Tulioingia kwenye kilimo tukaangukia pua tukutane hapa

kabila01

JF-Expert Member
Apr 21, 2009
4,235
4,949
Naanza kwa kutoa experience yangu.

Niliingia kwenye kilimo baada ya kushawishika na vipindi vya Clouds Media kuhusiana na fursa. Presenters walishawishi sana kuwa vijana hatujitumi na hatutumii brain zetu vizuri.

Nikajitosa kwenye kilimo cha tikiti Migoli Iringa na milioni zangu 2. Nikaingia front mwenyewe sikutaka kilimo cha simu. Nilikutana na changamoto katika kulima nikapambana nazo nilikuwa nalala shamba kwenye vibanda vya nyasi, vibarua wanazingua balaa na changamoto ya madawa. Baadae nikafanikiwa kuvuna na yalikubali sana.

Mziki ukaja kwenye soko sasa. Unatoka mjini na mfanyabiashara kuja shamba kununua mzigo, mjini umeacha bei ya tikiti 1 ni elfu 4. Mfanyabiashara shamba anataka kununua tikiti 1 sh 500, nikaamua kwenda nayo mwenyewe sokoni Dodoma. Kufika pale, dah! washaambizana wafanyabiashara wao hawanunui direct kutoka kwa mkulima; wananunua kupitia madalali, ikanibidi niwakabidhi madalali mzigo. Hapo nilichoka nilirudi nyumbani na laki 4.

Nikaingia kwenye kilimo cha vitunguu Ruaha Mbuyuni. Nikapambana nacho; jani lilikubali balaa kila siku nikawa napiga picha narusha social media. Wakati wa kuvuna kuja kuchimba chini chenga tu nikaishia kuuza reja reja nikatoka na laki 7.

Nikaja kulima mahindi ya kuchoma maarufu kama Gobo. Nilipambana nayo mpaka mwisho kwenye soko tena changamoto. Mfanyabiashara anakuja kuchagua mahindi shamba anataka kununua muhindi mmoja kwa sh 120 ilihali mjini muhindi mmoja sh 500, nikaghairi kuuza nikasubiri yakauke bahati nzuri bei ya mahindi nzuri.

My take: Katika kilimo madalali na wafanyabiashara ndiyo wanaonufaika sana kuliko wakulima.
 
Usilime kwa ushawishi fanya research ya soko kwanza. Kuna dada ninamfahamu wateja wake ni foreigners. Analima carrots, cabbage, hoho, nyanya, vitunguu. Kila siku anapeleka mzigo nyumbani kwa wateja. Ana list yao kabisa akifunga jumu shillings 10,000. Hakosi 200,000-250,000 kwa siku.
 
Mkuu, pongezi ziende kwako hapo bado misimu miwili tu utakuja na ushuhuda wa kutoboa vizuri. Usikate tamaa, mi nakomaa na ufugaji saizi nafuga kuku aisee nikawa na vifaranga 60 nikaona hapa fresh ulipita gonjwa nikabaki na vifaranga 2

Sikukata tamaa leo naona matunda na natumai kuanzia sikukuu zijazo basi story itabadilika tena.
 
Mimi nililima hekari 40 za mpunga Ifakara (signal). Nilitumia milioni kumi lakini nilikuja kuvuna gunia 14 tu. Na hizo gunia 14 ndiyo pesa ya vibarua; mfano kukata, kukusanya, kupiga kupepeta, kununua viroba. Kwa ufupi ziliishia humo tu.

Niliambulia kupata gunia moja la mpunga nikakoboa nikapata mchele kilo 70. Kesho yake nikapanda basi kurudi Dar Nikawaletea chakula tu kilichopatikana. Nipo Ilala nawaza bora ningefungua duka la spea, ILA YA MUNGU MENGI.
 
Mimi nililima hekari 40 za mpunga Ifakara (signal). Nilitumia milioni kumi lakini nilikuja kuvuna gunia 14 tu. Na hizo gunia 14 ndiyo pesa ya vibarua; mfano kukata, kukusanya, kupiga kupepeta, kununua viroba. Kwa ufupi ziliishia humo tu. Niliambulia kupata gunia moja la mpunga nikakoboa nikapata mchele kilo 70. Kesho yake nikapanda basi kurudi Dar Nikawaletea chakula tu kilichopatikana. Nipo Ilala nawaza bora ningefungua duka la spea, ILA YA MUNGU MENGI.
Nikiwaona vijana wana bet hawaendi kwenye kilimo hata sishangai kilimo sio game rahisi.
 
Ulivyofika Dodoma na tikiti mambo yalivyobadilika,ungekua mbunifu na kua na plan B ungepiga ela nzuri sana,.mfano bila kua na aibu unasambaza mwenyewe kitaa reja reja Miki kwa moko, mengine unakata vipande, unatafuta goli unaweka mzigo chini, unaenda kwenye mahotel kutafuta soko, yani mji mzima tikiti zao zingeenea.
 
Ulivyofika dodoma na tikiti mambo yalivyobadilika,vungekua mbunifu na kua na plan B, ungepiga ela nzuri sana. Mfano bila kua na aibu unasambaza mwenyewe kitaa reja reja Miki kwa moko, mengine unakata vipande,unatafuta goli unaweka mzigo chini,vunaenda kwenye mahotel kutafuta soko. Yani mji mzima tikiti zao zingeenea.
Kuongea ni rahis sana ingia field uone utamu wake. Unakodi eneo unaweka matikit then unakod gari unaanza kusambaza una mzigo fuso limejaa ukifika kwa wanunuzi mtaani anakwambia nachukua matikit 15, anaenda kwa mwingine anachukua 6, mwingine anataka mkopo. Kadri siku zinavyoenda yapoteza ubora wakati huko na we gharama zinazidi za kukaa Dodoma pamoja na za kusambaza mzigo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom