A FM na C FM waripoti, Mamilioni ya fedha za michango yazua mzozo CHADEMA. Wameamua kutumika kwenye siasa chafu?

A FM na C FM waripoti, Mamilioni ya fedha za michango yazua mzozo CHADEMA. Wameamua kutumika kwenye siasa chafu?

Mkalukungone Mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
2,913
Reaction score
6,512
Ila hivi vyombo vya habari bhana kuna muda wanatumika mchana kweupe!

Yani kuisoma hii habari ilio chapishwa na AFM na C FM zote ni za Dodoma unaona ni propaganda kabisa

Kuna mtu mmoja kawapa habari hiyo waichapishe nawao kwa sababu ya njaa zao wameruka nayo. Dah safari bado ni ndefu sana kwenye media zetu hapa nchini

Je ingekuwa tetesi hizi zinaigusa CCM wangeifanya na kuipelekeka hewani?
==============
UONGOZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), umeanza kuvurugana, baada ya Makamu Mwenyekiti wa chama hicho bara, John Heche, kudaiwa kutafuna mamilioni ya michango wanayokusanya kutoka kwa wadau.

Chama hicho, kimekuwa kikikusanya fedha kutoka kwa wanachama wake na wadau mbalimbali, taarifa kutoka chanzo cha kuaminika, zinadai sehemu ya fedha hizo zinaishia mifukoni mwa viongozi.

Hayo yamebainika juzi katika kikao cha viongozi wa chama hicho ‘Retreat’ kilichofanyika mkoani Kigoma na kuhusisha wajumbe wote wa Kamati Kuu.

Chanzo hicho kutoka miongoni mwa wajumbe walioshiriki kikao hicho, kinadai Mjumbe wa Kamati Kuu, Godbless Lema, ndiye aliyeanza kufichua mambo, baada ya kueleza Heche alipewa mchango wa Shilingi milioni 60 na mdau kwa ajili ya chama hicho, lakini hakuwasilisha hata senti moja.

Mambo yalikwenda mbali zaidi, hadi Lema alipomtaka Heche abishe hadharani kama hakuwahi kupokea kiasi hicho cha fedha. Katika utetezi wake, Heche amedai alidhani fedha hizo anazopewa ni kwa ajili yake binafsi.

Haikuishia hapo, chanzo hicho kinadai, kinasema Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Nyasa, Joseph Mbilinyi maarufu Sugu, naye alisema Heche amekula Shilingi milioni 10.

Inadaiwa katika maelezo yake ndani ya kikao hicho, Sugu alisema alimpeleka Heche kukutana na mmoja wa wadau wao kwa ajili ya kupokea mchango wa ujenzi wa chama, cha kushangaza fedha zote hizo hazikufikishwa kwenye chama, zikaishia mifukoni mwa Heche.

Ikumbukwe kuwa, viongozi hao wa Chadema akiwemo Heche, ndiyo wanaosimama majukwaani wakiomba wapewe nafasi ya kuliongoza Taifa kwa ahadi kuwa watasimamia fedha za umma, ilhali usimamizi wa vijisenti vya chama umewashinda.

Huo ni uthibitisho tosha kuwa, Chadema imejaa viongozi wanaofanya kila jambo kwa maslahi yao binafsi, wanajenga kila ushawishi kuwaumiza wananchi ili kujinufaisha na wanatafuta huruma ya umma, ili kukusanya fedha za kunufaisha familia zao.

Mwisho wa kikao hicho, inadaiwa Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika alimkingia kifua Heche, huku akionya kuwa, vitendo hivyo si vizuri kufanywa na viongozi.

Screenshot 2026-07-04 010442.png
Screenshot 2026-07-04 012338.png
 
Ila hivi vyombo vya habari bhana kuna muda wanatumika mchana kweupe!

