Tujadili uhalisia wa kilimo biashara cha sasa na kilimo afya

Gwappo Mwakatobe

JF-Expert Member
Nov 22, 2019
1,494
1,874
Uhalisia wa kilimo kiitwaacho cha kibiashara (agribusiness). Kwa uelewa wa wengi ni kutumia mbolea za viwandani kwa wingi, madawa kwa wingi kwa ajili ya kuuwa wadudu. Pia ipo mbolea (kemikali) inayopuliziwa kwenye majani, si kuunga ardhini.

Matokeo yake ekari moja unayopata gunia 5 au 10 za mpunga au alizeti kwa kilimo cha asili bila mbolea na madawa, utapata gunia 30 hadi 40.

Uhalisia, si tu kilimo cha kibiashara unachopata mavuno au mazao mengi, bali pia unapata magonjwa mengi mwilini na ardhi kuharibika kabisa. Ni kilimo cha uharibifu wa mwili kiafya na kuichakaza ardhi - udongo, maji na mimea yenyewe.

Tunajitia sumu mwilini na kuiharibu kabisa ardhi na maji yaliyomo. Je, tuendelee kulima kibiashara kwa kemikali ili tupate mazao mengi na magonjwa mengi? Kuna mantiki gani ya kupata pesa nyingi na magonjwa mengi kama kansa, kisukari, magonjwa ya moyo, magonjwa ya figo, kuharibu mazingira, nakadhalika?

Na uhalisia mwingine ni huu: mazao yaliyolimwa kwa asili na kuwekwa mbolea ya asili kama vile mboji na samadi au kinyesi cha kuku, ng'ombe nk.; yatakuwa na soko sana na bei kubwa, japo ni kidogo. Ni kama vile dhahabu au madini mengine yenye thamani, unapata kidogo lakini faida kubwa sana.

Na zaidi sana, ukila mazao hayo ya asili, unajenga afya njema, si kuibomoa kwa kujitia sumu mwilini. Tutafakari!

Tuanze kampeni ya agri-health (kilimo afya) na si agribusiness (kilimo biashara)! Hiyo agribusiness ya sasa ni biashara kichaa - ashakum si matusi!
 
Uhalisia wa kilimo kiitwaacho cha kibiashara (agribusiness). Kwa uelewa wa wengi ni kutumia mbolea za viwandani kwa wingi, madawa kwa wingi kwa ajili ya kuuwa wadudu. Pia ipo mbolea (kemikali) inayopuliziwa kwenye majani, si kuunga ardhini.

Matokeo yake ekari moja unayopata gunia 5 au 10 za mpunga au alizeti kwa kilimo cha asili bila mbolea na madawa, utapata gunia 30 hadi 40.

Uhalisia, si tu kilimo cha kibiashara unachopata mavuno au mazao mengi, bali pia unapata magonjwa mengi mwilini na ardhi kuharibika kabisa. Ni kilimo cha uharibifu wa mwili kiafya na kuichakaza ardhi - udongo, maji na mimea yenyewe.

Tunajitia sumu mwilini na kuiharibu kabisa ardhi na maji yaliyomo. Je, tuendelee kulima kibiashara kwa kemikali ili tupate mazao mengi na magonjwa mengi? Kuna mantiki gani ya kupata pesa nyingi na magonjwa mengi kama kansa, kisukari, magonjwa ya moyo, magonjwa ya figo, kuharibu mazingira, nakadhalika?

Na uhalisia mwingine ni huu: mazao yaliyolimwa kwa asili na kuwekwa mbolea ya asili kama vile mboji na samadi au kinyesi cha kuku, ng'ombe nk.; yatakuwa na soko sana na bei kubwa, japo ni kidogo. Ni kama vile dhahabu au madini mengine yenye thamani, unapata kidogo lakini faida kubwa sana.

Na zaidi sana, ukila mazao hayo ya asili, unajenga afya njema, si kuibomoa kwa kujitia sumu mwilini. Tutafakari!

Tuanze kampeni ya agri-health (kilimo afya) na si agribusiness (kilimo biashara)! Hiyo agribusiness ya sasa ni biashara kichaa - ashakum si matusi!
Mawazo mbadala, kwan hatuwez kulima kibiashara na still tukatunza afya zetu na afya ya udongo? Au mkuu una neno tu na slogan ya 'kilimo biashara'
 
Mawazo mbadala, kwan hatuwez kulima kibiashara na still tukatunza afya zetu na afya ya udongo? Au mkuu una neno tu na slogan ya 'kilimo biashara'
Kilimo Afya ndio biashara inayolipa zaidi. Soma vizuri bandiko. Mazao yanayolimwa kiasili yana bei kubwa na soko kubwa pia. Lima kiafya upate biashara zaidi pasipo kuharibu miili au ardhi. Je, umewahi kufuatilia bei ya kuku aliyefugwa kienyeji na kuku wengine?

Na kama unasoma kwa makini na kuujua muktadha na maana ya bandiko, tatizo si maneno "kilimo biashara" bali kemikali zinazotumika kuumua mazao na kutudhuru. Hakuna mahali popote ambapo slogan (maneno tu) ikawa sumu mwilini na ardhini!

Aidha, fuatilia taarifa mbalimbali za madhara ya kemikali zitumikazo kwenye Kilimo.
 
Uhalisia wa kilimo kiitwaacho cha kibiashara (agribusiness). Kwa uelewa wa wengi ni kutumia mbolea za viwandani kwa wingi, madawa kwa wingi kwa ajili ya kuuwa wadudu. Pia ipo mbolea (kemikali) inayopuliziwa kwenye majani, si kuunga ardhini.

Matokeo yake ekari moja unayopata gunia 5 au 10 za mpunga au alizeti kwa kilimo cha asili bila mbolea na madawa, utapata gunia 30 hadi 40.

Uhalisia, si tu kilimo cha kibiashara unachopata mavuno au mazao mengi, bali pia unapata magonjwa mengi mwilini na ardhi kuharibika kabisa. Ni kilimo cha uharibifu wa mwili kiafya na kuichakaza ardhi - udongo, maji na mimea yenyewe.

Tunajitia sumu mwilini na kuiharibu kabisa ardhi na maji yaliyomo. Je, tuendelee kulima kibiashara kwa kemikali ili tupate mazao mengi na magonjwa mengi? Kuna mantiki gani ya kupata pesa nyingi na magonjwa mengi kama kansa, kisukari, magonjwa ya moyo, magonjwa ya figo, kuharibu mazingira, nakadhalika?

Na uhalisia mwingine ni huu: mazao yaliyolimwa kwa asili na kuwekwa mbolea ya asili kama vile mboji na samadi au kinyesi cha kuku, ng'ombe nk.; yatakuwa na soko sana na bei kubwa, japo ni kidogo. Ni kama vile dhahabu au madini mengine yenye thamani, unapata kidogo lakini faida kubwa sana.

Na zaidi sana, ukila mazao hayo ya asili, unajenga afya njema, si kuibomoa kwa kujitia sumu mwilini. Tutafakari!

Tuanze kampeni ya agri-health (kilimo afya) na si agribusiness (kilimo biashara)! Hiyo agribusiness ya sasa ni biashara kichaa - ashakum si matusi!
Kilimo Afya, Mbolea unaweka kinyesi Cha kuku Hawa wa kizungu!?
 
Habari naomba nikusahihishe kidogo. Tukisema kilimo biashara hatusemi kuweka madawa na mbolea zaidi,mavuno makubwa hayatokani tu na mbolea au madawa zaidi bali hutokana na mbegu bora yenye uwezo wa kuzalisha zaidi.
Hivyo kilimo biashara ni kulima kisasa kuhakikisha unapata zaidi kwenye eneo dogo.
Wingi wa madawa au mmea hauongezi uzalishaji kama mmea unatoa kilo 3 hata uweke mbolea kg50 kwa shina bado utatoa kilo 3 tu, hivyo kuna sehemu tunakosea wakulima kuamini mbolea na madawa zaidi ndio mavuno wakati tunaharibu ardhi. Ziko dawa zimeandikwa kabisa puliza kila baada ya wiki 2 kwa mfano na tumia robo kwa ekari moja ila sisi hatusomi tunafanya kimazoea dawa inapigwa kila wiki na kiwango kikubwa zaidi mpaka mmea unadumaa yote ni madhara makubwa sana kwa mlaji na mmea pia. Kilimo biashara ni kufanya kila kitu ukiangalia mapato na matumizi na faida.
Hivyo namalizia kusema wanaoweka madawa na mbolea zaidi ni ukosefu wa taaluma na wala sio kilimo biashara.
Ahsante sana
 
