Tujikumbushe mambo Enzi za Mwalimu

Ninaongea juu ya wakati wa siasa za Ujamaa na Kujitegemea zilipokuwa zimeshika hatamu.Kunawakati bidhaa ziliadimika sana. Sukari, sabuni, chumvi zikawa bidhaa za anasa kuwa nazo. Kuvipata hadi kwa mgawo zaidi ya huu wa umeme wa TANESCO, na tena ikawa kwa foleni.

Msimuliaji wangu aliyeshuhudia enzi hizo anasema wakati huo kijijini kwao huwezi kufahamu bidhaa hizo zinauzwa wapi. Ikitokea, huwa kwa kificho sana.

Mwenye bidhaa anaweka mkaa kwenye chombo kisha anaweza nje juu ya kiti. Huo ni utambulisho ya kwamba hapo kuna bidhaa inauzwa. Unachotakiwa unapanga foleni hata kama hufahamu bidhaa gani inauzwa; utafahamu mwisho wa foleni. Chakushangaza: Ukifika mwisho "unaulizwa unataka nini wewe?". "Sukari," unamjibu.

Lakini, cha kusikitisha jibu linaweza kuwa: "hapa tunauza sabuni." Kwakuwa bado unahitaji bidhaa hiyo, ulipaswa kwenda kubahatisha sehemu nyingine hadi hapo utakapo fanikiwa.

Swali ni je, uzalendo huu na uvumilivu wa kiwango hiki,ulichangiwa na nini? Je, kwa kizazi chetu hiki?
 
Ninaongea juu ya wakati wa siasa za Ujamaa na Kujitegemea zilipokuwa zimeshika hatamu.Kunawakati bidhaa ziliadimika sana. Sukari, sabuni, chumvi zikawa bidhaa za anasa kuwa nazo. Kuvipata hadi kwa mgawo zaidi ya huu wa umeme wa TANESCO, na tena ikawa kwa foleni.

Msimuliaji wangu aliyeshuhudia enzi hizo anasema wakati huo kijijini kwao huwezi kufahamu bidhaa hizo zinauzwa wapi. Ikitokea, huwa kwa kificho sana.

Mwenye bidhaa anaweka mkaa kwenye chombo kisha anaweza nje juu ya kiti. Huo ni utambulisho ya kwamba hapo kuna bidhaa inauzwa. Unachotakiwa unapanga foleni hata kama hufahamu bidhaa gani inauzwa; utafahamu mwisho wa foleni. Chakushangaza: Ukifika mwisho "unaulizwa unataka nini wewe?". "Sukari," unamjibu.

Lakini, cha kusikitisha jibu linaweza kuwa: "hapa tunauza sabuni." Kwakuwa bado unahitaji bidhaa hiyo, ulipaswa kwenda kubahatisha sehemu nyingine hadi hapo utakapo fanikiwa.

Swali ni je, uzalendo huu na uvumilivu wa kiwango hiki,ulichangiwa na nini? Je, kwa kizazi chetu hiki?
 
575041_456191524408460_2079276517_n.jpg
 
Dah, kutokana umasikini wetu sikuweza kumiliki la halali, ila kulikuwa na kaka yangu alikuwa anaiba huko shuleni kwao ndio na mimi napata.
 
Dah, kutokana umasikini wetu sikuweza kumiliki la halali, ila kulikuwa na kaka yangu alikuwa anaiba huko shuleni kwao ndio na mimi napata.

Tabia hizi mmekuwanazo mpaka kwenye kuibarasilimali zetu, nyambafuuuuu. Wizi ndio mmeona sifa kumbe ni ujinga
 
Umenikumbusha mbali Mkuu. Lakini kwa Globu ilikuwa enzi za Jumbe. Yaani kila kitu bure, vitu vyote unapewa shule tena bureee. Natamani kulia, nikiona wanafunzi wanavyohangaika. Wizi mtupu.
 
Nlikuwa nanunua penseli 3 nazikata vipi vidogo vidogo mkebe unajaa then mi ndop nakuwa mjanja class mkebe umejaa mpaka haufungi
 
Dah! Ni KOMPASI aiseee, enzi hizoooo 1988!

Enzi za mwal unazojua wewe ndio hizi!!!

Unajua Azimio la Arusha weweyeeh ? Kampeni ya ... Wahujumu uchumi?
...ukiwa na hizo dude tatu ... ukisika wanakupitia siku hiyo ... unatupa mbili za ziada, mtoni!!!:A S angel: !!!
 
Ndani kwa chini huwa kuna kikaratasi kigumu, sasa chini ya kikaratasi nilikuwa naweka shilingi kumi ya noti.. ile ya kijani!
 
KOFA na BOFA, vyote bado vipo madukani. Tembelea Tahfif Stores utapata moja. Enzi hizo mambo ya Elimu Supplies ndani ya IPS Building.

Mitoto yetu ya siku hizi bure kabisa, haijui maktaba wala Dar es Salaam Bookshop. Lkn hata hivyo na serikali nayo zero, pale Dar Bookshop siku hizi utakuta Atlas 4 na Biblia 3 za Poboporian na watu wanuza sura. Vitabu vya watoto hakuna, na wazazi hatuoni kuwa muda wanaosoma magazeti ya Shigongo walitakiwa kusoma hadithi za umri wao

Naikumbuka zamani, naitamani..
 
Tatizo langu kubwa lilikuwa ni kupoteza vitu bana kuanzia viatu mapaka daftari yote sababu ya kucheza mpira, nilishawahi poteza mfuko mzima wa daftari na viatu uwanjani
 
KOFA na BOFA, vyote bado vipo madukani. Tembelea Tahfif Stores utapata moja. Enzi hizo mambo ya Elimu Supplies ndani ya IPS Building.

Mitoto yetu ya siku hizi bure kabisa, haijui maktaba wala Dar es Salaam Bookshop. Lkn hata hivyo na serikali nayo zero, pale Dar Bookshop siku hizi utakuta Atlas 4 na Biblia 3 za Poboporian na watu wanuza sura. Vitabu vya watoto hakuna, na wazazi hatuoni kuwa muda wanaosoma magazeti ya Shigongo walitakiwa kusoma hadithi za umri wao

Naikumbuka zamani, naitamani..

Ahsante kwa kunikumbusha Tanzania Elimu Supplies mkuu!!
 
Back
Top Bottom