Mara nyingi nimekuwa nikifuatilia Thread na Comment zinazotolewa
na pande hizi mbili na kujaribu kuzilinganisha. Nimegundua kuwa wanaume
wanaopatikana hapa JF- MMU ni Malaya ah! samahani ni vicheche sipendi kuzianika
baadhi ya Thread hapa au majina ya watu wanaoongoza kwa tabia hiyo
isipokuwa kila mmoja ni shahidi.
Mfano Mwanaume anaweza kupost Thread kuhusu wanawake wa Mbeya, Atawaelezea
kiunaga ubaga jambo linalothibitisha kuwa katembea na zaidi ya mmoja. Mwingine
atakwambia ah! wanawake wa mkoa fulani bwana wako hivi kitandani yaani
lugha anayoileta ni wazi kuwa katembea na mwanamke zaidi ya mmoja.
Pia zipo Comment ambazo mtu anakwambia tu huyo kandamiza kisha achana nae,
yaani ni wazi kuwa huyu mtu yuko hivyo. Kwa wanawake si jambo la kawaida sana
kukuta wakisifia wanaume wa mkoa huu na huu labda huko ma mambo ya kk....
Sasa sijui ndo kusema wanaume ndo vicheche zaidi?
Nakusudia wanaopatikana hapa MMU.
Krismas njema waungwana.