Tunaonewa sana

Tunaonewa sana

Kwa Hadi Putin ni Mfugo? Ila mifugo sisi Tunatofautiana Akili,Angalia wewe Ulivyo Mkorofi...
 
....mifugo ya Mungu au shetani...
Kwa nadharia hiyo kuku,mbuzi n.k ni mifugo ya binadamu au mwewe au fisi.
Kwa nini ukipe umiliki kitu ambacho hakiangaiki na mfugo husika?
Nasubiri jibu toka kwako wewe mfugo wa shetani.
 
Yaani ulikuwa unakuja na hoja jengefu sana ila ulipofika tu hapa nikakata tamaa na somo lako....


"Na siku binadamu akijua kwanini yupo hapa duniani ndiyo utakuwa mwisho wake wa kumwabudu Mungu na ataingia mgogoro mkubwa sana na Mungu uliojaa visasa....:"

Huyu unayemuita Mungu "Allah" ametuleta hapa dunianj kwa lengo moja tu ... kumuabudu yeye pekee..

Tukimuabudu Allah basi kuna malipo kesho tutakapokufa

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
I bet Allah na Mungu ni tofauti,ko inabid ujue unamwabudu nani kati ya Allah na Mungu na yupi atakupeleka nchi ya ahadi
 
Tafadhali msaada:-kwa nini asilimia kubwa kama sio wote wanaopinga uwepo wa MUNGU ni wakristo
...sijatoka nje ya mada wazo hili ni baada ya kusoma hii nyuzi
 
Haha sijui umewaza nini kwa hilo nalitafakari pia lingine kuwa je the biggest Scam in the world ni Ajira?
Yaani unafanya kazi miaka 40 halafu bado masikini tu

Kuna uhusiano wowote na KULIWA?
 
Habari zenu mifugo ya Mungu na Shetani? Naona mnazidi kusukuma siku mkingoja kuliwa tu.

Nimegundua kitu kuwa kila kinachofugwa huwa akiruhususiwi kujua dhima na dhamira ya yule aliyekifuga.

Yaani ni hivi binadamu hata afanye nini hatoweza kujua dhamira na dhima ya yeye kufugwa hapa duniani.

Kama ilivyo kwa kuku na ng'ombe, hata wafanye nini hawatoweza kamwe kujua dhamira na dhima ya wao kufugwa na binadamu.

Ebu fikiria Kuku, ng'ombe na mbuzi wanatuchukuliaje sisi binadamu?

Wanatuona sisi ni msaada mkubwa sana kwao, kwani tunawapa msaada mkubwa sana. Ikiwepo sehemu ya kulala, tunawapa chakula, tunawatibu magonjwa. Wanaamini bila ya sisi wao si lolote wala chochote. Kwani tunawaepusha na majanga mbalimbali ikiwepo kuliwa na paka, mbwa n.k.

Kama wewe unavyoamini Mungu ni msaada mkubwa sana kwako na yeye ndiye mwanzo na mwisho kwako. Kwasababu tu anakupa uhai, anakupa riziki, anakuponya magonjwa ukiumwa na anakuepusha na majanga mbalimbali.

Kama ilivyofungwa akili ya kuku na ng'ombe juu ya dhamira kuu ya wao kufugwa na binadamu hivyo ndivyo ilivyofungwa akili ya binadamu kujua dhima kuu ya kwanini wapo hapa duniani.

Na siku binadamu akijua kwanini yupo hapa duniani ndiyo utakuwa mwisho wake wa kumwabudu Mungu na ataingia mgogoro mkubwa sana na Mungu uliojaa visasa . Ebu fikilia siku mifugo yako ikipewa utambuzi kwamba umeifuga ili uichinje tu au uiuze. Najua unajua nini kitakachotokea.

Wazee nawaambia ukweli sisi ni mifugo tu tunaoliwa na Mungu au na Shetani. Dhima kuu ya sisi kuwepo hapa duniani ni kuwa kitoweo cha Mungu au Shetani. Ndiyo maana tupo tupo tu bila mwelekeo wowote. Achana na story za kwenye biblia ni saundi tupu.

Kubisha ruksa kwani hata kuku anaweza akabisha huwa haliwi na binadamu.

Tunaonewa sana.
Kitoweo !!!! Yaaani shetani au mungu anatukula sisi????
 
Wakati nikiwa mdogo nilikua nawaangalia kuku wakiwa bandani nikawa nashangaa sana. Nilikua najiuliza, kwanini hawa kuku kila siku wanaona tunamchukua mmoja wao na kumchinja, lakini hawa wanaobaki hawashtuki wala hawakimbii? Nikawa nashangaa kuku wanafunguliwa asubuhi lakini jioni wanarudi tena wenyewe bandani, kwanini wasikimbie?

Baadae nikaja kugundua kua kumbe hata sisi binadamu hatuna tofauti yoyote na kuku walioko bandani. Anaetufuga kila siku anakamata baadhi yetu na kuwachinja, lakini sisi wengine tupo tu.. hatuna cha kufanya, hatuna pa kukimbilia ni sawa tu na kuku walioko bandani. Kila mmoja wetu anasubiria zamu yake ya kuchinjwa ifike.
nacheka lakini naogopa
 
Kwahiyo mwanangu umeona tujilinganishe akili na kuku au ng'ombe dah!🙌 sasa tungekuwa na akili sawa tungekula nyama kweli? Tofauti ni kwamba hadi umeweza kulijua hilo basi ni dhahiri kuwa una uwezo mkubwa wa kufikiri na kuchanganua mambo kwa akili kimwili ila kuna mambo yapo kiroho zaidi ili uweze kuyapatia majibu unapaswa kumjua mungu kwanza ndipo ujue lengo lake.
 
Ninachoona,
Mungu ndo mfugaji mwenyewe mkuu na mwenye Mali, THE BIG BOSS.

Alimuweka shetan kama mmoja wapo wa wachungaji amsaidie kuchunga mifungo yake.

Nnahisi Kuna namna walizurumiana kwenye ubia wao, na shetan akaondoka na Siri kadhaa khs mifugo wa boss wake.

Ili kumkomoa ex-boss wake,
Ndo Pale edeni shetani Alikua kwenye harakati za kumsnitch na kumkomoa boss kwa kutupa uelewa (kutulelekeza tule tunda na mengineyo) ili kugain trust yetu tuondoke mle bandani,

Ila sio kwamba lengo Ni tuondoke mle bandani tukajitegemee, Bali tuhamie kwake maana na keshaanzisha zizi jipya halina wadau (kambi ya shetani).

Sasa bahat mbaya akachelewa na mfugaji akaingilia Kati na akarudishia komeo la Banda.

Ndo tukaishia kujigundua tuko uchi,kabla ya hapo tulikua hatujioni uchi Kama ilivyo kuku na ng'ombe.

Laiti Kama shetani angeendelea kumchombeza Eva, Kisha Adam.

Hakika tungeweza kuchomoka kabisa bandani maana Kuna mstari nakumbuka shetani alisema tungemsikiliza tusingekufa "tusingechinjwa"

Na kwa hasira
Mfugaji mkuu akahisi Kuna baadhi ya Siri tushazigundua, akaamua kutufukuza kwenye zizi zuri na lililokua karibu nae akatutupa duniani mbali naye ili tusije tukaendelea kuyajua mengi zaidi.
 
Wakati nikiwa mdogo nilikua nawaangalia kuku wakiwa bandani nikawa nashangaa sana. Nilikua najiuliza, kwanini hawa kuku kila siku wanaona tunamchukua mmoja wao na kumchinja, lakini hawa wanaobaki hawashtuki wala hawakimbii? Nikawa nashangaa kuku wanafunguliwa asubuhi lakini jioni wanarudi tena wenyewe bandani, kwanini wasikimbie?

Baadae nikaja kugundua kua kumbe hata sisi binadamu hatuna tofauti yoyote na kuku walioko bandani. Anaetufuga kila siku anakamata baadhi yetu na kuwachinja, lakini sisi wengine tupo tu.. hatuna cha kufanya, hatuna pa kukimbilia ni sawa tu na kuku walioko bandani. Kila mmoja wetu anasubiria zamu yake ya kuchinjwa ifike.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom