Msanii
Platinum Member
- Jul 4, 2007
- 22,606
- 29,755
Leo ni michano
Kuna watanzania ni machiriku wa kuongea. Wanaongea bila hata kujua maana ya wanachokiongea.
Desemba 28 2021 Spika wa Bunge Ndugai alikosoa kasi ya ukopaji inayofanywa na serikali akitoa tahadhari kuwa kuna siku nchi itakuja kuuzwa.
Wakali wa verse wakalipuka kuwa anaisaliti na kuipinga serikali. Alisutwa akajaa na kujitokea kuomba radhi kwa maoni yake yale. Ikumbukwe serikali inajinasibu kuheshimu Ibara ya 18 ya uhuru wa maoni lakini shahidi wa Nazareti uhuru wake baada ya maoni ulipigwa roba ya mbao na Utawala Bora. Hatimaye akajiuzulu na kukaa kimya.
Hata kabla hatujakaa sawa tukaanza kuona ishu zinapambamoto huko Loliondo, watu wanahamishwa kwa nguvu huku neno hiyari likitumika kuipaka rangi siasa.
Leo nchi nzima inabembelezwa ilie na wale wale machiriku wakidai bandari inauzwa. Wasichokijua ni kwamba hili suala la nchi kuanza kuuzwa halikuanza jana. Wanajua kuwa Ndugage alikuwa sahihi kwani mkataba huu wa Bandari ni chanzo tu cha kupima kina cha maji.
Mkurugenzi wa TPA anasema nchi zimeshaingia mkataba hivyo gelesha ya kuupeleka bungeni ni hadaa kwa wananchi ionekane wabunge waliridhia. Pia hili limevuja ili tusijadili kupinga sheria mbaya kwa taifa ya kutoa kinga kwa wale jamaa zetu wanaonyooshewa vidole kutumika kuua, kuteka, kutesa na kuhukumu wakosoaji wa serikali. Hayo marekebiaho yatapita na hakuna atakayetapinga. Mkataba utapita na povu tunalolitoa leo tutaenda kufulia nguo kesho.
Tufikirie miaka 100 ijayo wajukuu zetu wataishije. Tuache kuwaza kama hatujui kuna kesho. Akina Livingstone. Carl Peters etc walijitoa mhanga kwa ulaya ya leo. Waliishi ndoto na matumaini ya vizazi vya ulaya ya leo.
Sisi tunapambania matumbo yetu.
Unafiki tuache. Tuisaidie nchi. CCM ni kinara wa rushwa na ufisadi na hivi wanajua wananchi wamewachoka, basi wanaingia mikataba isiyoponyeka maana wao na familia zao wataishi kwenye hayo matendo yao maisha yote
Kuna watanzania ni machiriku wa kuongea. Wanaongea bila hata kujua maana ya wanachokiongea.
Desemba 28 2021 Spika wa Bunge Ndugai alikosoa kasi ya ukopaji inayofanywa na serikali akitoa tahadhari kuwa kuna siku nchi itakuja kuuzwa.
Wakali wa verse wakalipuka kuwa anaisaliti na kuipinga serikali. Alisutwa akajaa na kujitokea kuomba radhi kwa maoni yake yale. Ikumbukwe serikali inajinasibu kuheshimu Ibara ya 18 ya uhuru wa maoni lakini shahidi wa Nazareti uhuru wake baada ya maoni ulipigwa roba ya mbao na Utawala Bora. Hatimaye akajiuzulu na kukaa kimya.
Hata kabla hatujakaa sawa tukaanza kuona ishu zinapambamoto huko Loliondo, watu wanahamishwa kwa nguvu huku neno hiyari likitumika kuipaka rangi siasa.
Leo nchi nzima inabembelezwa ilie na wale wale machiriku wakidai bandari inauzwa. Wasichokijua ni kwamba hili suala la nchi kuanza kuuzwa halikuanza jana. Wanajua kuwa Ndugage alikuwa sahihi kwani mkataba huu wa Bandari ni chanzo tu cha kupima kina cha maji.
Mkurugenzi wa TPA anasema nchi zimeshaingia mkataba hivyo gelesha ya kuupeleka bungeni ni hadaa kwa wananchi ionekane wabunge waliridhia. Pia hili limevuja ili tusijadili kupinga sheria mbaya kwa taifa ya kutoa kinga kwa wale jamaa zetu wanaonyooshewa vidole kutumika kuua, kuteka, kutesa na kuhukumu wakosoaji wa serikali. Hayo marekebiaho yatapita na hakuna atakayetapinga. Mkataba utapita na povu tunalolitoa leo tutaenda kufulia nguo kesho.
Tufikirie miaka 100 ijayo wajukuu zetu wataishije. Tuache kuwaza kama hatujui kuna kesho. Akina Livingstone. Carl Peters etc walijitoa mhanga kwa ulaya ya leo. Waliishi ndoto na matumaini ya vizazi vya ulaya ya leo.
Sisi tunapambania matumbo yetu.
Unafiki tuache. Tuisaidie nchi. CCM ni kinara wa rushwa na ufisadi na hivi wanajua wananchi wamewachoka, basi wanaingia mikataba isiyoponyeka maana wao na familia zao wataishi kwenye hayo matendo yao maisha yote