwa sehemu ya kujifunga mkanda huku? Katika nchi huru, huna la kufanya.Mtu kama huyu anaweza hata kusamehewa kwa kuagiza vya nje ikiwa anaweza kukueleza alivyopata bidhaa hafifu kutoka hapa nyumbani.

Nakumbuka nilipokuwa shule ya msingi, nilikuwa napenda sana kuagiza vitu kila mara baba yangu alipokuwa akisafiri.Darasa la sita nikataka sana begi la mgongoni kutoka Paris, lakini baba aliniambia kama alivyopenda kuniambia mara nyingi -labda kwa kuwa na uMwanakijiji- kuwa mabegi yanapatikana tu hata Samora Avenue, lakini sikukubali.Mwishowe watoto wote tukapata mabegi ya mgongoni kutoka ulaya, roho zetu zikafurahi. Sasa nimekua naona baba alikuwa na maana gani, na mimi ninapatwa na yale yale wakati wapwa wanapoagiza vitu vya Marekani ambavyo vipi Tanzania.MAra nyingi kama si suala la ubora, linakuwa ni swala la ulimbwende.Tuchukue hili swala kama wito kwa viwanda vyetu vijue sio tu kutengeneza bidhaa zenye ubora zaidi (ubora ambao unajumuisha na mambo aliyoyataja CottonEyeJoe hapo juu kuhusu muda unaochukuliwa na ubora wa huduma nzima inayohusiana na upataji wa bidhaa) bali pia vijue kuvitangaza vizuri kiasi hata hawa walimbwende wapende kununua vitu vya Tanzania kwa hiyari yao, bila ya kushurutishwa kwa kodi na sheria.

Kama kuna kitu inabidi tukitilie mkazo, ni uwezo wetu wa kuweza kuuza nje bidhaa zetu kwa kiasi kikubwa kuliko tunavyoagiza kutoka nje.Na hili liangaliwe kutoka upande wa kutaka kuongeza bidhaa zinazouzwa nje kuliko upande wa kutaka kupunguza bidhaa zinazoagizwa kutoka nje, kwa sababu watu wanaagiza kutoka nje kwa sababu tofauti, na katika nchi huru inayofuatilisha mfumo wa soko huria, huwezi kumkataza mtu mwenye fedha zake asiagize kutoka nje.

Hongera na shukrani za dhati kwa kuzingatia ushauri wangu niluokupa jana wa kuandika kwa kiswahili au kiingereza rahisi kinachoeleweka na wengi. Hapa hata mimi nimekuelewa leo!!!
 
Ningefurahi zaidi kama ubora wa bidhaa zetu, ikiwa ni pamoja na utangazwaji wake, vitapanda maradufu na kusababisha wanaoagiza bidhaa kutoka nje waache wenyewe kwa hiyari yao kuliko kwa sababu za kiserikali.

Tukiweza kutengeneza bidhaa nzuri mpaka waarabu waje kununua sifikiri kama watu wengi wataenda uarabuni kununua bidhaa zao zinazofanana, utakuwa na wachache lakini halitakuwa swala kubwa.

Maji tushayavulia nguo, hatuna budi kuyaoga.Ni ubora wa bidhaa tu pamoja na wananchi kuelimika kuhusu kupenda chao, hamna haja ya shuruti.Ukianza shuruti ndiyo mwanzo wa kusema "Mwanakijiji ana import ideas kutoka blogs za Marekani, tuna waandishi wetu hapa hapa kwa hiyo hatumtaki"

I bet you would not want that.

Nadhani tuko upande mmoja katika hili. Kwangu mimi nafikiria vitu viwili hasa:

a. Kwa nchi kama za kwetu serikali bado ndiye mnunuzi na bila ya shaka muajiri mkubwa zaidi. Kwa mfano serikali ikisema tuna kiasi cha shilingi Bilioni 100 kwa ajili ya ununuzi wa samani za maofisi yetu kila mwaka (don't ask me why but they do) na tunataka fedha hizi ziishie hapa hapa Tanzania je maseremala wa kwetu mtaweza haya?

Sasa wanasema furniture tunazotaka zinatakiwa ziwe x,y, z n.k Ziwe tayari ndani ya miezi miwili na tutakagua kujiridhisha kiwango hicho. Sasa hapa wanahamisha mzigo kwa maseremala kuwa wafanye nini ili kufikia kiwango. Sasa Chama cha Maseremela kinasema "tafadhali serikali tuna watu, tuna wataalamu na tuna mahali pa kufanyia kazi hiyo lakini hatuna vifaa vya kutosha tunahitaji retooling, je katika hizo fedha mnaweza kutuwekea kama credit ya kuboresha vifaa vyetu"? Serikali inasema "Ok tunawatengea shilingi bilioni 20 kuwasaidia kuretool, kujipiga msasa n.k" Hayo yanafanyika, maseremela wanajipanga na kutengeneza bidhaa nzuri na bora kwa kiwango cha kimataifa, serikali inakuja inachukua order ya kwanza ofisi zinang'ara na jumba linapendeza na wanasema mwaka ujao tunaorder zenye thamani ya bilioni nyingine!

Mfano huo hauko hewani. Wakati Serikali ya Marekani inapotaka makampuni ya magari yatengeneze magari ya kisasa ya hybrid au hata electric au yanayotumia nguvu za jua wanasema kiwango halafu wanawawekea muda wa kufikia lengo hilo. Sasa makampuni ya magari yanasema "sawa lakini hatuna vifaa vya kisasa na tunahitaji kufanya utafiti zaidi, kwanini serikali isitugawie fedha kidogo kusaidia mipango yetu ya kufikia malengo yao?" Ndipo serikali ya Bush ikatoa dola bilioni 20 hivi kwa ajili hiyo na sasa hivi wanajadiliana kupewa msaada mwingine. Matokeo yake ni kuwa serikali inapata inachotaka, biashara inajiimarisha, na wote wawili wananufaika.

Sasa kwetu sisi Tanzania tunashindwa nini? Nitakumpa mfano mzuri kabisa wa Tanzania. Wakati Rais Kikwete amekuja Marekani mara ya mwisho mojawapo ya misaada aliyopokea ni msaada wa vitabu vya darasani wa karibu shilingi milioni mia mbili (dola laki 2). Msaada huo ukatolewa lakini hiyo hela ni sehemu ya zile 698 za Bush ambazo zinalipwa kwa kampuni ya Marekani kutuletea vitabu hivyo.

Sasa tunajiuliza kwa nini kiasi hicho kisipelekwe Tanzania kutoa ofa kwa waandishi wetu na wachapishaji wetu kufanya kazi hiyo kwa kiwango kinachotakiwa?
 
Back
Top Bottom