Tuambie sababu inayokufanya usipumzike.....

Tuambie sababu inayokufanya usipumzike.....

Leejay49

JF-Expert Member
Joined
Feb 10, 2023
Posts
19,299
Reaction score
60,932
Wakuu habari za nyie...

Mara nyingi nimekuwa nikiskia watu wanaambizana,. "Ukijiajiri unakuwa na mda mwingi wa kupumzika Kwasabu Kila kitu unajiamulia mwenyewe ufanye au usifanye".. kiuhalisia naona kama hii kauli haina ukweli,. Ila tuachane nayo tu kwanza tujikite kwenye mada

Tukiachana watumishi wa serikali najuwa likizo wanazo na wanazotumiaje hilo wanajua wenyewe,. Haya wewe ambaye umejiajiri kwanini hupumziki??,. Kwanini hujipi mda wa kupumzika japo hata miezi miwili au mitatu utulie tu upumzishe mwili na akili Au hata wiki au hata siku kadhaa ,. Kwanini hufanyi hivyo?..

Ni kwamba unaipenda sana KAZI au biashara Yako??, Au ni kwamba wewe hupendi kupumzika ( kutulia ) ,Bado hujatimiza malengo? Na unaamini ukifanya KAZI mfululizo bila kupumzika ndio utafanikiwa??,. Unayo majukumu mengi kiasi cha kwamba usipofanya KAZI wiki au mwezi mmoja Kila kitu kinavuruguika??,. Huna mtu wa kukusaidia ?? Au shida Nini??.... Tuambizane tu kidogo huenda ukapata namna ya kujipumzisha kutokana na maoni ya wadau..

Kwa upande wangu ni kwamba Bado sijaweza kujisimamia mwenyewe na watu ninaoshirikiana nao usipowasimamia KAZI zinaweza zisiende au zikafanyika sio Kwa kiwango kile ambacho inabidi kifanyike, Na mambo mengi ambayo yanahitaji kutimizwa Kwa wakati maana umri hausimami eti🥹
Nahitaji sana kujipumzisha ila changamoto ndio hiyo..

Tuambie na wewe tatizo nini???
 
Wakuu habari za nyie...

Mara nyingi nimekuwa nikiskia watu wanaambizana,. "Ukijiajiri unakuwa na mda mwingi wa kupumzika Kwasabu Kila kitu unajiamulia mwenyewe ufanye au usifanye".. kiuhalisia naona kama hii kauli haina ukweli,. Ila tuachane nayo tu kwanza tujikite kwenye mada

Tukiachana watumishi wa serikali najuwa likizo wanazo na wanazotumiaje hilo wanajua wenyewe,. Haya wewe ambaye umejiajiri kwanini hupumziki??,. Kwanini hujipi mda wa kupumzika japo hata miezi miwili au mitatu utulie tu upumzishe mwili na akili Au hata wiki au hata siku kadhaa ,. Kwanini hufanyi hivyo?..

Ni kwamba unaipenda sana KAZI au biashara Yako??, Au ni kwamba wewe hupendi kupumzika ( kutulia ) ,Bado hujatimiza malengo? Na unaamini ukifanya KAZI mfululizo bila kupumzika ndio utafanikiwa??,. Unayo majukumu mengi kiasi cha kwamba usipofanya KAZI wiki au mwezi mmoja Kila kitu kinavuruguika??,. Huna mtu wa kukusaidia ?? Au shida Nini??.... Tuambizane tu kidogo huenda ukapata namna ya kujipumzisha kutokana na maoni ya wadau..

Kwa upande wangu ni kwamba Bado sijaweza kujisimamia mwenyewe na watu ninaoshirikiana nao usipowasimamia KAZI zinaweza zisiende au zikafanyika sio Kwa kiwango kile ambacho inabidi kifanyike, Na mambo mengi ambayo yanahitaji kutimizwa Kwa wakati maana umri hausimami eti🥹
Nahitaji sana kujipumzisha ila changamoto ndio hiyo..

Tuambie na wewe tatizo nini???
Ukinipa mimi hiyo kazi nakuahidi utapumzika maana am genuine, humble and integrity!.

Mh! hebu kwanza niambie kazi gani baby wangu..?😁
 
Aliyejiajiri kupumzika inakuwa changamoto, maana anachoingiza ndicho anachotumia, kwa mfano unataka mama ntilie apumzike siku tatu, wakat huo huo anawaza kuongezeka?? haiwezekani.

Wanyakazi wa walioajiriwa wanapenda kupumzika sababu kubwa ni uvivu na kwa sababu anajua mwisho wa mwezi mshahara utaingia aumwe asiumwe, tofauti na aliyejiajiri labda wale ambao wameshasi mama na kuweza kuajir watu katika biashara zao wana nafasi ya kupumzika
 
Mimi nina partner wa biashara lakini wote tunafanya kwa bidii zote
Asikuambie mtu, hela ni kama uchawi vile

Kila unapopata unataka ziada
Nilipopata 100m ya kwanza nikasema niongeze x2 kama nitaweza

Siwezi kuacha kazi ya kujituma ila napumzika pia maana right hand wangu ni mzuri kwa biashara zote anazimudu

Nae anapumzika pia
Ila ukisema kazi haziendi bila wewe je umewaza kufa?
 
Yani ukisikiliza maneno ya wafanyabiashara na wajasiriamali wa bongo unaweza kudhani waliojiajiri wote ni matajiri na walioajiriwa wote ni masikini, kuna ukweli mwingi sana unafichwa sema ndio vile tena kila mtu anataka aonekane motivational speaker ila ukweli ni kwamba kwenye biashara, kama kweli unautaka huo utajiri basi hakuna huko kupumzika wanakokusema vinginevyo utaishia kuwa mid class au masikini kabisa, ni kama tulipokuwa shule tulikuwa tunaambiwa mkifika chuo mtakuwa na uhuru mnaoutaka hakuna wa kuwapangia maisha tofauti na shule lakini cha ajabu ukifika huko chuo, ni kweli hakuna wa kukuingilia ila hayo masomo tu yenyewe yatakuingilia na yatakupangia maisha hivyo ili ufaulu kihalali utalazimika kujiwekea ratiba kama ya mwanafunzi wa shule tu kiasi kwamba hata hiyo raha ya huo uhuru unaosemwa huioni
 
Yani ukisikiliza maneno ya wafanyabiashara na wajasiriamali wa bongo unaweza kudhani waliojiajiri wote ni matajiri na walioajiriwa wote ni masikini, kuna ukweli mwingi sana unafichwa sema ndio vile tena kila mtu anataka aonekane motivational speaker ila ukweli ni kwamba kwenye biashara, kama kweli unautaka huo utajiri basi hakuna huko kupumzika wanakokusema vinginevyo utaishia kuwa mid class au masikini kabisa, ni kama tulipokuwa shule tulikuwa tunaambiwa mkifika chuo mtakuwa na uhuru mnaoutaka hakuna wa kuwapangia maisha tofauti na shule lakini cha ajabu ukifika huko chuo, ni kweli hakuna wa kukuingilia ila hayo masomo tu yenyewe yatakuingilia na yatakupangia maisha hivyo ili ufaulu utalazimika kujiwekea ratiba kama ya mwanafunzi wa shule tu kiasi kwamba hata hiyo raha ya huo uhuru huioni
Ni kweli kabisa uyasemayo
Kuna wafanyakazi wanaishi kwa raha kuliko wafanya biashara wengi tu
Biashara zetu zingine kuendelea ni kama kutwanga maji tu

Kodi wakikusimamia unaona hawa wakusanyaji wana maisha mazuri zaidi ya duka

Especially kwetu
 
uwiano kati ya kazi na kupumzika ni jambo la msingi. Kupumzika kwa kiasi kunaweza kuwa njia ya kuongeza ufanisi, lakini kupumzika kupita kiasi kunaweza kuzuia maendeleo.

Mwisho wa siku, kila mtu ana njia yake ya kugundua kipimo sahihi cha mapumziko kulingana na malengo yake maishani. 😊
 
Back
Top Bottom