Tukumbushane watu wa Tabora-Mboka Manyema

Tukumbushane watu wa Tabora-Mboka Manyema

blueivvy nahisi zilikuwa za FRMP,sikumbuki vizuri,thobias kobelo mara ya mwisho nadhani alikuwa na kesi ya kuua kama sikosei na mwingine alifungwa au alikuwa na kesi,watoto walikuwa wanakula unga na bangi vibaya sana. na mchizi wao Mc bob C ndo alikuwa anawaongoza, mdogo wao tu ndo alikuwa ametulia. huyu dr kobello hospitali yake ilikuwa mitaa ya kanyenye karibu na fourways au tanesco..
I see ni kweli mkuu ofisi za forest resources management project nadhani hao kina kobello walikuwa wanakaa nyuma ya shule ya cheyo A
 
Mkuu umenikumbusha mbali sana...mwehu maarufu enzi zile alikuwa anaitwa malingumu mzee mmoja kichaa alikuwa soko kuu, mimi nilizaliwa ng'ambo mtaa maarufu unaitwa kwihara street, baba yangu alikuwa ana shamba kijiji cha usenge karibu na jumba la makumbusho(livingstone)...pale kwihara kulikuwa na waarabu kina zahoro nasikia aliuza ile ardhi kwa chuo cha st augustine au tumaini university......ujio wa papa binafsi ulinigusa sana nilikuwa mdogo ila kwa kweli papa John Paul II alikuwa charismatic...na kwa kweli huko alipo ni mtakatifu...jet yake ilitua uwanja wa tabora wa vumbi, tukiwa nyumbani mida ya saa tisa hivi tulishangaa ndege nyeupe ina mlio mkali(jet) ikitua....majambazi niliokuwa na wakumbuka mimi ni kina mohamed romba...pale ng'ambo kulikuwa na mpakistan mmoja na familia yake alikuwa anaitwa Nuru din alikuwa na wasichana mabinti wareeembo...hakika maisha ni safari yenye uchungu sana kwa sisi tuliopitia mambo magumu....kanisa katoliki ilikuwa ni nguzo muhimu ...namkumbuka marehemu padre John Mageda, ndiye alinibatiza......akikuwa anajua sana kuimba zile sala za ekaristi takatifu...bwaaana awe naaaanyiiiiiii, inuuueeeeeniiii mioyooooooooooo! tumeinuuua kwa bwanaaaaa! mimi nilisoma Uyui sekondari

Wewe wa Kwihara?mbona ndo mitaa yangu sana?unawajua watoto wa Saidi Kindamba?Waha walima miwa kule mbugani?vipi hujasoma shule ya Mkoani?unamjua Juma Lwelwe babu yake alikuwa mganga wa kienyeji?vipi kuhusu Mashenene?umecheza mpira kwenye makaburi ya Wabaniani?Ujio wa Papa ulinivuta sana...namkumbuka pia Padre Tengi,Padre Dino na Padre Lembeli...nakumbuka mazish ya Askofu Mihayo tulimzika kanisani!...Askofu Mario Abdalah Mgulunde..anahubiri zaidi ya saa moja...wanamaombi wa Fr.Nkwela walisumbua sana Tabora...wale waarabu kina Zahoro nilisoma na mtoto wake anaitwa Nasoro...mweusi tiii lakn nywele za kiarabu!hawa ni mabaki ya uzao wa Waarabu wafanyabiashara ya Utumwa...huwezi kukaa Tbr miaka hiyo usimjue mwehu Malingumu....Tabora kwanini huendelei my dear?Wapi Lipumba,Sita,Rage,Kapuya?
 
