Tuikubalie DR Congo kujiunga na EAC?

Mkuu Red Giant nilitoa ahadi ya kurudi na sasa nimerudi na nitachangia kidogo juu ya hii mada ambayo ni muhimu kabisa. Nitatoa maoni kama Mwanasiasa, pia nitatoa maoni kama Mwansheria. Naomba niende moja kwa moja kwenye mada:

Congo DRC isitengwe bali isiruhusiwe kuingia kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kwasababu itaongeza changamoto ambazo tayari EAC inazo na imeshindwa kuzimaliza kwa muda mrefu. Changamoto kubwa ni hii ifuatayo hapa chini:

Mosi, nchi wanachama wa EAC wanakumbwa na matatizo ya kisiasa ndani ya nchi zao ambayo kwa namna moja au nyingine yameugharimu huu ukanda muda na rasilimali nyingi ambazo zingewekezwa katika kufanya mambo ya msingi.

Uganda mpaka leo wanapigana na waasi wa Lord's Resistance Army wa Bwana Joseph Konyi. Upande wa pili kuna sintofahamu kubwa sana kwenye siasa zake za ndani na hatufahamu nini kitatokea nchini humo baada ya Raisi Museveni kutoka. Tunaweza kuhisi kwamba Uganda iko salama lakini kumbuka tangu nchi hiyo inapata uhuru hakujawahi kuwa na Raisi ambaye hatatoka kwa vimbwanga na kusababisha kuchafukwa kwa hali ya kisiasa nchini humo kuanzia Mutesa hadi Obote.

Rwanda nayo mpaka sasa iko kwenye vita isiyoisha na makundi ya waasi wa Kihutu ambao wako Congo DRC na duniani kote. Hivi karibuni siasa ya Rwanda imegubikwa na kiza kikali baada ya kusemekana kwamba kuna Watutsi ambao waliwahi kuwa ndani ya Serikali ya Raisi Paul Kagame wameunda mtandao mkubwa wa kutaka kumpindua. Rwanda kama nchi inaenda vizuri kwasasa lakini bado kuna sintofahamu kubwa kama Uganda ambako mpaka leo hawana uhakika na Smooth Transition of Power after the fall of their strongmen.

Burundi mpaka sasa unafahamu nini kimekuwa kinaendelea tokea mwaka 2015, na bado nako kuna sintofahamu kubwa sana na Serikali ya Raisi Nkurunzinza iko nje-ndani.

Tanzania na Kenya hazijatofautiani sana. Zimefanikiwa sana kwenye suala la Smooth Transition of Power hivyo kufanikiwa kukwepa sintofahamu nyingi za kisiasa ambazo zimewakuta mataifa ya jirani. Japo upande wa pili bado Kenya ina changamoto kubwa za kiusalama ambazo zimemfanya apoteze rasilimalu nyingi sana kule Somalia akipambana na kikundi cha Al Shabab huku Tanzania ikiwa inapita kwenye kipindi kigumu kisiasa ambacho pia kinaweza kuzaa sintofahamu kubwa sana huko mbeleni kama siasa yake itaendelea kwenye njia hii.

Ninachotaka kusema kwenye hoja hii ni hiki hapa: EAC iliundwa kama Jumuiya ya kiuchumi na siyo ya kisiasa. Haya ya siasa kama kuunda shirikisho ni malengo ya baadae sana (Future Objectives) ambayo hayatakiwi kuwa kwenye ajenda yoyote kwenye kipindi hiki.

Lengo kuu na ajenda ya sasa (Main and Primary Objective) inabidi iwe ni Uchumi kupitia soko la pamoja na sarafu moja. Kama tukifanikiwa kujenga uchumi wa pamoja basi ndiyo mambo ya siasa yaanze kuingia kwenye ajenda za vikao vyetu. Sasa machafuko ya kisiasa huwa yanatutoa kwenye mstari maana hutulazimisha kuacha kufanya mambo ya kiuchumi na kujiingiza kwenye siasa, kitu ambacho siyo lengo letu kama EAC.

Tokea EAC iundwe tumekuwa tukitatua matatizo ya kisiasa yanayogharimu rasilimali nyingi kuliko kufanya mambo muhimu: Tunalazimika kufanya hivyo kwasababu ni majirani zetu lakini haswa kwasababu ni wanajumuiya wenzetu. Tulianza na Kenya mwaka 2007-2008: Kenya na Alshabaab 2012:Tukaja Rwanda na Tanzania mwaka 2013: Burundi mwaka 2015: Uganda na Rwanda 2019. Sasa tukiileta DRC na ilivyo na matatizo lukuki basi fahamu kwamba tutabeba na changamoto zao kuanzia uchaguzi hadi waasi wa Kagame na Museveni.

Pili, Congo DRC kama nchi imeshaigharimu SADC ambayo ilijiunga mwaka 1997 punde tu baada ya kumtoa Mobutu Sese Seko madarakani. SADC ilijikuta inatumia muda mwingi sana kushughulika na CONGO DRC badala ya kujikita kufanya mambo ya msingi. Ikumbukwe Mzee Kabila alivutana sana na viongozi wenzake wa SADC pale alipotaka wamsaidie kupambana kwenye The Congo War lakini wakawa wanasuasua. Wakina Quett Masire wanataka kumsuluhisha yeye Kabila anasusia vikao. Unadhani nchi kama hii ikijiunga na EAC na ikapatwa na tatizo tutakwepa kweli kuhusika ???

Tatu, wengi tunatamani Congo DRC ijiunge EAC kwasababu ya rasilimali zake. Basi kama itijiunga na EAC itageuzwa rasmi kuwa kichaka cha mashindano ya wizi wa rasilimali zake baina ya nchi wanachama wa EAC. Mfano hai tu, Umoja wa Mataifa (UN) waliwahi kutoa taarifa ya uchunguzi kwamba kipindi cha Vita ya Congo Zimbabwe ilipewa na serikali ya Laurent Kabila malipo ya dola za Kimarekani Bilioni 5 ambazo zimetoka kwenye mali mbalimbali za watu wa Congo DRC. Haya malipo yalienda sambamba na mikataba ya madini ambayo Zimbabwe na Angola waliipata kwa kumsaidia Kabila.

Upande mwingine inasemekana mataifa ya nje yaliua zaidi ya tembo 12,000 kwenye mbuga ya Garamba. Umoja wa Mataifa uliilaani Rwanda na Uganda kwa kuiba maelfu ya rasilimali za watu wa Congo DRC kwa kisingizio cha kupigana na waasi.

Sasa hii ilikuwa miaka ya 1999-2003, unadhani DRC ikijiunga rasmi na EAC Tanzania, Kenya, Uganda na Rwanda watakaa tu kuziangalia zile rasilimali ??? Utatokea mvutano mkubwa sana baina yetu kuanzia kwenye uchaguzi wa DRC maana kila nchi mwanachama atataka aweke kwenye serikali mtu ambaye atakuwa na ushawishi mkubwa sana kwake: Rwanda na Uganda walishawahi kupigana kisa kutaka rasilimali za Congo DRC, sasa DRC ijiunge na EAC hapo waongezeka Tanzania na Kenya unadhani kuna utulivu hapo ???

Mfano mwingine ,angalia kilichotokea Burundi 2015 baina ya Tanzania na Rwanda kutaka kujenga ushawishi kwa serikali ya Bujumbura. Sasa piga picha Burundi alikuwa hana utajiri wowote ule, unadhani Congo mwenye utajiri atatuacha salama ???

Sisi Tanzania tuna utajiri mkubwa ambao Mungu ametupa na itakuwa ni ujinga kama tutaka Congo DRC iinge EAC kwasababu ya utajiri wake. Japo kimkakati (Strategically)ni jambo sahihi, lakini tatizo linakuja kwamba pale ambapo hatuna mpango maalumu na nini tutafanya na Congo DRC baada ya kuwa karibu na sisi. Hivyo tuiache tu na tusitafute matatizo yasiyo na ulazima wowote ule: Pia tusichume dhambi with this Imperialistic Mindset....

NINI KIFANYIKE KUHUSU CONGO DRC???
Hapa nitatoa maoni kama mwanasiasa:
Mosi, EAC ijikite kwenye kuimarisha taasisi zake yenyewe (Consolidation and Amalgmation of it's Institutions) na siyo kujitanua (Enlargement of the bloc) kwa kutafuta au kuruhusu wanachama wapya.

