domokaya
JF-Expert Member
- Apr 22, 2010
- 3,545
- 1,719
Namuangalia mama yangu aliyekuwa mwalimu wa shule ya msingi, yupo kitandani anaumwa, hana uwezo wa kujitibu. Ukweli ni kwamba tunasubiri siku yake tumzike, matibabu yake mpaka nje ya nchi na yeye ha qualify kupelekwa nje kwani umri wake ni mkubwa wanasema wenye mamlaka. lakini mama yangu si mtu mzima kama Waziri nanii na yule nani wa jeshi ambaye amepelekwa nje ingawa damu yake imeshachafuka.
Mdogo wake marehemu babu ametoka lakini hatujui kama atarudi, yeye ameenda kufuatilia madai ya marehemu kaka yake yale ya jumuiya ya afrika mashariki, najua wazee siku hizi wanapigwa virugu, maji ya kuwasha na mabomu ya machozi eti wanadai tangu 1977, miaka thelathini na ushee hivi, hata yule jamaa wa maamuzi magumu naye alikuwapo lakini mmmmhh
BBaba yeye bado anafuatilia kiinua mgongo chake, lakini miguu yake ndio inayomsumbua zaidi, wanamwambia sijui cheki iliandikwa hakwenda kuichukua sijui sasa imefanyaje sijui
Huyu mdogo wangu nae ni msumbufu, mi nilishamuambia kuwa hawa watu hawataki ukweli, yeye kaenda huku sijui ndo yudomu kachonga mdomo wake wamemwambia analeta siasa chuoni.
Sijui kama mama yangu atapona, sijui kama babu yangu atarudi salama, sijui kama baba yangu atalipwa haki yake au nae atakufa akiidai, na huyu mdogo wangu sijui hatima yake ni nini. Mimi kaka yake nilipangiwa kufundisha mpanda, nimekuja nyumbani mara moja, sijalipwa bado fedha zangu za kujikimu, sijui kama kweli nitalipwa kwani kaka yetu mkubwa yeye alipangiwa kufundisha shule moja hapa mjini mwaka 2004, alifanya kazi mwaka mmoja bila kulipwa mshahara wala chochote, akaaugua, akafa mpaka leo kaburi lake halijalipwa.
Hapa maeneo ya amana kuna kichaa mmoja anasema tuko vitani, tunapigana na adui, adui asiyeonekana adui anayeitwa SERIKALI YETU
Mdogo wake marehemu babu ametoka lakini hatujui kama atarudi, yeye ameenda kufuatilia madai ya marehemu kaka yake yale ya jumuiya ya afrika mashariki, najua wazee siku hizi wanapigwa virugu, maji ya kuwasha na mabomu ya machozi eti wanadai tangu 1977, miaka thelathini na ushee hivi, hata yule jamaa wa maamuzi magumu naye alikuwapo lakini mmmmhh
BBaba yeye bado anafuatilia kiinua mgongo chake, lakini miguu yake ndio inayomsumbua zaidi, wanamwambia sijui cheki iliandikwa hakwenda kuichukua sijui sasa imefanyaje sijui
Huyu mdogo wangu nae ni msumbufu, mi nilishamuambia kuwa hawa watu hawataki ukweli, yeye kaenda huku sijui ndo yudomu kachonga mdomo wake wamemwambia analeta siasa chuoni.
Sijui kama mama yangu atapona, sijui kama babu yangu atarudi salama, sijui kama baba yangu atalipwa haki yake au nae atakufa akiidai, na huyu mdogo wangu sijui hatima yake ni nini. Mimi kaka yake nilipangiwa kufundisha mpanda, nimekuja nyumbani mara moja, sijalipwa bado fedha zangu za kujikimu, sijui kama kweli nitalipwa kwani kaka yetu mkubwa yeye alipangiwa kufundisha shule moja hapa mjini mwaka 2004, alifanya kazi mwaka mmoja bila kulipwa mshahara wala chochote, akaaugua, akafa mpaka leo kaburi lake halijalipwa.
Hapa maeneo ya amana kuna kichaa mmoja anasema tuko vitani, tunapigana na adui, adui asiyeonekana adui anayeitwa SERIKALI YETU