Habari naomba nikusahihishe kidogo. Tukisema kilimo biashara hatusemi kuweka madawa na mbolea zaidi,mavuno makubwa hayatokani tu na mbolea au madawa zaidi bali hutokana na mbegu bora yenye uwezo wa kuzalisha zaidi.
Hivyo kilimo biashara ni kulima kisasa kuhakikisha unapata zaidi kwenye eneo dogo.
Wingi wa madawa au mmea hauongezi uzalishaji kama mmea unatoa kilo 3 hata uweke mbolea kg50 kwa shina bado utatoa kilo 3 tu, hivyo kuna sehemu tunakosea wakulima kuamini mbolea na madawa zaidi ndio mavuno wakati tunaharibu ardhi. Ziko dawa zimeandikwa kabisa puliza kila baada ya wiki 2 kwa mfano na tumia robo kwa ekari moja ila sisi hatusomi tunafanya kimazoea dawa inapigwa kila wiki na kiwango kikubwa zaidi mpaka mmea unadumaa yote ni madhara makubwa sana kwa mlaji na mmea pia. Kilimo biashara ni kufanya kila kitu ukiangalia mapato na matumizi na faida.
Hivyo namalizia kusema wanaoweka madawa na mbolea zaidi ni ukosefu wa taaluma na wala sio kilimo biashara.
Ahsante sana
Nimeandika uelewa wa wengi, si wa wote (wewe ukiwemo)
Habari naomba nikusahihishe kidogo. Tukisema kilimo biashara hatusemi kuweka madawa na mbolea zaidi,mavuno makubwa hayatokani tu na mbolea au madawa zaidi bali hutokana na mbegu bora yenye uwezo wa kuzalisha zaidi.
Hivyo kilimo biashara ni kulima kisasa kuhakikisha unapata zaidi kwenye eneo dogo.
Wingi wa madawa au mmea hauongezi uzalishaji kama mmea unatoa kilo 3 hata uweke mbolea kg50 kwa shina bado utatoa kilo 3 tu, hivyo kuna sehemu tunakosea wakulima kuamini mbolea na madawa zaidi ndio mavuno wakati tunaharibu ardhi. Ziko dawa zimeandikwa kabisa puliza kila baada ya wiki 2 kwa mfano na tumia robo kwa ekari moja ila sisi hatusomi tunafanya kimazoea dawa inapigwa kila wiki na kiwango kikubwa zaidi mpaka mmea unadumaa yote ni madhara makubwa sana kwa mlaji na mmea pia. Kilimo biashara ni kufanya kila kitu ukiangalia mapato na matumizi na faida.
Hivyo namalizia kusema wanaoweka madawa na mbolea zaidi ni ukosefu wa taaluma na wala sio kilimo biashara.
Ahsante sana
Nimeandika uelewa wa wengi, si wa wote (ukiwemo wewe). Aidha, nimetaja matumizi mbadala ya mboji au samadi ambayo ni rafiki kwa afya na mazingira. Labda umeelewa tofauti na muktadha wa bandiko ulivyo.
 
Hongera kwa mawazo mazuri na chanya!

Terms ulizotumia haziendani na maelezo yako! Nadhani ulitaka kusema organic farming and inorganic farming

Maana mtu anaefanya organic farming hufanya agribusiness pia, mfano karanga ya korosho-hai inaweza kuwa kidogo lakini ikawa na bei kubwa mara tatu ya karanga ya korosho- mfu japo ipo kwa wingi
 
Wapi ilipofanyika,... nami nikajifunze kwa mkulima aliyelima angalau ekari moja!
Wapo wakulima wengi tu maeneo mengi nchini, wana hata zaidi ya ekari moja, nikiwemo mimi. Njoo Rukwa uone mashamba ya mahindi, alizeti, ngano, maharage, soya au karanga yaliyowekwa mboji au samadi. Mengine hayajawekwa mbolea yoyote.

Hata usipoona fanya mwenyewe au kapate ushauri wa kitaalamu SUA.

Aidha, samadi ni nafuu sana na wafugaji wengine hugawa bure kwenye mazizi yao.
 
Hongera kwa mawazo mazuri na chanya!