EAC imeiga vitu vingi kutoka European Union (EU) ambayo zamani ilikuwa ni European Economic Community (EEC) lakini haifanyi vizuri kama ambavyo EEC ilifanya. Umoja wa Ulaya ulianza kama Umoja wa Uchumi (Economic Union) na siyo Umoja wa Kisiasa (Political Union), lakini baadae ndiyo ukafika hapa ulipo. Ulipitia hatua

Ulianza kutengeneza kitu kinachoitwa The European Coal and Steel Community mwaka 1951 ambayo ilikuwa ni taasisi iliyoundwa kwa lengo la kuhakikisha makaa ya mawe na chuka vinasimamiwa na Chombo/Taasisi moja ya kimataifa inayojitegemea ili kuzuia mvutano baina ya nchi kubwa kama Ujerumani na Ufaransa ambao ulipelekea kutokea vita ya kwanza na ya pili ya dunia.

Aliyesuka huu mpango anaitwa Jean Monet ambaye alisema ili tuweze kujenga umoja imara ni lazima tuhakikishe mataifa yenye nguvu na rasilimali nyingi ya Ujerumani na Ufaransa yanaungwanishwa kiuchumi kiasi kwamba nchi yeyote haiwezi kufikiria kwenda vitani na mwenzake. Kweli walifanikiwa sana maana mkataba huu ulisainiwa na mataifa sita (Ujerumani Magharibi, Ufaransa, Italia, Ubelgiji na Luxembourg) hata yale ambayo yalikuwa hayana rasilimali kama Ubelgiji na Luxembourg walinufaika.

Mwaka 1957 wakasaini mkata wa kuunda taasisi nyingine iitwayo The European Atomic Energy Community ambayo kazi yake ilikuwa kuzimamia uzalisha wa nishati ya nyuklia Ulaya ili kuwasaidia wanachama kupunguza utegemezi kwenye mafuta, pia kuuza nishati ya akiba kwa mataifa yasiyo wanachama. Hili nalo walifanikiwa sana.

Mwaka 1957 wakatengeneza sasa Umoja wa Uchumi wa Ulaya ambao leo ndiyo Umoja wa Ulaya. Lakini hawakuwa na haraka na hili liliwezekana kwasababu wao walikuwa na hali nzuri ya kisiasa nchini mwao. Mwaka 1967 taasisi za European Economic Community, European Steel and Coal Community na European Atomic Energy Community ziliungwanishwa kuwa chombo kimoja. Biashara baina ya wanachama ilikuwa kwa asilima 28.4%.

Hawakukimbilia kujitanua bali walijijenga kwanza wao kiuchumi na kisiasa kabla ya kuhakikisha wanayakaribisha mataifa mengine kama Uingereza mwaka 1973. Japo wanafanya vizuri lakini bado wana matatizo sana, Raisi wa Ufaransa Charles De Gaulle miaka ya 1969 hakupenda Uingereza ijiunge na EEC kwasababu alisema italeta matatizo kwenye jumuiya hivyo alipinga sana hadi anafariki.

Uingereza aliruhusiwa kujiunga baada ya De Gaulle kufariki. Lakini mbali na yote yale siasa za Uingereza zimeutikisa Umoja wa Ulaya kama ambavyo De Gaulle alionya. Sasa Uingereza taifa lililoendelea sana kuliko Congo DRC matatizo yake ya ndani yamevuruga Umoja wa Ulaya unadhani ni busara kuleta tena mgeni ???

Hapa hoja yangu ni hii: Kichwa na Moyo wa EAC ni Kenya na Tanzania wala siyo rasilimali za Congo DRC. Kama tunataka EAC imara basi ni lazima tuhakikishe Kenya na Tanzania zinaelewana na kuzungumza lugha moja. Maana binafsi naamini ushawishi wa Kenya na Tanzania wakiwa wanaongea lugha moja ni hatari kuliko mlipuko wa bomu la kiatomiki na hakuna taifa la Afrika linaweza kuwashinda. Raisi Kwame Nkhuruma alilifahamu vizuri hili suala ndiyo maana alipinga sana EAC isiwe nchi moja.

Kenya na Tanzania wakiungana basi lazima Uganda, Rwanda na Burundi watafuata tu. Kenya na Tanzania zina Uchumi mkubwa, ushawishi mkubwa sana kikanda na kimataifa, zimekaa pazuri sana kijiografia, zina rasilimali nyingi na zina watu wengi wanaozungumza lugha moja. Wakenya na Watanzania hawapatani kwasababu wamefanana mno tabia, fanya uchunguzi utaligundua hili.

Mtifuano wa kiuchumi na kihistoria baina ya Kenya na Tanzania ndiyo unavuruga EAC. Tunafanyiana hujuma badala ya kuunganisha nguvu za kitaasisi ili tujikwamue hapa tulipo. Hujuma kwenye kilimo, hujuma kwenye bandari na hujuma kwenye viwanda bila kufahamu kwamba Afrika Mashariki yote tunaweza kuwa Mamlaka moja ya Bandari ambayo ingetusaidia sana.

AU tungeweza kuanzisha Joint Venture Agreement kupitia Special Purpose Vehicle kwenye kuratibu biashara ya Usafiri wa anga. AU tukaunganisha nguvu kwenye tafiti za Uchimbaji wa mafuta na gesi mbona tungefika mbali sana tu. Wazungu walitwangana ndiyo wakapata akili kwamba kumbe tunaweza kushirikiana bila mabomu na vifaru.

Lakini sisi tunataka kushindana kisa kulipizana visasi vya ugomvi wa Mzee Kenyatta na Mzee Nyerere. Leo hii kwa mitandao ya kibiashara ambayo Kenya na Tanzania tunayo kupitia nguvu za diplomasia za nchi zetu kama tukishirikiana sauti yetu itafika hadi mwisho wa dunia. Nashangaa kwanini hatulioni hili. Binafsi Kenya and Tanzania is a key, ndiyo maana hata Rwanda, Burundi na Uganda walipovutana hakikutokea kitu sana lakini Kenyatta na Jakaya wakivutana lazima EAC iyumbe. Hujiulizi kwanini ???


Pili, na mwisho kabisa natoa ushauri kama mwanasheria sasa. Congo DRC asiwe mwanachama ila aidha apewe nafasi ya mtazamaji (Observer Status) kwanza ndani ya EAC huku akijifunza mwenendo mzima wa EAC. Sambamba na hilo EAC tunaweza kusaini mkataba maalumu wa Congo DRC (Sui Generis Treaty) ambao utampa nafasi ya kipekee kunufaika kiuchumi bila kuwa mwanachama. Anaweza akaandaliwa vipengele (Extracts Clause with Limitations ) kutoka mikataba mbalimbali (Protocols) ambayo EAC ameshasaini. Anaweza kufanya kama ambavyo Uingereza na Umoja wa Ulaya walifanya miaka ya 1960's- 1970's au ambavyo wanataka kufanya baada ya Brexit.

Tujijenge kwanza sisi ndiyo turuhusu waliovurugwa kama Congo DRC wajiunge.
Mkuu Malcom Lumumba umemaliza kila kitu, binafsi sikuwahi kuafiki Rwanda, na Burundi kujiunga EAC pia siafiki hili la Congo DRC kujiunga EAC, lakini sababu ulizozitoa zimenifundisha vitu vingi sana na the moment namaliza kuisoma nukta ya mwisho tayari kichwa changu kilishajenga Action Plan.
Uliyoyaongea naona yanafanyika kinyume yakionyesha tabia halisi za kiafrika ni kama tunataka kuanzia pale wenzetu walipofikia yaani kwenye success point za wenzetu badala ya kurudi chini na kutengeneza njia zetu.
Pia, kwa kudhani wingi wa rasilimali ndiyo huleta nguvu na mshikamano wenye tija tunakosea sana, kwetu Congo DRC anaweza akawa ni fursa nzuri kuliko mwana jumuia mzuri, tunaangalia zaidi rasilimali na rangi yake hatujiulizi rasilimali za Kenya na Tanzania zimeinufaisha vipi Jumuiya.
Kwa mchanganuo ulioutoa EAC inaweza ikajulikana zaidi kama EAVC (East Africa Violence Community)
 
Mkuu umetoa nondo za maana sana na kiukweli mtazamo wangu umebadilika sana kwenye hili suala. usi-bite more than you can chew. Hapo kwenye Tz na Kenya kupinganapingana sababu tunafanana sana ni kweli kabisa, kwenye saikolojia wanaita Narcissism of small differences. Tz na Kenya tungejua ushindani wetu ni psychological na tukaamua kuwa na sauti moja tusingeshikika. inabidi Chige na Wick na Denvers waione hii nondo.
Mkuu Red Giant!

Malcom Lumumba amemaliza kila kitu, na nikiongeza tu, NITAHARIBU!!

Unajua kwanini nitaharibu?!

Mosi, nami nilitaka kuongea hivyo hivyo kwamba DRC tusimkaribishe, lakini kinyume na Malcom ambae ameongea Kizalendo zaidi na kwa hoja zilizoshiba mbolea, mimi nilitaka kuweka maneno ya kizalendo na ya kibeberu kama yale ya kutaka tuwaunge mkono Misri dhidi ya Ethiopia kwenye suala zima la matumizi ya maji ya mto Nile!

Wakati malofa wangetupongeza kwa "ubinadamu" wa kuwahurumia Mafarao wasio na chanzo kingine cha maji, kumbe moyoni tunataka kumzuia Ethiopia asiwe ndie Super Power wa Umeme kwenye ukanda huu!!!

Kwanini tuwaache Ethiopia wawe ndio East and Central Africa Energy Pool tena kwa umeme cheap wa maji wakati na sisi tuna gas kibao ya kuweza kuzalisha umeme na hatimae kuwa ndio kuwa East and Central Africa Energy Pool?!

Yaani ningekuwa na hoja zile zile za Kibeberu za kutaka "tuwaunge mkono" ndugu zetu Wakenya dhidi ya Mchina pale iliposemekana eti kwa madeni waliyokuwa nayo Wapwa zetu Wakenya, basi kulikuwa na hatari Wachina wangeibeba Bandari ya Mombasa kama ilivyosemekana kuhusu Wachina na Hambantota Port.

Dunia na Afrika kwa ujumla wangetushangilia na kutupongeza kwa "kuwapigania" Wapwa zetu Wakenya kumbe deep inside our imperialism mentality, tunajua Mchina akiingia Mombasa basi Bandari ya Dar es salaam ijiandae kuwa bandari ya kupokea majahazi yenye mizigo kutoka Mombasa!!

Ni mawazo hayo hayo ya Kibeberu ambayo kimsingi yamejaa "umimi na ubinafsi", ndiyo yangenisukuma zaidi kutaka DRC isiingie EAC!!

Kwanini nisilete Ubeberu ili hatimae potential ya DRC tuifaidi peke yetu?! Na ninaposema potential, wala sizungumzii raslimali za DRC, kwanza I don't believe in mining economy na ndio maana mara kadhaa nimekuwa nikizungumzia "too much" energy anayowekeza JPM kwenye sekta ya madini.

Hapa nazungumzia Geographical Potential!!

Na Malcom umeongea jambo la msingi sana... kwamba sisi na Wakenya tumefanana mno, na matokeo yake tumekuwa kama Sunche na Kapeto!!! Ni kutokana na hilo, ndo maana mara zote tumekuwa ni watu wa kuhujumiana tu! Na upande mmoja unapokuwa na Mabeberu kama chige, ndo basi tena!!!

Ila tuache masihara! Hawa Wapwa zetu ni Manyang'au yaliyokubuhu haya!! Usipoyaendea Kinyang'au nyang'au haya, yanakutoa nishai mapemaaa halafu yanakucheka 🤣🤣🤣!!!

All in all, Malcom Lumumba umeongea mambo mazito sana, tena umeyaelezea kisomi sana ingawaje kwa lugha nyepesi inayoeleweka!!

Much respect!
 
Mkuu Red Giant!

Malcom Lumumba amemaliza kila kitu, na nikiongeza tu, NITAHARIBU!!

Unajua kwanini nitaharibu?!

Mosi, nami nilitaka kuongea hivyo hivyo kwamba DRC tusimkaribishe, lakini kinyume na Malcom ambae ameongea Kizalendo zaidi na kwa hoja zilizoshiba mbolea, mimi nilitaka kuweka maneno ya kizalendo na ya kibeberu kama yale ya kutaka tuwaunge mkono Misri dhidi ya Ethiopia kwenye suala zima la matumizi ya maji ya mto Nile!

Wakati malofa wangetupongeza kwa "ubinadamu" wa kuwahurumia Mafarao wasio na chanzo kingine cha maji, kumbe moyoni tunataka kumzuia Ethiopia asiwe ndie Super Power wa Umeme kwenye ukanda huu!!!

Kwanini tuwaache Ethiopia wawe ndio East and Central Africa Energy Pool tena kwa umeme cheap wa maji wakati na sisi tuna gas kibao ya kuweza kuzalisha umeme na hatimae kuwa ndio kuwa East and Central Africa Energy Pool?!

Yaani ningekuwa na hoja zile zile za Kibeberu za kutaka "tuwaunge mkono" ndugu zetu Wakenya dhidi ya Mchina pale iliposemekana eti kwa madeni waliyokuwa nayo Wapwa zetu Wakenya, basi kulikuwa na hatari Wachina wangeibeba Bandari ya Mombasa kama ilivyosemekana kuhusu Wachina na Hambantota Port.

Dunia na Afrika kwa ujumla wangetushangilia na kutupongeza kwa "kuwapigania" Wapwa zetu Wakenya kumbe deep inside our imperialism mentality, tunajua Mchina akiingia Mombasa basi Bandari ya Dar es salaam ijiandae kuwa bandari ya kupokea majahazi yenye mizigo kutoka Mombasa!!

Ni mawazo hayo hayo ya Kibeberu ambayo kimsingi yamejaa "umimi na ubinafsi", ndiyo yangenisukuma zaidi kutaka DRC isiingie EAC!!

Kwanini nisilete Ubeberu ili hatimae potential ya DRC tuifaidi peke yetu?! Na ninaposema potential, wala sizungumzii raslimali za DRC, kwanza I don't believe in mining economy na ndio maana mara kadhaa nimekuwa nikizungumzia "too much" energy anayowekeza JPM kwenye sekta ya madini.

Hapa nazungumzia Geographical Potential!!

Na Malcom umeongea jambo la msingi sana... kwamba sisi na Wakenya tumefanana mno, na matokeo yake tumekuwa kama Sunche na Kapeto!!! Ni kutokana na hilo, ndo maana mara zote tumekuwa ni watu wa kuhujumiana tu! Na upande mmoja unapokuwa na Mabeberu kama chige, ndo basi tena!!!

Ila tuache masihara! Hawa Wapwa zetu ni Manyang'au yaliyokubuhu haya!! Usipoyaendea Kinyang'au nyang'au haya, yanakutoa nishai mapemaaa halafu yanakucheka !!!

All in all, Malcom Lumumba umeongea mambo mazito sana, tena umeyaelezea kisomi sana ingawaje kwa lugha nyepesi inayoeleweka!!

Much respect!
Hawa wakina MK254 ni watu wenye tamaa na manyang'au kweli, wala siyo wongo lakini ni watu muhimu sana kwetu: Yani Tanzania na Kenya ni kama Siamese Twins inabidi tushirikiane sana kujijenga. Tukiwa imara ndiyo tuanze kupeleka mikono huko kwingine. Japo nafahamu siyo jambo rahisi hata kidogo kwa watanzania kuwaamini hawa jamaa.
 
Mkuu Red Giant nilitoa ahadi ya kurudi na sasa nimerudi na nitachangia kidogo juu ya hii mada ambayo ni muhimu kabisa. Nitatoa maoni kama Mwanasiasa, pia nitatoa maoni kama Mwansheria. Naomba niende moja kwa moja kwenye mada:

Congo DRC isitengwe bali isiruhusiwe kuingia kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kwasababu itaongeza changamoto ambazo tayari EAC inazo na imeshindwa kuzimaliza kwa muda mrefu. Changamoto kubwa ni hii ifuatayo hapa chini:

Mosi, nchi wanachama wa EAC wanakumbwa na matatizo ya kisiasa ndani ya nchi zao ambayo kwa namna moja au nyingine yameugharimu huu ukanda muda na rasilimali nyingi ambazo zingewekezwa katika kufanya mambo ya msingi.

Uganda mpaka leo wanapigana na waasi wa Lord's Resistance Army wa Bwana Joseph Konyi. Upande wa pili kuna sintofahamu kubwa sana kwenye siasa zake za ndani na hatufahamu nini kitatokea nchini humo baada ya Raisi Museveni kutoka. Tunaweza kuhisi kwamba Uganda iko salama lakini kumbuka tangu nchi hiyo inapata uhuru hakujawahi kuwa na Raisi ambaye hatatoka kwa vimbwanga na kusababisha kuchafukwa kwa hali ya kisiasa nchini humo kuanzia Mutesa hadi Obote.

Rwanda nayo mpaka sasa iko kwenye vita isiyoisha na makundi ya waasi wa Kihutu ambao wako Congo DRC na duniani kote. Hivi karibuni siasa ya Rwanda imegubikwa na kiza kikali baada ya kusemekana kwamba kuna Watutsi ambao waliwahi kuwa ndani ya Serikali ya Raisi Paul Kagame wameunda mtandao mkubwa wa kutaka kumpindua. Rwanda kama nchi inaenda vizuri kwasasa lakini bado kuna sintofahamu kubwa kama Uganda ambako mpaka leo hawana uhakika na Smooth Transition of Power after the fall of their strongmen.

Burundi mpaka sasa unafahamu nini kimekuwa kinaendelea tokea mwaka 2015, na bado nako kuna sintofahamu kubwa sana na Serikali ya Raisi Nkurunzinza iko nje-ndani.

Tanzania na Kenya hazijatofautiani sana. Zimefanikiwa sana kwenye suala la Smooth Transition of Power hivyo kufanikiwa kukwepa sintofahamu nyingi za kisiasa ambazo zimewakuta mataifa ya jirani. Japo upande wa pili bado Kenya ina changamoto kubwa za kiusalama ambazo zimemfanya apoteze rasilimalu nyingi sana kule Somalia akipambana na kikundi cha Al Shabab huku Tanzania ikiwa inapita kwenye kipindi kigumu kisiasa ambacho pia kinaweza kuzaa sintofahamu kubwa sana huko mbeleni kama siasa yake itaendelea kwenye njia hii.

Ninachotaka kusema kwenye hoja hii ni hiki hapa: EAC iliundwa kama Jumuiya ya kiuchumi na siyo ya kisiasa. Haya ya siasa kama kuunda shirikisho ni malengo ya baadae sana (Future Objectives) ambayo hayatakiwi kuwa kwenye ajenda yoyote kwenye kipindi hiki.

Lengo kuu na ajenda ya sasa (Main and Primary Objective) inabidi iwe ni Uchumi kupitia soko la pamoja na sarafu moja. Kama tukifanikiwa kujenga uchumi wa pamoja basi ndiyo mambo ya siasa yaanze kuingia kwenye ajenda za vikao vyetu. Sasa machafuko ya kisiasa huwa yanatutoa kwenye mstari maana hutulazimisha kuacha kufanya mambo ya kiuchumi na kujiingiza kwenye siasa, kitu ambacho siyo lengo letu kama EAC.

Tokea EAC iundwe tumekuwa tukitatua matatizo ya kisiasa yanayogharimu rasilimali nyingi kuliko kufanya mambo muhimu: Tunalazimika kufanya hivyo kwasababu ni majirani zetu lakini haswa kwasababu ni wanajumuiya wenzetu. Tulianza na Kenya mwaka 2007-2008: Kenya na Alshabaab 2012:Tukaja Rwanda na Tanzania mwaka 2013: Burundi mwaka 2015: Uganda na Rwanda 2019. Sasa tukiileta DRC na ilivyo na matatizo lukuki basi fahamu kwamba tutabeba na changamoto zao kuanzia uchaguzi hadi waasi wa Kagame na Museveni.

Pili, Congo DRC kama nchi imeshaigharimu SADC ambayo ilijiunga mwaka 1997 punde tu baada ya kumtoa Mobutu Sese Seko madarakani. SADC ilijikuta inatumia muda mwingi sana kushughulika na CONGO DRC badala ya kujikita kufanya mambo ya msingi. Ikumbukwe Mzee Kabila alivutana sana na viongozi wenzake wa SADC pale alipotaka wamsaidie kupambana kwenye The Congo War lakini wakawa wanasuasua. Wakina Quett Masire wanataka kumsuluhisha yeye Kabila anasusia vikao. Unadhani nchi kama hii ikijiunga na EAC na ikapatwa na tatizo tutakwepa kweli kuhusika ???

Tatu, wengi tunatamani Congo DRC ijiunge EAC kwasababu ya rasilimali zake. Basi kama itijiunga na EAC itageuzwa rasmi kuwa kichaka cha mashindano ya wizi wa rasilimali zake baina ya nchi wanachama wa EAC. Mfano hai tu, Umoja wa Mataifa (UN) waliwahi kutoa taarifa ya uchunguzi kwamba kipindi cha Vita ya Congo Zimbabwe ilipewa na serikali ya Laurent Kabila malipo ya dola za Kimarekani Bilioni 5 ambazo zimetoka kwenye mali mbalimbali za watu wa Congo DRC. Haya malipo yalienda sambamba na mikataba ya madini ambayo Zimbabwe na Angola waliipata kwa kumsaidia Kabila.

Upande mwingine inasemekana mataifa ya nje yaliua zaidi ya tembo 12,000 kwenye mbuga ya Garamba. Umoja wa Mataifa uliilaani Rwanda na Uganda kwa kuiba maelfu ya rasilimali za watu wa Congo DRC kwa kisingizio cha kupigana na waasi.

Sasa hii ilikuwa miaka ya 1999-2003, unadhani DRC ikijiunga rasmi na EAC Tanzania, Kenya, Uganda na Rwanda watakaa tu kuziangalia zile rasilimali ??? Utatokea mvutano mkubwa sana baina yetu kuanzia kwenye uchaguzi wa DRC maana kila nchi mwanachama atataka aweke kwenye serikali mtu ambaye atakuwa na ushawishi mkubwa sana kwake: Rwanda na Uganda walishawahi kupigana kisa kutaka rasilimali za Congo DRC, sasa DRC ijiunge na EAC hapo waongezeka Tanzania na Kenya unadhani kuna utulivu hapo ???

Mfano mwingine ,angalia kilichotokea Burundi 2015 baina ya Tanzania na Rwanda kutaka kujenga ushawishi kwa serikali ya Bujumbura. Sasa piga picha Burundi alikuwa hana utajiri wowote ule, unadhani Congo mwenye utajiri atatuacha salama ???

Sisi Tanzania tuna utajiri mkubwa ambao Mungu ametupa na itakuwa ni ujinga kama tutaka Congo DRC iinge EAC kwasababu ya utajiri wake. Japo kimkakati (Strategically)ni jambo sahihi, lakini tatizo linakuja kwamba pale ambapo hatuna mpango maalumu na nini tutafanya na Congo DRC baada ya kuwa karibu na sisi. Hivyo tuiache tu na tusitafute matatizo yasiyo na ulazima wowote ule: Pia tusichume dhambi with this Imperialistic Mindset....

NINI KIFANYIKE KUHUSU CONGO DRC???
Hapa nitatoa maoni kama mwanasiasa:
Mosi, EAC ijikite kwenye kuimarisha taasisi zake yenyewe (Consolidation and Amalgmation of it's Institutions) na siyo kujitanua (Enlargement of the bloc) kwa kutafuta au kuruhusu wanachama wapya.

EAC imeiga vitu vingi kutoka European Union (EU) ambayo zamani ilikuwa ni European Economic Community (EEC) lakini haifanyi vizuri kama ambavyo EEC ilifanya. Umoja wa Ulaya ulianza kama Umoja wa Uchumi (Economic Union) na siyo Umoja wa Kisiasa (Political Union), lakini baadae ndiyo ukafika hapa ulipo. Ulipitia hatua

Ulianza kutengeneza kitu kinachoitwa The European Coal and Steel Community mwaka 1951 ambayo ilikuwa ni taasisi iliyoundwa kwa lengo la kuhakikisha makaa ya mawe na chuka vinasimamiwa na Chombo/Taasisi moja ya kimataifa inayojitegemea ili kuzuia mvutano baina ya nchi kubwa kama Ujerumani na Ufaransa ambao ulipelekea kutokea vita ya kwanza na ya pili ya dunia.

Aliyesuka huu mpango anaitwa Jean Monet ambaye alisema ili tuweze kujenga umoja imara ni lazima tuhakikishe mataifa yenye nguvu na rasilimali nyingi ya Ujerumani na Ufaransa yanaungwanishwa kiuchumi kiasi kwamba nchi yeyote haiwezi kufikiria kwenda vitani na mwenzake. Kweli walifanikiwa sana maana mkataba huu ulisainiwa na mataifa sita (Ujerumani Magharibi, Ufaransa, Italia, Ubelgiji na Luxembourg) hata yale ambayo yalikuwa hayana rasilimali kama Ubelgiji na Luxembourg walinufaika.

Mwaka 1957 wakasaini mkata wa kuunda taasisi nyingine iitwayo The European Atomic Energy Community ambayo kazi yake ilikuwa kuzimamia uzalisha wa nishati ya nyuklia Ulaya ili kuwasaidia wanachama kupunguza utegemezi kwenye mafuta, pia kuuza nishati ya akiba kwa mataifa yasiyo wanachama. Hili nalo walifanikiwa sana.

Mwaka 1957 wakatengeneza sasa Umoja wa Uchumi wa Ulaya ambao leo ndiyo Umoja wa Ulaya. Lakini hawakuwa na haraka na hili liliwezekana kwasababu wao walikuwa na hali nzuri ya kisiasa nchini mwao. Mwaka 1967 taasisi za European Economic Community, European Steel and Coal Community na European Atomic Energy Community ziliungwanishwa kuwa chombo kimoja. Biashara baina ya wanachama ilikuwa kwa asilima 28.4%.

Hawakukimbilia kujitanua bali walijijenga kwanza wao kiuchumi na kisiasa kabla ya kuhakikisha wanayakaribisha mataifa mengine kama Uingereza mwaka 1973. Japo wanafanya vizuri lakini bado wana matatizo sana, Raisi wa Ufaransa Charles De Gaulle miaka ya 1969 hakupenda Uingereza ijiunge na EEC kwasababu alisema italeta matatizo kwenye jumuiya hivyo alipinga sana hadi anafariki.

Uingereza aliruhusiwa kujiunga baada ya De Gaulle kufariki. Lakini mbali na yote yale siasa za Uingereza zimeutikisa Umoja wa Ulaya kama ambavyo De Gaulle alionya. Sasa Uingereza taifa lililoendelea sana kuliko Congo DRC matatizo yake ya ndani yamevuruga Umoja wa Ulaya unadhani ni busara kuleta tena mgeni ???

Hapa hoja yangu ni hii: Kichwa na Moyo wa EAC ni Kenya na Tanzania wala siyo rasilimali za Congo DRC. Kama tunataka EAC imara basi ni lazima tuhakikishe Kenya na Tanzania zinaelewana na kuzungumza lugha moja. Maana binafsi naamini ushawishi wa Kenya na Tanzania wakiwa wanaongea lugha moja ni hatari kuliko mlipuko wa bomu la kiatomiki na hakuna taifa la Afrika linaweza kuwashinda. Raisi Kwame Nkhuruma alilifahamu vizuri hili suala ndiyo maana alipinga sana EAC isiwe nchi moja.

Kenya na Tanzania wakiungana basi lazima Uganda, Rwanda na Burundi watafuata tu. Kenya na Tanzania zina Uchumi mkubwa, ushawishi mkubwa sana kikanda na kimataifa, zimekaa pazuri sana kijiografia, zina rasilimali nyingi na zina watu wengi wanaozungumza lugha moja. Wakenya na Watanzania hawapatani kwasababu wamefanana mno tabia, fanya uchunguzi utaligundua hili.

Mtifuano wa kiuchumi na kihistoria baina ya Kenya na Tanzania ndiyo unavuruga EAC. Tunafanyiana hujuma badala ya kuunganisha nguvu za kitaasisi ili tujikwamue hapa tulipo. Hujuma kwenye kilimo, hujuma kwenye bandari na hujuma kwenye viwanda bila kufahamu kwamba Afrika Mashariki yote tunaweza kuwa Mamlaka moja ya Bandari ambayo ingetusaidia sana.

AU tungeweza kuanzisha Joint Venture Agreement kupitia Special Purpose Vehicle kwenye kuratibu biashara ya Usafiri wa anga. AU tukaunganisha nguvu kwenye tafiti za Uchimbaji wa mafuta na gesi mbona tungefika mbali sana tu. Wazungu walitwangana ndiyo wakapata akili kwamba kumbe tunaweza kushirikiana bila mabomu na vifaru.

Lakini sisi tunataka kushindana kisa kulipizana visasi vya ugomvi wa Mzee Kenyatta na Mzee Nyerere. Leo hii kwa mitandao ya kibiashara ambayo Kenya na Tanzania tunayo kupitia nguvu za diplomasia za nchi zetu kama tukishirikiana sauti yetu itafika hadi mwisho wa dunia. Nashangaa kwanini hatulioni hili. Binafsi Kenya and Tanzania is a key, ndiyo maana hata Rwanda, Burundi na Uganda walipovutana hakikutokea kitu sana lakini Kenyatta na Jakaya wakivutana lazima EAC iyumbe. Hujiulizi kwanini ???


Pili, na mwisho kabisa natoa ushauri kama mwanasheria sasa: Congo DRC asiwe mwanachama ila aidha apewe nafasi ya mtazamaji (Observer Status) kwanza ndani ya EAC huku akijifunza mwenendo mzima wa EAC. Sambamba na hilo EAC tunaweza kusaini mkataba maalumu wa Congo DRC (Sui Generis Treaty) ambao utampa nafasi ya kipekee kunufaika kiuchumi bila kuwa mwanachama. Anaweza akaandaliwa vipengele (Extracts Clause with Limitations ) kutoka mikataba mbalimbali (Protocols) ambayo EAC ameshasaini. Anaweza kufanya kama ambavyo Uingereza na Umoja wa Ulaya walifanya miaka ya 1960's- 1970's au ambavyo wanataka kufanya baada ya Brexit.

Tujijenge kwanza sisi ndiyo turuhusu waliovurugwa kama Congo DRC wajiunge.
Mkuu Malcom Lumumba umemaliza kila kitu, binafsi sikuwahi kuafiki Rwanda, na Burundi kujiunga EAC pia siafiki hili la Congo DRC kujiunga EAC, lakini sababu ulizozitoa zimenifundisha vitu vingi sana na the moment namaliza kuisoma nukta ya mwisho tayari kichwa changu kilishajenga Action Plan.
Uliyoyaongea naona yanafanyika kinyume yakionyesha tabia halisi za kiafrika ni kama tunataka kuanzia pale wenzetu walipofikia yaani kwenye success point za wenzetu badala ya kurudi chini na kutengeneza njia zetu.
Pia, kwa kudhani wingi wa rasilimali ndiyo huleta nguvu na mshikamano wenye tija tunakosea sana, kwetu Congo DRC anaweza akawa ni fursa nzuri kuliko mwana jumuia mzuri, tunaangalia zaidi rasilimali na rangi yake hatujiulizi rasilimali za Kenya na Tanzania zimeinufaisha vipi Jumuiya.
Kwa mchanganuo ulioutoa EAC inaweza ikajulikana zaidi kama EAVC (East Africa Violence Community)
Points muhimu ziko ktk posts hizi

Kikubwa kwanza Congo ijijenge zaidi ndani ,kisha ndio ifikirie kujiunga EAC ,Congo siasa za ndani bado kdg

Harakati za sasa za kupunguza mapigano Mashariki ziongezwe
 
Hawa wakina MK254 ni watu wenye tamaa na manyang'au kweli, wala siyo wongo lakini ni watu muhimu sana kwetu: Yani Tanzania na Kenya ni kama Siamese Twins inabidi tushirikiane sana kujijenga. Tukiwa imara ndiyo tuanze kupeleka mikono huko kwingine. Japo nafahamu siyo jambo rahisi hata kidogo kwa watanzania kuwaamini hawa jamaa.
Of course, na mimi ni mfuasi mkubwa sana, tena sana kwenye masuala ya ushirikiano na ndio maana mara nyingi kwenye hili suala nimekuwa nikitumia terms mbili... Ushirikiano na Uhusiano!

Linapokuja suala la ushirikiano, I don't judge no body provided taifa kama taifa linanufaika kwenye ushirikiano! Ni kama ambavyo nilipata kusema kwamba, there's no way taifa kama Israel linaweza kuwa na undugu na Tanzania (international relation) lakini hiyo haiwezi kuwa sababu ya kufanya Tanzania isifanye partnership na Israel (international cooperation)!

Kwa Kenya, weather we like it or not, sisi ni ndugu tena ni undugu unaoenda mbali zaidi ya common international relation! Lakini mbali na kuwa na uhusiano, Kenya ni partner in business kwa levels zote... from individual to state level, so there's no way unaweza kukwepa ushirikiano na taifa lenye sifa kama hizo!

Na ukichukua nchi zote za Afrika Mashariki (tradional + modern EA), pamoja na ujanja ujanja wao wote, bado Tanzania tuna nafasi kubwa zaidi (in terms of monetary value) ya kuuza Kenya kuliko nchi nyingine yoyote ile ukanda huu!

Pamoja na unyang'au wao wote, kwangu mimi Kenya is an Opportunity and not a Threat! Kenya anaweza kuwa threat only if you don't know how to handle mataifa kama ya Kenya!

Isitoshe, Tanzania anaweza kuwa na fursa ya kuuza zaidi Kenya kuliko Kenya alivyo na fursa kama hiyo kwa Tanzania ukiondoa financial sector, ambayo mabenki ya Tanzania ni kama yamesharidhika na soko la ndani ingawaje ukweli ni kinyume chake!
 
Of course, na mimi ni mfuasi mkubwa sana, tena sana kwenye masuala ya ushirikiano na ndio maana mara nyingi kwenye hili suala nimekuwa nikitumia terms mbili... Ushirikiano na Uhusiano!

Linapokuja suala la ushirikiano, I don't judge no body provided taifa kama taifa linanufaika kwenye ushirikiano! Ni kama ambavyo nilipata kusema kwamba, there's no way taifa kama Israel linaweza kuwa na undugu na Tanzania (international relation) lakini hiyo haiwezi kuwa sababu ya kufanya Tanzania isifanye partnership na Israel (international cooperation)!

Kwa Kenya, weather we like it or not, sisi ni ndugu tena ni undugu unaoenda mbali zaidi ya common international relation! Lakini mbali na kuwa na uhusiano, Kenya ni partner in business kwa levels zote... from individual to state level, so there's no way unaweza kukwepa ushirikiano na taifa lenye sifa kama hizo!

Na ukichukua nchi zote za Afrika Mashariki (tradional + modern EA), pamoja na ujanja ujanja wao wote, bado Tanzania tuna nafasi kubwa zaidi (in terms of monetary value) ya kuuza Kenya kuliko nchi nyingine yoyote ile ukanda huu!

Pamoja na unyang'au wao wote, kwangu mimi Kenya is an Opportunity and not a Threat! Kenya anaweza kuwa threat only if you don't know how to handle mataifa kama ya Kenya!

Isitoshe, Tanzania anaweza kuwa na fursa ya kuuza zaidi Kenya kuliko Kenya alivyo na fursa kama hiyo kwa Tanzania ukiondoa financial sector, ambayo mabenki ya Tanzania ni kama yamesharidhika na soko la ndani ingawaje ukweli ni kinyume chake!
Hakika Mkuu, Hakika!
 
Of course, na mimi ni mfuasi mkubwa sana, tena sana kwenye masuala ya ushirikiano na ndio maana mara nyingi kwenye hili suala nimekuwa nikitumia terms mbili... Ushirikiano na Uhusiano!

Linapokuja suala la ushirikiano, I don't judge no body provided taifa kama taifa linanufaika kwenye ushirikiano! Ni kama ambavyo nilipata kusema kwamba, there's no way taifa kama Israel linaweza kuwa na undugu na Tanzania (international relation) lakini hiyo haiwezi kuwa sababu ya kufanya Tanzania isifanye partnership na Israel (international cooperation)!

Kwa Kenya, weather we like it or not, sisi ni ndugu tena ni undugu unaoenda mbali zaidi ya common international relation! Lakini mbali na kuwa na uhusiano, Kenya ni partner in business kwa levels zote... from individual to state level, so there's no way unaweza kukwepa ushirikiano na taifa lenye sifa kama hizo!

Na ukichukua nchi zote za Afrika Mashariki (tradional + modern EA), pamoja na ujanja ujanja wao wote, bado Tanzania tuna nafasi kubwa zaidi (in terms of monetary value) ya kuuza Kenya kuliko nchi nyingine yoyote ile ukanda huu!

Pamoja na unyang'au wao wote, kwangu mimi Kenya is an Opportunity and not a Threat! Kenya anaweza kuwa threat only if you don't know how to handle mataifa kama ya Kenya!

Isitoshe, Tanzania anaweza kuwa na fursa ya kuuza zaidi Kenya kuliko Kenya alivyo na fursa kama hiyo kwa Tanzania ukiondoa financial sector, ambayo mabenki ya Tanzania ni kama yamesharidhika na soko la ndani ingawaje ukweli ni kinyume chake!
Moja ya vitu ambavyo Rais Felix anajaribu kuviweka sawa ni hilo la USHIRIKIANO NA UHUSIANO

Lkn hayo hayatofanyika km kule mashariki hapajatulia ,na juhudi za sasa EAC na SADC ni kusolve issue ya kule kisha kuangalia hili tunalojadili

Mashariki pakitulia na Congo ikatulia ,Hili linawezekana
 
Mkuu Malcom Lumumba , ahsante

Hili suala tulilijadili sana kabla ya Rwanda na Burundi na hata South Sudan au Somalia

Nitaanzia kwa hoja ya Chige kuhusu mahusiano ya Tanzania na Kenya na ushindani uliopo

Tanzania ijalaumu ndani ya EA. Ni nchi iliyo na rasiliamali arable land , utalii na madini.

Uwepo wa EA ilikuwa fursa ya soko la Tanzania. Tuna mifano michache.

Katika miaka ya karibuni Kenya imeitegemea sana Tanzania kwa nafaka kama Mahindi.
Bado Kenya ina export Ulaya vitunguu vya Karatu na Maua ya Arusha.

Soko la nafaka kwa EA na SADC ni kubwa sana, tunashindwaje kutumia ardhi kuliteka?

Hii maana yake kama tungetumia ardhi yetu kwa Kilimo sisi ndio tungelisha EA na SADC

Tungeuza matunda ya Tanga, Vitunguu, mboga mboga, Maharagwe, Mchele, Mahindi n.k.

Nyanya zinazooza Morogoro na Iringa, matunda yanaharibika Muheza na Lushoto.
Mahindi yamekwama Sumbawanga , Mbeya na Ruvuma.

Mpunga hauna soko Shinyanga, Morogoro n.k. Sababu kubwa ni kushindwa kuuza, kushindwa kuhamasisha uzalishaji wa biashara.

Tunatumia muda mwingi kufanya ''intelejensia'' za watu wetu na si za uchumi

Kosa letu ni kushindana na Kenya maeneo ya Utalii na Viwanda wao wakiwa na upper hand

Tunaweza kufanya utalii na viwanda huku tukilisha EAC yote bila tatizo.

Kuhusu Kupanuka kwa EAC, hili ni kama ulivyoeleza.

Nchi za Ulaya hazikuanza juzi zilianza kuanzia miaka ya 50.
Kilichotokea siku za karibuni ni Expansion hasa kutoka na mabadiliko geopolitical ya dunia.

Tulipaswa kuimarisha EAC ya Kenya , Uganda na Tanzania ili wajao wakute misingi imara

Expansion ya kuwaingiza Rwanda na Burundi imerudisha nyuma sana jitihda za Jumuiya
Migogoro ya nchi kama Burundi ilisababisha mkutano wa wakuu kutofanyika

Tulitegemea South Sudan kama nchi yenye rasiliamali, nako ni matatizo tu.
Tumeshindwa kutumia fursa ya soko lililopo na linalopanuka, leo tunadhani DRC ni muhimu

Ikiwa DRC ni muhimu kwa rasilimali kama wanavyodai, basi wasingekuwa na matatizo
Kuwakaribisha ni kukaribisha migogoro zaidi ya mafanikio

EAC ya 1977 ilikuwa na nguvu sana na tungeweza kutumia ushirikiano na mataifa jirani

Kuwakaribisha hakujaonyesha kama kuna tija kiuchumi zaidi ya changamoto za usalama

EAC inatakiwa ijengwe kwanza kiuchumi halafu ipanuke kukiwa na misingi imara
Ndivyo EU ilivyojengwa na mataifa machache kisha kuwakaribisha akina Lativia n.k.

Kwa Tanzania, tunapakana na nchi 8 kubwa! swali tusilojiuliza na tusilotaka kuuliza, ni kwanini tumeshindwa kutumia fursa iliyopo kwanza hadi tudhani tunahitaji DRC na Somalia?

JokaKuu
 
Mkuu Nguruvi3!!

Umemaliza kila kitu! Na hata niliposema Tanzania ina fursa zaidi ya kuuza Kenya in terms of monetary value kuliko ilivyo Kenya kwa Tanzania, focus yangu ilikuwa ndiyo eneo hilo hilo uliloelezea... agribusiness! Inasikitisha kuona hatuitumii fursa hii ipasavyo!
 
Moja ya vitu ambavyo Rais Felix anajaribu kuviweka sawa ni hilo la USHIRIKIANO NA UHUSIANO

Lkn hayo hayatofanyika km kule mashariki hapajatulia ,na juhudi za sasa EAC na SADC ni kusolve issue ya kule kisha kuangalia hili tunalojadili

Mashariki pakitulia na Congo ikatulia ,Hili linawezekana
Na Tanzania tupo vizuri sana kwenye suala la siasa za uhusiano lakini huwa tunafeli kwenye suala la ushirikiano! Kuna siku niliwahi kueleza hapa kwamba, moja ya maeneo tunayofeli ni pale kwenye balozi tunazotakiwa kuwa na wabobezi wa masuala ya ushirikiano wa kimataifa, tunajaza wabobezi wa masuala ya uhusiano wa kimataifa!
 
Na Tanzania tupo vizuri sana kwenye suala la siasa za uhusiano lakini huwa tunafeli kwenye suala la ushirikiano! Kuna siku niliwahi kueleza hapa kwamba, moja ya maeneo tunayofeli ni pale kwenye balozi tunazotakiwa kuwa na wabobezi wa masuala ya ushirikiano wa kimataifa, tunajaza wabobezi wa masuala ya uhusiano wa kimataifa!
Nakubaliana na wewe kwa asilimia kubwa, Tanzania kdg ina mapungufu ktk balozi zetu

Ila kwa Congo kdg ilikua tuzembee ila naona kuna juhudi zinafanyika kuboresha ushirikiano na uhusiano
 
Moja ya vitu ambavyo Rais Felix anajaribu kuviweka sawa ni hilo la USHIRIKIANO NA UHUSIANO

Lkn hayo hayatofanyika km kule mashariki hapajatulia ,na juhudi za sasa EAC na SADC ni kusolve issue ya kule kisha kuangalia hili tunalojadili

Mashariki pakitulia na Congo ikatulia ,Hili linawezekana
Juzi kati M7 na Tshisekedi wamekubaliana kusafisha waasi huko mashariki. Macroni naye kaahidi kumsaidia kwa kigezo kuwa hao ADF wanamahusiano na ISIS, ni mwanzo mzuri. Kama ulivyosema, EAC na SADC zinaweza saidia kama ilivyoundwa ECOMOG japo kwahili kufanikiwa mnatakiwa wote kuongea lugha moja msije ongeza ukubwa wa tatizo.
 
Mkuu Nguruvi3!!

Umemaliza kila kitu! Na hata niliposema Tanzania ina fursa zaidi ya kuuza Kenya in terms of monetary value kuliko ilivyo Kenya kwa Tanzania, focus yangu ilikuwa ndiyo eneo hilo hilo uliloelezea... agribusiness! Inasikitisha kuona hatuitumii fursa hii ipasavyo!
Hili suala nimewahi uliza humu, kwanini tusiwe na soko huru la chakula EAC? Tungefaidika sana. Mapinduzi ya kilimo hayaletwi na ruzuku bali soko la uhakika na bei nzuri. Leo EAC kuna soko la watu 168mln. Tumepoteza sana hapa. hatuna sababu ya kujifungia, maana, paradoxically, kufunga mipaka huleta njaa kuliko uhakika wa chakula.
 
Tuangalie vizuri..
Nchi wenye misuguano kila siku hakufai .
Adui ana milango mingi ya kupitia...
 
Mkuu Red Giant nilitoa ahadi ya kurudi na sasa nimerudi na nitachangia kidogo juu ya hii mada ambayo ni muhimu kabisa. Nitatoa maoni kama Mwanasiasa, pia nitatoa maoni kama Mwansheria. Naomba niende moja kwa moja kwenye mada:

Congo DRC isitengwe bali isiruhusiwe kuingia kwenye Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) kwasababu itaongeza changamoto ambazo tayari EAC inazo na imeshindwa kuzimaliza kwa muda mrefu. Changamoto kubwa ni hii ifuatayo hapa chini:

Mosi, nchi wanachama wa EAC wanakumbwa na matatizo ya kisiasa ndani ya nchi zao ambayo kwa namna moja au nyingine yameugharimu huu ukanda muda na rasilimali nyingi ambazo zingewekezwa katika kufanya mambo ya msingi.

Uganda mpaka leo wanapigana na waasi wa Lord's Resistance Army wa Bwana Joseph Konyi. Upande wa pili kuna sintofahamu kubwa sana kwenye siasa zake za ndani na hatufahamu nini kitatokea nchini humo baada ya Raisi Museveni kutoka. Tunaweza kuhisi kwamba Uganda iko salama lakini kumbuka tangu nchi hiyo inapata uhuru hakujawahi kuwa na Raisi ambaye hatatoka kwa vimbwanga na kusababisha kuchafukwa kwa hali ya kisiasa nchini humo kuanzia Mutesa hadi Obote.

Rwanda nayo mpaka sasa iko kwenye vita isiyoisha na makundi ya waasi wa Kihutu ambao wako Congo DRC na duniani kote. Hivi karibuni siasa ya Rwanda imegubikwa na kiza kikali baada ya kusemekana kwamba kuna Watutsi ambao waliwahi kuwa ndani ya Serikali ya Raisi Paul Kagame wameunda mtandao mkubwa wa kutaka kumpindua. Rwanda kama nchi inaenda vizuri kwasasa lakini bado kuna sintofahamu kubwa kama Uganda ambako mpaka leo hawana uhakika na Smooth Transition of Power after the fall of their strongmen.

Burundi mpaka sasa unafahamu nini kimekuwa kinaendelea tokea mwaka 2015, na bado nako kuna sintofahamu kubwa sana na Serikali ya Raisi Nkurunzinza iko nje-ndani.

Tanzania na Kenya hazijatofautiani sana. Zimefanikiwa sana kwenye suala la Smooth Transition of Power hivyo kufanikiwa kukwepa sintofahamu nyingi za kisiasa ambazo zimewakuta mataifa ya jirani. Japo upande wa pili bado Kenya ina changamoto kubwa za kiusalama ambazo zimemfanya apoteze rasilimalu nyingi sana kule Somalia akipambana na kikundi cha Al Shabab huku Tanzania ikiwa inapita kwenye kipindi kigumu kisiasa ambacho pia kinaweza kuzaa sintofahamu kubwa sana huko mbeleni kama siasa yake itaendelea kwenye njia hii.

Ninachotaka kusema kwenye hoja hii ni hiki hapa: EAC iliundwa kama Jumuiya ya kiuchumi na siyo ya kisiasa. Haya ya siasa kama kuunda shirikisho ni malengo ya baadae sana (Future Objectives) ambayo hayatakiwi kuwa kwenye ajenda yoyote kwenye kipindi hiki.

Lengo kuu na ajenda ya sasa (Main and Primary Objective) inabidi iwe ni Uchumi kupitia soko la pamoja na sarafu moja. Kama tukifanikiwa kujenga uchumi wa pamoja basi ndiyo mambo ya siasa yaanze kuingia kwenye ajenda za vikao vyetu. Sasa machafuko ya kisiasa huwa yanatutoa kwenye mstari maana hutulazimisha kuacha kufanya mambo ya kiuchumi na kujiingiza kwenye siasa, kitu ambacho siyo lengo letu kama EAC.

Tokea EAC iundwe tumekuwa tukitatua matatizo ya kisiasa yanayogharimu rasilimali nyingi kuliko kufanya mambo muhimu: Tunalazimika kufanya hivyo kwasababu ni majirani zetu lakini haswa kwasababu ni wanajumuiya wenzetu. Tulianza na Kenya mwaka 2007-2008: Kenya na Alshabaab 2012:Tukaja Rwanda na Tanzania mwaka 2013: Burundi mwaka 2015: Uganda na Rwanda 2019. Sasa tukiileta DRC na ilivyo na matatizo lukuki basi fahamu kwamba tutabeba na changamoto zao kuanzia uchaguzi hadi waasi wa Kagame na Museveni.

Pili, Congo DRC kama nchi imeshaigharimu SADC ambayo ilijiunga mwaka 1997 punde tu baada ya kumtoa Mobutu Sese Seko madarakani. SADC ilijikuta inatumia muda mwingi sana kushughulika na CONGO DRC badala ya kujikita kufanya mambo ya msingi. Ikumbukwe Mzee Kabila alivutana sana na viongozi wenzake wa SADC pale alipotaka wamsaidie kupambana kwenye The Congo War lakini wakawa wanasuasua. Wakina Quett Masire wanataka kumsuluhisha yeye Kabila anasusia vikao. Unadhani nchi kama hii ikijiunga na EAC na ikapatwa na tatizo tutakwepa kweli kuhusika ???

Tatu, wengi tunatamani Congo DRC ijiunge EAC kwasababu ya rasilimali zake. Basi kama itijiunga na EAC itageuzwa rasmi kuwa kichaka cha mashindano ya wizi wa rasilimali zake baina ya nchi wanachama wa EAC. Mfano hai tu, Umoja wa Mataifa (UN) waliwahi kutoa taarifa ya uchunguzi kwamba kipindi cha Vita ya Congo Zimbabwe ilipewa na serikali ya Laurent Kabila malipo ya dola za Kimarekani Bilioni 5 ambazo zimetoka kwenye mali mbalimbali za watu wa Congo DRC. Haya malipo yalienda sambamba na mikataba ya madini ambayo Zimbabwe na Angola waliipata kwa kumsaidia Kabila.

Upande mwingine inasemekana mataifa ya nje yaliua zaidi ya tembo 12,000 kwenye mbuga ya Garamba. Umoja wa Mataifa uliilaani Rwanda na Uganda kwa kuiba maelfu ya rasilimali za watu wa Congo DRC kwa kisingizio cha kupigana na waasi.

Sasa hii ilikuwa miaka ya 1999-2003, unadhani DRC ikijiunga rasmi na EAC Tanzania, Kenya, Uganda na Rwanda watakaa tu kuziangalia zile rasilimali ??? Utatokea mvutano mkubwa sana baina yetu kuanzia kwenye uchaguzi wa DRC maana kila nchi mwanachama atataka aweke kwenye serikali mtu ambaye atakuwa na ushawishi mkubwa sana kwake: Rwanda na Uganda walishawahi kupigana kisa kutaka rasilimali za Congo DRC, sasa DRC ijiunge na EAC hapo waongezeka Tanzania na Kenya unadhani kuna utulivu hapo ???

Mfano mwingine ,angalia kilichotokea Burundi 2015 baina ya Tanzania na Rwanda kutaka kujenga ushawishi kwa serikali ya Bujumbura. Sasa piga picha Burundi alikuwa hana utajiri wowote ule, unadhani Congo mwenye utajiri atatuacha salama ???

Sisi Tanzania tuna utajiri mkubwa ambao Mungu ametupa na itakuwa ni ujinga kama tutaka Congo DRC iinge EAC kwasababu ya utajiri wake. Japo kimkakati (Strategically)ni jambo sahihi, lakini tatizo linakuja kwamba pale ambapo hatuna mpango maalumu na nini tutafanya na Congo DRC baada ya kuwa karibu na sisi. Hivyo tuiache tu na tusitafute matatizo yasiyo na ulazima wowote ule: Pia tusichume dhambi with this Imperialistic Mindset....

NINI KIFANYIKE KUHUSU CONGO DRC???
Hapa nitatoa maoni kama mwanasiasa:
Mosi, EAC ijikite kwenye kuimarisha taasisi zake yenyewe (Consolidation and Amalgmation of it's Institutions) na siyo kujitanua (Enlargement of the bloc) kwa kutafuta au kuruhusu wanachama wapya.

EAC imeiga vitu vingi kutoka European Union (EU) ambayo zamani ilikuwa ni European Economic Community (EEC) lakini haifanyi vizuri kama ambavyo EEC ilifanya. Umoja wa Ulaya ulianza kama Umoja wa Uchumi (Economic Union) na siyo Umoja wa Kisiasa (Political Union), lakini baadae ndiyo ukafika hapa ulipo. Ulipitia hatua

Ulianza kutengeneza kitu kinachoitwa The European Coal and Steel Community mwaka 1951 ambayo ilikuwa ni taasisi iliyoundwa kwa lengo la kuhakikisha makaa ya mawe na chuka vinasimamiwa na Chombo/Taasisi moja ya kimataifa inayojitegemea ili kuzuia mvutano baina ya nchi kubwa kama Ujerumani na Ufaransa ambao ulipelekea kutokea vita ya kwanza na ya pili ya dunia.

Aliyesuka huu mpango anaitwa Jean Monet ambaye alisema ili tuweze kujenga umoja imara ni lazima tuhakikishe mataifa yenye nguvu na rasilimali nyingi ya Ujerumani na Ufaransa yanaungwanishwa kiuchumi kiasi kwamba nchi yeyote haiwezi kufikiria kwenda vitani na mwenzake. Kweli walifanikiwa sana maana mkataba huu ulisainiwa na mataifa sita (Ujerumani Magharibi, Ufaransa, Italia, Ubelgiji na Luxembourg) hata yale ambayo yalikuwa hayana rasilimali kama Ubelgiji na Luxembourg walinufaika.

Mwaka 1957 wakasaini mkata wa kuunda taasisi nyingine iitwayo The European Atomic Energy Community ambayo kazi yake ilikuwa kuzimamia uzalisha wa nishati ya nyuklia Ulaya ili kuwasaidia wanachama kupunguza utegemezi kwenye mafuta, pia kuuza nishati ya akiba kwa mataifa yasiyo wanachama. Hili nalo walifanikiwa sana.

Mwaka 1957 wakatengeneza sasa Umoja wa Uchumi wa Ulaya ambao leo ndiyo Umoja wa Ulaya. Lakini hawakuwa na haraka na hili liliwezekana kwasababu wao walikuwa na hali nzuri ya kisiasa nchini mwao. Mwaka 1967 taasisi za European Economic Community, European Steel and Coal Community na European Atomic Energy Community ziliungwanishwa kuwa chombo kimoja. Biashara baina ya wanachama ilikuwa kwa asilima 28.4%.

Hawakukimbilia kujitanua bali walijijenga kwanza wao kiuchumi na kisiasa kabla ya kuhakikisha wanayakaribisha mataifa mengine kama Uingereza mwaka 1973. Japo wanafanya vizuri lakini bado wana matatizo sana, Raisi wa Ufaransa Charles De Gaulle miaka ya 1969 hakupenda Uingereza ijiunge na EEC kwasababu alisema italeta matatizo kwenye jumuiya hivyo alipinga sana hadi anafariki.

Uingereza aliruhusiwa kujiunga baada ya De Gaulle kufariki. Lakini mbali na yote yale siasa za Uingereza zimeutikisa Umoja wa Ulaya kama ambavyo De Gaulle alionya. Sasa Uingereza taifa lililoendelea sana kuliko Congo DRC matatizo yake ya ndani yamevuruga Umoja wa Ulaya unadhani ni busara kuleta tena mgeni ???

Hapa hoja yangu ni hii: Kichwa na Moyo wa EAC ni Kenya na Tanzania wala siyo rasilimali za Congo DRC. Kama tunataka EAC imara basi ni lazima tuhakikishe Kenya na Tanzania zinaelewana na kuzungumza lugha moja. Maana binafsi naamini ushawishi wa Kenya na Tanzania wakiwa wanaongea lugha moja ni hatari kuliko mlipuko wa bomu la kiatomiki na hakuna taifa la Afrika linaweza kuwashinda. Raisi Kwame Nkhuruma alilifahamu vizuri hili suala ndiyo maana alipinga sana EAC isiwe nchi moja.

Kenya na Tanzania wakiungana basi lazima Uganda, Rwanda na Burundi watafuata tu. Kenya na Tanzania zina Uchumi mkubwa, ushawishi mkubwa sana kikanda na kimataifa, zimekaa pazuri sana kijiografia, zina rasilimali nyingi na zina watu wengi wanaozungumza lugha moja. Wakenya na Watanzania hawapatani kwasababu wamefanana mno tabia, fanya uchunguzi utaligundua hili.

Mtifuano wa kiuchumi na kihistoria baina ya Kenya na Tanzania ndiyo unavuruga EAC. Tunafanyiana hujuma badala ya kuunganisha nguvu za kitaasisi ili tujikwamue hapa tulipo. Hujuma kwenye kilimo, hujuma kwenye bandari na hujuma kwenye viwanda bila kufahamu kwamba Afrika Mashariki yote tunaweza kuwa Mamlaka moja ya Bandari ambayo ingetusaidia sana.

AU tungeweza kuanzisha Joint Venture Agreement kupitia Special Purpose Vehicle kwenye kuratibu biashara ya Usafiri wa anga. AU tukaunganisha nguvu kwenye tafiti za Uchimbaji wa mafuta na gesi mbona tungefika mbali sana tu. Wazungu walitwangana ndiyo wakapata akili kwamba kumbe tunaweza kushirikiana bila mabomu na vifaru.

Lakini sisi tunataka kushindana kisa kulipizana visasi vya ugomvi wa Mzee Kenyatta na Mzee Nyerere. Leo hii kwa mitandao ya kibiashara ambayo Kenya na Tanzania tunayo kupitia nguvu za diplomasia za nchi zetu kama tukishirikiana sauti yetu itafika hadi mwisho wa dunia. Nashangaa kwanini hatulioni hili. Binafsi Kenya and Tanzania is a key, ndiyo maana hata Rwanda, Burundi na Uganda walipovutana hakikutokea kitu sana lakini Kenyatta na Jakaya wakivutana lazima EAC iyumbe. Hujiulizi kwanini ???


Pili, na mwisho kabisa natoa ushauri kama mwanasheria sasa: Congo DRC asiwe mwanachama ila aidha apewe nafasi ya mtazamaji (Observer Status) kwanza ndani ya EAC huku akijifunza mwenendo mzima wa EAC. Sambamba na hilo EAC tunaweza kusaini mkataba maalumu wa Congo DRC (Sui Generis Treaty) ambao utampa nafasi ya kipekee kunufaika kiuchumi bila kuwa mwanachama. Anaweza akaandaliwa vipengele (Extracts Clause with Limitations ) kutoka mikataba mbalimbali (Protocols) ambayo EAC ameshasaini. Anaweza kufanya kama ambavyo Uingereza na Umoja wa Ulaya walifanya miaka ya 1960's- 1970's au ambavyo wanataka kufanya baada ya Brexit.

Tujijenge kwanza sisi ndiyo turuhusu waliovurugwa kama Congo DRC wajiunge.
Una akili kuliko serikali nzima ya magufuli combined, kuanzia mawazili mpaka watendaji.
 
Back
Top Bottom