Uchaguzi 2020 Tulia Ackson: 2020 nitagombea

Mbona wengi walishajua kwamba anaandaliwa kugombea jimbo huko Mbeya.. Na imeenda mbele zaidi kwamba anaandaliwa kuwa spika wa bunge lijalo 2020-2025..
 
Ana haki ya kugombea! Nawachukia sana watu wanaojimilikisha majimbo eti mtu asisogee. Iwe CCM au CHADEMA, au CUF, n.k. Waachieni wananchi waamue nani wanampenda. Hata ndani ya CCM wapo wengi wanaotaka nafasi hiyo. Nami nakuja jimboni tupambane kupata hiyo mishahara mizuri muliyorundika Bungeni.
 
Beutifull with Brain Tulia Mimi Ntakupa kura yangu ukigombea ata niwe wapi ntarudi Nyumbani Mbeya Kukupigia Kura
 
ni haki yake Tulia kugombea hakuna mwenye hati miliki na jimbo ndio maana hata Sugu alipata sababu aliyekuwepo hakuwa na hati miliki.Ubunge kikatiba ni miaka mitano baada ya hapo yeyote ana haki kugombea hakuna wa kujitunisha vimisuli kwa mkwara mbuzi kuwa mimi ndio nina hati miliki
Ila kwny urais mwanachama wa CCM akionyesha nia audio zake lazima zivujishwe.
 
Hii kauli hamnyimi usingizi Sugu, lakini Ndugai halali akisikia hivi. Kumbuka huyu mama/dada alikwishautaka Uspika ila wazee wakatumia busara zao kumtuliza na Unaibu Spika.
Ameyasema hayo alipokuwa anahojiwa katika kipindi cha East Africa Breakfast Leo kinachorushwa na kituo cha redio cha East Africa.

"Mwenyezi Mungu akitupa Uhai 2020 nitagombea, ila nitagombea wapi? naomba watulie kwa sababu chama chetu kina utaratibu wake ila nashukuru ninavyoonekana nina uwezo wa kugombea maeneo mengi."Naibu Spika @TuliaAckson

View attachment 1185297
 
Kugombea ni haki ya kila mtu kama hajaziuliwa na sheria yoyote.

Dr. Tulia
Bernard Membe
Tundu Lissu
Luke na Ollachuga Oc na wengine wote tuna haki ya kugombea.

Tofauti ni Ollachuga Oc yeye atagombea umeneja wa Chelsea, anataka kumtoa Lampard.
 
Labda aende akachukue jimbo linalomilikiwa na S.H.Amon kwa sasa, pale Tukuyu. Vinginevyo atatafuta vita na Sugu pale Mbeya mjini.
 
Ameyasema hayo alipokuwa anahojiwa katika kipindi cha East Africa Breakfast Leo kinachorushwa na kituo cha redio cha East Africa.

"Mwenyezi Mungu akitupa Uhai 2020 nitagombea, ila nitagombea wapi? naomba watulie kwa sababu chama chetu kina utaratibu wake ila nashukuru ninavyoonekana nina uwezo wa kugombea maeneo mengi."Naibu Spika @TuliaAckson

View attachment 1185297
Kwa utaratibu wa CCM ameshakiuka utaratibu wa kujitangaza hadharani atakatwa asipo katwa basi na wengine wasikatwe
 
Jimbo LA Arusha mjini,Kigoma mjini na kwa Bashe kule-Nzega..

ndio size yake..akagombee huko!
 
ni haki yake Tulia kugombea hakuna mwenye hati miliki na jimbo ndio maana hata Sugu alipata sababu aliyekuwepo hakuwa na hati miliki.Ubunge kikatiba ni miaka mitano baada ya hapo yeyote ana haki kugombea hakuna wa kujitunisha vimisuli kwa mkwara mbuzi kuwa mimi ndio nina hati miliki

Sio ubunge tu, hata urais na udiwani mwisho ni miaka mitano, baada ya hapo unatakiwa upambane na hali yako.
 
Mbona wengi walishajua kwamba anaandaliwa kugombea jimbo huko Mbeya.. Na imeenda mbele zaidi kwamba anaandaliwa kuwa spika wa bunge lijalo 2020-2025..
Ana haki ya kugombea ila tunamshauri aende kwao Busokelo. Mbeya Mjini ni kwa wana Mbeya Mjini ila kuna watu wamemdanganya kuwa Mbeya Mjini hakuna watu wa kugombea. Tunasubiri Bashiru Ally atakaposema GO, ndiyo Tulia atajua kuwa Mbeya ina wenyewe.

Kamwe Tulia hana sura ya kuwakilisha Mbeya Mjini.
 
Jimbo LA Arusha mjini,Kigoma mjini na kwa Bashe kule-Nzega..

ndio size yake..akagombee huko!
Mbona chadema mnajiita chama Cha demokrasia Lakini hamtaki Tulia atumie demokrasia yake kugombea.Mkoje ninyi ? Ilitakiwa ninyi muwe was kwanza kutamka kuwa Ni haki yake ya kidemokrasia kugombea.Unajua munaonekana matapeli You don't walk the talk.Mnaimba demokrasia demokrasia ikifika kuifanyia kazi mnageuka!!!
 
Ana haki ya kugombea ila tunamshauri aende kwao Busokelo. Mbeya Mjini ni kwa wana Mbeya Mjini ila kuna watu wamemdanganya kuwa Mbeya Mjini hakuna watu wa kugombea. Tunasubiri Bashiru Ally atakaposema GO, ndiyo Tulia atajua kuwa Mbeya ina wenyewe.

Kamwe Tulia hana sura ya kuwakilisha Mbeya Mjini.
Hakuna chama Wala mgombea mwenye hati miliki na Jimbo lolote Tanzania Hilo ulijue
 
Back
Top Bottom