Tukumbushane watu wa Tabora-Mboka Manyema

Tukumbushane watu wa Tabora-Mboka Manyema

Kulikuwa na majambazi kama kina Jackson kuku in hatari huyu jamaa.nilikuwa na padri mmoja anaitwa mihayo alikuwa anaonyesha cinema za yesu daudi MUSA na wengine wengi
 
Nasikia kuna dogo mmoja wa Posta Bank ametikisa sana kule Mboka toka mwaka uanze...janja yooote kumbe kapiga hela ya posta.Msako mkali unaendelea kakimbia vitega uchumi,mke na magari.Vijana acheni tamaa
 
ukweli tabora tumesomea wengi,Inga wa wenyeji walikuwa wachache
 
Hahaha, sinema diamond, disco Tabora hotel, timu mirambo bwana, Quresh ufunguo, job ayoub, feruz teru!! Kwenye maisha yangu yote sijawahi ona winga ana kipaji kama Feruz Teru! Yaan unaweza mfananisha na J. J. Okocha tu kwa kupiga chenga, sema kitu kilikuwa kinamzuia kucheza ni enka, mabeki ndo ikawa kumkanyaga hapohapo. Mboka.. Mji unaoongoza kwa vichaa Tanzania. Nakumbuka mwalimu Nyerere alikuwa kwa mwaka anakuja ipuli kwa kwa yule mama Asha Maswezi. Waswezi ndo walikuwa wanaenda kumpokea uwanja wa ndege. Sijui alikuwa anaenda kufanya nini kwa yule maza, alikuwa ana mamizimu makali sana ya Maswezi. Mboka kipindi hicho kama huchezi kung-fu hujakamilika. Ushirikina mwingi, kila njia panda nazi zimevunjwa, mavitu kibao. kila kona wanapiga ngoma za kutoa majini, au kupandisha mizimu.
 
real cool post! tumezaliwa dar though huko ni kwetu its nicwe to hear some stories!
 
Mimo nakumbuka polisi walivyopIga marufuku viatu vilivyochongoka kuviita "WANCHOMA"
 
Mi nilikuwa mjini kabisa pale karibu na jamatini ule msikiti wa wahindi, pale NBC opposite na shule ya mihayo secondari. Enzi hizo unaandikiwa wimbo tu wa kizungu ambao uko kwenye chat basi ujumbe umeupata, dah old is gold kwa kweli.

Hahaaa mitaa y adam fundikira mzee wa totoz ndio alikua anakaa mitaa hiyo n kijana mmoja wa kiarabu anaitwa gibu alikua anakaa hpo jirani na mayor hotel
 
Tabora enzi hizo miaka ya kuna demu alikuwa anaitwa Veronica Mhina alisoma unyanyembe

Student center watu walikuwa wanaenda Ku record ngoma kwa Aziz

National kulikuwa na totoz Kali kama kina magreth

Tatizo Moja kulikuwa hamna makahaba

Huyu mage alisoma kazima sec au
 
kuna mama mmoja alikuwa kichaa na matusi kibao. Kichaa kikipanda zaidi anatembea wizauti
 
kuna mama mmoja alikuwa kichaa na matusi kibao. Kichaa kikipanda zaidi anatembea wizauti ni LOSHI
 
Familia ya Dr Kobelo wengi walifariki,akiwepo Dr mwenyewe,mkewe na yule mtoto wao aliyekuwa ana akili sana baadae akawa chizi ,Yule alikuwa anatembea kama amekata centre bolt ya bega la kushoto alikuwa anaitwa Steve. Thobias baadae ya kufungwa alirudi uraiani na mara ya mwisho nilisikia anapiga tempo pale Orion Tabora Hotel, sasa sijui kama bado yupo hapo maana mwaka jana mmiliki wahoteli hiyo Bw POLLE a.k.a Kanyenyela alifariki dunia pia.

Mnaikumbuka ile bustani ya wanyama kule national? Nasikia ilishafungwa siku hizi. Nilikwenda Mboka mwaka juzi sikubaliani na nyie kuwa mji haubadiriki kimaendeleo maana nimeshuhudia majumba ya kufuru Mitaa ya mihogoni kule kama unakwenda kiwanda cha tumbaku Miemba na maeneo ya Ipuli na Cheyo. Kweli maendeleo siyo ya haraka lakini tunajikongoja taratibu.

Yule alisoma uyui sec.mfuga rumba.
 
Kwa waliosoma Gongoni shule ya msingi miaka ya72 mpaka 80 kulikuwa na mwalimu Mary mkuu wa shule, mwalimu Kimiti mwalimu mbutu mwalimu maugo . Kwa kweli mmenikumbusha mbali .
 
Umeshau milambo wanaume VS Tabora boys siku moja tabora boys walikimbizwa mpaka mabwenini na Milambo wanaume. Aly mayai alikuwa anasoma Uyui sec, na victor mihayo, kidau na renatus njohore walikuwa tabora boys, pia kuna mtoto wa kiarabu wa tabora boys alikuwa hatari. milambo wanaume kulikuwa na kimti, goliati, mathew, na nk.

Duuh umenikumbusha mbali sana. Kulikuwa na mechi Milambo na Tabora Boys . Ghafla vagi likaanza, na mechi ikaishia hapo. Nilikuwa nasoma tabora Boys, wakati tukinyukana makonde, nilikuwa nimeshika jezi tuliyokuwa tumemnyang'anya mchezaji wa Milambo wanaume, alikuja mshkaji mmoja mcheza wa milambo anaitwa Eddo, alinilamba ngwala moja matata sana, akanisindikiza na kipepsi....nilijuta kwann nilijifanya kidume kuzuia Jezi..
 
Dahhh Kumbe Steve alifariki!!! R.I.P Bro

Nani anamkumbuka power chuma?
Kuna mtu anaijua REMEMBER MEMBER Uyui sec?
Huyu Sheikh Ilunga alikua mchezaji mzuri wa basket, Kuna mtu anakumbuka?
R.I.P Major.
R.I.P Mzee Kassimu muuza kahawa wa diamond.
R.I.P Issa Kibira.
Nani anamkumbuka Chande mwehu aka Chui. Ukimwita chui umekwisha.
Nani anamkumbuka Profesa? (epaina bisso) anakaa kama unaenda kiloleni alikua mtata saana mwanamke kama ana mimba akipanda basi lake ajue nauli analipa mara mbili yaani yeye na mtoto aliye tumboni haa haaa haaa.
Mnamkumbuka Cast wa mwanaisungu?
Je Patel head master Uyui Sec?
Haya wadau leteni story za mboka....

Profesa a.k.a PapaWemba gari lake lilikuwa kimeandikwa Nokili ya nzambe,R.I.P papaaaaa
 
Wale walosoma Chemchem S/Msingi, kulikuwa na mwalimu Said Nkungu alikuwa anapenda kufundisha chipukizi huyooo! Af kuna mwalimu Manyori alikuwa head teacher mzee wa bakora, kulikuwa tena na akina mwalimu Msigallah, Bejumula na wengineo,. Afu pande zile kuelekea uwanja wa milambo sekondari kulikuwa na vijana wanavuta ganja haoo..
 
Back
Top Bottom