Tujifunze pamoja na tuelimishane kuhusu program ya Excel

Tujifunze pamoja na tuelimishane kuhusu program ya Excel

Uzuri ukiijua Excel watu wataanza kukuita IT IT IT IT.

Baada ya kuijua Excel vizur nikasoma programming nasi nikawa nimeua kabisa
Kweli kabisa, mimi nilikuwa najua bahadhi ya functions na formula za excel Kwa ajili ya kuchakata matokeo ya Wanafunzi, Walimu wenzangu wakawa wananiita "Mtaalamu wa IT". Nikawa najichekea tu.
 
Mm bianfs nazichezea sana Excel lkn mnyama vlookup amegoma kichwani, naniulizaga hii kichwa inataka nini
VLookup function ni nzuri, tena sana, Kwa kuwa inarahisisha mambo mengi. Vile vile unaweza kuchakata taarifa mbalimbali pasipo kuumiza kichwa. Ni nzuri sana.
 
Mmeongelea ualimu mkanikumbusha function moja nilikua naitumia kwaajili ya kuandaa ripoti ya matokeo kwa kia mwanafunzi kwa kutumia Excell kama source na Word kama destinationation halafu nakua kama nina Mai hizo data.
Nikipata nafasi kesho jioni nitaielezea, unaweza kuitumia kuandaa individual reports mbali mbali zenye source moja
 
Hivi namna ya kuondoa zile link za vloookup kwenye formular bar baada ya michakoto yote inakuwaje?
Kwa formula zote kama unataka kuondoa ibakie data tu peke yake copy tu hizo data alafu paste hapo hapo kama Value only, formula zitatoka lkn data na format itabakia ile ile.
 
Kweli kabisa, mimi nilikuwa najua bahadhi ya functions na formula za excel Kwa ajili ya kuchakata matokeo ya Wanafunzi, Walimu wenzangu wakawa wananiita "Mtaalamu wa IT". Nikawa najichekea tu.
Unaweza tuelekeza namna ya kutengeneza ratiba ya vipindi.

Niingize majina ya walimu na madarasa, then excel inioneshe collision na suggestions.?
 
Excel ni moja ya spreadsheet pana sana,binafsi naitumia excel na google sheets kwa ajili ya kutrack KPI na kufanya baadhi ya Analysis, si lazima kumaster kila kitu kwenye hizo labda kama wewe ni mkufunzi, cha muhimu kuwa deep sehemu zinazokusaidia kwenye shughuli zako, baadhi ya functions ambazo nazitumia sana ni
1.Count & Sum functions - hizi ni countif, countifs, counta,sumif, sumifs sum n.k
2.Lookup functions - vlookup, match and index, sumproduct
3.Logic functions - if, ifs, nested ifs, and , or n.k
4.Errors - iserror, isna n.k
5.Importrange - kulink data kutoka sehemu mbalimbali ktk google sheets

Zipo nyingine ambazo nazitumia mara moja moja kutokana na situation mfano average,average if, mode,mean,max,min,filter, query n.k. Zaidi ya formula & function natumia pivot table kufanya quick analysis, na natumia Charts kwa ajili ya kusummarize matokeo na kutengeneza dashboard pia natumia Power query kwa ajili ya kuandaa data kabla ya kuzianalyse, Macros na VBA natumia mara chache sana kama nimetingwa.
Hizo za Error zinakua zipoje big
 
Kweli kabisa, mimi nilikuwa najua bahadhi ya functions na formula za excel Kwa ajili ya kuchakata matokeo ya Wanafunzi, Walimu wenzangu wakawa wananiita "Mtaalamu wa IT". Nikawa najichekea tu.
Hata Mimi aisee hii ngoma inawashinda walimu wengi sana na wengi hufanya Kwa kulazimisha
 
Unaweza tuelekeza namna ya kutengeneza ratiba ya vipindi.

Niingize majina ya walimu na madarasa, then excel inioneshe collision na suggestions.?
Mi ninachojua Kuna program maalumu inayofanya kazi ya kupanga ratiba, nimeisahahu jina, unachokielezea bado sija "experience" Kwa excel. Kwangu huwa naandaa ratiba ya kawaida ya vipindi vyangu Kwa kutumia excel, lakini kuandaa ya Shule yote Kwa Walimu wote na vipindi vyote, Kwa kutumia excel, bado sijawahi jaribu.
 
Mi ninachojua Kuna program maalumu inayofanya kazi ya kupanga ratiba, nimeisahahu jina, unachokielezea bado sija "experience" Kwa excel. Kwangu huwa naandaa ratiba ya kawaida ya vipindi vyangu Kwa kutumia excel, lakini kuandaa ya Shule yote Kwa Walimu wote na vipindi vyote, Kwa kutumia excel, bado sijawahi jaribu.
Hata kwa Excel pia inawezekana, mi ninayo hiyo template niliitengenezaga, inakuonesha na collision ya vipindi
 
Back
Top Bottom