Tunaadhimisha miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania au wa Tanganyika?

  1. Tanganyika ndio nchi iliyopata uhuru wake, 9 Desemba, 1961. 1964 Tanganyika ikaungana na Zanzibar kwa muungano wa union wa nchi mbili kuwa nchi moja, hivyo tulipoungana, tuliitwa Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, jina la Tanzania lilikuja mwezi September 1964.
  2. Ile siku tunaungana, utaifa wa Jamhuri ya Tanganyika (sovereignty) na utaifa wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, zote zilikwisha, na kuwa sio nchi tena, hiyo sovereignty ilikabidhiwa kwa nchi mpya ya Tanganyika na Zanzibar.
  3. Tanzania nayo pia ilipitishwa rasmi kule UN kama Taifa huru, la Jamuhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mnamo tarehe 14 May, 1964 kufuatia kuwasilishwa kwa taarifa rasmi ya maandishi, Note Verbale toka kwa Balozi wa Tanganyika kwenye Umoja wa Mataifa, wakati huo, Chief Arasto Mang'enya na kuitambulisha United Republic of Tanganyika and Zanzibar. Wakati huo, jina la Tanzania halijaanza kutumika. Mwezi June Balozi Mang'enya aliteuliwa rasmi kuwa balozi wa kudumu wa Jamhuri ya Tanganyika na Zanzibar kwenye Umoja wa Mataifa, na mwezi September ndipo akawasilisha rasmi hati zake za utambulisho na jina rasmi la United Republic of Tanzania kuwasilishwa UN.
  4. Nchi ikiishapoteza sovereignty inakuwa sio nchi tena, hivyo baada ya kupatikana jina la Tanzania, jina la Tanganyika likafutwa, likafa, likazikwa. Eneo la iliyokuwa Tanganyika sasa ndio Tanzania Bara, na iliyokuwa Zanzibar iliendelea kuitwa Tanzania Visiwani, au Tanzania Zanzibar kwa jina ila sio nchi.
  5. Sasa kwa vile Tanganyika haipo, tunaposhereherekea uhuru ni kumbukumbu ya uhuru wa Tanganyika, ila inayosherekewa ni shrehe ya Tanzania iliyopo na sio maadhimisho ya sherehe ya uhuru wa Tanzania, kumbukumbu ndio ya Tanganyika lakini maadhimisho ni ya Tanzania.
 
Kwanza kabisa nchi bado haijapata uhuru. Tupo chini ya mkoloni mwingine anaitwa CCM. Tukijikomboa kutoka kwa huyu ndiyo tutaanza kuhesabu miaka ya uhuru
 
Kiukweli somo la historia linahitajika kwa wenzetu wengi humu. Haujui kuwa mipaka mingi ya bara letu la Afrika imewekwa na wakoloni baada ya ule mkutano wa Berlin wa mwaka 1884?. Katafute historia ya pre colonial Africa kabla ya ujio wa wakoloni, ndipo urejee hapa.

P
Wakati huo kulikuwa na German East Africa siyo Tanganyika. Tanganyika ilianza rasmi na ilikuwa chini ya Waingereza kutokana na League of Nations Mandate ya 1920. Nyerere aliitupa chooni kama kinyesi halafu akai flashi Tanganyika mwaka 1964.
 
Kwanza kabisa nchi bado haijapata uhuru. Tupo chini ya mkoloni mwingine anaitwa CCM. Tukijikomboa kutoka kwa huyu ndiyo tutaanza kuhesabu miaka ya uhuru
Ni kweli Tanzania haijawahi kupata uhuru, iliyopata uhuru ilikuwa ni Tanganyika chini ya chama cha TANU.

Labda unataka kutuambia Tanzania itafute uhuru kama ambavyo Tanganyika ilivyotupatia uhuru enzi hizo.
 
Sawa Ni Uhuru wa Tanganyika mgeni rasmi anatakiwa kuwa waziri mkuu Kassim Majaliwa sababu Uhuru wa nchi hizi mbili sio Jambo la muungano .Raisi wa muungano hayamhusu .Yeye anatakiwa kuwa mgeni rasmi sherehe ya muungano tu na sio sherehe ya Uhuru wa Tanganyika au Zanzibar

Una hoja
Kwahyo waziri mkuu sio wa muunganoHUNA AKILI
 
Duuh tarehe 9/12/1961 nchi gani ilipata uhuru Tanganyika au Tanzania?
Unaposema Tanganyika doesn't exit labda kichwani mwako, uko shule mlenda kusomea ujinga
Tanganyika ndyo Tanzania bara ya sasa, shida ulikua chooni wakati wenzio wanasoma history
 
Tanganyika Nyerere aliiflashi chooni mwaka 1964. Haipo tena. Angalia kwenye Atlas leo, Tanganyika haipo tena, angalia Google maps huoni Tanganyika.
Kwahiyo Tanzania ilipata uhuru 1961??? Hebu jiongeze kiakili.
 
Mbona mnatuchanyanya hivi mkisema Miaka 60 ya UHURU wa TANZANIA mnakusudia hii Tanzania iliyozaliwa 64 au kuna nyengine?

Hivi waandishi wa habari na wanasiasa mnaosema UHURU WA TANZANIA hivi kweli hamjui historia yenu? Kwanini munainyanyapaa TANGANYIKA kiasi hiki?

Historia itabakia ni historia tuu hata mkitumia nguvu kiasi gani kuipotosha

Au Mimi ndio sifahamu haya mambo? Kama NI hivyo nielewesheni ni Tanzania gani iliyopata UHURU 1961?

Ni haya tu
Ccm ndo ilipata Uhuru, Tanzania bado. Ccm ikitokea wakaja kutolewa madarakani huo ndo Uhuru kamili wa Tanzania
 
Kwahyo waziri mkuu sio wa muunganoHUNA AKILI
Kiutendaji sio wa muungano Ni wa Tanzania bara tu.Shughuli zake hazigusi Zanzibar Hana sauti kule

Hawezi mfokea au mfanyie chochote mkuu wa Mkoa au wilaya wa Zanzibar

Huyo ndie kiongozi wetu wa Tanganyika
 
Tunaadhimisha miaka 60 ya uhuru wa Tanzania, japo iliyopata uhuru ni Tanganyika. Kwa vile Tanganyika doesn't exist anymore, kilichopo ni Tanzania.
P
Tanzania haikuwahi kupata uhuru hivyo hakuna mantiki ya kusheherekea kumbukumbu ya uhuru wake.

Pia unapaswa kufahamu kuwa Tanzania na Tanganyika ni nchi mbili tofauti hata kama kihistoria zinahusiana.

Mwisho unapaswa kufahamu kuwa; Tanganyika haikuwahi kubadilishwa jina ili iitwe Tanzania, bali Tanzania ni jina la nchi mpya iliyoundwa mwaka 1964.
 
Kiutendaji sio wa muungano Ni wa Tanzania bara tu.Shughuli zake hazigusi Zanzibar Hana sauti kule

Hawezi mfokea au mfanyie chochote mkuu wa Mkoa au wilaya wa Zanzibar

Huyo ndie kiongozi wetu wa Tanganyika
Uko sahihi kabisa.
 
Kabisaaa brother Pascal?? Uhuru wa Tanzania Ni Miaka 60???
Kwani Tanzania ilipata Uhuru lini?
Tanzania ilipata uhuru tarehe 9 Desemba 1961, wakati huo ikiitwa Tanganyika, hivyo tunavyosherehekea, tunafanya mambo mawili, jambo la kwanza ni kumbukizi, kumbukizi ni kumbukumbu ya uhuru wa Tanganyika. Jambo la pili ni kusherehekea, tunasherehekea siku ya uhuru wa Tanzania Bara, kwa kivupi Tanzania.
P
 
Ni Uhuru wa Tanzania bara

Jina lilibadlishwa kisheria kuwa Tanzania Kama wewe unavyoweza badili jina tukasema Leo birthday ya Juma jina lako jipya baada ya kuslimu ukubwani na kubadili jina la asili la Chapombe na kuitwa Juma badala ya kuendelea nalo jina la Chapombe msikitini

Ni Uhuru wa Tanzania bara

Ila Zanzibar huwa hawataki Hilo wao huadhimisha uhuru.wa Zanzibar sio wa Tanzania visiwani!

Linatakiwa kuongeza neno bara nyuma kuwa ni uhuru wa Tanzania bara
Unapaswa kufahamu kuwa hakuna nchi inaitwa Tanzania bara, na haijawahi kutokea hiyo nchi hapa duniani. Tanzania bara sio nchi ni neno tu la kuelezea eneo la nchi kavu katika jamhuri ya muungano. Hivyo hatuwezi kusheherekea uhuru wa nchi ambayo haikuwahi kuwepo na haipo popote.
 
Tanganyika haikuwahi kubadilishwa jina ili iitwe Tanzania, bali Tanzania ni jina la nchi mpya iliyoundwa mwaka 1964.
All the facts are right, ni katika kuelimishana, baada ya Tanzania kuwa ni jina la nchi mpya iliyoundwa mwaka 1964, baada ya muungano, then nchi ya Tanganyika, ambayo haikuwahi kubadili jina, ilikwenda wapi?. Kwa faida yako na wengine kama wewe, baada ya Muungano, nchi iliyokuwa Tanganyika, ilibadili jina na kuwa Tanzania Bara, na nchi iliyokuwa Zanzibar ilibadili jina na kuwa Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar. Nchi hizi zote mbili zinatumia majina ya kifupi kwa Tanzania Bara kuitwa Tanzania na Tanzania Zanzibar kuitwa Zanzibar, ila the official name ya Tanzania kama nchi inaitwa JMT.
P
 
Tanzania ilipata uhuru tarehe 9 Desemba 1961, wakati huo ikiitwa Tanganyika, hivyo tunavyosherehekea, tunafanya mambo mawili, jambo la kwanza ni kumbukizi, kumbukizi ni kumbukumbu ya uhuru wa Tanganyika. Jambo la pili ni kusherehekea, tunasherehekea siku ya uhuru wa Tanzania Bara, kwa kivupi Tanzania.
P
Pascal Mayalla huo uhuru wa Tanzania ulitokeaje mwaka 1961 wakati nchi ya Tanzania iliundwa 1964?
Pili, nchi ya Tanganyika haikuwahi kubadilishwa jina kuwa nchi ya Tanzania au Tanzania bara.

Mpaka leo hii, historia zote rasmi za waingereza zinatamka kuwa, taifa la uingereza liliacha Tanganyika kuwa nchi huru mwaka 1961.

Tusilazimishe Tanganyika kuwa ndio Tanzania.
 
Pascal Mayalla huo uhuru wa Tanzania ulitokeaje mwaka 1961 wakati nchi ya Tanzania iliundwa 1964?
Pili, nchi ya Tanganyika haikuwahi kubadilishwa jina kuwa nchi ya Tanzania au Tanzania bara.

Mpaka leo hii, historia zote rasmi za waingereza zinatamka kuwa, taifa la uingereza liliacha Tanganyika kuwa nchi huru mwaka 1961.

Tusilazimishe Tanganyika kuwa ndio Tanzania.
Mkuu Zanzibar-ASP , ni mambo ya kuelimishana tuu,
karibu pande hizi
Na kwa faida ya wavivu kufata link, nawawekea contents.
  1. Ili taifa lolote liweze kuwepo, ule tuu uwepo wake wa being, likiwa na eneo na mipaka inayotambulika, ni tayari taifa hilo lipo, litambulike au lisitambulike, linakuwa lipo tuu, ila lisipotambulika, linakuwa japo lipo, ila ni lipo lipo tuu!. Hivyo Tanzania kama taifa, japo lipo kuhalali, kisheria Taifa la Tanzania lipo lipo tuu!.
  2. Ili taifa lolote liwepo kihalali kwa kisheria (de jure) au isivyo kihalali kisheria lakini lipo (de factor) taifa hilo lazima lijitambulishe Umoja na Mataifa na umoja huo ulipitishe rasmi kama Taifa.
  3. Tanzania nayo pia ilipitishwa rasmi kule UN kama Taifa huru, la Jamuhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mnamo tarehe 14 May, 1964 kufuatia kuwasilishwa kwa taarifa rasmi ya maandishi, Note Verbale toka kwa Balozi wa Tanganyika kwenye Umoja wa Mataifa, wakati huo, Chief Arasto Mang'enya na kuitambulisha United Republic of Tanganyika and Zanzibar. Wakati huo, jina la Tanzania halijaanza kutumika. Mwezi June Balozi Mang'enya aliteuliwa rasmi kuwa balozi wa kudumu wa Jamhuri ya Tanganyika na Zanzibar kwenye Umoja wa Mataifa, na mwezi September ndipo akawasilisha rasmi hati zake za utambulisho na jina rasmi la United Republic of Tanzania kuwasilishwa UN.
  4. Hii ni taarifa rasmi ya UN kuhusu kuungana kwa mataifa -MERGER OF MEMBER STATES, during the period under review, the issue of the merger of Member States arose in the United Nations in connexion with the formation of the United Republic of Tanganyika and Zanzibar, later called the United Republic of Tanzania. Tanganyika and Zanzibar, which had been admitted in the United Nations since 14 December 1961 and 16 December 1963 respectively, informed the Secretary-General by a note verbale dated 6 May 1964 of the following:
  5. Hiki ndicho kilichokuwemo ndani ya Note Verbale ile
    " . . . the Republic of Tanganyika and the People's Republic of Zanzibar were united as one Sovereign State on 26 April 1964, under the name of the United Republic of Tanganyika and Zanzibar and under the presidency of Mwalimu Julius K. Nyerere. A copy of the said Articles of Union is enclosed herewith.
    "The Secretary-General is asked to note that the United Republic of Tanganyika and Zanzibar declares that it is now a single Member of the United Nations bound by the provisions of the Charter, and that all international treaties and agreements in force between the Republic of Tanganyika or the People's Republic of Zanzibar and other States or international organizations will, to the extent that their implementation is con- sistent with the constitutional position established by the Articles of Union, remain in force within the regional limits prescribed on their conclusion and in accordance with the principles of international law."
  6. On 14 M a y , the Secretary-General, at the request of the Government of the United Republic of Tanganyika and Zanzibar, communicated the note to all States Members of the United Nations, to the principal organs of the United Nations and to the subsiding organs of the United Nations to which Tanganyika or Zanzibar had been appointed or admitted, and to the specialized agencies and to the International Atomic Energy Agency, by a note verbale which included the following statement:
  7. Hili ndilo Tamko la Katibu Mkuu wa UN wakati huo, kulitangaza rasmi taifa la Tanganyika and Zanzibar (Tanzania) "The Secretary-General is taking action, within the limits of his administrative responsibilities, to give effect to the declaration in the attached note that the United Republic of Tanganyika and Zanzibar, is now a single Member of the United Nations bound by the provisions of the Charter. This action is undertaken without prejudice to and pending such action as other organs of the United Nations may take on the basis of the notification of the establishment of the United Republic of Tanganyika and Zanzibar."
  8. Hivyo majina ya nchi iliyokuwa Jamhuri ya Tanganyika, na Jamhuri ya Watu wa Zanzibar yalifutwa rasmi kwa a merge na kugeuka nchi moja ya JMT!.
P
 
All the facts are right, ni katika kuelimishana, baada ya Tanzania kuwa ni jina la nchi mpya iliyoundwa mwaka 1964, baada ya muungano, then nchi ya Tanganyika, ambayo haikuwahi kubadili jina, ilikwenda wapi?. Kwa faida yako na wengine kama wewe, baada ya Muungano, nchi iliyokuwa Tanganyika, ilibadili jina na kuwa Tanzania Bara, na nchi iliyokuwa Zanzibar ilibadili jina na kuwa Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar. Nchi hizi zote mbili zinatumia majina ya kifupi kwa Tanzania Bara kuitwa Tanzania na Tanzania Zanzibar kuitwa Zanzibar, ila the official name ya Tanzania kama nchi inaitwa JMT.
P
Mmmh!
Lazima hapo nitofautiane na wewe.
Nature ya muungano wa nchi mbili tuliofanya 1964, ulipelekea mambo matatu tu.
1. Kuundwa kwa taifa moja jipya lililopewa jina jipya la Tanzania. (Hivyo Tanzania ni nchi mpya na jina jipya).

2. Kuundwa kwa serikali mbili ndani ya taifa moja la Tanzania (yaani serikali ya muungano na serikali ya Zanzibar)

3. Kufa kwa nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar AU Kuendelea kuwepo (kihistoria) kwa nchi za Tanganyika na Zanzibar mbili zilizokufa!

Kwa kifupi sana Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964 ili kuunda nchi mpya ya Tanzania, iliziua nchi zote mbili, Tanganyika ilizikwa siku ile ile na Zanzibar japokuwa nayo ilikufa siku ile lakini ikagoma kuzikwa, na mara kadhaa imepambana kufufuka (na ikafanikiwa!) japokuwa iko mahututi.
 
Mmmh!
Lazima hapo nitofautiane na wewe.
Nature ya muungano wa nchi mbili tuliofanya 1964, ulipelekea mambo matatu tu.
1. Kuundwa kwa taifa moja jipya lililopewa jina jipya la Tanzania. (Hivyo Tanzania ni nchi mpya na jina jipya).

2. Kuundwa kwa serikali mbili ndani ya taifa moja la Tanzania (yaani serikali ya muungano na serikali ya Zanzibar)

3. Kufa kwa nchi mbili za Tanganyika na Zanzibar AU Kuendelea kuwepo (kihistoria) kwa nchi za Tanganyika na Zanzibar mbili zilizokufa!

Kwa kifupi sana Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mwaka 1964 ili kuunda nchi mpya ya Tanzania, iliziua nchi zote mbili, Tanganyika ilizikwa siku ile ile na Zanzibar japokuwa nayo ilikufa siku ile lakini ikagoma kuzikwa, na mara kadhaa imepambana kufufuka (na ikafanikiwa!) japokuwa iko mahututi.
ZANZIBAR haipo mahututi na kila leo inazidi kuwa strong kuliko Jana kikazi kipya ni kiazi cha kuhoji hamuezi kutuletea Stori za kina karume
 
Back
Top Bottom