Habari zenu mifugo ya Mungu na Shetani? Naona mnazidi kusukuma siku mkingoja kuliwa tu.
Nimegundua kitu kuwa kila kinachofugwa huwa akiruhususiwi kujua dhima na dhamira ya yule aliyekifuga.
Yaani ni hivi binadamu hata afanye nini hatoweza kujua dhamira na dhima ya yeye kufugwa hapa duniani.
Kama ilivyo kwa kuku na ng'ombe, hata wafanye nini hawatoweza kamwe kujua dhamira na dhima ya wao kufugwa na binadamu.
Ebu fikiria Kuku, ng'ombe na mbuzi wanatuchukuliaje sisi binadamu?
Wanatuona sisi ni msaada mkubwa sana kwao, kwani tunawapa msaada mkubwa sana. Ikiwepo sehemu ya kulala, tunawapa chakula, tunawatibu magonjwa. Wanaamini bila ya sisi wao si lolote wala chochote. Kwani tunawaepusha na majanga mbalimbali ikiwepo kuliwa na paka, mbwa n.k.
Kama wewe unavyoamini Mungu ni msaada mkubwa sana kwako na yeye ndiye mwanzo na mwisho kwako. Kwasababu tu anakupa uhai, anakupa riziki, anakuponya magonjwa ukiumwa na anakuepusha na majanga mbalimbali.
Kama ilivyofungwa akili ya kuku na ng'ombe juu ya dhamira kuu ya wao kufugwa na binadamu hivyo ndivyo ilivyofungwa akili ya binadamu kujua dhima kuu ya kwanini wapo hapa duniani.
Na siku binadamu akijua kwanini yupo hapa duniani ndiyo utakuwa mwisho wake wa kumwabudu Mungu na ataingia mgogoro mkubwa sana na Mungu uliojaa visasa . Ebu fikilia siku mifugo yako ikipewa utambuzi kwamba umeifuga ili uichinje tu au uiuze. Najua unajua nini kitakachotokea.
Wazee nawaambia ukweli sisi ni mifugo tu tunaoliwa na Mungu au na Shetani. Dhima kuu ya sisi kuwepo hapa duniani ni kuwa kitoweo cha Mungu au Shetani. Ndiyo maana tupo tupo tu bila mwelekeo wowote. Achana na story za kwenye biblia ni saundi tupu.
Kubisha ruksa kwani hata kuku anaweza akabisha huwa haliwi na binadamu.
Tunaonewa sana.