HorsePower
JF-Expert Member
- Aug 22, 2008
- 3,612
- 2,569
Imagine kama ni ww umeishi na kijana kama 6month hivi halafu mnashindwana tabia, jamii itakuchukuliaje? baada ya hapo unatafuta mwingine ambae mtaoana hapo baadae nae unaishi nae miezi mitano mnasomana tabia kisha unagundua hafai. Unatafuta mwingine tena inakuwa mwendelezo..........endless.
Nafikiri ndoa ni muhimu sana kama nafasi ya kufunga ndoa ipo kuliko kuishi na mtu. Ndoa na harusi Inakupa amani, uhuru, uhalali na umiliki na pia hata uvumilivu kwa yule uliye naye. Hii ya kuishi na huyu, mnakorofishana kesho uko na mwingine unaweza kujikuta umeishi na watu hata 5 jamb linaloweza kukufanya uonekane muhuni. Binafsi jambo la kuishi na mtu bila ndoa huwa nalifananisha na mtu kukwambia wewe fanya kazi tu, mwisho wa mwezi ukifika au kazi ikikamilika tutakubaliana na kulipana. Baada ya kazi kuisha, chochote chaweza kutokea ikiwepo kupunjwa haki yako.
Nakuunga mkono hapa.