Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Kuna mzee anaitwa Masoud Masoud yuko TBC nafikiri mpaka sasa, namuelewa sana kwenye simulizi za historia ya mziki wa zamani na ndiye aliyetangaza msiba wa Michael Jackson
 
Kuna mzee anaitwa Masoud Masoud yuko TBC nafikiri mpaka sasa, namuelewa sana kwenye simulizi za historia ya mziki wa zamani na ndiye aliyetangaza msiba wa Michael Jackson
Huyo mzee huwa napenda sana sauti yake. Sijaona mwandishi mwenye sauti kama Masoud Masoud.

Na kuna mama mmoja nae alikiwa DW kastahafu nais mwaka huu nae nilikuwa na mkubar sana
 
kuna jamaa alikuwa anatangaza kipindi cha "Nani ni Nani" chanel 10 kitambo,Nimetoka kumkumbuka huyu jamaa.
(nakumbuka aliaga anaenda mbele baada ya kupata demu wa kizungu)
 
"Kahawa ni zao lenye faida kubwaaa....eeeh tulimeni kahawa....." Hapo saa moja moja usiku unasubiri ubweche upakuliwe hapo.......

"Pokeaa salaaam.....".........saa sita hapo umetoka shule njaa inauma homr hukuti mtu wapo shambaa....ungonga viazi na maji mambo yanaendelea

Dah those days bana......
 
Nilienda kipindi fulani kwenye maonyesho ya sabasaba, nikaingia banda la TBC/ Radio Tanzania.... Nikauliza kama naweza kupata michezo ya radio ya akina Havijawa , au vituko vya Pwagu na Pwaguzi na jingle kama za kipindi cha majira, michezo ile saa mbili kasoro..

Niliishia kupata fedheha , nikakuta vijana kwenye banda hawajui hata naongelea kitu gani.. Sikurudi tena ....

Kuna historia na kumbukumbu nzuri.. Ilikuwepo Radio Tanzania
 
Nilienda kipindi fulani kwenye maonyesho ya sabasaba, nikaingia banda la TBC/ Radio Tanzania.... Nikauliza kama naweza kupata michezo ya radio ya akina Havijawa , au vituko vya Pwagu na Pwaguzi na jingle kama za kipindi cha majira, michezo ile saa mbili kasoro..

Niliishia kupata fedheha , nikakuta vijana kwenye banda hawajui hata naongelea kitu gani.. Sikurudi tena ....

Kuna historia na kumbukumbu nzuri.. Ilikuwepo Radio Tanzania
Hili ni tatizo kwa taasisi nyingi la kuwapa wafanyakazi majukumu wasiyoweza. Taasisi kama TBC inatakiwa kuwa na wafanyakazi wenye uelewa mpana wa historia ya sekta na mwajiri wao, wapi ilitokea, wapi iliko na wapi iendako.
 
Namkumbuka marehemu Dj unle J "Julius Nyaisanga" alikuwa anagonga ngoma za mbele kwenye kipindi kimoja Ijumaa/Jumamosi usiku saa nne miaka ya mapema 90's.
 
Take a break, na tujikumbushe enzi zile za RTD, ambapo kulikuwa hakuna FMs rado kama sasa. Hakika kulikuwa na watangazaji, vipindi bomba na hata nyimbo za kutambulisha vipindi zilikuwa makini sana. Hebu ngoja niwakumbushe baadhi ya watangazaji wa wakati huo.

1. Nassoro Nsekeli- alikuwa na sauti kama ya mafua hivi alikuwa mtaalamu wa kipindi cha Majira- ndiye aliyetangaza kifo cha Nico Zengekala

2. Bujago Izengo wa Kadago- Kibesi chake kilikuwa safi sana

3. David Wakati (DG) - kipindi cha Nipe habari- Kwaherini wote, mungu awalinde na mmbaki salama, mungu akipenda..............

4, Khalid Ponera- Zilipendwa

5. Ahmed Kipozi- taarifa ya habari

6. Hassan Mkumba- matangazo ya vifo

7. Siwatu Luwanda

8. Salama Mfamao
9. Mohamed Amani (Mohamed Dahman)

10. Salim Seif Nkamba

12. CHisunga Steven- kipindi cha Ugua pole duu

13. Bathoromeo KOmbwa (bati Kombwa) - WAkati wa Kazi

14. Ahmed Jongo- Mpira

15. Christina Chokunogela

16. Dominic Chilambo- Mpira

17. Edda Sanga
18. Debora Mwenda- Mama na Mwana
19. Aloycea Maneno- Ombi lako, cheichei Shangazi, mama na mwana

Duu nawamiss sana hawa watu tofauti na watangazaji wa sasa
Umemsahau Ben Kiko
 
Fauziyat Abood (ITV)
Suzzy Lukindo /Suzan Mungi (ITV)
Rukia Mtingwa (ITV)
Neema Mbuja (ITV)
Rehema Mwakangale (ITV)
Albert Nitwa (ITV)
Mikidad Mahamood (ITV)
Farouk Kharim (ITV Zanzibar tangu ITV ianze mwaka 1994 hadi leo 2022)
 
Back
Top Bottom