Gelion Kayombo
Senior Member
- Feb 17, 2018
- 149
- 193
Hebu tuzungumze leo juu ya ubaguzi. Mara nyingi huwa tunasikia na kuangalia kwenye vyombo vya habari juu ya ubaguzi dhidi ya watu wengine. Mara nyingi habari zinazosikika zaidi ni kwamba watu wenye ngozi nyeupe(wazungu), wanawabagua watu wa rangi(weusi). Utasikia watu waishio nje ya bara la Afrika na ndani ya bara la Afrika hasa kama umeajiriwa na watu weupe wanalalamika kwamba washawahi kubaguliwa kwa mwonekano wao, rangi, umbo na katika kazi.
Hata hivyo habari za ubaguzi huwa zinasikika sana kama mtu au watu mashuhuri wamepatwa na kadhia hii hasa, wanamichezo wa kandanda wenye rangi, wanaochezea vilabu vya nje ya bara la Afrika. Mara nyingine utasikia wananchi waishio ndani ya nchi (ambao wamewahi kufanya kazi na watu weupe) wanalalamika juu ya kubaguliwa kwa namna moja au nyingine.
Lakini mimi nataka kujua, hivi ni kweli watu wenye ngozi nyeupe pekee ndio wanaowabagua watu wenye rangi nyeusi?. Kama ni ndiyo, je, sisi watu wenye rangi huwa hatubaguani sisi kwa sisi kwa namna moja au nyingine? Kwa maana utaona mtu mwenye rangi anamtukana mwenye rangi mwenzie kwamba ni mweusi sana, au mweupe sana, mfupi sana au mrefu sana. Vivi hivyo na kwenye kazi utaona watu wa rangi wanabaguana.
Je, wewe ushawahi kubaguliwa na Mwafrika mwenzako kwa namna moja au nyingine iwe ni kwa mwonekano wako, rangi yako, umbo lako na hata katika kazi?. Kama ni ndiyo je, huo siyo ubaguzi?. Au ubaguzi ni pale tu ukifanywa na watu weupe(wazungu) kwa mtu mwenye rangi? Na vipi kama Mzungu akimbagua Mzungu mwenzie au Mwafrika akimbagua Mwafrika mwenzie, hapo utakuwa ubaguzi au kuna neno jingine la kutumia?.
Karibuni kwa mjadala.
Hata hivyo habari za ubaguzi huwa zinasikika sana kama mtu au watu mashuhuri wamepatwa na kadhia hii hasa, wanamichezo wa kandanda wenye rangi, wanaochezea vilabu vya nje ya bara la Afrika. Mara nyingine utasikia wananchi waishio ndani ya nchi (ambao wamewahi kufanya kazi na watu weupe) wanalalamika juu ya kubaguliwa kwa namna moja au nyingine.
Lakini mimi nataka kujua, hivi ni kweli watu wenye ngozi nyeupe pekee ndio wanaowabagua watu wenye rangi nyeusi?. Kama ni ndiyo, je, sisi watu wenye rangi huwa hatubaguani sisi kwa sisi kwa namna moja au nyingine? Kwa maana utaona mtu mwenye rangi anamtukana mwenye rangi mwenzie kwamba ni mweusi sana, au mweupe sana, mfupi sana au mrefu sana. Vivi hivyo na kwenye kazi utaona watu wa rangi wanabaguana.
Je, wewe ushawahi kubaguliwa na Mwafrika mwenzako kwa namna moja au nyingine iwe ni kwa mwonekano wako, rangi yako, umbo lako na hata katika kazi?. Kama ni ndiyo je, huo siyo ubaguzi?. Au ubaguzi ni pale tu ukifanywa na watu weupe(wazungu) kwa mtu mwenye rangi? Na vipi kama Mzungu akimbagua Mzungu mwenzie au Mwafrika akimbagua Mwafrika mwenzie, hapo utakuwa ubaguzi au kuna neno jingine la kutumia?.
Karibuni kwa mjadala.