Tujikumbushe enzi za ufalme wa Inspector Haroun

Gangwe Mobb hao wakiwa na GWM upande wa kushoto Inspector kainamia meza anaandika na wa mbele yake Dogo Side, na upande wa kulia D-Chief kushoto na KR Mullah kulia. ....

Wakati wa tamasha la 'Mwaka Elfu Mbili' lililoandaliwa na Madunia Foundation mnamo tarehe 09/05/1999....
GangweGWM.jpg
 
Aliingia kujaza nafasi tu, maana mule ndani kuna vichwa vilikuwa vinaandika kweli kama Prof Jay, SoloThang,JayMo,Afande,Mwanafalsafa,Soggy, sasa hapo angetoboaje?, sema kwa rap katuni hakuwa na mpinzani. Nature alilalamika kwakuwa hakuingizwa kwenye mashindano, nikamshangaa aingizwe kwa mistari ipi?. Nakumbuka mwaka uliofatia walijaribu kutafuta Mkali wa Rhymes tena ila ikafeli za chini chini zilisema alipangwa mshindi washiriki wakajitoa, sema Fid alikuwa na nafasi ya kuchukua ndio alikuwa kwenye peak kwa wakati huo. Kwenye mistari yake anakwambia 'Washanitabiri watu wangu wa mtaani, mi ndio mfalme nitayefuata baada ya Suleiman...'
Lakinj huyo Inspector ndo alichukua nafasi ya pili baada ya Afande, huku nafasi ya 3 ikienda kwa Mandojo na Domokaya
 
Hahah!!

Watoto wa Temeke hawakua wanastahili kuingia kwenye yale mashindano ila kama Nature angeingia labda angeshinda kwa ifluence ya mashabiki tu...

Mashindano yenyewe kipindi kashinda Afande yaliingia dosari maana wasanii kama Sollo walilalamika sana kua kuna namna imefanyika nakumbuka alitoa hadi ngoma akiongelea hilo swala ililua inaitwa 'kilio changu' kama sikosei
Nature mbona alikuwepo katika shindano na Sitaki demu? Watu kumbukumbu zenu mnaziacha wapi?
 
Hahaha we jamaa una furahisha sana Amin amin nakuambia juma nature na kismat chake ajawahi fika ata nusu ya diamond sembuse inspector harun (babu) in jesus’s Voice
Hapa unamkosea Juma nature ..huwezi kufananisha zama hizi ambazo sisi mashabiki ndo tunatafuta mziki na zama za nature ambazo mziki ndo ulikuwa unatafuta mashabiki.
 
Baadae kidogo binti huyu MTANASHAATI.. ili mradi tu vina vitimie hata kama havina maana.. labda ndo sababu wakaiita rap katuni
In fact hii RAP KATUNI aliichukia sana Solo Thang, na kuwadiss sana Gangwe Mobb kwamba wanaharibu hip hop. Ukisikiliza wimbo wa Wateule unaoitwa "Tumerudi Tena" Solo kawananga sana Gangwe mobb na staili yao ya rap katuni.
 
we mshabiki umepoteza kumbukumbu inspector hajawai kujiunga tmk wanaume..

by 2001 juma nature hakuwa na nyimbo yake mwenyewe.. alitamba na kigeto geto ambayo alishirikishwa na king sepeto.. maskin jeuri alishirikushwa na manduli mob, mtulize alishirikishwa na mabaga fresh..

nature alianza tamba kwa kushirikishwa kabla hajatoa nyimbo yake mwenyewe
Uko sahihi ndg. Wimbo wa kwanA wa Nature unaitwa "JINSI KIJANA".
 
Nature katoka 2000 mwishoni, ilianza julietha ya dully, ikaja kigetogeto ya kingsepeto, biko na nature, ikaja machozi lady jay dee, ikaja kigetogeto remix ya nature na mr paul, ikaja niko gado, ikaja mtoto wa geti kali, ikaja jinsi kijana ya nature, hizi ni 2000 mwishoni, nyimbo za 2001 ni km bongo dsm ya prof jay, mtani jirani ya gwm na nature, maskini jeuri ya manduli mobb(humu yupo bwana mkubwa na mh temba feat nature) wakaja kina sister p, dah joh, balozi kwenye chat, jose mtambo, salome ya dully nk
unazungumzia GADO wakati kuna NGANGARI ishatoka kitambo kabla.
 
Mimi nilikua mdogo sana nilitekwa na upepo wa darubini ila nilivyopata upeo wa kupambanua mambo nikaona Prof. alistahili kupata ule ushindi...
Prof Jay ni zaidi ya wote hao, sema ushabiki tu si unajua Afande alikuja na kikosi chake kutoka Moro
 
Gangwe Mobb hao wakiwa na GWM upande wa kushoto Inspector kainamia meza anaandika na wa mbele yake Dogo Side, na upande wa kulia D-Chief kushoto na KR Mullah kulia. ....

Wakati wa tamasha la 'Mwaka Elfu Mbili' lililoandaliwa na Madunia Foundation mnamo tarehe 09/05/1999....View attachment 754479
Dah hawa jamaa wamelitoa game mbali sana lakini hawajafaidi kabisa matunda, nimewahi kumuona KR Mullar anagombea kudandia daladala la kwenda TMK pale baharini Posta nikashikwa na huruma, hawakustahili kuishi hivi. Wasanii wa dizaini hii hata Mungu akiwachukua jamii haiwapi uzito, ila hao wakina Masogange mabingwa wa kuonesha makalio watu hadi wanazimia.
 
Ya kwanza alifanya Nature na Dolo ikafanya vizuri kiasi, ilipoachiwa Remix ya Inspecta ile OG ikasahaulika kabisa. Ukisikia tu OHoo HOoo... (Sauti ya Inspekta) unajua nini kinafuatia.
nakumbuka ilikuwa Nature na KR sio Dolo...
 
Dah hawa jamaa wamelitoa game mbali sana lakini hawajafaidi kabisa matunda, nimewahi kumuona KR Mullar anagombea kudandia daladala la kwenda TMK pale baharini Posta nikashikwa na huruma, hawakustahili kuishi hivi. Wasanii wa dizaini hii hata Mungu akiwachukua jamii haiwapi uzito, ila hao wakina Masogange mabingwa wa kuonesha makalio watu hadi wanazimia.
Mkuu acha tu yani inasikitisha sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom