Watu wengine akili zenu hamzishughulishi hata kidogo yaani lawama mpaka mnaboa Kiukweli wewe unadharau hatua ya serikali kutoa elim bure? Jiulize ni watoto wangapi ambao walikosa haki ya kusoma kwa sababu ya michango ya shule? Je, ukianza na wewe mwenyewe, umechangia kipi kusaidia kila mnyonge anapata hii haki ya kibinadam?
Elewa kuwa kila jambo lina changamoto zake, pia jua kuwa mara tu baada ya kutangazwa elimu bure idadi kubwa ya watoto kuanzia ngazi ya elimu ya msingi mpaka sekondari kwa wanaojiunga imeongezeka pia hivyo kuleta changamoto ya madawati, vitabu, madarasa, waalim n.k, hatua ya serikali kutoa elimu bure ni ya kuungwa mkono na sio kulaumulaum bila mantiki, wewe umesaidia nini kuwezesha hata watoto maskini wapate haki hii? Au wewe unaona serikali iache kutoa elimu bure? Nchi hii ni yetu lawama zingine hazijengi tuungane pamoja kusaidia hatua hii kwenda mbele ili kila mtoto apate haki hii.