Tukumbushane watu wa Tabora-Mboka Manyema

Tukumbushane watu wa Tabora-Mboka Manyema

Ha ha ha ha Musoma Betrii??watu walikua wanaenda kuchajisha mabatry yao kwako Aliwika sna Tabora nae enz zetu,ah aha aha Taaa Bora
 
Watu wa Mboka Manyema.....Bado mnampenda Rage?Nasikia ana radio yake inaitwa VOT
 
Ha ha ha kweli ukipita mitaa ya Bhachu kwenye kuta unakuta maandishi "FIFI ana ukimwi" au "Fifi kapita"...yani wakati huo Ukimwi ni balaa mtu akiwa nao!ITV tunafunga safari kuangalizia pale Community Centre kwenye sanamu ya Nyerere opp. Na Ofis za CCM mkoa!mahali ambapo TANU na ANC ya Mtemvu iliibuka!cinema za ukimwi na kanda Bongoman!Shekhe Ilunga alikuwa Basketballer mzuri sana..anapiga dua kabla ya mechi kuanza,japo alikuwa mtemi sana kwenye Court ya Basketbol Uhazili na pale Chuo cha Ualimu Tbra.....mbunge alikuwa Aboubakari Mgumia...Meya alikuwa Mzee Mpepo Diwani wa Ng'ambo jiran na mtaa wa makaranga!Jamaa wanaosoma chuo Madrasa walikuwa wanatishia kusoma Albadil....

Umenikumbusha mbali sana enzi za basketbal uhazili kulikua na watoto wa national walikua wachezaji wazuri sana.mimi nlisoma uyui high school group langu walikua major,mansour marjebi,adam fundikira,menchi
 
Dahhh Kumbe Steve alifariki!!! R.I.P Bro

Nani anamkumbuka power chuma?
Kuna mtu anaijua REMEMBER MEMBER Uyui sec?
Huyu Sheikh Ilunga alikua mchezaji mzuri wa basket, Kuna mtu anakumbuka?
R.I.P Major.
R.I.P Mzee Kassimu muuza kahawa wa diamond.
R.I.P Issa Kibira.
Nani anamkumbuka Chande mwehu aka Chui. Ukimwita chui umekwisha.
Nani anamkumbuka Profesa? (epaina bisso) anakaa kama unaenda kiloleni alikua mtata saana mwanamke kama ana mimba akipanda basi lake ajue nauli analipa mara mbili yaani yeye na mtoto aliye tumboni haa haaa haaa.
Mnamkumbuka Cast wa mwanaisungu?
Je Patel head master Uyui Sec?
Haya wadau leteni story za mboka....

Major alikua best yangu sana pamoja na mansour marjebi,menchi,adam fundikira ulikua hutukosi uhazili court ya basketbalk,nimesoma uyui frm 5 na 6
 
Tabora ina historia ya kumuwekan mbunge kwa msimu mmoja tu,toka enzi za kina Aboubakari Mgumia mpaka leo
 
Daaaa nimekumbuka maeneo ya kiloleni kulikuwa na mzee mmoja aliitwa Papa Wemba gari lake aliandika Mokili ya Nzambe aliishi checkline ya kiloleni maarufu "matenkini" enzi hizo hukatiz pekeyako.

Wilka hotel,zero bar n.k. Hahahaha post nzuri.nimesomea Uyui high school Mwl Diaz au babu Diaz na Mama Shaniiii

Nimesoma miaka ta "97 na akina Yona,Medi,Shabani Topi,idd kalega,Javan Sakvatory,Sasa nane,Baby Happy Susa,Balaaaaaaaaaaaaaaa.
 
Ochard ya WARSO, Kipalapala, isukamahela,Kaze Hill,kwihara,national Housing, mwl makweta,kimalamashwi,mikomangwa,kanyabwoya,nkumba,kongela,Sambala,Mageni(Mamba), Lujuo,Kanijo,LUENA, Shendu yuko Dodoma,Pambe,Masele,Kansimba,Madafu,mwandu,Chambo,Matata,Mgumba,Rohobadi,Ntonge,Dr. Malya,Matumbo,Nyanda,Katendele,Mrs. MIRISHO,.......................................................................
 
