Parabolic
JF-Expert Member
- Dec 3, 2013
- 2,743
- 2,600
Tume ya Afrika kuhusu Haki za Binadamu na Watu (ACHPR), imeeleza wasiwasi wake kwa Tanzania kuhusu kukiuka haki za binadamu, hususani uzimaji wa intaneti wakati wa kuelekea kwenye uchaguzi mkuu Oktoba 2025.
Azimio kuhusu Hali ya Haki za Binadamu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililotolewa Agosti 6, 2025 lililotokana na kikao cha ACPHR cha 84 cha Kawaida, kilichofanyika kwa njia ya mtandao, limetaja matukio ya uvunjifu wa haki za binadamu yakiwemo madai ya kunyanyaswa kwa wanaharakati wa Kenya na Uganda waliohudhuria kesi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Mei 19, 2025.
"Ikiwa na wasiwasi zaidi kuhusu vikwazo katika upatikanaji wa taarifa, uhuru wa vyombo vya habari na uhuru wa kujieleza nchini Tanzania, ikiwemo kuzuiwa kwa mitandao ya kijamii kama X (zamani Twitter) tarehe 04 Juni 2025, pamoja na kuzuiwa kwa upatikanaji wa Youtube (baadhi ya maudhui), na kutofikika kwa Clubhouse na Telegram bila kutumia mitandao ya kibinafsi (VPN).
Katika hilo ACHPR imerejea azimio lake 580(LXXVIII) 2024 kuhusu Kuzimwa kwa Mtandao na Uchaguzi barani Afrika, ambalo linazitaka Nchi Wanachama kuchukua hatua za kisheria na nyingine zinazofaa kuhakikisha upatikanaji wa intaneti ulio wazi na salama kabla, wakati na baada ya uchaguzi, ikiwemo kuhakikisha kuwa watoa huduma za mawasiliano na intaneti wanachukua hatua madhubuti kutoa huduma bila vikwazo wala kukatizwa;
ACPHR pia imeeleza wasiwasi wake kuhusu taarifa za ukandamizaji wa maandamano na mikusanyiko mingine ya umma kwa nguvu, ikiwemo tukio la tarehe 09 Aprili 2025 kufuatia kukamatwa kwa Bw. Tundu Lissu, na tukio la tarehe 24 Aprili 2025 katika Mahakama ya Kisutu ambapo viongozi wa upinzani na wafuasi wao walizuiwa kuhudhuria kesi ya Bw. Lissu;" imesemantaarifa hiyo.
Pia imeeleza wasiwasi wake kuhusu tuhuma za kupotezwa kwa watu kwa nguvu, mateso, na ukamataji kiholela, ambazo zimekashifiwa na wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa, Bunge la Ulaya, na wadau wengine.
"Ikilaani vikali taarifa za kufukuzwa nchini kwa aliyekuwa Waziri wa Sheria na aliyekuwa Jaji Mkuu wa Kenya pamoja na timu yao tarehe 18 Mei 2025, pamoja na kuwekwa kizuizini bila sababu za kisheria na kunyanyaswa kwa wanaharakati wa haki za binadamu kutoka Uganda na Kenya, ambao walifukuzwa nchini tarehe 19 Mei 2025 bila kupewa nafasi ya kukata rufaa au kusikilizwa na mahakama."
ACPHR imeitaka Tanzania kutambua wajibu wake katika Mkataba wa Afrika na mikataba mingine ya kikanda na kimataifa ya haki za binadamu ambayo imeiridhia.
Imeitaka kuheshimiwa kwa viwango vya haki za binadamu vya kikanda na kimataifa kwa ujumla, na hasa kuhusiana na uchaguzi uliopangwa kufanyika mwezi Oktoba 2025;
"Kufanya uchunguzi wa kina kuhusu taarifa za ukiukwaji wa haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na kupotezwa kwa watu kwa nguvu, mateso, ukamataji kiholela, na ukandamizaji wa maandamano na mikusanyiko mingine ya umma;
"Kuhakikisha uhuru wa kujieleza na upatikanaji wa taarifa katika kipindi cha uchaguzi, ikiwa ni pamoja na kutoa huduma ya intaneti bila vikwazo wala kukatizwa;
"Kuweka mazingira rafiki yanayowezesha kufanyika kwa uchaguzi wa amani, huru, wa haki na wa uwazi, ili kuruhusu wananchi kutumia haki yao ya kupiga kura katika mazingira yasiyo na vitisho, vurugu, au kikwazo chochote;
"Kuhakikisha ulinzi wa watetezi wa haki za binadamu na wanaharakati nchini Tanzania, na kuchunguza taarifa zote za ukiukwaji wa haki dhidi yao;
"Kufanya uchunguzi kuhusu taarifa za kuwekwa kizuizini na kunyanyaswa kwa wanaharakati wa haki za binadamu kutoka Uganda na Kenya, kwa lengo la kuwabaini na kuwafikisha mahakamani wahusika wa ukiukwaji huo na kuhakikisha fidia kwa waathirika kwa wakati muafaka.