Terms ulizotumia haziendani na maelezo yako! Nadhani ulitaka kusema organic farming and inorganic farming

Maana mtu anaefanya organic farming hufanya agribusiness pia, mfano karanga ya korosho-hai inaweza kuwa kidogo lakini ikawa na bei kubwa mara tatu ya karanga ya korosho- mfu japo ipo kwa wingi
Nimeandika lugha rahisi ya Kiswahili inayoeleweka na wengi. Unapochanganya Kiingereza na Kiswahili maelezo yako yanaweza yasieleweke kabisa pasipo tafsiri! Kwa kukusaidia "Organic forming" tafsiri rahisi sana ni matumizi ya mboji au samadi inayoeleweka na mengi.

Ama andika mbolea ya asili (si ya viwandani) au itokanayo na mimea na wanyama. Nasisitiza unapoandika Kiingereza weka bayana tafsiri yake!
 
Wapo wakulima wengi tu maeneo mengi nchini, wana hata zaidi ya ekari moja, nikiwemo mimi. Njoo Rukwa uone mashamba ya mahindi, alizeti, ngano, maharage, soya au karanga yaliyowekwa mboji au samadi. Mengine hayajawekwa mbolea yoyote.

Hata usipoona fanya mwenyewe au kapate ushauri wa kitaalamu SUA.

Aidha, samadi ni nafuu sana na wafugaji wengine hugawa bure kwenye mazizi yao.
"mashamba ya mahindi, alizeti, ngano, maharage, soya au karanga"

Mazao haya yote yaliyotajwa kwa asili si yanayotumia Mbolea kwa wingi, pia hayashambuliwi Sana na wadudu!

Unaongeleaje, Matikiti, Nyanya, Vitunguu... mmeshalima kwa mfumo huo?
 
"mashamba ya mahindi, alizeti, ngano, maharage, soya au karanga"

Mazao haya yote yaliyotajwa kwa asili si yanayotumia Mbolea kwa wingi, pia hayashambuliwi Sana na wadudu!

Unaongeleaje, Matikiti, Nyanya, Vitunguu... mmeshalima kwa mfumo huo?
Inawezekana unaishi mijini ambako hujawahi kuona mbegu za mahindi zikitiwa dawa au mahindi yakiungwa mbolea za viwandani kuanzia kupanda na kukuzia, kupaliliwa kwa madawa na kuhifadhiwa kwa madawa. Kama ndivyo mjadala huu haukuhusu!

Kama unafuatilia mazao ya mbogamboga yanayonunuliwa kwa bei kubwa Ulaya ni yale ambayo yana alama za kuliwa na wadudu pasipo kuwapulizia dawa. Wadudu si kemikali! Aidha, nikupanue ufahamu kidogo kuwa kuna mimea ambayo ukipanda na mazao yako pamoja haishambuliwi na wadudu. Pia zipo njia za asili za kuondoa wadudu.

Niongezee kwamba mahindi siku hizi yanatunzwa kwenye mifuko maalum isiyoingiza wadudu miaka yote pasipo kuwekewa dawa. Nenda SUA wakakupe elimu ya Kilimo Afya pasipo kutumia mbolea za viwandani na kemikali ili ulime nyaya, matiki, bamia, nk.; pasina madawa!
 
Inawezekana unaishi mijini ambako hujawahi kuona mbegu za mahindi zikitiwa dawa au mahindi yakiungwa mbolea za viwandani kuanzia kupanda na kukuzia, kupaliliwa kwa madawa na kuhifadhiwa kwa madawa. Kama ndivyo mjadala huu haukuhusu!

Kama unafuatilia mazao ya mbogamboga yanayonunuliwa kwa bei kubwa Ulaya ni yale ambayo yana alama za kuliwa na wadudu pasipo kuwapulizia dawa. Wadudu si kemikali! Aidha, nikupanue ufahamu kidogo kuwa kuna mimea ambayo ukipanda na mazao yako pamoja haishambuliwi na wadudu. Pia zipo njia za asili za kuondoa wadudu.

Niongezee kwamba mahindi siku hizi yanatunzwa kwenye mifuko maalum isiyoingiza wadudu miaka yote pasipo kuwekewa dawa. Nenda SUA wakakupe elimu ya Kilimo Afya pasipo kutumia mbolea za viwandani na kemikali ili ulime nyaya, matiki, bamia, nk.; pasina madawa!
Nimezurura Gaza vya kutosha, niambie uhalisia nisioujua usinitume kididimo nikakutane na mugru wa kitambo!
 
Nimezurura Gaza vya kutosha, niambie uhalisia nisioujua usinitume kididimo nikakutane na mugru wa kitambo!
Mathalani, kusema mahindi kwa asili hayatumii mbolea ni kutojua uhalisia. Nenda kwa wenye mashamba ya mahindi wakupe uhalisia. Na labda watakuambia walivyopoteza mbegu za asili.
 
Uhalisia wa kilimo kiitwaacho cha kibiashara (agribusiness). Kwa uelewa wa wengi ni kutumia mbolea za viwandani kwa wingi, madawa kwa wingi kwa ajili ya kuuwa wadudu. Pia ipo mbolea (kemikali) inayopuliziwa kwenye majani, si kuunga ardhini.

Matokeo yake ekari moja unayopata gunia 5 au 10 za mpunga au alizeti kwa kilimo cha asili bila mbolea na madawa, utapata gunia 30 hadi 40.

Uhalisia, si tu kilimo cha kibiashara unachopata mavuno au mazao mengi, bali pia unapata magonjwa mengi mwilini na ardhi kuharibika kabisa. Ni kilimo cha uharibifu wa mwili kiafya na kuichakaza ardhi - udongo, maji na mimea yenyewe.

Tunajitia sumu mwilini na kuiharibu kabisa ardhi na maji yaliyomo. Je, tuendelee kulima kibiashara kwa kemikali ili tupate mazao mengi na magonjwa mengi? Kuna mantiki gani ya kupata pesa nyingi na magonjwa mengi kama kansa, kisukari, magonjwa ya moyo, magonjwa ya figo, kuharibu mazingira, nakadhalika?

Na uhalisia mwingine ni huu: mazao yaliyolimwa kwa asili na kuwekwa mbolea ya asili kama vile mboji na samadi au kinyesi cha kuku, ng'ombe nk.; yatakuwa na soko sana na bei kubwa, japo ni kidogo. Ni kama vile dhahabu au madini mengine yenye thamani, unapata kidogo lakini faida kubwa sana.

Na zaidi sana, ukila mazao hayo ya asili, unajenga afya njema, si kuibomoa kwa kujitia sumu mwilini. Tutafakari!

Tuanze kampeni ya agri-health (kilimo afya) na si agribusiness (kilimo biashara)! Hiyo agribusiness ya sasa ni biashara kichaa - ashakum si matusi!
Mkuu Gwappo...

Ahsante kwa maada hii fikirishi. Maendeleo ya wagu, ongezeko la watu duniani yameleta haya tunayaita mapinduzi ya kilimo duniani. Hapo zamani katika maeneo yetu mengi idadi ya watu ilikuwa ni ndogo saana hivi kulima kwa asili ama kwa kutumia mbegu za asili kuliweza kusaidia katika kutosheleza mahitaji husika ya watu.

Tulikuwa na mbegu za asili ambazo huzalisha kidogo , hukabiliwa na magonjwa saana,hazistahimili ukame n.k.

Ongezeko la joto duniani , kukauka kwa vyanzo vya maji ukame na mengine mengine yamepelekea kuwa na tafiti zitakazo leta mbadala wa changamoto zote hizi na kusaidia kuongeza idadi ya uzalishaji na kuepukana na changamoto za usalama wa chakula duniani.

Hata hivyo kulima kibishara kwa maana ya chakula chenye afya inawezekana tuu ... changamoto ni kuwa mtu atazalisha kidogo kwa muda mrefu na kuleta hasara katika maana ya value ya muda.

N.B.
Kilimo cha kuangalia afya ndicho kilicho bora katika kuyapa maisha yetu maana . Lakini changamoto tuliyonayo katika maendeleo yetu hayatupi nafasi nzuri katika hili
 
Mathalani, kusema mahindi kwa asili hayatumii mbolea ni kutojua uhalisia. Nenda kwa wenye mashamba ya mahindi wakupe uhalisia. Na labda watakuambia walivyopoteza mbegu za asili.
Mche wa mhindi unaweza kutoa matokeo kwa gm 15 za Mbolea ya kiwandani wakati mche wa Nyanya unahiataji gm 45!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom