tpaul
JF-Expert Member
- Feb 3, 2008
- 21,818
- 18,241
Mwaka jana nilibahatika kwenda Arusha kikazi ambako nililazimika kukaa kwa muda wa majuma mawili. Kuna mambo ya maana nimejifunza kutoka kwa kabila la wachaga, ambayo kama watanzania tukiyatilia maanani, yanaweza kutuletea maendeleo kwa haraka.
Katika pitapita zangu sikuwahi kuwaona wachaga wakiwa wamekaa kwenye vijiwe au vikundi vya kupiga sogakila mtu yupo serious na kazi au shughuli inayomuingizia kipato. Kuna baa moja maarufu ambayo nilipenda kwenda kula chakula ambako pia nilijifunza jambo kuhusu kabila hili. Sikuweza kuwakuta wachaga wakilewa ovyo kama watu wa makabila mengine. Mchaga akitoka kazini hupitia baa na kunywa bia zake 2 au 3 na kisha huondoka kwenda nyumbani kujipumzisha ili kesho awahi kazini kwake kuchapa kazi bila kuathiriwa na mninginio (hangover) wa ulevi. Wachaga huwa hawakeshi kwenye mabaa wakilewa chakali. Hawana utamaduni huo hata kidogo.
Aidha, wachaga ni watu ambao wanaheshimu sana kazi. Kazi wanayoiweza na ambayo imewapa sifa sana ni biashara. Sote ni mashahidi jinsi ambavyo watu wa kabila hili wametapakaa nchi nzima wakifanya shuguli za biashara kuanzaia ya duka (Dukani kwa Mangi) hadi biashara kubwa kabisa. Hakuna mtaa katika nchi hii ambako utakosa duka la Mangi. Nadhani mazingira ya mikoa wanayotoka (Arusha & Kilimanjaro) inachangia sana kuwafanya wawe wajasiriamali na watafuta mali/utajiri. Katika mikoa hii, hakuna ardhi ya kutosha kuendesha shughuli za kilimo. Hivyo, inawalazimu kuwa wajasiriamali moja kwa moja tangu wakiwa na umri mdogo.
Wazazi wa kichaga huwarithisha watoto wao ELIMU badala ya ARDHI (ambayo hawana). Mzazi akishamsomesha mwanae hadi akahitimu chuo au kozi fulani, ndio nitolee. Usitegemee kwamba atakupa urithi mwingine zaidi ya huo hata kama ana utajiri wa kutishasahau kabisa! Hili nalo linasaidia kuwafanya watoto wa kichaga wasome kwa bidii na kufaulu vizuri. Ushahidi wa hili ni kwenye matokeo ya mitihani ya kitaifa. Mara nyingi mikoa ya Arusha na Kilimanjaro hufanya vizuri kila mwaka. Ndio maana wachaga wengi hushiikilia nafasi za juu serikalini na katika sekta muhimu hapa nchini. Sio kwamba wanapendelewa au kupendeleana kikabila bali inatokana na juhudi zao za kusaka elimu na maendeleao kwa bidii zao zote.
Ikiwa kila mtanzania akiiga utamaduni huu wa wachaga ni wazi kwamba nchi hii itapata maendeleo haraka kuliko tunavyotarajia. Kwa bahati mbaya makabila mengine wanaweza sana kujikweza na kujisifu (Wahaya), kukatana mapanga na kupigana vita (Wakurya), kucheza ngoma na bao (Wakwere, Wadengereko na Wakwere na baadhi ya makbila ya pwani), kujinyonga (watani zangu Wahehe), kula chamaki nchanga na (watani zangu Wamakonde na Wahehe), n.k.
Utamaduni huu wa maendeleo kutoka kwa watani zangu wachaga nimeupenda sana na ningeomba kila mtanganyika mpenda maendeleo auige.
Nawasilisha.
yield
Katika pitapita zangu sikuwahi kuwaona wachaga wakiwa wamekaa kwenye vijiwe au vikundi vya kupiga sogakila mtu yupo serious na kazi au shughuli inayomuingizia kipato. Kuna baa moja maarufu ambayo nilipenda kwenda kula chakula ambako pia nilijifunza jambo kuhusu kabila hili. Sikuweza kuwakuta wachaga wakilewa ovyo kama watu wa makabila mengine. Mchaga akitoka kazini hupitia baa na kunywa bia zake 2 au 3 na kisha huondoka kwenda nyumbani kujipumzisha ili kesho awahi kazini kwake kuchapa kazi bila kuathiriwa na mninginio (hangover) wa ulevi. Wachaga huwa hawakeshi kwenye mabaa wakilewa chakali. Hawana utamaduni huo hata kidogo.
Aidha, wachaga ni watu ambao wanaheshimu sana kazi. Kazi wanayoiweza na ambayo imewapa sifa sana ni biashara. Sote ni mashahidi jinsi ambavyo watu wa kabila hili wametapakaa nchi nzima wakifanya shuguli za biashara kuanzaia ya duka (Dukani kwa Mangi) hadi biashara kubwa kabisa. Hakuna mtaa katika nchi hii ambako utakosa duka la Mangi. Nadhani mazingira ya mikoa wanayotoka (Arusha & Kilimanjaro) inachangia sana kuwafanya wawe wajasiriamali na watafuta mali/utajiri. Katika mikoa hii, hakuna ardhi ya kutosha kuendesha shughuli za kilimo. Hivyo, inawalazimu kuwa wajasiriamali moja kwa moja tangu wakiwa na umri mdogo.
Wazazi wa kichaga huwarithisha watoto wao ELIMU badala ya ARDHI (ambayo hawana). Mzazi akishamsomesha mwanae hadi akahitimu chuo au kozi fulani, ndio nitolee. Usitegemee kwamba atakupa urithi mwingine zaidi ya huo hata kama ana utajiri wa kutishasahau kabisa! Hili nalo linasaidia kuwafanya watoto wa kichaga wasome kwa bidii na kufaulu vizuri. Ushahidi wa hili ni kwenye matokeo ya mitihani ya kitaifa. Mara nyingi mikoa ya Arusha na Kilimanjaro hufanya vizuri kila mwaka. Ndio maana wachaga wengi hushiikilia nafasi za juu serikalini na katika sekta muhimu hapa nchini. Sio kwamba wanapendelewa au kupendeleana kikabila bali inatokana na juhudi zao za kusaka elimu na maendeleao kwa bidii zao zote.
Ikiwa kila mtanzania akiiga utamaduni huu wa wachaga ni wazi kwamba nchi hii itapata maendeleo haraka kuliko tunavyotarajia. Kwa bahati mbaya makabila mengine wanaweza sana kujikweza na kujisifu (Wahaya), kukatana mapanga na kupigana vita (Wakurya), kucheza ngoma na bao (Wakwere, Wadengereko na Wakwere na baadhi ya makbila ya pwani), kujinyonga (watani zangu Wahehe), kula chamaki nchanga na (watani zangu Wamakonde na Wahehe), n.k.
Utamaduni huu wa maendeleo kutoka kwa watani zangu wachaga nimeupenda sana na ningeomba kila mtanganyika mpenda maendeleo auige.
Nawasilisha.
yield