Yani kuisoma hii habari ilio chapishwa na AFM na C FM zote ni za Dodoma unaona ni propaganda kabisa

Kuna mtu mmoja kawapa habari hiyo waichapishe nawao kwa sababu ya njaa zao wameruka nayo. Dah safari bado ni ndefu sana kwenye media zetu hapa nchini

Je ingekuwa tetesi hizi zinaigusa CCM wangeifanya na kuipelekeka hewani?
==============
UONGOZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), umeanza kuvurugana, baada ya Makamu Mwenyekiti wa chama hicho bara, John Heche, kudaiwa kutafuna mamilioni ya michango wanayokusanya kutoka kwa wadau.

Chama hicho, kimekuwa kikikusanya fedha kutoka kwa wanachama wake na wadau mbalimbali, taarifa kutoka chanzo cha kuaminika, zinadai sehemu ya fedha hizo zinaishia mifukoni mwa viongozi.

Hayo yamebainika juzi katika kikao cha viongozi wa chama hicho ‘Retreat’ kilichofanyika mkoani Kigoma na kuhusisha wajumbe wote wa Kamati Kuu.

Chanzo hicho kutoka miongoni mwa wajumbe walioshiriki kikao hicho, kinadai Mjumbe wa Kamati Kuu, Godbless Lema, ndiye aliyeanza kufichua mambo, baada ya kueleza Heche alipewa mchango wa Shilingi milioni 60 na mdau kwa ajili ya chama hicho, lakini hakuwasilisha hata senti moja.

Mambo yalikwenda mbali zaidi, hadi Lema alipomtaka Heche abishe hadharani kama hakuwahi kupokea kiasi hicho cha fedha. Katika utetezi wake, Heche amedai alidhani fedha hizo anazopewa ni kwa ajili yake binafsi.

Haikuishia hapo, chanzo hicho kinadai, kinasema Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Nyasa, Joseph Mbilinyi maarufu Sugu, naye alisema Heche amekula Shilingi milioni 10.

Inadaiwa katika maelezo yake ndani ya kikao hicho, Sugu alisema alimpeleka Heche kukutana na mmoja wa wadau wao kwa ajili ya kupokea mchango wa ujenzi wa chama, cha kushangaza fedha zote hizo hazikufikishwa kwenye chama, zikaishia mifukoni mwa Heche.

Ikumbukwe kuwa, viongozi hao wa Chadema akiwemo Heche, ndiyo wanaosimama majukwaani wakiomba wapewe nafasi ya kuliongoza Taifa kwa ahadi kuwa watasimamia fedha za umma, ilhali usimamizi wa vijisenti vya chama umewashinda.

Huo ni uthibitisho tosha kuwa, Chadema imejaa viongozi wanaofanya kila jambo kwa maslahi yao binafsi, wanajenga kila ushawishi kuwaumiza wananchi ili kujinufaisha na wanatafuta huruma ya umma, ili kukusanya fedha za kunufaisha familia zao.

Mwisho wa kikao hicho, inadaiwa Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika alimkingia kifua Heche, huku akionya kuwa, vitendo hivyo si vizuri kufanywa na viongozi.

View attachment 3621822View attachment 3621826
Kuna njia moja tu kuwafanya hawa wana propaganda za uongo wapelekwe mahakamani na kudaiwa mabilioni hivyo watakoma kama alivyonyooshwa Musiba
 
Kuna njia moja tu kuwafanya hawa wana propaganda za uongo wapelekwe mahakamani na kudaiwa mabilioni hivyo watakoma kama alivyonyooshwa Musiba
Sio kirahis hivo waliowatuma ndiyo watakao toa hukumu
Kesi ya nyani unampelekea ngedere

Musiba ilikuwa vile maana godfaza wake hakuwepo wazee wa kuhukumu waka dance according to beat lililokuwepo kwa wakati tuliopo
 
Ila hivi vyombo vya habari bhana kuna muda wanatumika mchana kweupe!

Yani kuisoma hii habari ilio chapishwa na AFM na C FM zote ni za Dodoma unaona ni propaganda kabisa

Kuna mtu mmoja kawapa habari hiyo waichapishe nawao kwa sababu ya njaa zao wameruka nayo. Dah safari bado ni ndefu sana kwenye media zetu hapa nchini

Je ingekuwa tetesi hizi zinaigusa CCM wangeifanya na kuipelekeka hewani?
==============
UONGOZI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), umeanza kuvurugana, baada ya Makamu Mwenyekiti wa chama hicho bara, John Heche, kudaiwa kutafuna mamilioni ya michango wanayokusanya kutoka kwa wadau.

Chama hicho, kimekuwa kikikusanya fedha kutoka kwa wanachama wake na wadau mbalimbali, taarifa kutoka chanzo cha kuaminika, zinadai sehemu ya fedha hizo zinaishia mifukoni mwa viongozi.

Hayo yamebainika juzi katika kikao cha viongozi wa chama hicho ‘Retreat’ kilichofanyika mkoani Kigoma na kuhusisha wajumbe wote wa Kamati Kuu.

Chanzo hicho kutoka miongoni mwa wajumbe walioshiriki kikao hicho, kinadai Mjumbe wa Kamati Kuu, Godbless Lema, ndiye aliyeanza kufichua mambo, baada ya kueleza Heche alipewa mchango wa Shilingi milioni 60 na mdau kwa ajili ya chama hicho, lakini hakuwasilisha hata senti moja.

Mambo yalikwenda mbali zaidi, hadi Lema alipomtaka Heche abishe hadharani kama hakuwahi kupokea kiasi hicho cha fedha. Katika utetezi wake, Heche amedai alidhani fedha hizo anazopewa ni kwa ajili yake binafsi.

Haikuishia hapo, chanzo hicho kinadai, kinasema Mwenyekiti wa Chadema Kanda ya Nyasa, Joseph Mbilinyi maarufu Sugu, naye alisema Heche amekula Shilingi milioni 10.

Inadaiwa katika maelezo yake ndani ya kikao hicho, Sugu alisema alimpeleka Heche kukutana na mmoja wa wadau wao kwa ajili ya kupokea mchango wa ujenzi wa chama, cha kushangaza fedha zote hizo hazikufikishwa kwenye chama, zikaishia mifukoni mwa Heche.

Ikumbukwe kuwa, viongozi hao wa Chadema akiwemo Heche, ndiyo wanaosimama majukwaani wakiomba wapewe nafasi ya kuliongoza Taifa kwa ahadi kuwa watasimamia fedha za umma, ilhali usimamizi wa vijisenti vya chama umewashinda.

Huo ni uthibitisho tosha kuwa, Chadema imejaa viongozi wanaofanya kila jambo kwa maslahi yao binafsi, wanajenga kila ushawishi kuwaumiza wananchi ili kujinufaisha na wanatafuta huruma ya umma, ili kukusanya fedha za kunufaisha familia zao.

Mwisho wa kikao hicho, inadaiwa Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika alimkingia kifua Heche, huku akionya kuwa, vitendo hivyo si vizuri kufanywa na viongozi.

View attachment 3621822View attachment 3621826
kama heche atashindwa tena kwenda kuilipia Crown yake TRA iliyomshinda wakati ule analia gharama ni kubwa, basi itaozea bandari, maana muda wa yeye kutusua pesa bwerere ndio huu.

Na kama ni uzushi, watu wawe wastahilivu na wenye subra tu, masuala ya fedha hayanaga tetesi na wala hayafichikagi.

Lazima watavurugana tu, kwasababu haiwezekani michango ikusanywe hadharani halafu matumizi yafanyike sirini kwa kificho 🐒
 
kama heche atashindwa tena kwenda kuilipia Crown yake TRA iliyomshinda wakati ule analia gharama ni kubwa, basi itaozea bandari, maana muda wa yeye kutusua pesa bwerere ndio huu.

Na kama ni uzushi, watu wawe wastahilivu na wenye subra tu, masuala ya fedha hayanaga tetesi na wala hayafichikagi.

Lazima watavurugana tu, kwasababu haiwezekani michango ikusanywe hadharani halafu matumizi yafanyike sirini kwa kificho 🐒
Hivi wewe tahira wazazi wako bado wapo hai?
 
Hivi wewe tahira wazazi wako bado wapo hai?
Gentleman,
itapendeza zaidi ukijita kwenye hoja mahususi mezani bila kuweweseka wala mihemko nonsense dhidi ya comment za wadau 🐒
 
Radio Zenyewe Zinajitafuta Na Bado Zinatangaza Uzushi Kama Vile Hakuna Wahariri
 
kama heche atashindwa tena kwenda kuilipia Crown yake TRA iliyomshinda wakati ule analia gharama ni kubwa, basi itaozea bandari, maana muda wa yeye kutusua pesa bwerere ndio huu.

Na kama ni uzushi, watu wawe wastahilivu na wenye subra tu, masuala ya fedha hayanaga tetesi na wala hayafichikagi.

Lazima watavurugana tu, kwasababu haiwezekani michango ikusanywe hadharani halafu matumizi yafanyike sirini kwa kificho 🐒
Mashoga na mapumbavu ya ccm hayana nafasi yoyote kwenye hii Dunia kwa sasa
 
Kwani hawajui pesa ilipo, mbona wanahangaika kusikolipa.

Hawawezi kumsifu Samia Suluhu Hassan, badala ya kuhangaika na CHADEMA?

Jinsi taarifa ilivyokaa ni kama wanawapigia kampeni CHADEMA!
Labla huko chadema ndo content ipo
 
Namuonea huruma mmiliki wa CFM....ataua redio...aachane na wanasiasa wa kibongo ambao ni uchwara tu...
Akikomaa shauri yake..watu wana mafaili yake
 
Gentleman,
itapendeza zaidi ukijita kwenye hoja mahususi mezani bila kuweweseka wala mihemko nonsense dhidi ya comment za wadau 🐒
Umeulizwa Wewe Tahira wazazi wako bado wapo hai? Jibu swali PUNGUZA kukata viunooo. Au acha kabisa
 
Kwa mujibu wa madai yanayodaiwa kutolewa na Sugu na Lema, tuhuma dhidi ya Heche zilianza baada ya viongozi hao kudai kuwa walimtambulisha kwa baadhi ya wadau ili kukusanya michango ya kuendesha shughuli za chama.

Inadaiwa kuwa Sugu alimpeleka kwa mdau mmoja aliyetoa mchango wa shilingi milioni 10. Kwa mujibu wa simulizi hilo, fedha hizo hazikuwasilishwa kwa chama. Baada ya Sugu kumuuliza Katibu Mkuu, John Mnyika, alidai kuambiwa kuwa fedha hizo hazijapokelewa. Sugu alipomhoji Heche kuhusu suala hilo, inadaiwa Heche alimtumia shilingi milioni 1.

Vilevile, Lema anadaiwa kumpeleka Heche kwa mdau mwingine aliyetoa mchango wa shilingi milioni 60, lakini fedha hizo nazo zinadaiwa kutowasilishwa kwenye chama.

Kwa mujibu wa madai hayo, masuala hayo ndiyo yaliyoibuliwa ndani ya Kamati Kuu, ambapo inadaiwa Heche alikiri baadhi ya hoja zilizokuwa zimewasilishwa. Baadaye kulikuwa na juhudi za maridhiano, lakini baadhi ya wajumbe walidai kuwa alikuwa hataki kushiriki kikamilifu katika mchakato huo huku kukiwa na madai kwamba alikuwa akiwasiliana na baadhi ya viongozi serikalini, akiwemo Mwigulu Nchemba.

Kutokana na hali hiyo, baadhi ya wajumbe walifikia hatua ya kupendekeza Heche ajiuzulu. Hata hivyo, kwa mujibu wa simulizi hilo, Mnyika aliingilia kati na kuwaomba wajumbe watulize hasira, akieleza kuwa endapo mgogoro huo ungevuja hadharani, ungeweza kuleta madhara makubwa kwa taswira y
a Chama
 
Back
Top Bottom