Goodluck Mshana
JF-Expert Member
- Aug 7, 2011
- 1,271
- 1,119
USHURU DARAJA LA KIGAMBONI
Hongera kwa waliofanikisha mradi wa daraja la Kigamboni. Iwe ni serikali ama NSSF. Juhudi zote hizo lengo ni kumsaidia mtanzania. Kumpunguzia adha na bugdha mkazi wa Kigamboni. Kumhakikishia mwananchi usalama wa maisha yake haswa ukilinganisha na ule mchezo wa feri zetu zilizokuwa zikizima na kuharibika mara kwa mara.
Hongera Rais JPM kwa uzinduzi na hivyo kubariki matumizi yake.
Anyway, hoja yangu sio kufurahia uzinduzi wa daraja.. Ama kuzungumzia katumbuliwa kwa Bi. Anne Kilango Malecela. Hoja yangu ni malipo ya matumizi kwa daraja hilo. Labda tujiulize swali moja lakini yenye mantiki kidogo na linalobeba dhana nzima ya matumizi ya daraja.
Swali: Daraja limejengwa na Serikali au mtu binafsi?
Labda tuanze na mifano. Ukifika nchini India utakutana na madaraja, barabara na treni zenye uasili wa daraja la Kigamboni. Kwa maana ya kutoza watumiaji wake. Ukichukua barabara ya kutoka Nerhu Place mpaka ilipo Taj Mahal utakutana na vizuizi njiani. Kila baada ya kilometres kadhaa unalipia matumizi ya barabara. Malipo yote utakayoyafanya yatategemea umbali uendao. Kwa maana ya kwamba ukimua kuendesha gari lako hapa hadi Kibaha. Utalipia umbali wa Kibaha. Ukienda Mbeya au Kilimanjaro, utalipia vivyo hivyo.
Kadhalika kwenye njia za treni. Malipo yote hufanyika kwenye vituo vya treni (metro station). Ukitaka kulipa cash money utalipa. Ukitaka kutumia rechargeable card ni wewe tu. Lakini mifumo yote hii ni tofauti.
Wenzetu wana miuondo mbinu ya aina mbili. Private na Government infrastructure. Kwa miuondo msingi ambayo ni private lazima mtumiaji alipe. Achangie investment cost ili mwisho wa siku watu watengeneze faida. Upande wa pili ni wa serikali. Ambapo matumizi yake ni bure kabisa. Mwananchi halazimiki kulipia popote maana ni miradi ya serikali. Ni miradi inaonekana na kodi za wananchi. Ni miradi iliyoanzishwa kusaidia kizazi cha maskini na mtu wa daraja la kati ambaye hawezi nunua helicopter. Miradi kwaajili ya mtu asiyeweza kupewa tenda za polisi kama Lugumi.
Sasa unaweza shangaa. Kwanini watu wanatumia hiyo ya kulipia na kuacha ya bure ya serikali?! Jibu ni kwamba miuondo mbinu ya serikali ni chakavu na haijatunzwa. Road map yake ni ndevu kuelekea uendako. Hii ya private imetunzwa na humchukua muda mfupi mtumiaji kufika anakokwenda. Ina security cameras. In case unapata shida basi wahusika watakuja on the spot na kukusaidia.
Sasa daraja la Kigamboni linapaswa kulipiwa! Daraja la serikali. Mali ya wananchi wanailipia. Kuna utofauti gani kati ya daraja hili na lile la Salender, lile la Mkapa kule Kibiti, daraja la Wami n.k? Je hili limejengwa na Lugumi Investment Co. Ltd?! Hata kama limejengwa na NSSF. Je serikali haiwezi kurejesha deni hilo kwa NSSF na kuwaacha wananchi wakafaidi matunda ya kodi zao?! Kila mwaka deni la Taifa linapanda. Huyo mkopaji ni nani? Na hizo pesa huwa zinaenda wapi?
Rai yangu kwa JPM.
Mh. Rais wapo waliojenga imani kubwa na wewe. Wapo Watanzania ambao wamerejesha utamaduni wa kuwahi taarifa ya Habari ya saa mbili wakitaka kujua Rais wao kafanya nini leo. Utamaduni huu ulishatoweka na kurejea kwake ni imani ya wananchi waliyonayo kwako. Wapunguzie adha Watanzania kwa kutembea bure juu ya daraja Lao. Wapite bure maana mradi huu huenda ulikuwa ni deal la watu. Kama kweli makatibu wataenda Bungeni kwa mabasi na hivyo kuokoa kiasi hicho cha pesa. Basi pesa hiyo ikalipe deni la NSSF kama ilivyokuwa kwa pesa za sherehe za Uhuru.
Washawishi matajiri wa nchi hii kuungana na kuanzisha miradi ya treni za umeme, private roads, n.k Serikali haiwezi fanya kila kitu. Wapeni uwezo wa kuwekeza. Pawepo na monitoring and evaluation ya uendeshwaji miradi hiyo ili siku ya mwisho irudi na kuwa mali ya serikali (baada ya wao kutengeneza faida).
Daraja la Kigamboni liwe huru, lilindwe na litunze na wote. Liwe la BURE kama ilivyo TBC.
By Goodluck Mshana
Hongera kwa waliofanikisha mradi wa daraja la Kigamboni. Iwe ni serikali ama NSSF. Juhudi zote hizo lengo ni kumsaidia mtanzania. Kumpunguzia adha na bugdha mkazi wa Kigamboni. Kumhakikishia mwananchi usalama wa maisha yake haswa ukilinganisha na ule mchezo wa feri zetu zilizokuwa zikizima na kuharibika mara kwa mara.
Hongera Rais JPM kwa uzinduzi na hivyo kubariki matumizi yake.
Anyway, hoja yangu sio kufurahia uzinduzi wa daraja.. Ama kuzungumzia katumbuliwa kwa Bi. Anne Kilango Malecela. Hoja yangu ni malipo ya matumizi kwa daraja hilo. Labda tujiulize swali moja lakini yenye mantiki kidogo na linalobeba dhana nzima ya matumizi ya daraja.
Swali: Daraja limejengwa na Serikali au mtu binafsi?
Labda tuanze na mifano. Ukifika nchini India utakutana na madaraja, barabara na treni zenye uasili wa daraja la Kigamboni. Kwa maana ya kutoza watumiaji wake. Ukichukua barabara ya kutoka Nerhu Place mpaka ilipo Taj Mahal utakutana na vizuizi njiani. Kila baada ya kilometres kadhaa unalipia matumizi ya barabara. Malipo yote utakayoyafanya yatategemea umbali uendao. Kwa maana ya kwamba ukimua kuendesha gari lako hapa hadi Kibaha. Utalipia umbali wa Kibaha. Ukienda Mbeya au Kilimanjaro, utalipia vivyo hivyo.
Kadhalika kwenye njia za treni. Malipo yote hufanyika kwenye vituo vya treni (metro station). Ukitaka kulipa cash money utalipa. Ukitaka kutumia rechargeable card ni wewe tu. Lakini mifumo yote hii ni tofauti.
Wenzetu wana miuondo mbinu ya aina mbili. Private na Government infrastructure. Kwa miuondo msingi ambayo ni private lazima mtumiaji alipe. Achangie investment cost ili mwisho wa siku watu watengeneze faida. Upande wa pili ni wa serikali. Ambapo matumizi yake ni bure kabisa. Mwananchi halazimiki kulipia popote maana ni miradi ya serikali. Ni miradi inaonekana na kodi za wananchi. Ni miradi iliyoanzishwa kusaidia kizazi cha maskini na mtu wa daraja la kati ambaye hawezi nunua helicopter. Miradi kwaajili ya mtu asiyeweza kupewa tenda za polisi kama Lugumi.
Sasa unaweza shangaa. Kwanini watu wanatumia hiyo ya kulipia na kuacha ya bure ya serikali?! Jibu ni kwamba miuondo mbinu ya serikali ni chakavu na haijatunzwa. Road map yake ni ndevu kuelekea uendako. Hii ya private imetunzwa na humchukua muda mfupi mtumiaji kufika anakokwenda. Ina security cameras. In case unapata shida basi wahusika watakuja on the spot na kukusaidia.
Sasa daraja la Kigamboni linapaswa kulipiwa! Daraja la serikali. Mali ya wananchi wanailipia. Kuna utofauti gani kati ya daraja hili na lile la Salender, lile la Mkapa kule Kibiti, daraja la Wami n.k? Je hili limejengwa na Lugumi Investment Co. Ltd?! Hata kama limejengwa na NSSF. Je serikali haiwezi kurejesha deni hilo kwa NSSF na kuwaacha wananchi wakafaidi matunda ya kodi zao?! Kila mwaka deni la Taifa linapanda. Huyo mkopaji ni nani? Na hizo pesa huwa zinaenda wapi?
Rai yangu kwa JPM.
Mh. Rais wapo waliojenga imani kubwa na wewe. Wapo Watanzania ambao wamerejesha utamaduni wa kuwahi taarifa ya Habari ya saa mbili wakitaka kujua Rais wao kafanya nini leo. Utamaduni huu ulishatoweka na kurejea kwake ni imani ya wananchi waliyonayo kwako. Wapunguzie adha Watanzania kwa kutembea bure juu ya daraja Lao. Wapite bure maana mradi huu huenda ulikuwa ni deal la watu. Kama kweli makatibu wataenda Bungeni kwa mabasi na hivyo kuokoa kiasi hicho cha pesa. Basi pesa hiyo ikalipe deni la NSSF kama ilivyokuwa kwa pesa za sherehe za Uhuru.
Washawishi matajiri wa nchi hii kuungana na kuanzisha miradi ya treni za umeme, private roads, n.k Serikali haiwezi fanya kila kitu. Wapeni uwezo wa kuwekeza. Pawepo na monitoring and evaluation ya uendeshwaji miradi hiyo ili siku ya mwisho irudi na kuwa mali ya serikali (baada ya wao kutengeneza faida).
Daraja la Kigamboni liwe huru, lilindwe na litunze na wote. Liwe la BURE kama ilivyo TBC.
By Goodluck Mshana