"Kutekeleza mabadiliko ya kikatiba na kisheria yaliyotolewa na Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu, ikiwa ni pamoja na kuruhusu wagombea binafsi kushiriki katika uchaguzi, na kuhakikisha mahakama za kitaifa zina mamlaka ya kushughulikia migogoro ya uchaguzi."
Azimio kuhusu Hali ya Haki za Binadamu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania lililotolewa Agosti 6, 2025 lililotokana na kikao cha ACPHR cha 84 cha Kawaida, kilichofanyika kwa njia ya mtandao, limetaja matukio ya uvunjifu wa haki za binadamu yakiwemo madai ya kunyanyaswa kwa wanaharakati wa Kenya na Uganda waliohudhuria kesi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Mei 19, 2025.
"Ikiwa na wasiwasi zaidi kuhusu vikwazo katika upatikanaji wa taarifa, uhuru wa vyombo vya habari na uhuru wa kujieleza nchini Tanzania, ikiwemo kuzuiwa kwa mitandao ya kijamii kama X (zamani Twitter) tarehe 04 Juni 2025, pamoja na kuzuiwa kwa upatikanaji wa Youtube (baadhi ya maudhui), na kutofikika kwa Clubhouse na Telegram bila kutumia mitandao ya kibinafsi (VPN).
Katika hilo ACHPR imerejea azimio lake 580(LXXVIII) 2024 kuhusu Kuzimwa kwa Mtandao na Uchaguzi barani Afrika, ambalo linazitaka Nchi Wanachama kuchukua hatua za kisheria na nyingine zinazofaa kuhakikisha upatikanaji wa intaneti ulio wazi na salama kabla, wakati na baada ya uchaguzi, ikiwemo kuhakikisha kuwa watoa huduma za mawasiliano na intaneti wanachukua hatua madhubuti kutoa huduma bila vikwazo wala kukatizwa;
ACPHR pia imeeleza wasiwasi wake kuhusu taarifa za ukandamizaji wa maandamano na mikusanyiko mingine ya umma kwa nguvu, ikiwemo tukio la tarehe 09 Aprili 2025 kufuatia kukamatwa kwa Bw. Tundu Lissu, na tukio la tarehe 24 Aprili 2025 katika Mahakama ya Kisutu ambapo viongozi wa upinzani na wafuasi wao walizuiwa kuhudhuria kesi ya Bw. Lissu;" imesemantaarifa hiyo.
Pia imeeleza wasiwasi wake kuhusu tuhuma za kupotezwa kwa watu kwa nguvu, mateso, na ukamataji kiholela, ambazo zimekashifiwa na wataalamu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa, Bunge la Ulaya, na wadau wengine.
"Ikilaani vikali taarifa za kufukuzwa nchini kwa aliyekuwa Waziri wa Sheria na aliyekuwa Jaji Mkuu wa Kenya pamoja na timu yao tarehe 18 Mei 2025, pamoja na kuwekwa kizuizini bila sababu za kisheria na kunyanyaswa kwa wanaharakati wa haki za binadamu kutoka Uganda na Kenya, ambao walifukuzwa nchini tarehe 19 Mei 2025 bila kupewa nafasi ya kukata rufaa au kusikilizwa na mahakama."
ACPHR imeitaka Tanzania kutambua wajibu wake katika Mkataba wa Afrika na mikataba mingine ya kikanda na kimataifa ya haki za binadamu ambayo imeiridhia.
Imeitaka kuheshimiwa kwa viwango vya haki za binadamu vya kikanda na kimataifa kwa ujumla, na hasa kuhusiana na uchaguzi uliopangwa kufanyika mwezi Oktoba 2025;
"Kufanya uchunguzi wa kina kuhusu taarifa za ukiukwaji wa haki za binadamu, ikiwa ni pamoja na kupotezwa kwa watu kwa nguvu, mateso, ukamataji kiholela, na ukandamizaji wa maandamano na mikusanyiko mingine ya umma;
"Kuhakikisha uhuru wa kujieleza na upatikanaji wa taarifa katika kipindi cha uchaguzi, ikiwa ni pamoja na kutoa huduma ya intaneti bila vikwazo wala kukatizwa;
"Kuweka mazingira rafiki yanayowezesha kufanyika kwa uchaguzi wa amani, huru, wa haki na wa uwazi, ili kuruhusu wananchi kutumia haki yao ya kupiga kura katika mazingira yasiyo na vitisho, vurugu, au kikwazo chochote;
"Kuhakikisha ulinzi wa watetezi wa haki za binadamu na wanaharakati nchini Tanzania, na kuchunguza taarifa zote za ukiukwaji wa haki dhidi yao;
"Kufanya uchunguzi kuhusu taarifa za kuwekwa kizuizini na kunyanyaswa kwa wanaharakati wa haki za binadamu kutoka Uganda na Kenya, kwa lengo la kuwabaini na kuwafikisha mahakamani wahusika wa ukiukwaji huo na kuhakikisha fidia kwa waathirika kwa wakati muafaka.
"Kutekeleza mabadiliko ya kikatiba na kisheria yaliyotolewa na Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu na Watu, ikiwa ni pamoja na kuruhusu wagombea binafsi kushiriki katika uchaguzi, na kuhakikisha mahakama za kitaifa zina mamlaka ya kushughulikia migogoro ya uchaguzi."