Tulipopata GPA za upper second class and above tukutane hapa

Tulipopata GPA za upper second class and above tukutane hapa

Ila walikuwaga wachache sana, ilikuwa inatulazimu kuwaona wazuri tu hata mama wabaya, maana wa CBE na IFM walikuwa wanajiona sanaaaa... kuna mmoja wa CBE nilimtoaga out, nimenlewesha kinoma, akaja jamaa akamchukua alafu demu akajidai ananikataaa .. nikaondoka kwa uchungu sana.. next day demu ananiambia yule ni kaka yake 😂😂😂😂
Achana kbs na mademu wa cbe na ifm..watamu sana!ila alikudharau sana aise🤣! Hahahaaa...tafuta hela wewe!
 
Heshima yenu wakuu.. tuliopata GPA za 3.5 na kuendelea tukutane hapa kubadilishana mawazo positively.. je GPA kubwa imekusaidia baada ya maisha ya chuoni na kwenye kutafuta riziki??? Ni zipi fursa ulizozipata na zilizokufaidisha kutokana na GPA yako kubwa?

Binafsi nilipata GPS ya 4.1 from the school of Architecture - Ardhi University. Lakini GPA haijawahi kunisaidia lolote kwenye fursa za utafutaji, maana mimi ni mjasiriamali tu.

Karibuni wadau.
GPA ya kuanzia 3.8 inaweza kukusaidia zaidi kwenye nafasi za u-lecture au kwenye vituo vya utafiti. Ila sehemu nyingine GPA yeyote Ile anaajirika bila shida. Chamsingi amefaulu interview Yao
 
Achana kbs na mademu wa cbe na ifm..watamu sana!ila alikudharau sana aise🤣! Hahahaaa...tafuta hela wewe!
mwisho wa siku tulipotezana kama miaka 9, akawaaatafuta nyumba ya kupanga, dalali akamleta kwangu bila kujua, ule msemo binadamu hukutana.. aliishiwa pozi na aibu juu .. aipoteza confidence yote.. na mie kwakua sikua naishi pale nilimuachaga rafiki yangu, nikampanganisha nikaanza jilia vitu for raha zangu nikitoka kubeba zege langu, hadi leo kapanga kwangu, sema nilisha acha kabisa hata kwenda hapo nimewaachia wazazi ndio wasiamie show.. 😂😂😂😂😂.. mtu wa Dar tech kumiliki demu CBE au IFM ilikuwa ujiko 😂😂😂 haikuwa kazi rahisi atii
 
Unawezaje kua na mashaka na taasisi kubwa kama Ardhi University??
Mkuu kwa mtu ambae amemaliza kozi kama yako miaka hyo ya 2009-2014,mbona naona kama ungekomaa ungekua vizuri, labda tu uliona ni kazi ngumu.
Mimi labda naona kama ulipata njia nyepesi ya kutengeneza pesa, ukaamua kuachana nayo, mimi nimemaliza ardhi, nafikiri mpaka sasa school inaitwa SACEM(inajumlisha architects, Engineers na Quantity surveyors).
Nikiwangalia wenzangu ambao ni Engineers,Quantity surveyors na Architects wengi washaanza tengeneza pesa japo sio nyingi ila inawasogeza vizuri.
 
ofisi niliyomo kuna gpa zote mshahara na cheo ni kilekile, mkuu wa kitengo ana lower second.

pia Kuna watu wenye first class wanaripoti kwangu na kuna watu wana second lower naripoti kwao.

maisha huku kazini ni vyeo, promosheni, n.k hizo gpa tupa kule
Makazini humu hakuna cha gpa wala kasoma uk
 
Kwa shule yangu ya chuo ilivyokuwa ngumu, hii nilionayo nimejipendelea sana. Sikustahili.

GPA yangu ndogo inanipa limit za fursa zinazohitaji GPA kubwa.

Je ninyi wenye GPA kubwa hali ikoje huko kileleni?
Unataka kua mkufunzi ? Researcher? Jambo gani hilo linakulimit sababu ya GPA?
 
Kila unacho fanya fanya ubora wa juu wa uwezo wako, kama ni kusoma soma kwa bidii kwa kiasi Cha uwezo wako na kama n kufanya biashara fanya kwa bidii vile uwezavyo
Hakuna Cha kujutia

Respect kwako mkuu kwa ujumbe huu.

Mimi nisichopendea mada za dizaini hii, na zile zinazoponda elimu kwamba kusoma sio dili, ooh kuna watu hawajasoma na wana hela nk, ni kwamba sisi wote tunaosema hivyo tayari tulishasoma na tukahitimu. Sasa tuna watoto / wadogo zetu ambao wapo shule/vyuoni sasa hivi na wengine tunawalipia ada. Wanaposoma mada kama hizi zinawavunja moyo na kuona kumbe wanapoteza muda tu vyuoni hivyo kuwafanya wasizingatie masomo.

Matokeo yake wakifeli sisi sisi tunaanza kuwaponda tena na kulalamika kwamba vijana siku izi hawapo siriaz! Wakiharibu huko maofisini tunaanza kulalamika ooh wasomi wa siku hizi hamna kitu. Kumbuka tunapozungumzia wasomi, tunazungumzia madaktari, ma pilot, wahandisi nk ambao kuna wakati tunaweka maisha yetu mikononi mwao!

Mimi watu wote mnaodharau/ponda elimu, regardless ya kwamba wewe ulisoma wapi na ulipata GPA gani chuoni, nakuona wewe ni mbumbumbu tu! Na inawezekana ndio maana elimu haijakusaidia. Huenda wewe ulienda chuoni kushiriki sio kusoma. Kwa mtu yoyote aliesoma, akaelimika, akafaulu kwa GPA kubwa, na anajua kujieleza vizuri, huwezi kukosa kazi!!
 
Heshima yenu wakuu.. tuliopata GPA za 3.5 na kuendelea tukutane hapa kubadilishana mawazo positively.. je GPA kubwa imekusaidia baada ya maisha ya chuoni na kwenye kutafuta riziki??? Ni zipi fursa ulizozipata na zilizokufaidisha kutokana na GPA yako kubwa?

Binafsi nilipata GPS ya 4.1 from the school of Architecture - Ardhi University. Lakini GPA haijawahi kunisaidia lolote kwenye fursa za utafutaji, maana mimi ni mjasiriamali tu.

Karibuni wadau.

Shule ni muhimu ila wengi wamefanikiwa kwa upigaji sehemu wanazofanya kazi.
 
GPA ya kuanzia 3.8 inaweza kukusaidia zaidi kwenye nafasi za u-lecture au kwenye vituo vya utafiti. Ila sehemu nyingine GPA yeyote Ile anaajirika bila shida. Chamsingi amefaulu interview Yao
Na mpaka uitwe kwenye hiyo interview unadhani wanachuja kwa vigezo gani?
 
Mm ndio mwalimu wao job hao wenye GPA kubwa,kila kitu wanauliza,hata cha kujiongeza tu utaulizwa,"flani hapa tunafanyaje,ikiwa hv inakuaje n.k na hapo tumeajiriwa mwaka mmoja
Kwa vyuo vyetu TZ na utoaji wa elimu vyuoni ulivyo, kuna mazingira huwa nakosa connection ya gpa vs utendaji kazi/maarifa ya mwenye hiyo gpa kubwa...
Gpa pia hutegemea umesoma chuo gani,kuna vyuo vinagawa hizo gpa kama njugu(no ku-fail kwenye mitihani,no sup,no carry over kwa wanafunzi,hata kama watakuwepo wanahesabika,haswa private institutions mf. vyuo vya kidini...
 
Back
Top Bottom