Tujadili nyumba wanazojengewa Marais Wastaafu Tanzania

Hii ni hulka ya viongozi wote wa nchi masikini na hasa Afrika. Hujifikiria wao na kutaka kujikusanyia kila kitu.

Marais wote wanapokuwa madarakani nyumba zao hukarabatiwa kwa gharama ya serikali kwavile zinakuwa ni ''Ikulu'' wakati wowote. Hivyo, Rais Mwinyi na Kikwete wana nyumba zao.

Pili, viongozi wastaafu wanapewa asilimia 80% ya mshahara wao( Rejea mafao ya viongozi wa juu)
Wanapewa ulinzi na huduma zote kama zile walizopata wakiwa Ikulu.

Hawa si wanyonge

Nyumba wanazojengewa thamani zake ni kubwa kuliko vituo vya afya.

Lakini muhimu ni kuwatazama kama wana manufaa yoyote kwa Taifa baada ya uongozi.
Hawa kazi yao ni kupigia debe CCM na chama kingefanya taratibu za kuwahudumia si kodi za wananchi

Hawana kingine tunachoweza kujivunia kama walipa kodi. Hili ni hulka tu ya kujikusanyia na kujilimbikizia kwa gharama za wananchi. Tunahitaji vituo vya afya vya umma si nyumba binafsi

JokaKuu tindo Pascal Mayalla
Umeeleweka vizuri

Ova

Sent from my SM-N920T using JamiiForums mobile app
 
1. Naomba kujua nyumba Mwalimu aliyojengewa na serikali ilijengwa lini na wapi?

2. Naomba kujua Mkapa alijengewa nyumba yake wapi?

3. Naomba kujua kwa changamoto wananchi tulizonazo Hawa wazee wakitoa sadaka hizo pesa za nyumba zikajenga japo hospital haitakubalika?

4. Hawa viongozi wanaojengewa nyumba baada yakuondoka madarakani wakiwa wazee, awali walikua wanaishi wapi?

5. Natambua ni takwa la kisheria ila najiuliza kwanini sasa? Mwinyi kastaafu muda gani?

6. Kwa marais wa Zanzibar, je huu utaratibu unawahusu?

Ushauri
Haya mafao ya nyumba za marais yafutwe, sheria itamkwe atalipwa kiasi flani (thamani ya hiyo nyumba) na Mstaafu atawajibika kuchagua eneo ambapo fedha hizo zitatumika kujenga mradi wa wananchi Kama ukumbusho.
Siasa ni Sayansi
 
Ben alimjengeaga JkN kule Mwitongo kwa kuwa aliona hakuwa na nyumba ya hadhi ila hawa wazee ambao walikula hela zetu mabilion kwa mabilion siungi mkono

Marais WOTE wana MAHEKALU YAO TAYARI,

HII MAMBO Magufuli UMETOA WAPI?

YANINI?

KWA FAIDA GANI?

Msoga = Kikwete
Lushoto = Rip Mkapa
Mjimwema = Mwinyi
Mwitongo = Baba wa Taifa

HUKO MASAKI NANI KASEMA?

HUO NI UHUJUMU WA MALI YA UMMA.
 
1. Naomba kujua nyumba Mwalimu aliyojengewa na serikali ilijengwa lini na wapi?

2. Naomba kujua Mkapa alijengewa nyumba yake wapi?

3. Naomba kujua kwa changamoto wananchi tulizonazo Hawa wazee wakitoa sadaka hizo pesa za nyumba zikajenga japo hospital haitakubalika?

4. Hawa viongozi wanaojengewa nyumba baada yakuondoka madarakani wakiwa wazee, awali walikua wanaishi wapi?

5. Natambua ni takwa la kisheria ila najiuliza kwanini sasa? Mwinyi kastaafu muda gani?

6. Kwa marais wa Zanzibar, je huu utaratibu unawahusu?

Ushauri
Haya mafao ya nyumba za marais yafutwe, sheria itamkwe atalipwa kiasi flani (thamani ya hiyo nyumba) na Mstaafu atawajibika kuchagua eneo ambapo fedha hizo zitatumika kujenga mradi wa wananchi Kama ukumbusho.
Acha wivu
 
Suala sio kujengewa tu aina/ukubwa wa nyumba unafikirisha sana kitu kinachopelekea gharama ya nyumba kuwa kubwa kuliko idadi ya watu kwenye familia za wahusika! Halafu kuna mwananchi kule Kigoma anashuhudia haya huku akinywa Maji kwenye kisima ambacho mifugo hunywa maji pia!
inaumiza sana....ngoja niishie kukaa kmya
 
Hujasoma mahali imeandikwa kuwa;

".....kila mwenye nacho huongezewa na asiyekuwa nacho hunyang'anywa hata kile kidogo alichonacho....?"

Yes, sisi hatuna hata mfano tu wa nyumba, lakini hawa waliokuwa tunawalipa mishahara ya mamilioni kila mwezi, posho na marupurupu ya kila namna leo eti wanajengewa nyuma toka katika michango yetu kidogo dogo tunayolipa kama kodi..

Kama siyo kituko unadhani ni nini?
Walikuwa na nyumba sasa wanajengewa makasri ambayo pengine hawakuwa nayo kuonyesha utukufu wao!
 
Je wamkumbuka yule rais wa Uruguay?! Kastaafu na kajumba ka kawaida tu na ka gari beetle, na ukumbuke Uruguay ni nchi tajiri kuliko sisi, sasa viongozi wetu lazima wawe na mahekalu kadhaa, magari makubwa kadhaa, ac bank iliyonona, wafanyakazi na vijakazi wakutosha...inasikitisha sana kwa kweli. Kabla ya kujengewa kwani walikuwa wanalala nje?!
Halafu eti tuzidi kuwapa kura wale zaidi?! Hakuna kabisa.
 
Ni kweli uliyoyasema, lakini kwa nini nyumba ya raisi wa awamu ya pili imechelewa kujengwa wakati nyumba ya awamu ya tatu ilishakamilika na kukabidhiwa muhusika? Na kwa nini zinakabidhiwa sasa hivi wakati nyumba ya mheshimiwa Kikwete bado haijakamilika? Jee haya si mambo ya kampeni tu? Au mheshimiwa raisi anaona bora ayamalize kabisa huko mbele hakutabiriki?
Wakati ile sheria inaanza utekelezwaji ilikuwa awamu ya Mkapa na ndiyo maana alijengewa baada ya kustaafu akakabidhiwa 2007. Baada ya hapo wakaona kwanini wasimjengee Mzee Mwinyi naye. Mchakato ukaanza pia awamu ya Jakaya ila mradi haukukamilika baada ya Serikali kutotoa pesa kwa wakati na kusababisha mkandarasi kuondoka Site.

Awamu ya Magufuli ndiyo ikaufufua mradi ule ambapo mkandarasi aliyeachia njiani akaleta gharama kubwa mno, Si unajua tena Magufu akasema TBA na Suma JKT walete bajeti zao ambapo makadirio yao yalikuwa chini Tsh. BILIONI 1.1 na ushee kulinganisha na makandarasi wa awali, Suma JKT wakala shavu.

Nina maana kwamba hizi siyo kampeni kivile ile timing ndo imepelekea uone kampeni.
 
1. Naomba kujua nyumba Mwalimu aliyojengewa na serikali ilijengwa lini na wapi?

2. Naomba kujua Mkapa alijengewa nyumba yake wapi?

3. Naomba kujua kwa changamoto wananchi tulizonazo Hawa wazee wakitoa sadaka hizo pesa za nyumba zikajenga japo hospital haitakubalika?

4. Hawa viongozi wanaojengewa nyumba baada yakuondoka madarakani wakiwa wazee, awali walikua wanaishi wapi?

5. Natambua ni takwa la kisheria ila najiuliza kwanini sasa? Mwinyi kastaafu muda gani?

6. Kwa marais wa Zanzibar, je huu utaratibu unawahusu?

Ushauri
Haya mafao ya nyumba za marais yafutwe, sheria itamkwe atalipwa kiasi flani (thamani ya hiyo nyumba) na Mstaafu atawajibika kuchagua eneo ambapo fedha hizo zitatumika kujenga mradi wa wananchi Kama ukumbusho.
Hii ni mojawapo ya sababu LUKUKI za kupigia Lissu kura ili kuwaondosha hawa wanyonyaji WAKOLONI WEUSI.
 
1. Naomba kujua nyumba Mwalimu aliyojengewa na serikali ilijengwa lini na wapi?

2. Naomba kujua Mkapa alijengewa nyumba yake wapi?

3. Naomba kujua kwa changamoto wananchi tulizonazo Hawa wazee wakitoa sadaka hizo pesa za nyumba zikajenga japo hospital haitakubalika?

4. Hawa viongozi wanaojengewa nyumba baada yakuondoka madarakani wakiwa wazee, awali walikua wanaishi wapi?

5. Natambua ni takwa la kisheria ila najiuliza kwanini sasa? Mwinyi kastaafu muda gani?

6. Kwa marais wa Zanzibar, je huu utaratibu unawahusu?

Ushauri
Haya mafao ya nyumba za marais yafutwe, sheria itamkwe atalipwa kiasi flani (thamani ya hiyo nyumba) na Mstaafu atawajibika kuchagua eneo ambapo fedha hizo zitatumika kujenga mradi wa wananchi Kama ukumbusho.

Wabinafsi Marais wenzao wanajali mambo waliyofanya na wanajenga Library za kumbukumbu zao wakati wa uongozi lakini wenzetu wanahitaji wajengewe ikulu za binafsi wakati tayari wana nyumba. Kikwete ana nyumba ya serikali, Mkapa, Magufuli tena kajenga na apartment pale St Peter's. Sasa nyumba za nini? wakati nchi masikini.
 
Yawezekana ikawa ni nia njema tu ya Serikali ila 'Kinachonishangaza' na 'Kunisikitisha' hawa Wote 'wanaojengewa' wana Majumba yao mengi sana.
CCM wamehalalisha wizi wa mali za Umma, mchana kweupe. Aibu sana hii.
 
Back
Top Bottom