Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,809
- 15,409
Mnamo mwaka 1996 nilifukuzwa chuoni. Lakini kilichonifukuzisha chuoni, ni kufuata mkumbo. Wenzangu waligoma kwa sababu ya posho, kwa upande wangu niliona dhahiri sababu ya kugoma kwao haikuwa na mashiko. Lakini nilishindwa kukataa kugoma, nikajikuta naungana nao. Labda utashangaa nikikwambia kuwa mimi niliyefuata mkumbo sikurudishwa kabisa chuoni, wakati wale waanzilishi wa mgomo wote walirudishwa na kuendelea na masomo.
Inashangaza eh!
Inashangaza eh!