IDADI YA WAHADHIRI NA RANK ZAO
Senior Lecturers - 09
Lecturers - 12
Assistant Lecturers - 46
Ni jambo linalostua chuo kikuu kinachojinasibu kutoa PhD kinaendeshwa kwa 70% na wahadhiri wasaidizi ambao wana-hold elimu ya kiwango cha Masters, hawa ndio wanaofundisha programa za Masters. Mtu mwenye Masters anafundisha Masters program halafu mnatuambia TCU walipitia pale, waliangalia nini, Wizara iwafuatilie maafisa waliotumwa pale pengine wameshikishwa Rupia. Kile chuo kina Associate Professors watatu (03), tena wengine ni wastaafu, kina PhD holders 06 tu, Law wawili, Education wawili na wengine ni wa Theology. Unakuta Mhadhiri moja anafundisha course 6 na ole wako ukatae uaoneshwa mlango tena bila kulipwa chohote. Waziri wa Elimu mama Prof Joyce Ndalichako njoo utembele hiki chuo u-prove hizi claims elimu inauawa. Muda ujao nita-attach Timetable ya semester iliyomalozika hivi punde muone walimu wanavyofundisha masomo mengi tena mengine siyo fani zao.
- KODI YA SERIKALI ILIYOIBIWA TANGIA 1997-2018
Katika chuo Kikuu cha Tumaini Makumira Mishahara hulipwa mara 2 kwa mwezi, mwisho wa mwezi wanalipa basic salary tu. Allowances zote hulipwa katikati ya mwezi yaani kuanzia tar 15-17 ya kila mwezi. Allowances zinahusisha House allowance (200,000 – 300,000 kutegemeana na rank ya MFANYAKAZI), Transport Allowance (60,000 – 100,000), Special Faculty allowance (Tshs 550,000), na Responsibility allowance kwa wale wenye nazo ( wenye vyeo chuoni). MALIPO HAYA HUFANYWA MARA 2 KWA MWEZI kwa malengo makuu mawili:
- Kukwepa kodi za Serikali – maana malipo yote yanayofanywa katikati ya mwezi hayakatwi kodi
- Kudhulumu wahadhiri na wafanyakazi wengine mawasilisho yao kwenye mifuko ya hifadhi za jamii (NSSF na LAPF ndiyo mifuko unayoruhusiwa kujiunga ukiajiriwa Tumaini University Makumira )
- Jedwali lililoambatanishwa linaonesha idadi ya wahadhiri, rank zao, miaka waliyoajiriwa na kiasi cha allowance wanacholipwa kila mwezi ambazo hazijakatwa kodi za serikali na Jumla ya fedha zote ambazo hazijakatwa kodi.
Baada ya ukokotoaji ktk jedwali ambalo nimei-attach utaona kwamba kiasi cha Tshs
6,959,400,000 (Almost 7 Billion) ndiyo kiasi cha hela ambayo haikulipiwa kodi za Serikali tangia Chuo hiki kianzishwe mwaka 1997. Kiasi hali halisi yaweza kuwa zaidi ya haya makadirio, kilichobaki ni kwa vyombo husika vya Serikali kufutilia taarifa hizi.
B: KIASI CHA HELA AMBAYO HAIKUWASILISHWA MIFUKO YA HIFADHI ZA JAMII (NSSF & LAPF)
- Jedwali lililoambatanishwa linaonesha kiasi cha pesa ambayo chuo kimekwepa kuwasilisha ktk mifuko ya hifadhi za jamii. Ukokotoji (calulation) hufanyika kwenye basic pay tu inayokatwa na kuwasilishwa kila mwisho wa mwezi. Ukokotoaji hauhusishi allowances zinazolipwa katikati ya kila mwezi hivyo kuwadhulumu wahadhiri na wafanyakazi wengine pesheni zao mwisho wa siku. Si hivyo tu pesa hizi zilizokwepwa zingetumiwa na mifuko hii ktk shughuli mbalimbali za uwekezaji na kuinua uchumi wa nchi. Kwa kufanya hivi chuo hiki kimehujumu uchumi wa nchi yetu.
- Jedwali lililoambatanishwa linaonesha allowance kwa mwezi, asilimia inayokatwa na mfuko, miaka(wastani), miezi ktk mwaka na idadi ya wahadhiri ktk rank zao
Katika Jedwali lililoambatanishwa utaona kwa wastani kila Senior Lecturer ameibiwa na chuo kiasi cha Tshs
43,200,000/= mpaka sasa, kila Lecturer chuo kimemwibia kiasi cha
Tshs 28,800,000/= na kila Assistant Lecturer ameibiwa na chuo kiasi cha
Tshs 18,360,000/= kwa wastan mpaka sasa. Pesa ambzo hazijawasilishwa ktk mifuko ya hifadhi z jamii ni Jumla
ya Tshs 1,570,320,000/=. Hii kiasi ni makadirio tu maana data zingine hazikuwa rahisi kuzipata km zilivyo (yaani exact figures). Kiasi halisi ni zaidi ya haya makadirio. Kazi imebaki upande wa mifuko husika kuzifuatilia taarifa hizi kwa undani zaidi.