Wewe wa Kwihara?mbona ndo mitaa yangu sana?unawajua watoto wa Saidi Kindamba?Waha walima miwa kule mbugani?vipi hujasoma shule ya Mkoani?unamjua Juma Lwelwe babu yake alikuwa mganga wa kienyeji?vipi kuhusu Mashenene?umecheza mpira kwenye makaburi ya Wabaniani?Ujio wa Papa ulinivuta sana...namkumbuka pia Padre Tengi,Padre Dino na Padre Lembeli...nakumbuka mazish ya Askofu Mihayo tulimzika kanisani!...Askofu Mario Abdalah Mgulunde..anahubiri zaidi ya saa moja...wanamaombi wa Fr.Nkwela walisumbua sana Tabora...wale waarabu kina Zahoro nilisoma na mtoto wake anaitwa Nasoro...mweusi tiii lakn nywele za kiarabu!hawa ni mabaki ya uzao wa Waarabu
wafanyabiashara ya Utumwa...huwezi kukaa Tbr miaka hiyo usimjue mwehu Malingumu....Tabora kwanini huendelei my dear?Wapi Lipumba,Sita,Rage,Kapuya?

Mkuu mimi kwetu ni kwihara street karibu na duka la ushirika enzi hizo, kuna mzee mmoja anaitwa selemani mzee na zaidin mzee, au mwingine kwa marehemu musa kiombo pale makaburi ya baniani nimecheza sana ila nakumbuka kuna kijana mmoja anaitwa kurukutu aliwahi kunifanyia mchezo mbaya sasa miaka ya 80 ila kwa kuwa ni marehemu mungu amuweke mahala pema, yes nawafahamu watoto wa kindamba kaka yangu Joseph Bizumo alisoma na Rajabu Kindamba..nasikia mtoto mmoja wa zahoro aliehuka alikuwa anaitwa zeheri na mwenzie kadongo walilogwa..kule kwa waha ndiyo viwanja vyangu kulikuwa na mashamba ya miwa shule ya mkoani sikusoma ila tulikuwa tunapita kwenda usenge kijijini kwa baba yangu.....si ile shule iko kwenye majaruba?
Yule padre dino, acha kaka yake yule mdogo alikuwa ipuli ni Muhuni sana ametuharibia sana dada zetu hastahili kuwa paroko...wale hawakuwa na wito sema walikimbilia misheni kama sehemu ya kupata ajira...siku anazikwa mihayo mimi nilikuwepo tulikaa upande wa mihayo hall...mzee wetu yule maskini alifariki kwa kweli mji wa tabora umesheheni historia ila nilitokea kuuchukia sana kutokana na ushirikina...mtu huwezi kujulikana kama si mtoto wa Tambwe, haruna, ...UNAMKUMBUKA DJ Eddo? alikuwa anapiga hits zile kama london beat....have been thinking about yoooou..tinti tinti...have been thinking about youu!!! uuuu!!
 
Nilibahatika kupita huko mwezi wa 11 mwaka jana nikielekea Kahama, Shy. Kwa kweli Tabora ni mkoa uliokwisha, hakuna maendeleo yeyote zaidi ya kuwa na nyoka na vichaa wengi mjini. Mtu ukiiba kibiriti kwa mwarabu dukani basi unatupiwa ukichaa, yaani hakuna cha maana pale. Kila mtu anajifanya alwatani na ukiwa mwarabu unaogopewa kwani wakazi wanakuona wewe ni Mungu mtu.


Wewe utakuwa mpita njia tu kama unavyosema, Tabora warabu watu wakawaida sana, hadi kuna wehu na vibaka waarabu!Katiza chemchem ukutane na waarabu wanakaa nyumba za tope.
 
Familia ya Dr Kobelo wengi walifariki,akiwepo Dr mwenyewe,mkewe na yule mtoto wao aliyekuwa ana akili sana baadae akawa chizi ,Yule alikuwa anatembea kama amekata centre bolt ya bega la kushoto alikuwa anaitwa Steve. Thobias baadae ya kufungwa alirudi uraiani na mara ya mwisho nilisikia anapiga tempo pale Orion Tabora Hotel, sasa sijui kama bado yupo hapo maana mwaka jana mmiliki wahoteli hiyo Bw POLLE a.k.a Kanyenyela alifariki dunia pia.

Mnaikumbuka ile bustani ya wanyama kule national? Nasikia ilishafungwa siku hizi. Nilikwenda Mboka mwaka juzi sikubaliani na nyie kuwa mji haubadiriki kimaendeleo maana nimeshuhudia majumba ya kufuru Mitaa ya mihogoni kule kama unakwenda kiwanda cha tumbaku Miemba na maeneo ya Ipuli na Cheyo. Kweli maendeleo siyo ya haraka lakini tunajikongoja taratibu.
 
Shule nilianzia chemchem duuh ikifika saa nne mbio simbamwene kwenye maembe nilipofika la tatu baba akanihamishia mwenge mazoezi mbona utoro uliisha maana nidhamu, walimu walikuwa wanafundisha vizuri, usafi ole wako uende bila kuoga unaogeshwa Shule, usipovaa soksi fimbo, kulikuwa na mwl chiboni, getaback, makore, dah kama kuna aliyesoma mwenge miaka ya 80_90 atanisaidia ooh chipukizi na skaut ni vitu ambavyo nimevitumikia sana kungekuwa na ajira nadhani ningekuwa na cheo kikubwa sana

mwalimu Getabaki Amefariki miezi miwili iliyopita...
 
Wewe utakuwa mpita njia tu kama unavyosema, Tabora warabu watu wakawaida sana, hadi kuna wehu na vibaka waarabu!Katiza chemchem ukutane na waarabu wanakaa nyumba za tope.

Pengine ni kweli unavyosema ila kwa mtizamo wangu nimeona kama vile wanaogopewa. Maana kia kitu nenda pale kwa mwarab au kule kwa waarab utapata hicho unachokitafuta.
 
Pengine ni kweli unavyosema ila kwa mtizamo wangu nimeona kama vile wanaogopewa. Maana kia kitu nenda pale kwa mwarab au kule kwa waarab utapata hicho unachokitafuta.



Trust me Mkuu! Mimi nimezaliwa na kukulia huko so napafahamu kwa undani kupita kiasi!Njia ya kwenda Sikonge kuna kijiji kinaitwa tutuo na kama unakwenda urambo kuna kijiji kinaitwa uyumbu huko wamejaa waarabu wakufa mtu ndiyo maana nakwambia waarabu Tabora ni kama wanyamwezi tu kwanza hata hawajisikii kama niliowakuta huku Dar es salaam, yaani wanajichanganya uswazi kama kawa na wengine hadi kinywamwezi kinapanda.
 
Nilibahatika kupita huko mwezi wa 11 mwaka jana nikielekea Kahama, Shy. Kwa kweli Tabora ni mkoa uliokwisha, hakuna maendeleo yeyote zaidi ya kuwa na nyoka na vichaa wengi mjini. Mtu ukiiba kibiriti kwa mwarabu dukani basi unatupiwa ukichaa, yaani hakuna cha maana pale. Kila mtu anajifanya alwatani na ukiwa mwarabu unaogopewa kwani wakazi wanakuona wewe ni Mungu mtu.

acha uongo wewe tabora ya mwaka 90 wanayoiongelea wadau hapa si tabora ya leo mkubwa shaishi hapo enzi hizo na nikapata bahati ya kwenda kikazi hapo mwaka jana, sehemu anazosema kama maua bar leo wanapaita zero, mwanaisungu bado unapigwa mziki ila panajina jipya, tabora ya leo inamitaa mipya ipuli, mwinyi kulikuwa mapoli so ukisema tabora haijabadilika nakuona waajabu, sehemu nilyoenda nakukuta imebadilika ni rufita club na tabora hotel kwani enzi zile tumeenda sana na mzee tukawa tunacheza table tenis, dast, tenis na michezo kibao ila leo imebaki magofu tu so tabora ipo bwana na wenyeji wake.
 
Familia ya Dr Kobelo wengi walifariki,akiwepo Dr mwenyewe,mkewe na yule mtoto wao aliyekuwa ana akili sana baadae akawa chizi ,Yule alikuwa anatembea kama amekata centre bolt ya bega la kushoto alikuwa anaitwa Steve. Thobias baadae ya kufungwa alirudi uraiani na mara ya mwisho nilisikia anapiga tempo pale Orion Tabora Hotel, sasa sijui kama bado yupo hapo maana mwaka jana mmiliki wahoteli hiyo Bw POLLE a.k.a Kanyenyela alifariki dunia pia.

Mnaikumbuka ile bustani ya wanyama kule national? Nasikia ilishafungwa siku hizi. Nilikwenda Mboka mwaka juzi sikubaliani na nyie kuwa mji haubadiriki kimaendeleo maana nimeshuhudia majumba ya kufuru Mitaa ya mihogoni kule kama unakwenda kiwanda cha tumbaku Miemba na maeneo ya Ipuli na Cheyo. Kweli maendeleo siyo ya haraka lakini tunajikongoja taratibu.

Dahhh Kumbe Steve alifariki!!! R.I.P Bro

Nani anamkumbuka power chuma?
Kuna mtu anaijua REMEMBER MEMBER Uyui sec?
Huyu Sheikh Ilunga alikua mchezaji mzuri wa basket, Kuna mtu anakumbuka?
R.I.P Major.
R.I.P Mzee Kassimu muuza kahawa wa diamond.
R.I.P Issa Kibira.
Nani anamkumbuka Chande mwehu aka Chui. Ukimwita chui umekwisha.
Nani anamkumbuka Profesa? (epaina bisso) anakaa kama unaenda kiloleni alikua mtata saana mwanamke kama ana mimba akipanda basi lake ajue nauli analipa mara mbili yaani yeye na mtoto aliye tumboni haa haaa haaa.
Mnamkumbuka Cast wa mwanaisungu?
Je Patel head master Uyui Sec?
Haya wadau leteni story za mboka....
 
kwenye vichaa hapo umemsahau makamba jeki bana!........jamaa mmoja alikua kibarua maarufu tunamuita fulu saba......anapeleka pwani huyoooo!!!!nakumbuka nikiwa 'kinda' tu mwanajeshi mmoja aliuawa majaruba ya isevya kutokea stesheni pale.......basi 'wajeda' wakaenda zika mtu wao kimya kimya halafu wakaingia mtaani sasa.......weee....wiki nzima msako,waliokuwa watuhumiwa wa hata udokozi miaka ile walikufa vibaya kwa singe na vipigo vya washkaji,vilio vikatawala mji mzima na amani ya hata kulala mlango wazi ikarejea!

FIFI alikuwa anatuhumiwa kuwaambukiza ukimwi dada zetu kwa makusudi,one day alionekana mitaa ya kwetu na dada mmoja wa pale pale mtaani kwetu anaitwa Tatu Mazegembe........alikuwa na makalio makubwa huyooo wacha.........basi wacha tumtoe nduki na mawe huku tunamwambia yule dada 'unaenda kufa wewe!!!'......aaaaa mboka matata wee.....mji wangu wa utotoni uliokataa kukua!

dah! Umenikumbusha FIFI mwaka 93 hiyo mitaa ya bachu kila ukuta unakuata wameandika fifi anaukimwi fifi anaukimwi dah jamaa alivuma sana mjini pale .
 
Hadi kipindi naondoka, pale uyui mkuu alikua mama shani na msaidizi wake mzee mugasha....
Dahhh Kumbe Steve alifariki!!! R.I.P Bro

Nani anamkumbuka power chuma?
Kuna mtu anaijua REMEMBER MEMBER Uyui sec?
Huyu Sheikh Ilunga alikua mchezaji mzuri wa basket, Kuna mtu anakumbuka?
R.I.P Major.
R.I.P Mzee Kassimu muuza kahawa wa diamond.
R.I.P Issa Kibira.
Nani anamkumbuka Chande mwehu aka Chui. Ukimwita chui umekwisha.
Nani anamkumbuka Profesa? (epaina bisso) anakaa kama unaenda kiloleni alikua mtata saana mwanamke kama ana mimba akipanda basi lake ajue nauli analipa mara mbili yaani yeye na mtoto aliye tumboni haa haaa haaa.
Mnamkumbuka Cast wa mwanaisungu?
Je Patel head master Uyui Sec?
Haya wadau leteni story za mboka....
 
acha uongo wewe tabora ya mwaka 90 wanayoiongelea wadau hapa si tabora ya leo mkubwa shaishi hapo enzi hizo na nikapata bahati ya kwenda kikazi hapo mwaka jana, sehemu anazosema kama maua bar leo wanapaita zero, mwanaisungu bado unapigwa mziki ila panajina jipya, tabora ya leo inamitaa mipya ipuli, mwinyi kulikuwa mapoli so ukisema tabora haijabadilika nakuona waajabu, sehemu nilyoenda nakukuta imebadilika ni rufita club na tabora hotel kwani enzi zile tumeenda sana na mzee tukawa tunacheza table tenis, dast, tenis na michezo kibao ila leo imebaki magofu tu so tabora ipo bwana na wenyeji wake.

Ni vema wewe unaona kuna tofauti ila mimi mpita njia naona ni nyang'anyang'a tu, yaani haina tofauti na Kigoma ama Katavi. Sasa hapa najiuliza, leo TB iko hivi, je hiyo miaka ya 90 ule mji ulikuwaje?
 
Trust me Mkuu! Mimi nimezaliwa na kukulia huko so napafahamu kwa undani kupita kiasi!Njia ya kwenda Sikonge kuna kijiji kinaitwa tutuo na kama unakwenda urambo kuna kijiji kinaitwa uyumbu huko wamejaa waarabu wakufa mtu ndiyo maana nakwambia waarabu Tabora ni kama wanyamwezi tu kwanza hata hawajisikii kama niliowakuta huku Dar es salaam, yaani wanajichanganya uswazi kama kawa na wengine hadi kinywamwezi kinapanda.

Sijakubishia ila nimesema tu yale niliyoyaona mimi huko. Nimeeleweka?
 
ah ah! Chips ni kwa Babu ebi watoto wa st, mary unawakuta kibao... Karibu tbr mboka manyema Ipuli paris mkuuu tunakula mema yaliyopo
Simbamwene tulikuwa tunaenda kuangua zambalau na embe boribo juu ya makaburi...vp umekuwa mji?ha ha ha ha ha ha umenikumbusha Mwajuma Ringa?ivi kwanini Mboka Manyema vichaa wengi?...dah Hamis Mambwa aliogopwaje?Diamond near by TMP uwanja wa Chipukizi?ukumbi wa Disco hapo Mwanaisungu geti la kuingia Uhazili...video tunangalizia Maua Bar Opposite na Central Police
 
Ni vema wewe unaona kuna tofauti ila mimi mpita njia naona ni nyang'anyang'a tu, yaani haina tofauti na Kigoma ama Katavi. Sasa hapa najiuliza, leo TB iko hivi, je hiyo miaka ya 90 ule mji ulikuwaje?
umekariri wewe una exposure ya kutosha that is why huoni tofauti
 
Hadi kipindi naondoka, pale uyui mkuu alikua mama shani na msaidizi wake mzee mugasha....

Nahisi tumepishana miaka kati yangu mimi na wewe maana hao uliowataja hata mimi siwajui kama ilvyo wewe humjui Patel, Alikuwepo Uyui sec as head master kama sikosei mpaka early 90s
 
Ha ha ha kweli ukipita mitaa ya Bhachu kwenye kuta unakuta maandishi "FIFI ana ukimwi" au "Fifi kapita"...yani wakati huo Ukimwi ni balaa mtu akiwa nao!ITV tunafunga safari kuangalizia pale Community Centre kwenye sanamu ya Nyerere opp. Na Ofis za CCM mkoa!mahali ambapo TANU na ANC ya Mtemvu iliibuka!cinema za ukimwi na kanda Bongoman!Shekhe Ilunga alikuwa Basketballer mzuri sana..anapiga dua kabla ya mechi kuanza,japo alikuwa mtemi sana kwenye Court ya Basketbol Uhazili na pale Chuo cha Ualimu Tbra.....mbunge alikuwa Aboubakari Mgumia...Meya alikuwa Mzee Mpepo Diwani wa Ng'ambo jiran na mtaa wa makaranga!Jamaa wanaosoma chuo Madrasa walikuwa wanatishia kusoma Albadil....
 
R.I.P Getaback sikuwa na habari masikini alinifundisha na pia ndie alikuwa headmaster wakati nasoma Ahsante mkuu kwa kunijuza
 
Back
Top Bottom