Namkumbuka profesa pale reli ya kigoma,chizi mmoja anaitwa subisubi kila mwingine alikuwa anashinda mahakamani anaitwa kalumanzila,dr othuman,dr kisenge,mtaani kwetu subeti kulikuwa name mzee Omar mnyonge,maziku mlinzi Moravian church tulipambana nae kwenye mapera
 
Ochard ya WARSO, Kipalapala, isukamahela,Kaze Hill,kwihara,national Housing, mwl makweta,kimalamashwi,mikomangwa,kanyabwoya,nkumba,kongela,Sambala,Mageni(Mamba), Lujuo,Kanijo,LUENA, Shendu yuko Dodoma,Pambe,Masele,Kansimba,Madafu,mwandu,Chambo,Matata,Mgumba,Rohobadi,Ntonge,Dr. Malya,Matumbo,Nyanda,Katendele,Mrs. MIRISHO,.......................................................................

Mkuu CHETTA we utakuwa umesoma Tabora wewe sio bureeee
 
Last edited by a moderator:
Siku hizi Tabora kwishiney sehemu nzuri ni shimoni tu
 
Major alikua best yangu sana pamoja na mansour marjebi,menchi,adam fundikira ulikua hutukosi uhazili court ya basketbalk,nimesoma uyui frm 5 na 6

Mkuu unamzungumzia major yule mwembamba alikuwa rafiki wa JUMA' NGE', mansouri kaka wa mahsen wale waarabu wa bachu? menchi ngonyani? Hee Tabora jamani utafikiri kuna chuo cha michezo kila kitu kilikua hot. Wadada wa uhazili, mabinti wa kota za NBC, walitingisha haswa.
 
Mkuu unamzungumzia major yule mwembamba alikuwa rafiki wa JUMA' NGE', mansouri kaka wa mahsen wale waarabu wa bachu? menchi ngonyani? Hee Tabora jamani utafikiri kuna chuo cha michezo kila kitu kilikua hot. Wadada wa uhazili, mabinti wa kota za NBC, walitingisha haswa.

Hahaaa wewe mtata kumbe unawajua wote hao.....ilikia group yangu hiyo mimi nlisoma uyui A level major alikua anakaa hpo nyuma y ukumbi w cinema....n mansour ndio huyo wa bachu mzee wke alikuaa almaarufu sana mzee mzee marjebi....enzi hizo uhazili,ttc ndio sehemu y kuuza sura
 
Tabora enzi hizo miaka ya kuna demu alikuwa anaitwa Veronica Mhina alisoma unyanyembe

Student center watu walikuwa wanaenda Ku record ngoma kwa Aziz

National kulikuwa na totoz Kali kama kina magreth

Tatizo Moja kulikuwa hamna makahaba
 
Nani analikumbuka shindano la wowowo liliofanyika mwanaisungu ?
 
Hahaaa wewe mtata kumbe unawajua wote hao.....ilikia group yangu hiyo mimi nlisoma uyui A level major alikua anakaa hpo nyuma y ukumbi w cinema....n mansour ndio huyo wa bachu mzee wke alikuaa almaarufu sana mzee mzee marjebi....enzi hizo uhazili,ttc ndio sehemu y kuuza sura

Dah, kina mansour wame mega haswa mabinti, Juma NGe, R.I.P Cast wa Isungu enzi hizo ndio vijana matajiri, kina JUMA MSONGA walikuwa makaka lakini noma kwa mabinti, kuna gheto lilikuwa kanyenye pale kona kama unaelekea uhazili, lile geto lile lilivunja bi,,kra sana za vibinti. Waarabu wale watoto wa mzee Hazam kina haji na dada zake lutfia, zamzam ndio walikua matajiri wa kiarabu eti kwao kuna gorofa, aisee long time.
 
