Tulichokunywa na kula Ikulu Chamwino

Tulichokunywa na kula Ikulu Chamwino

Manyerere Jackton

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
2,438
Reaction score
4,463
Rais John Magufuli, amekuwa akisisitiza azma ya Serikali yake ya kufufua na kuanzisha viwanda vipya.

Lakini huwezi kuwa na viwanda vipya kama sisi wenyewe hatutumii bidhaa zinazozalishwa kwenye viwanda hivyo.

Leo nimeona jambo la faraja sana Ikulu ya Chamwino. Juisi (sharbati) zote zilikuwa ni za hapa hapa nchini, hasa kutoka Azam.

Zilikuwapo za kila aina kuanzia za machungwa, mananasi, maembe, mapela, na kadhalika. Kwa maji ya kunywa, yalikuwapo Kilimanjaro kutoka kwa Mzee Mengi.

Mvinyo haukuwapo, pengine kwa sababu muda haukuruhusu; kama ungekuwapo, basi bila shaka ungekuwa ni Dompo, Dodoma, Presidential, n.k kutoka hapa hapa Dodoma.

Kama Ikulu wameanza kuthamini bidhaa za ndani, huu ni mwanzo mzuri wa kuimarisha viwanda vyetu vya ndani.

Hakuna sababu ya kunyeshwa juisi za Afrika Kusini au Kenya, ilhali sisi wenyewe tunazo za kiwango cha juu. Huu ni mwanzo mwema.
 
Manyerere Jackton


Kama hilo ni kweli lilikuwa lengo basi naweza kusema kwamba Raisi Magufuli ameanza na mguu mzuri na huko mbele mambo yatanyooka tu, kinachofwata aanze na furniture za maofisini maseremala wetu wapewe kazi, kwanza wawezeshwe kwa kuwapa utaalamu tuna veta zakutosha tu au hata magereza pia wanatengeneza furniture, hapo itakuwa ni win win situation kwani tutazalisha ajira kwa watu wetu na pia kuongeza ubora wa bidhaa zetu hali itakayopelekea kuanza kuexport nje ya nchi!

Safi sana Magufuli!
 
Last edited by a moderator:
...Lakini huwezi kuwa na viwanda vipya kama sisi wenyewe hatutumii bidhaa zinazozalishwa kwenye viwanda hivyo...
"Huwezi kuwa na viwanda vipya (maana yake havipo) ... kama sisi wenyewe hatutumii bidhaa zinazozalishwa kwenye viwanda hivyo (maana yake vipo)."

Swali:

Una maana gani kuanzisha viwanda vipya ambavyo unatusihi tutumie bidhaa zinazozalishwa na hivyo hivyo viwanda vipya? Ni vipya au vipo? Kama ni vipya, hizo bidhaa zinatoka wapi? Kama vipo, huo upya wake unatoka wapi?
 
Ni jambo jema kupunguza matumizi yasiyoyalazima na kutukuza za kwetu.
Ila sasa asiishie katika vikao anvyohudhuria yeye tu bali vikao vyote vya taasisi za serikali na mashirika ya umma kwa sababu huko ndiko kunapigwa kila uchwao
 
Kama hilo ni kweli lilikuwa lengo basi naweza kusema kwamba Raisi Magufuli ameanza na mguu mzuri na huko mbele mambo yatanyooka tu, kinachofwata aanze na furniture za maofisini maseremala wetu wapewe kazi, kwanza wawezeshwe kwa kuwapa utaalamu tuna veta zakutosha tu au hata magereza pia wanatengeneza furniture, hapo itakuwa ni win win situation kwani tutazalisha ajira kwa watu wetu na pia kuongeza ubora wa bidhaa zetu hali itakayopelekea kuanza kuexport nje ya nchi!

Safi sana Magufuli!
Magufuli amekuwa kiongozi wa msaada tangu akiwa waziri wa kawaida serikalini hakika mungu katupa kiongozi wa mfano tumuunge mkono atatufaa sana.
 
Nitafurahi sana endapo Raisi huyu akapiga marufuku Mitumba ili vile viwanda vyote vilivyokufa vianze kufanya kazi!
 
Lile sebene la kampeni lazima atie akili ili awe na reference next campaign aiseee chezea wewe?
 
Manyerere Jackton

Weka picha isije kuwa Propaganda za Lumumba kama inavyooneka kila mahali kwenye Jukwaa hili.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom