Tujikumbushe kidogo Primary School.

Tujikumbushe kidogo Primary School.

mimi nakumbuka kitambu cha english book 7 toleo la mwaka 1968

unit one;
KALAGESYE

Everybody in the village of ibigi knew Kalagesye
my own first memory of him went back to time when
i was a very small boy, my sister and i were going to our glandmother's house.

sunddenly we heard, Alealealealeaa1" sung in good voice
"Quick, let's hide in the bush1" hissed my sister.
'but what for?" I said.
"there's a madman coming," she replied.
'No, he's not mad. he's just singing

Ahee ! Kana ka nsungu, ka nsung' umwelu
Ahee1kana ka nsu..........
 
Vile vile nakumbuka siku akija Mkaguzi shuleni zinachaguliwa daftari za wenye akili tu, ndizo zikaguliwe
huku za wajinga zikiachwa. ...................nimekumbuka mbali sana
 
nakumbuka kulikuwa na mti mkubwa pembezoni mwa njia ya kuelekea shuleni tulipaita makutano,,,,hapa ilikuwa ni kwa ajili ya ngumi tu
 
Na wimbo wa kumlaani Nduli Je: "Iddi Amin akifa mimi siwezi kulia nitamtupa kagera (mto) awe chakula cha mamba"
 
Vile vile nakumbuka siku akija Mkaguzi shuleni zinachaguliwa daftari za wenye akili tu, ndizo zikaguliwe
huku za wajinga zikiachwa. ...................nimekumbuka mbali sana

Siku hiyo walimu wote wanakuwa wastaarabu sana. Wanaelewesha vizuri sana. Sasa ngoja mkaguzi aondoke aliyezingua darasani wakati mkaguzi yupo atachezeaje bakora.
 
shule ilikuwa raha tu. ku-march na school band, chakula cha mcha tena tofauti tofauti, michezo, kila kitu bure na kwa wingi, madarasa mazuri tena madirisha ya vioo. mara nyingi huota kipindi hicho!
 
mimi nakumbuka kipindi namaliza darasa la pili naingia la tatu, ulikuwa ndo wakati wa kuacha kuandikia kalamu ya risasi na kuanza kuandikia kalamu ya wino! wee! hiyo pen ilikuwa inateleza kwenye karatasi ni balaa! afu mwandiko unakuwa mbayaa!
 
shule ilikuwa raha tu. ku-march na school band, chakula cha mcha tena tofauti tofauti, michezo, kila kitu bure na kwa wingi, madarasa mazuri tena madirisha ya vioo. mara nyingi huota kipindi hicho!

mwenzetu ulisoma wapi?
 
ikiwa zamu ya darasa kusafisha choo cha shule...eee ilikuwa majanga!
 
ule wimbo: tazama ramani utaona nchi nzuri, yenye mito na mabonde mengi ya nafaka.
majira yetu haya yangekuwaje sasa utumwa wa nchi nyerere ameukomesha!
 
nazikumbuka nyimbo kama
  • mama paka
  • Nyere yupo, nyerere yupo
  • mary alikuwa na kondoo wake mzuri
  • nina ndege wango
  • ngong ngong twaingia salamu twazileta kwa baba na mama
mashairi kama katoka baba mmoja toka safari ya mbali n.k
shule za siku hizi mchakamchaka ni msamiati
 
Aisee nilikua sipendi kushika masikio,nilikua napenda rede weee siku nikivaa chupi mpya watakomajee sketi inabinuliwaa juu! !
 
mimi nakumbuka kipindi namaliza darasa la pili naingia la tatu, ulikuwa ndo wakati wa kuacha kuandikia kalamu ya risasi na kuanza kuandikia kalamu ya wino! wee! hiyo pen ilikuwa inateleza kwenye karatasi ni balaa! afu mwandiko unakuwa mbayaa!

Da umenikumbusha one of my teacher bana kwenye swala la mwandiko ilikua baraaa, alikua mkali hatari kulikua na daftari ya mistari mikubwa na midogo ishu ilikua ukifika wakati wa Aa Bb Cc Dd Ee Ff Gg Hh Ii . . . apo me hoii, wale wazeeee wa kuweka lebo nyekundu za ugonjwa mabegani kukwepa bakoraaaaaa tupoooooo apa na mkumbuka Headteacher JD mzee wa uparaa, Mr komba a.k.a scout, Mrs D. Nyambele (mrs speak English) alikua anabutua huyooo. hiyo ilikua Sinde prmary 1996 ucpimeeee
 
Eeeh mambo ya 1998 std 1 hapo ilikuwa balaa.

Nilikuwa nawakimbiza kwenye test balaa ndipo Mzee akanitafutia Shule ya private.

Kufika huko nakuta madogo wanachana ngeli na kifaransa kama hawana akili nzuri halafu genius WA kijiji hata kiswahili Tu Ni cha ugoko(full kilugha) Ikabidi niwekilaza kwa muda nikashika mkia mfululizo mpaka lugha ilipokaa sawa.

Kutokujua lugha kulinifanya mnyonge na nilinyanyasika balaa lakini mwisho WA siku walikuja kutia heshima.
 
Back
Top Bottom