Wacha nikarudie haka kacomenti kangu pia;
Poa ngoja tuamue kutembea na hiyo nadharia yako bila kupinga;
Tuongeze nadharia ya mfano kwamba labda mchicha ukiula wewe binadamu, mchicha unakuwa sehemu ya binadamu na unafaidi ile experience ya kuwa binadamu. Utaishi nyumba nzuri utaendesha magari etc
Mchicha hautapenda kuliwa na mbuzi kwa sababu ona experience ya kuwa mbuzi sio tamu kivile, analala sehemu chafu, anapigwa jua,hathaminiwi etc. Kwa hiyo bora mchicha uliwe na binadamu na sio mbuzi. Uuexperience ubinadamu na sio umbuzi.
Kwani we unajuaje kwa nini ukila mchicha unaona zaidi? Ni kwa sababu mchicha ukiingia mwilini mwingi unajaa kwenye macho kwanza baadae ndo uende na kwingine. Kama tu ambavyo mshamba mwingine yeyote[toka shamba] <'pun intended'😂🤣🤣🤣🤣> akifika mjini au sebuleni ni macho ndo yanakuwa active zaidi! Kwa hiyo ndugu hata kama mchicha kiukweli ukawa hauna uwezo huo[kiuelewa/akili].
Tambua kwamba kwa binadamu ndivyo ilivyo, tumeumbwa na uelewa na utambuzi kujitambua na kutambua. Ukiliwa na Mungu utauexperience umungu[uhai],upendo, amani, uzuri, ukweli vyote utafaidi LAKINI ukiliwa na shetani utauexperience ushetani[kifo], chuki, taabu, ubaya machukizo.
Chagua sasa kuja kuliwa na Mungu na utafaidi milele pale utambuzi/consciousness wako utakuwa makaoni pa Mwenyezi Mungu.