Tukiwa tunaelekea Mei Mosi, TUCTA waomba Rais Samia asikilize kilio chao

Trust None

JF-Expert Member
Feb 12, 2018
1,260
4,415
Shirikisho huru la vyama vya wafanyakazi Tanzania (TUCTA), limesema lina matumaini na Rais mpya wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan atashughulikia madai yao ya muda mrefu yalipwe kwa wakati ili kuinua maisha ya wafanyakazi.

Shirikisho huru la vyama vya wafanyakazi Tanzania (TUCTA), limesema lina matumaini na Rais mpya wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan atashughulikia madai yao ya muda mrefu yalipwe kwa wakati ili kuinua maisha ya wafanyakazi.

Tucta imesema Hayati Dkt. John Magufuli alishaanza kufanyia kazi malalamiko yao kupitia vikao maalumu alivyokuwa anafanya na viongozi wa TUCTA, hivyo ni mategemeo yao Samia ataendeleza pale alipoishia mtangulizi wake kuhakikisha anamaliza changamoto hiyo kabisa.

Akizungumza Dar es Salaam leo (jana) Machi 28,2021 kwa njia ya simu na gazeti hili, kuelezea matarajio yao kwa Rais mpya.

Kaimu Katibu Mkuu wa TUCTA, Said Wamba amesema wanaanzia walipoishi na Hayati Magufuli kwamba madai yao ya mishahara na hali bora ya maisha kwa wafanyakazi yanaendelea.

“Na matumaini yetu, rais mpya na watendaji wake watayaona madai yetu ni ya maana na ya msingi kwa maendeleo ya wafanyakazi na wananchi kwa ujumla. Mishahara, kodi, na tulishaandika barua kwenda serikalini kuwaomba watupunguzie kiwango cha kodi ya mapato ambayo wanafanyakazi wanalipa kupitia fedha zao. Tunashukuru mwaka jana walipunguza kwa kiasi fulani lakini safari hii tunaomba wapunguze pia ,”

“Mishahara na marupurupu ya wafanyakazi ambayo yalisimama kwa muda mrefu sasa tunaomba yaanze kupatikana ,” anasema

Wamba ameeleza wana miaka minane sasa hawajaongezewa kiwango cha mshahara na mara ya mwisho kuongezewa ilikuwa mwaka 2013, licha ya kwamba uongozi wa shirikisho hilo umekuwa ukijitahidi kudai madai hayo kila mwaka kupitia sikukuu ya wafanyakazi inayofanyika Mei Mosi kila mwaka lakini bado hawaja timiziwa.

“ Tunaamini Rais atatumia busara na watendaji wake wengine kuangalia kilio chetu na akituongezea itasaidia kuinua morali ya ufanyaji kazi,” anasema Wamba.

Pia amesema Rais Magufuli aliwawekea utaratibu wa kukutana naye mara mbili au tatu kila mwaka na kupitia mikutano hiyo, ilikuwa inasaidia kumaliza baadhi ya changamoto ndogo ndogo zilizokuwa zinawakwamisha kwenye shughuli zao.

“Tunafikiri naye Rais mpya kurithi utaratibu huo wa kukutana na vyama vya wafanyakazi kila wakati kuondoa matatizo madogo madogo kwa mazungumzo ya kawaida kupata ufumbuzi kuliko kuamini kufuata sheria au kuanzisha mapambano ambayo kimsingi yanawapotezea muda,” alisema.

Wamba amemaliza kwa kutoa wito kwa wafanyakazi wote katika kipindi hiki wanatakiwa kuwa na subra kumpa muda wa kutosha Rais mpya kwa kuwa anakabiliwa na majukumu mengi ya kufanya, huku akiwataka kuendelea kutimiza wajibu wao wakati viongozi wa TUCTA wakifanya utaratibu wa kufuatilia madai hayo.

Chanzo: Tucta waomba Rais Samia asikilize kilio chao

My take:
Wakati wa kupandisha madaraja ningeomba aanze na wale ambao hawajawi kupanda daraja kabisa tangu waajiriwe. Kwa mfano, ajira mpya ya 2013 na wachache wa 2012.
 
Wafanyakazi wanazaidi ya miaka 8 hawajapanda madaraja.

Nadhani hapa sasa wakati umefika compensation ifanyike.

Imagine, watu mnafanya kazi sekta moja ila HALMASHAURI tofauti unakuta wenzako uliona nao kazi wanakuzidi DARAJA zima achilia mbali swala la baadhi ya elimu kusema hazitambuliki husisani (masters)
 
Hawa wapumbavu wa TUCTA wamekumbuka shuka baada ya Magufuli kufariki dunia. Walikuwa wamepoa kama barafu na busy kusifia sifia ujinga wa mzee Meko.
Sasa kama mtu alikuwa hasikilizi ushauri yeye ni anaamka na kufanya anachotaka TUCTA ulitaka wafanyeje?
 
Back
Top Bottom