Hahaaa wewe mtata kumbe unawajua wote hao.....ilikia group yangu hiyo mimi nlisoma uyui A level major alikua anakaa hpo nyuma y ukumbi w cinema....n mansour ndio huyo wa bachu mzee wke alikuaa almaarufu sana mzee mzee marjebi....enzi hizo uhazili,ttc ndio sehemu y kuuza sura

Uhazili walikuwa wanateja mji kweli, na wanafunzi wa uyui walikuwa watata kweli mabinti wa o level wanapiga mambo kama wa chuo, ila chuo cha ualimu walikuwa hawa sikiki kabisa, cast nae alimega kweli mademu . r.i.p. geto la uyui pale kona la kina JUMA MSONGA nalo liliharibu sana mabinti aisee, watoto wa kishua wanazuga kwenda kanisani wanapishana geto, mhh kufaulu shule kwa mabinti pale ni shiida kweli maana vijana wanaimbisha balaa halafu ilikuwa BURE tu hakuna kitu unahonga.
 
Uhazili walikuwa wanateja mji kweli, na wanafunzi wa uyui walikuwa watata kweli mabinti wa o level wanapiga mambo kama wa chuo, ila chuo cha ualimu walikuwa hawa sikiki kabisa, cast nae alimega kweli mademu . r.i.p. geto la uyui pale kona la kina JUMA MSONGA nalo liliharibu sana mabinti aisee, watoto wa kishua wanazuga kwenda kanisani wanapishana geto, mhh kufaulu shule kwa mabinti pale ni shiida kweli maana vijana wanaimbisha balaa halafu ilikuwa BURE tu hakuna kitu unahonga.

Hahaaa kweli wewe w mboka kipindi hicho kongoa mzigo haikua gharama zaidi y kuuza sura 2....mimi nlikua nakaa cheo kule karibia n nyumba z nyuzi
 
Hahaaa kweli wewe w mboka kipindi hicho kongoa mzigo haikua gharama zaidi y kuuza sura 2....mimi nlikua nakaa cheo kule karibia n nyumba z nyuzi

Mi nilikuwa mjini kabisa pale karibu na jamatini ule msikiti wa wahindi, pale NBC opposite na shule ya mihayo secondari. Enzi hizo unaandikiwa wimbo tu wa kizungu ambao uko kwenye chat basi ujumbe umeupata, dah old is gold kwa kweli.
 
kwenye vichaa hapo umemsahau makamba jeki bana!........jamaa mmoja alikua kibarua maarufu tunamuita fulu saba......anapeleka pwani huyoooo!!!!nakumbuka nikiwa 'kinda' tu mwanajeshi mmoja aliuawa majaruba ya isevya kutokea stesheni pale.......basi 'wajeda' wakaenda zika mtu wao kimya kimya halafu wakaingia mtaani sasa.......weee....wiki nzima msako,waliokuwa watuhumiwa wa hata udokozi miaka ile walikufa vibaya kwa singe na vipigo vya washkaji,vilio vikatawala mji mzima na amani ya hata kulala mlango wazi ikarejea!

FIFI alikuwa anatuhumiwa kuwaambukiza ukimwi dada zetu kwa makusudi,one day alionekana mitaa ya kwetu na dada mmoja wa pale pale mtaani kwetu anaitwa Tatu Mazegembe........alikuwa na makalio makubwa huyooo wacha.........basi wacha tumtoe nduki na mawe huku tunamwambia yule dada 'unaenda kufa wewe!!!'......aaaaa mboka matata wee.....mji wangu wa utotoni uliokataa kukua!

Issue ya fifi ilivuma sanaa hata sisi tulio ku kijiji cha zugimlole kaliua tulijawa hofu ya fifi,mbokaaaaa
 
Back
Top Bottom