Tujikumbushe Kipindi kileeee JAMBOFORUM!!

Tujikumbushe Kipindi kileeee JAMBOFORUM!!

Nadhani ujio wa CM zenye NET umechangia sana! kuwa na Member wa Ajabu ajabu na mambo haya ya maGAMBA na maGWANDA ndo yameharibu kabisa utakuta watu wanabishana kwa mambo yakiPUMBAVU kabisa nadhani ndomana wanachama Seriuos hawaonekani! Ila kuna Jukwaa la Great Thinkers kule! Ingawa pia kunakuwaga na Ushabiki bt angalau kuna mijadala ya watu timamu!
 
Namkumbuka mwafrika wa kike alikuwa anamwaga data kweli.. Halafu Kuhani alikuwa msumbufu na mbishi kweli... Hakika JF ya miaka 2009 ilikuwa Shule kweli kweli..
 
Kaka memory card yako ina gb kubwa mno. Jukuwaa wakati ule lilikuwa tamu, unatafut rafiki online na
kuchat nae live. Mwenye matusi alikuwa anapuuzwa hadi anajirekebisha, Jukuwaa za sijui siasa au mapenzi zilikuwa hazipo. Unaaanzisha topic na watu husika sanachangia, zikaingia siasa zikatuharibu.

Inabidi warudishe utaratibu huo.
Uchangiaji wa watu kwenye mada umeshuka kiwango kwa sana siku hizi.
Mada za maana zimekuwa adimu siku hizi hapa jukwaani.
 
Haaa haa haaa! Mtu wa Pwani yupo, hupita akichungulia chungulia tu na hasa kwenye yale mabandiko yaliohusu Visiwani, ama nawe umepotea kiania fulani hivi...

Mi nipo,

Huwa nakuja nachungulia kama kuna kitu muhimu. Manase siku hizi ni habari za CHADEMA hiv mara CHADEMA vile mara CCM hivi, CCM vile. Yaani hao watu wameigeuza JF kuwa extension ya PR offices zao mpaka inakera.

So sometimes you just go back down memory lane, feel nostalgic and reminisce over the old JamboForums then move on.

By the way ingawa tunatumia virtual ID's, ila JF inakuwa kama vile mko shuleni, mkimaliza shule mkapoteana, inabaki kumbukumbu tu na nostalgia. Ndivyo ilivyo kuwakosa baadhi ya wenzetu wengi wa JamboForums ya 2006-2008 to mid 2009 in particular.
 
​Pia enzi hizo za jambo forum kuliibuka matapeli kama Field Marshall ES na utapeli wake wa kutafutia wabongo kazi US ila mpaka kwanza ulipe dollar 300....teeehteeh.

hahaaa na le mutuz alikuwa wapi!!??
cc FaizaFoxy kumbe field marshall id ya kitambo
 
Last edited by a moderator:
Kuna mtu alikuwa anaitwa Mtindio wa ubongo hahahaaah!! Jamaa alikuwa mtata balaa, ila mpaka sasa yupo na ID nyingine.....
 
Heheheh Mkuu Malafyale si useme tu tulikuwa watata!! Umenikumbusha mbali, akina frg, YournameIsmine, caddy, pinky, sweetNcute,hasheemThabit, cleopatra, na wengine wengi, then 2006 tukampoteza jibaba aliye kuwa ameuawa kinyama Brazil.
RIP Jibaba namkumbuka sana mshikaji si alikuwa UK? kifo chake kilisikitisha sana.
Aahaha Sweet,Mizz nawakumbuka
Daaah najivunia kuwa mmoja watu wa mwanzo ku log in kwenye hizi social net works!

Enzi hizo MgonjwaUkimwi ni mtata kweli kweli na mwenzake fgrt ahahaha
FGRT yuko wapi huyu bingwa? acha kabisa enzi zile ilikuwa raha sana ukiingia kwenye chat unatoka na chakula cha ubongo.
Kabla ya jambo forum kulikuwa na bsctimes, na kabla ya bsctimes kulikuwa na tanzanet, hizi zilikuwa forums zilizokwenda shule. Jambo radio kulikuwa na DJ Sure (if I remember correctly) pia tulikuwa tunaweza kusoma post au kujibu bandiko huku mziki unapiga. Kila ukikiingia Tanzanet ulitakiwa uandike "Subscribe" na "Unsubscribe" unapoondoka. Far we come from.
MKuu umenikumbusha mbali sana DJ Sure alikuwa anatupa burudani kweli huku tuna chat Jambo radio
 
Mi nipo,

Huwa nakuja nachungulia kama kuna kitu muhimu. Manase siku hizi ni habari za CHADEMA hiv mara CHADEMA vile mara CCM hivi, CCM vile. Yaani hao watu wameigeuza JF kuwa extension ya PR offices zao mpaka inakera.

So sometimes you just go back down memory lane, feel nostalgic and reminisce over the old JamboForums then move on.

By the way ingawa tunatumia virtual ID's, ila JF inakuwa kama vile mko shuleni, mkimaliza shule mkapoteana, inabaki kumbukumbu tu na nostalgia. Ndivyo ilivyo kuwakosa baadhi ya wenzetu wengi wa JamboForums ya 2006-2008 to mid 2009 in particular.
Mkuu,
JF ya sasa haina mashiko hoja ni CCM na CDM na udini.Mimi siku hizi kusema ukweli JF sio source yangu ya news kama zamani na huwa naweza kumaliza hata miezi miwili sijaingia JF.Hamna jipya.I really miss Jambo forum
 
RIP Jibaba namkumbuka sana mshikaji si alikuwa UK? kifo chake kilisikitisha sana.
Aahaha Sweet,Mizz nawakumbuka

FGRT yuko wapi huyu bingwa? acha kabisa enzi zile ilikuwa raha sana ukiingia kwenye chat unatoka na chakula cha ubongo.

MKuu umenikumbusha mbali sana DJ Sure alikuwa anatupa burudani kweli huku tuna chat Jambo radio

FGRT yupo Dar afisa wa wizara ya kilimo upande wa kitengo cha Tumbaku!
Waghasusu"Wagha"unajua alipo?
 
MKuu kumbe ulichukua moja kwa moja Tina? alikuwa na busara sana yule dada.Hongereni sana Kilakshari kapotelea wapi? na yule Tunu?

Kilakshari yupo Oklahoma kikazi na mwezi jana kaoa mzungu hapo hapo!
Tunu ni afisa wa CRBD tawi la Lumumba-Dar
 
MKuu kumbe ulichukua moja kwa moja Tina? alikuwa na busara sana yule dada.Hongereni sana Kilakshari kapotelea wapi? na yule Tunu?

Tina ndiyo mke wangu na tuna mtoto mmoja wa kike!

Enzi hizo Jambo forum balaa ilikuwa,mwanzilishi wa hii kitu kijana wetu Max Melo siku hizi mambo yake mazuri anapaka poda hata watu wake sisi hatukumbuki kabisa ahahahaha
 
Mkuu,
JF ya sasa haina mashiko hoja ni CCM na CDM na udini.Mimi siku hizi kusema ukweli JF sio source yangu ya news kama zamani na huwa naweza kumaliza hata miezi miwili sijaingia JF.Hamna jipya.I really miss Jambo forum

Kweli Mkuu, inasikitisha. Siku hizi hata nyuzi zisizokuwa za siasa au dini zinaishia kwenye CDM Vs CCM au Ukristo Vs Uislam. Mtu akiuliza swali kwa kutaka kuelimika, ataishia kubezwa na/au kutukanwa, hadi unashangaa JF imekuwaje?! I do miss JamboForums too
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom