Tufanye nini kushinda vita ya Uchumi?

pansophy

JF-Expert Member
Nov 13, 2011
502
320
Mara kadha wa kadha tumesikia serikali yetu ipo kwenye vita ya uchumi (Economic War). Kwa miaka ya hivi karibuni hii vita ya uchumi imekuwa ikihusisha mataifa makubwa mawili, Marekani na China. Walau kwa wenzetu tunaweza kuona mpambano unaendaje mathalan China anashusha thamani ya pesa yake, wanashindana kupata mikataba ya kibiashara na nchi mbalimbali (Trade agreements) na njia nyingine mbalimbali.



Tukiacha haya mataifa makubwa kuna vitu bado vinanitaza kwa upande wetu;

a)Tanzania ipo kwenye vita ya Uchumi na nani?
b)Mbinu zetu za kivita ni zipi?
c)Tutashinda vipi (vigezo vitakavyotufanya tuseme tumeshinda au tunaongoza kwenye mpambano huu.

Sitegemei majibu mepesi kama uchumi wa kati na viwanda kama yanatosha kuonyesha namna tulivyojipanga kwenye hii vita.

NB: Usilete majibu ya mepesi au kejeli na kelele za wachumia matumbo. Lengo ni kujifunza na kutaka kujua ili tusonge mbele. Sio lazima wote tujibu.

Karibuni wana jamvi
 
Dude we are not fighting with anyone, Economic war for us is targeting to increase our capitals

Tanzania is trying to solve his long time devil enemies poverty is one of those.
 
CCM iondoke madarakani, Kwa miaka zaidi ya 50 wamedidimizs uchumi. Mpaka sasa hivi maji na umeme na vitu vya kifahari. Kula mayai na maziwa ni anasa.
 
Tuache ukurupukaji, uchumi ni sayansi,haongozwi kwa husia na mizuka ya kishamba na ulimbukeni.
 
Usalama wa taifa wajikite kwenye kutafuta taarifa za kijasusi hasa zile za kiuchumi.


Wapunguze kutafuta taarifa za kijasusi zinazomuhusu Membe na mbowe.

Labda wewe unafahamu zaidi usalama wa taifa unavyofanya kazi, lakini mada ni tutumie njia gani kushinda vita ya uchumi? Usalama wa Taifa na uchumi wapi na wapi?
 
Tuache ukurupukaji, uchumi ni sayansi,haongozwi kwa husia na mizuka ya kishamba na ulimbukeni.
Sasa nani anayekurupuka? Nimeangalia dira ya Taifa sijaona sehemu ikigusia vita ya uchumi ndio maana ikanibidi niulize
 
Tanzania ipo kwenye vita ya kiuchumi na Kenya na Rwanda ingawa Tanzania sidhani kama ilianza hii vita.
Tanzania mpaka sasa imeshindwa hii vita haijajua vitu gani vinaweza yanyua uchumi wake yaani sie bado ni “reactive country” na sio “pro active”.
Mbinu za kushinda vita bado sijaona ila kama kweli tuna nia ya kupigana hii vita Africa inabidi turudi ubaoni.... ila hii viwanda tunadanganyana bado na hata nchi kubwa zimeacha kupigana maana zimeachwa mbali na Asia
 
Huo msemo wa Tanzania tunapigana vita ya kiuchumi ni propaganda iliyotungwa na Magufuli kujilinda anapokosolewa au kusemwa vibaya ama kunyimwa mikopo na misaada na taasisi za kimataifa kutokana na sera mbovu na uongozi wa mabavu

Anawaaminisha Watanzania yeye yupo sahihi wakati wote na kila anayemkosoa basi ni adui anayetaka kuihujumu Tanzania

Sasa jiulize Tanzania tunapigana hiyo vita na nani? Kenya? Ulaya? Marekani? China?

Kama ni vita na Ulaya au Marekani mbona tungeshashindwa dk 0 na shilingi yetu kuporomoka mara dufu

Wanaopigana vita za kiuchumi ni Korea Kaskazin, Iran, China, Urusi ambao wanapigwa vikwazo na kodi kubwa za bidhaa zao wanapo export nje, nyingine hadi dunia nzima imepigwa marufuku kununua bidhaa zao ama kuwauzia
Hizo ndio vita za kiuchumi

Tanzania tunaweza kununua bidhaa popote tukiwa na hela ama kuuza bidhaa zetu popote kama zikiwa na quality nzuri na zikiwa cheaper kuliko za competitor.

Hatupo kwenye vita ya uchumi na nchi yoyote

Sio sisi ambao hatuwezi kufuga hata nyuki hadi wawekezaji waje, ni vita gani tunaweza kupigana?
 
Huo msemo wa Tanzania tunapigana vita ya kiuchumi ni propaganda iliyotungwa na Magufuli kujilinda anapokosolewa au kusemwa vibaya ama kunyimwa mikopo na misaada na taasisi za kimataifa kutokana na sera mbovu na uongozi wa mabavu

Anawaaminisha Watanzania yeye yupo sahihi wakati wote na kila anayemkosoa basi ni adui anayetaka kuihujumu Tanzania

Sasa jiulize Tanzania tunapigana hiyo vita na nani? Kenya? Ulaya? Marekani? China?

Kama ni vita na Ulaya au Marekani mbona tungeshashindwa dk 0 na shilingi yetu kuporomoka mara dufu

Wanaopigana vita za kiuchumi ni Korea Kaskazin, Iran, China, Urusi ambao wanapigwa vikwazo na kodi kubwa za bidhaa zao wanapo export nje, nyingine hadi dunia nzima imepigwa marufuku kununua bidhaa zao ama kuwauzia
Hizo ndio vita za kiuchumi

Tanzania tunaweza kununua bidhaa popote tukiwa na hela ama kuuza bidhaa zetu popote kama zikiwa na quality nzuri na zikiwa cheaper kuliko za competitor.

Hatupo kwenye vita ya uchumi na nchi yoyote

Sio sisi ambao hatuwezi kufuga hata nyuki hadi wawekezaji waje, ni vita gani tunaweza kupigana?
Vita ya mdomo, bado nafikiri kuna haja kubwa ya think tank ambao watatusaidia kwenye hili.
 
Tanzania ipo kwenye vita ya kiuchumi na Kenya na Rwanda ingawa Tanzania sidhani kama ilianza hii vita.
Tanzania mpaka sasa imeshindwa hii vita haijajua vitu gani vinaweza yanyua uchumi wake yaani sie bado ni “reactive country” na sio “pro active”.
Mbinu za kushinda vita bado sijaona ila kama kweli tuna nia ya kupigana hii vita Africa inabidi turudi ubaoni.... ila hii viwanda tunadanganyana bado na hata nchi kubwa zimeacha kupigana maana zimeachwa mbali na Asia
Nini kifanyike?
 
Back
Top Bottom