Tulichokunywa na kula Ikulu Chamwino

Tulichokunywa na kula Ikulu Chamwino

mzungu ni mzungu tu.juice ya azam kwenye glass ya made in france.hapo wote mzungu angesema kila mtu abaki na nguo made in tanzania mngebaki uchi


Wewe unarudi kulekule, hilo ndo tatizo lilikuwepo kwahiyo mchangia mada ametoa mfano kupitia Magufuli, tuanze kutumia vyetu vya ndani ya nchi, japo changamoto zipo kwenye ubora ndo issue lakini pia inawezekana kuboresha na kutumia vyetu...kwasabab kuna nguo kutoka china ubora wake ni ovyoooooo kabsaaa, naamini madesigner wa ndani ya nchi waksihirikiana na viwanda vilivyopo tunaweza kutoa nguo zetu za kisaasa zinazoendana na wakati.
 
Tz tukiamua inawezekana, wazee wa Kilimanjaro ni wataalam sana wa moka, kama kiwanda kikubwa kikifunguliwa natumai vijana wengi toka shule ya msingi mpaka chuo kikuu na wafanya kazi watamudu kununua! Ubora na ubunifu ndilo jambo la msingi.
 
Watu wanataka tuwe tunamponda tu rais. Sijui wakoje hawa watanzania wenzetu. Hata kwa jambo zuri tusisifie?
 
Rais John Magufuli, amekuwa akisisitiza azma ya Serikali yake ya kufufua na kuanzisha viwanda vipya.

Lakini huwezi kuwa na viwanda vipya kama sisi wenyewe hatutumii bidhaa zinazozalishwa kwenye viwanda hivyo.

Leo nimeona jambo la faraja sana Ikulu ya Chamwino. Juisi (sharbati) zote zilikuwa ni za hapa hapa nchini, hasa kutoka Azam.

Zilikuwapo za kila aina kuanzia za machungwa, mananasi, maembe, mapela, na kadhalika. Kwa maji ya kunywa, yalikuwapo Kilimanjaro kutoka kwa Mzee Mengi.

Mvinyo haukuwapo, pengine kwa sababu muda haukuruhusu; kama ungekuwapo, basi bila shaka ungekuwa ni Dompo, Dodoma, Presidential, n.k kutoka hapa hapa Dodoma.

Kama Ikulu wameanza kuthamini bidhaa za ndani, huu ni mwanzo mzuri wa kuimarisha viwanda vyetu vya ndani.

Hakuna sababu ya kunyeshwa juisi za Afrika Kusini au Kenya, ilhali sisi wenyewe tunazo za kiwango cha juu. Huu ni mwanzo mwema.

Uroho tu ndio kilichokupeleka nyambafu ww uroho tu na cc tunazulumiwa
 
Back
Top Bottom